Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Muziki wa Akapela "Tokeo Lililofikiwa kwa Kumjua Mungu" (Video Rasmi ya Muziki)

Hayuko katika upeo wa mbali, wala hajajificha juu mawinguni. Yuko kando yako, akiwa na mamlaka juu ya kila kitu chako, Yeye ni kila kitu ulicho nacho, na Yeye ni kitu pekee ulicho nacho.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Nyimbo-za-Uzoefu-wa-Maisha. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Nyimbo-za-Uzoefu-wa-Maisha. Onyesha machapisho yote

Alhamisi, 11 Oktoba 2018

Swahili Christian Music Video | "Ni Watu Waaminifu Pekee Walio na Mfano wa Binadamu" | God Led Me Onto the Right Path of Life

 Swahili Christian Music Video | "Ni Watu Waaminifu Pekee Walio na Mfano wa Binadamu" | God Led Me Onto the Right Path of Life


I

Kwa ajili ya faida niliacha viwango vyote vya mwenendo,

na bila haya nikatumia udanganyifu kutafuta riziki yangu.

Sikujali chochote kuhusu dhamiri au maadili, chochote kuhusu uadilifu au heshima.

Niliishi tu kuridhisha tamaa na uroho wangu vilivyozidi kukua.

Kwa moyo usio na amani, nilitembea katika matope ya dhambi,

bila njia yoyote ya kuepuka giza hii isiyo na mipaka.

Utajiri wa maisha na raha za muda mfupi

hazingeweza kuficha utupu na maumivu ndani ya moyo wangu.

Ni rahisi kuandika neno "mwanadamu."

Lakini kuwa mwaminifu na mwenye kusadikika ni vigumu kuliko ngumu.

Ni nani anayeweza kuniokoa kutoka katika shimo hili la dhambi?

Ni nani anayeweza kuniokoa kutoka katika shimo hili la dhambi?

II

Sauti ya Mungu imeniongoza mbele Yake.

Leo ninaweza kumfuata Mungu na kumtumikia.

Moyo wangu umejaa utamu kutoka kwa kusoma maneno ya Mungu kila siku.

Kwa kuelewa ukweli, sasa nina kanuni za tabia za kibinadamu.

Kila kitu ninachofanya na kusema ni kulingana na maneno ya Mungu.

Kukubali uchunguzi wa Mungu katika mambo yote huufanya moyo wangu uwe mtulivu na wenye amani.

Hakuna udanganyifu, hakuna uongo, ninaishi katika nuru.

Kwa moyo ulio wazi, mimi ni mtu mwaminifu, na ninaishi kwa kudhihirisha mfano wa kibinadamu mwishowe.

Hukumu ya Mungu na kuadibu kumeniokoa,

na kuniwezesha kuzaliwa upya katika maneno ya Mungu.

Mimi nina shukrani milele kwa upendo wa Mungu na kwa wokovu wa Mungu!

Mimi nina shukrani milele kwa upendo wa Mungu na kwa wokovu wa Mungu!

Mimi nina shukrani milele kwa upendo wa Mungu na kwa wokovu wa Mungu!

kutoka kwa Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

     Tufuate : Kuhusu Mwenyezi Mungu

Jumatatu, 4 Desemba 2017

Wimbo wa Uzoefu wa Maisha | Nimeuona uzuri wa Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu,

Wimbo wa Uzoefu wa Maisha | Nimeuona uzuri wa Mungu

I
Nasikia sauti ijulikanayo ikiniita mara kwa mara. Nikaamka na kuangalia kuona, ni nani aliye pale akizungumza. Sauti yake ni nyororo lakini kali, picha Yake nzuri! Nateseka kupigwa na kuvumilia maumivu makubwa, nikipapaswa na mkono Wake wenye upendo. Halafu natambua ni Mwenyezi ambaye nilipigana naye. Najichukia mwenyewe, kwa majuto makubwa, fikiria niliyoyafanya. Nimepotoka kwa kina, hakuna wanadamu, sasa nauona ukweli. Pamoja na mwanzo mpya, kujiingiza katika maisha halisi, kutimiza wajibu wangu. Kwa hali, kushindana na Mungu, mimi siheshimiki. Mungu bado Mungu, mtu ni mtu—mimi ni mjinga sana. Mjinga na mwenye kiburi kiasi cha kutoijua nafsi yangu halisi. Nilikosa aibu na kutahayarika; moyo wangu umejaa majuto. Najichukia mwenyewe, bila kujua kile ninachoishia. Shetani alinikanyaga kwa miaka mingi sana, nikawa mdharauliwa. Wakishapewa sumu na yule Mwovu, wanadamu wamepotea. Kama sitabadilishwa na kuzaliwa upya, sina maisha ya kweli.
II
Tabia yangu potovu hunisumbua, huduma yangu bado i bure. Ni mjinga wa kumjua Mungu, na kujawa na dhana; jinsi gani mimi singepinga? Mungu hunihukumu, kwa uasi wangu, na ukosefu wa uadilifu. Nimeuona upendo wa kweli wa kuadibu na kuhukumu. Mungu ni mwenye haki, mimi nina hakika kabisa. Niko ana kwa ana naye. Wokovu wa vitendo wa Mungu umenisaidia kufika umbali huu. Uhalisi wa Mungu na uweza wake, vimefichuliwa kikamilifu kwa mtu. Kwa kuishi katika mwanga, namjua Mungu na kuuona uzuri wake. Nikiwa na nia ya kutimiza wajibu, Nitamtosheleza Mungu na kumpenda.
kutoka kwa Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya
Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.