Jumamosi, 24 Februari 2018

Wakati wa Uzoefu Mmoja Niliona Ulinzi wa Mungu

 Wakati wa Uzoefu Mmoja Niliona Ulinzi wa Mungu


Yongxin, Jiji la Yibin, Mkoa wa Sichuan
Hatukuwahi kumwamini Mungu kabla. Mnamo mwaka wa 2005, tukitiwa moyo na Mungu, mume wangu, baba mkwe wangu, mjomba wangu, na mimi wote tuliikubali kazi ya Mungu ya siku za mwisho. Baada ya muda mfupi, kanisa lilinipangia kufanya wajibu wa kuhifadhi vitabu. Baadaye, nyumba yetu ilishika moto, na wakati wa moto huu tulipokea ulinzi wa Mungu wa ajabu. Mungu kwa hakika ni mwenyezi!
      Siku moja mwezi wa Machi ya mwaka wa 2006, baada ya chakula cha mchana takriban saa saba adhuhuri, kulikuwa kukinya theluji sana nje. Mume wangu, binti yangu na mimi tulikuwa ndani, tukijipasha joto kando ya moto na kubambua mahindi, wakati tuliposikia kwa ghafla sauti kutoka nje ikipiga yowe kwa sauti kubwa, “Nyumba yenu inachomeka! Haraka, tokeni nje na kuizima!” Kwa haraka tulikimbia nje, na kuona kwamba moto ulikuwa tayari umechoma paa la jikoni na banda la nguruwe. Wasioamini watatu walitusaidia kuuzima moto, na wakapaaza sauti, “Njooni msaidie kuzima moto!” Vijiji viwili jirani vilisikia ukelele wetu, na mara moja watu 30 au 40 wakaja kutusaidia kuzima moto. Wakati huo, nikasikia mtu akisema, “Je, familia hii haimwamini Mungu? Je, moto ungewafikaje? Sasa vile nyumba yao inawaka, ona kama bado wanamwamini Mungu.” Wakati huu, sikujali kile walichokuwa wakisema. Niliona kuwa moto ulikuwa unazidi kuwa mkali zaidi. Upepo mkali uliusukuma moto uliosukasuka moja kwa moja kuelekea sehemu kuu ya nyumba yetu. Nilikuwa na wasiwasi sana moyoni mwangu, kwa sababu ndani ya nyumba kulikuwa na vitabu vya kanisa na nafaka za familia yetu. Katika wakati huu wa kukata tamaa, ningemwita tu Mungu bila kukoma: “Ewe Mungu! Uweze kutunza na kulinda vitabu vya kanisa na nafaka zetu, usiviache vichomeke.” Baada ya mimi kuomba, muujiza ulifanyika. Upepo ghafla ukabadilisha mwelekeo; ni hapo tu nilipopunguza wasiwasi moyoni mwangu, kwa kuwa nilijua kwamba vitu vilivyokuwa ndani ya nyumba yetu vyote vilihifadhiwa. Baada ya kusikia watu waliokuwa wakiuzima moto wakiongea kuhusu vitu vilivyochomeka vilikuwa vya thamani gani ya fedha, tulikumbuka kwa ghafla kuwa kulikuwa na nguruwe wawili katika banda la nguruwe. Mume wangu akakimbia kuwaokoa; mara alipokuwa ameingia, ghafla kipande cha kifusi kilichowaka moto kilianguka na kuuziba mlango. Baada ya kuona hili nilijawa na hofu, na nikamlilia Mungu kabisa ndani ya moyo wangu, nikimsihi Amtunze na kumlinda mume wangu. Wale wasioamini wote walikuwa na wasiwasi kwamba mume wangu alikuwa katika hatari kubwa. Hata hivyo, kila mtu alipokuwa akitazama, mume wangu hatimaye aliibuka kutoka kwa moto akiwa salama salimini, akiwasongesha mbele nguruwe wawili kila mmoja akiwa na uzito wa zaidi ya kilo 50. Kwa wakati huu, moyo wangu hatimaye ukawa mtulivu. Moto huo uliwaka kwa saa moja au zaidi, kwa jumla ukichoma jikoni na mabanda mawili ya nguruwe, na kusababisha hasara ya takriban yuan elfu nne.Ilikuwa baadaye tu tulipokuja kujua kwamba moto huu mkubwa ulikuwa umeanzishwa na mtoto aliyekuwa akicheza na moto. Kwa wakati huu, nilikumbuka maneno ya Mungu: “Katika kila hatua ya kazi anayoifanya Mungu ndani ya watu, kwa nje inaonekana kama maingiliano kati ya watu, kana kwamba yalizaliwa kwa mipango ya wanadamu au kutokana na kuingilia kwa wanadamu. Ila kisirisiri, hatua ya kazi, na kila kitu kinachotendeka, ni pingamizi la Shetani kwa Mungu, na huhitaji watu kuwa imara katika ushuhuda wao kwa Mungu. Kwa mfano, tazama wakati Ayubu alijaribiwa: kisirisiri, Shetani alikuwa akiwekeana dau na Mungu, na kilichomtokea Ayubu kilikuwa ni matendo ya wanadamu, na kuingilia kwa wanadamu. Kuna pingamizi la Shetani kwa Mungu katika kila hatua ambayo Mungu anatenda ndani yenu—katika kila kitu kuna vita. … Wakati Mungu na Shetani wanapigana katika milki ya kiroho, utamridhishaje Mungu, na utasimamaje imara katika ushuhuda wako Kwake? Unapaswa kujua kuwa kila