Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Muziki wa Akapela "Tokeo Lililofikiwa kwa Kumjua Mungu" (Video Rasmi ya Muziki)

Hayuko katika upeo wa mbali, wala hajajificha juu mawinguni. Yuko kando yako, akiwa na mamlaka juu ya kila kitu chako, Yeye ni kila kitu ulicho nacho, na Yeye ni kitu pekee ulicho nacho.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Video-za-Nyimbo-na-Kucheza. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Video-za-Nyimbo-na-Kucheza. Onyesha machapisho yote

Jumapili, 14 Aprili 2019

Wimbo wa Kuabudu | "Sifa kwa Maisha Mapya katika Ufalme" | Watu wa Mungu Humsifu na Kumwabudu Mungu


Wimbo wa Kuabudu | "Sifa kwa Maisha Mapya katika Ufalme" | Watu wa Mungu Humsifu na Kumwabudu Mungu

Tumesikia sauti ya Mungu na kurudi nyumbani Kwake.
Mikutanoni tunakula na kunywa maneno ya Mungu, tunahudhuria karamu.
Sisi tunaaga huzuni na vifungo vyetu, tunaishi maisha mapya.
Tunapofungua mioyo yetu katika ushirika wa kweli, mioyo yetu inaangazwa sana.
Maneno ya Mungu yako nasi kila siku, tunastarehe ndani yake.
Tunaondolewa vizuizi na ubaguzi wetu, tunaishi ndani ya upendo wa Mungu.
Tunatafakari, kufikiri maneno ya Mungu, Roho Mtakatifu anatuangazia.
Tunaelewa moyo wa Mungu, sisi si hasi tena.

Jumapili, 28 Oktoba 2018

Swahili Gospel Movie Segment "Mungu Anashikilia Ukuu Juu Ya Kila Kitu Katika Ulimweng"


Swahili Gospel Movie Segment "Mungu Anashikilia Ukuu Juu Ya Kila Kitu Katika Ulimweng"

Wanadamu wamekuwa wakitafuta majibu haya kwa miaka elfu kadhaa: Miili ya mbingu katika ulimwengu inawezaje kwendelea mbele kwa taratibu timilifu kama hiyo? Kwa nini vitu vyote vilivyo hai daima husogea kwa miviringo inayofuata kanuni zisizobadilika? Kwa nini watu huzaliwa, na halafu kwa nini sisi hufa? Ni nani kweli aliyeamua kanuni na sheria hizi zote? Ni nani kweli huutawala ulimwengu na vitu vyote? Sehemu hii ya ajabu kutoka kwa filamu ya Kikristo, "Yule Anayeshikilia Ukuu Juu Ya Kila Kitu", itakuongoza ufikie kiini cha maswali haya na kufunua mafumbo yote haya.

Usomaji Unaohusiana:Kanisa la Mwenyezi MunguMwenyezi Mungu

Jumanne, 25 Septemba 2018

Worship and Praise Dance | "Wale Wanaompenda Mungu kwa Dhati Wote ni Watu Waaminifu" | The Kingdom of Christ Is Paradise for the Honest (Swahili Subtitles)


Worship and Praise Dance | "Wale Wanaompenda Mungu kwa Dhati Wote ni Watu Waaminifu" | The Kingdom of Christ Is Paradise for the Honest (Swahili Subtitles)

Safi na mwaminifu kama mtoto, asiye na hatia na mchangamfu, aliyejawa na nguvu za ujana,

wao ni kama malaika wanaokuja ulimwenguni.

Hakuna uongo, udanganyifu au hadaa, na moyo ulio wazi na mwaminifu, wanaishi na heshima.

Wanaitoa mioyo yao kwa Mungu, Mungu anawaamini, na wao ni watu waaminifu ambao Mungu anapenda.

Wale wanaopenda ukweli wote wana mioyo ya uaminifu.

Watu waaminifu hufurahia kutenda ukweli, na kwa kumtii Mungu mioyo yao ina amani.

Wanamcha Mungu, wanaepuka maovu na wanaishi kulingana na maneno ya Mungu.

Wanaishi katika maneno ya Mungu na wamewekwa huru na kuachiliwa.

Wanakubali uchunguzi wa Mungu na kuishi mbele Yake. Kumpenda Mungu ni kuwa na furaha na mwenye shangwe.

Ndugu, tumemwamini Mungu tangu tulipokuwa wadogo. Je, tuna furaha?

Ndiyo, tuna furaha!

Nina furaha pia!


Ninapompenda Mungu, moyo wangu una utulivu na una furaha,

na ninaishi kwa urahisi ninapotenda kulingana na maneno ya Mungu.