kitu unachokipitia ni majaribu makubwa na ndipo Mungu hukuhitaji kuwa na ushuhuda. … Ikiwa utawavutia ndugu na dada zako, wanafamilia, na kila aliye karibu nawe; ikiwa siku moja wasioamini watakuja na wavutiwe na yote unenayo na utendayo, na kuona kuwa yote afanyayo Mungu ni ya ajabu, basi utakuwa umekuwa na ushuhuda” (“Kumpenda Mungu Tu Ndiko Kumwamini Mungu Kweli” katika Neno Laonekana katika Mwili). Katika maneno ya Mungu nilielewa kuwa leo wakati familia yangu ilipoukabili uchomekaji wa nyumba yetu, kijuujuu ilionekana kuwa ulianzishwa na mtoto aliyekuwa akicheza na moto, lakini katika ulimwengu wa kiroho ilikuwa kwa kweli ni Shetani na Mungu wakiwa na dau. Shetani alitaka kutumia hili kunifanya nimlaumu Mungu, kumsaliti Mungu, na kumkana Mungu. Wakati wasioamini waliposema, “Nyumba ya familia hii inachomeka, ona kama bado wanamwamini Mungu,” hiki kilikuwa ni kishawishi cha Shetani kikinikabili. Kama ningewafuata wasioamini katika kumlaumu Mungu na kumhukumu Mungu, basi ningekuwa nimepoteza ushuhuda. Nilipofahamu mapenzi ya Mungu, nilimwomba Mungu: “Ee Mungu! Nilichokikabili leo ni jaribio Lako kwangu, na pia ni kishawishi cha Shetani. Uweze kunipa imani na nguvu, na uniepushe na malalamiko katika jambo hili ili nipate kuwa shahidi kwa ajili Yako mbele ya Shetani. Ninaamini kwamba mambo yote na vitu viko mikononi Mwako. Jaala yangu iko mikononi Mwako, nami nitaitii ukuu Wako na mipango.”
Jioni hiyo, familia yetu ilikusanyika pamoja kama kawaida ili kula na kunywa maneno ya Mungu, na nikamuuliza mume wangu, “Mbao zako zimechomwa moto, je, unamlaumu Mungu?” Akasema, “Kuna nini cha kulalamikia? Nilipokwenda kwa banda la nguruwe kuwafungulia nguruwe, nyote mliona wasiwasi kwa maisha yangu, na kuwa na hofu kwamba kitu kingenitendekea, lakini moyoni mwangu sikuwa natishika hata kidogo, na hatimaye niliibuka salama salimini. Je, si huu ni ulinzi wa Mungu? Kama si kwa ulinzi wa Mungu, nyumba yetu yote ingeteketezwa, na kuhusu maisha yangu ni vigumu kusema. Tuna kile tulicho nacho leo, na tunapaswa kumshukuru Mungu kwa utunzaji na ulinzi Wake, na kumshukuru kwa upendo Wake kwetu.” Kweli, wakati wa uzoefu huu, niliona kwa kweli Mungu akitutunza na kutulinda. Baada ya nyumba yetu kuchomeka, kama si kwa Mungu kuwahamasisha watu kadhaa kuja na kuuzima moto huo, basi kuitegemea nguvu za familia yetu peke yake hakungekuwa njia ya kuuzima moto. Upepo ulipokuwa ukisukuma moto chini kwelekea sehemu kuu ya nyumba yetu, kama si kwa Mungu kutumia nguvu Zake kuu kubadili mwelekeo wa upepo, basi vitabu vya kanisa, nafaka zetu na nyumba yetu yote ingekuwa imeteketezwa. Wakati mume wangu alipoukabili moto bila woga ili kuwaokoa nguruwe, kama haingekuwa ulinzi wa Mungu, chini ya ukali wa moto mkubwa kama huo ingewezekana kabisa kuwa mume wangu angechomeka hadi kufa, hangeweza kutoka nje tu bila kuumia hata unywele mmoja kichwani mwake. Tulivyozidi kuwasiliana kwa karibu, ndivyo tulivyozidi kuona nguvu kubwa ya Mungu na upendo. Hatukulalamika u, lakini mioyo yetu ilijaa shukrani isiyo na kikomo kwa Mungu.
Kutokana na uzoefu huu, niliona kwa macho yangu mwenyewe uweza wa Mungu na matendo Yake ya ajabu, na pia nilihisi wema Wake na uzuri Wake. Ingawa baada ya moto, hali ya familia yetu ilikuwa mbaya kidogo kuliko hapo awali, haikubadilisha kabisa moyo wangu ambao humfuata Mungu. Bila kujali wengine husema nini, naamini kabisa kwamba bila kujali jinsi ambavyo Mungu hutenda, daima ni kuwaokoa watu, na kuwakamilisha. Najua kwamba kulingana na hadhi yangu mwenyewe ilikuwa haiwezekani kabisa kuwa shahidi. Wakati wa jaribio hili, niliweza kuwa shahidi na kumwaibisha Shetani, na yote ni matokeo ya kazi ya Mungu. Kuanzia sasa kwendelea, nitasoma maneno ya Mungu zaidi, kujiandaa na ukweli zaidi, na wakati wa majaribu ya aina zote kuwa shahidi kwa Mungu na hadhi yangu halisi. Utukufu wote uweze kupewa Mwenyezi Mung Mwenyezi
Soma Zaidi: Kuhusu Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki Hutoka wapi?

0 评论:

Chapisha Maoni