Moyoni mwangu kuna Mungu tu, kuna ukweli tu, maneno ya Mungu yamekuwa maisha yangu.

Nikiishi chini ya uongozi wa maneno ya Mungu kila siku, ninabarikiwa na Mungu na Roho Mtakatifu ananiongoza.

Wanakubali uchunguzi wa Mungu na kuishi mbele Yake. Kumpenda Mungu ni kuwa na furaha na mwenye shangwe.

Nikiishi chini ya uongozi wa maneno ya Mungu kila siku, ninabarikiwa na Mungu na Roho Mtakatifu ananiongoza.

Ufalme wa Kristo ni mbinguni kwa watu waaminifu,

na ni makao yao ya kupendeza.

kutoka kwa Mfuate Mwanakondoo na Imba Nyimbo Mpya


    Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.

Ijumaa, 8 Juni 2018

Best Swahili Gospel Worship Song "Njoo Mbele Ya Mungu Mara kwa Mara" | Uso kwa uso na Mungu


Best Swahili Gospel Worship Song "Njoo Mbele Ya Mungu Mara kwa Mara" | Uso kwa uso na Mungu


Chukua fursa unapokuwa na wakati, keti kimya mbele ya Mungu. Soma neno Lake, jua ukweli Wake, rekebisha makosa yaliyo ndani yako.
Majaribu huja, yakabili;
ijue nia ya Mungu na utakuwa na nguvu.
Mwambie ni vitu gani unavyokosa, shiriki ukweli Wake kila mara. Roho yako ina furaha unapomwabudu Yeye.
Njoo mara kwa mara mbele ya Mungu, usipinge tena.
Kujali kwako mwili, kunamuumiza Yeye sana.
Soma neno Lake, elewa ukweli Wake.
Njoo mara kwa mara mbele ya Mungu.
Njoo mara kwa mara mbele ya Mungu.
Hivyo ishi kama mwanadamu mtakatifu!
Haijalishi ni jaribio lipi ama hukumu inayokuja, tutafanya kazi kumfurahisha Yeye.
Njoo mara kwa mara mbele ya Mungu. Njoo mara kwa mara mbele ya Mungu na uishi ukweli Wake. Ingawa tunakosa, tunapaswa kutafuta kumpenda Mungu.
Mradi tunampenda Yeye, bila shaka tutapokea sifa Yake.
Lazima tufuatilie ukweli na kumshuhudia Mungu.
Huu ni wajibu wetu ambao lazima tuufanye.
Roho yako ina furaha unapomwabudu Yeye.
Njoo mara kwa mara mbele ya Mungu, usipinge tena.
Kujali kwako mwili, kunamuumiza Yeye sana.
Soma neno Lake, elewa ukweli Wake.
Njoo mara kwa mara mbele ya Mungu.
Njoo mara kwa mara mbele ya Mungu.
Hivyo ishi kama mwanadamu mtakatifu!
Haijalishi ni jaribio lipi ama hukumu inayokuja, tutafanya kazi kumfurahisha Yeye.
Njoo mara kwa mara mbele ya Mungu.
Njoo mara kwa mara mbele ya Mungu na uishi ukweli Wake.
Hivyo ishi kama mwanadamu mtakatifu!
Haijalishi ni jaribio lipi ama hukumu inayokuja, tutafanya kazi kumfurahisha Yeye.
Njoo mara kwa mara mbele ya Mungu.
Njoo mara kwa mara mbele ya Mungu na uishi ukweli Wake, na uishi ukweli Wake, na uishi ukweli Wake.
Njoo mara kwa mara mbele ya Mungu na uishi ukweli Wake.
kutoka kwa Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Nyimbo na Kucheza,

     Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na 

mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana. 

Alhamisi, 22 Februari 2018

Sifa Kamili | Dansi ya Kilatini "Tukuzeni Ufanikishaji wa Kazi ya Mungu"


Sifa Kamili | Dansi ya Kilatini "Tukuzeni Ufanikishaji wa Kazi ya Mungu"

Tukuzeni Ufanikishaji wa Kazi ya Mungu

Kazi kubwa ya Mungu hubadilika haraka sana, vigumu kuipima, kuridhisha kwa mtu.
Angalia kandokando yako, si kama awali, kila kitu ni kizuri na kipya.
Kila kitu kimehuishwa, vyote vimetengenezwa upya, vyote vimetakaswa.
Tunamsifu Mungu, tukijawa furaha, nyimbo za sifa zinapepea mbinguni Kwake.
Mtukuzeni Yeye! Imbeni utukufu kwa jina Lake! Watu wote msifuni Mungu kwa vigelegele.
Mtukuzeni Yeye! Imbeni utukufu kwa jina Lake! Watu wote msifuni Mungu kwa vigelegele.
Sifa kwa matendo ya Mungu ya ajabu, isifuni hekima Yake, isiyoshindwa.
Isifuni tabia Yake yenye haki, msifuni kwa kuwa ni Mungu mwaminifu.
Kazi halisi ya Mungu imebadilisha tabia yangu ya kutotii.
Nimeadhimiwa na kazi iliyoteuliwa ya Mungu, kushuhudia kwa matendo Yake matakatifu.
Mtukuzeni Yeye! Imbeni utukufu kwa jina Lake!
Kuimba sifa Kwake kutoka kwa nyoyo zetu zenye furaha.
Mtukuzeni Yeye! Imbeni utukufu kwa jina Lake!
Kuimba sifa kwa Mungu kutoka kwa nyoyo zetu zenye furaha.
Wale wanaompenda Mungu, mtiini daima, na kuishi kwa kudhihirisha uhalisi wa neno Lake.
Baada ya kuacha dhambi zao na uchafu, wote huwa watakatifu.
Kuwa na ushuhuda kwa jina takatifu la Mungu, baada ya kuutosheleza moyo wa Mungu.
Uadilifu na utakatifu kujaa katika ulimwengu huu,
kila mahali ni pazuri na papya.
Mtukuzeni Yeye! Imbeni utukufu kwa jina Lake!
Kuimba sifa Kwake kutoka kwa nyoyo zetu zenye furaha.
Mtukuzeni Yeye! Imbeni utukufu kwa jina Lake!
Kuimba sifa kwa Mungu kutoka kwa nyoyo zetu zenye furaha.
Tukuzeni ufanikishaji wa kazi ya Mungu, Mungu ametukuzwa kikamilifu,
wote na yeyote anafanya kutii, kila mmoja ana mahali pa mwisho pa kupumzika.
Watu wa Mungu, watakatifu hata zaidi, humtukuza Mungu wa kweli.
Pamoja na Yeye, wametota kwa furaha.
Wametota kwa furaha.
Mtukuzeni! Pamoja, sisi humtukuza!
Nyimbo zetu za sifa hazitafika kikomo kamwe.
Mtukuzeni! Pamoja, sisi humtukuza!
Nyimbo zetu za sifa hazitafika kikomo kamwe, hazitafika kikomo.

kutoka kwa Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya


Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, upendo wa Mungu
Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.

Jumatano, 14 Februari 2018

Mbingu Mpya na Nchi imeonekana | "Ulimwengu na Eneo Kubwa Zamsifu Mungu"

Mbingu Mpya na Nchi imeonekana | "Ulimwengu na Eneo Kubwa Zamsifu Mungu"

Ulimwengu na Eneo Kubwa Zamsifu Mungu

Ha … nyimbo ni nyingi na ngoma ni za madaha;
ulimwengu na miisho ya dunia zinakuwa bahari inayosisimka.
Ha … mbingu ni mpya na dunia ni mpya.
Eneo kubwa la ulimwengu limejaa kusifu; tunapiga ukelele na kuruka kwa shangwe.
Milima yajiunga na milima na maji mengi kujiunga na maji mengi, ndugu wote wa kiume na kike ni wandani.
Twamsifu Mungu bila kukoma. Viumbe wampenda Mungu,
wakija, mbele ya kiti chake cha enzi kwa furaha kuabudu pamoja.
Mungu Amefichua katika Sayuni kwa ulimwengu uadilifu Wake na utakatifu Wake.
Watu wote wa Mungu wanachangamka kwa furaha, wakimtukuza Mungu bila kukoma.
Msifuni Mungu, msifuni Mungu!
Haleluya! Msifuni Mungu, msifuni Mungu!
Kumpenda Mungu, lazima kwanza tutoe moyo wa kweli.
Imbeni na kucheza kumsifu Mwenyezi Mungu.
Sauti inayosifu yapasua mbingu.
Acha sisi, waume kwa wake, wazee kwa vijana, tuwahi pamoja.
Watoa nyimbo nami natoa ngoma, uimbe nami nishirikiane.
Aliyetiwa aibu ni shetani—joka kubwa jekundu; lililotukuzwa ni jina la Mwenyezi Mungu wa kweli.

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, neema
Tumeona tabia adilifu ya Mungu kutoka kwa kazi Yake.
Mwenyezi Mungu ni Mungu mwadilifu. Watu wote wa Mungu wameiona sura Yake tukufu.
Sisi sote hufuata kumpenda na kumtosheleza Mungu, tukipenda kuwa waaminifu Kwake milele.
Msifuni Mungu, msifuni Mungu!
Haleluya! Msifuni Mungu, msifuni Mungu!
Njooni! Hebu tumsifu Mungu!
Njooni! Hebu tumsifu Mungu!
Kuja!
Milima inashangilia na maji mengi yanacheka,
mataifa yote na watu wote wanacheka kwa furaha. Mtazamo mpya ulioje!
Hiyo mbingu mpya, dunia mpya, na ufalme mpya!
Tunacheza na kuimba nyimbo mpya kwa Mungu; tumefurahi sana!
Nyimbo nzuri sana zaimbiwa Mungu, ngoma za madaha zaidi zawasilishwa kwa Mungu.
Moyo mnyofu umeinuliwa juu kwa Mungu, moyo wa kweli umetolewa juu kwa Mungu.
Watu wote wa Mungu na vitu vyote watamsifu Yeye milele bila kukoma. Ha!
Lo! Sayuni ni tukufu sana!
Makao ya Mungu hung'aa kwa miale ya mwanga. Utukufu wake hung'aa kotekote ulimwengu mzima.
Mwenyezi Mungu huvaa tabasamu, na hukalia enzi Yake akitazama umbo jipya la ulimwengu mzima. Ala

kutoka kwa Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

Jumapili, 3 Desemba 2017

Ukaribisheni Urejeaji wa Bwana Yesu | Sifa na Ibada "Furaha katika Nchi Nzuri ya Kanaani"

Ukaribisheni Urejeaji wa Bwana Yesu | Sifa na Ibada "Furaha katika Nchi Nzuri ya Kanaani"

I
Nimerudi kwa familia ya Mungu, mchangamfu na mwenye furaha. Mikono yangu imemshika mpendwa wangu, moyo wangu ni miliki Yake. Japo nimepitia Bonde la Machozi, nimeyaona mapenzi ya Mungu. Mapenzi yangu kwa Mungu hukua siku baada ya siku, Mungu ndiye chanzo cha furaha yangu. Nikiduwazwa na uzuri wa Mungu, moyo wangu umeshikizwa kwa Mungu. Siwezi kumpenda Mungu vya kutosha, nyimbo za sifa huchemka moyoni mwangu. Nikiduwazwa na uzuri wa Mungu, nyimbo za sifa huchemka moyoni mwangu. Siwezi kumpenda Mungu vya kutosha, nyimbo za sifa huchemka moyoni mwangu.
II
Katika nchi hii iliyobarikiwa ya Kanaani, yote ni mabichi, yote ni mapya, yakifurika na nafsi ya uhai ya maisha. Maji ya uzima hutiririka kutoka kwa Mungu wa vitendo, hunifanya niruzukike na maisha. Naweza kufurahia baraka kutoka mbinguni, hakuna tena kutafuta, kuchakura, kuwa na uchu. Nimewasili katika nchi iliyobarikiwa ya Kanaani, furaha yangu haina kifani! Upendo wangu kwa Mungu huniletea nguvu isiyoisha. Sauti za kusifu hupaa juu mbinguni, zikimwambia upendo wangu wa ndani. Ni haiba ilioje mpendwa wangu aliyo nayo! Uzuri Wake huiteka roho yangu. Manukato ya mpendwa wangu hunifanya nione ugumu wa kumwacha.
III
Nyota mbinguni zatabasamu kwangu, jua lanikubali kutoka juu. Pamoja na mwanga wa jua, na mvua na umande, tunda la uzima hukua kwa uthabiti na ubivu. Maneno ya Mungu, mengi na ya fahari, hutuletea sikukuu tamu. Riziki nzima na ya kutosha ya Mungu hutufanya tutosheke. Nchi ya Kanaani, ulimwengu wa maneno ya Mungu; upendo Wake hutuletea furaha isiyokoma. Nchi ya Kanaani, ulimwengu wa maneno ya Mungu; upendo Wake hutuletea furaha isiyokoma. Harufu nzuri ya matunda hujaa hewani. Ukikaa hapa kwa siku chache, utapapenda kuliko chochote kingine. Hakuna wakati utataka kuondoka.
IV
Mwezi wa fedha hunurisha mwanga wake. Mzuri na mchangamfu, ni maisha yangu. Uliye mpendwa moyoni mwangu, uzuri Wako umepita maneno yote. Moyo wangu u katika mapenzi matamu Nawe, siwezi kujizuia kuruka kwa furaha. Daima Uko moyoni mwangu, nitakuwa nawe maisha yangu yote. Moyo wangu hukutamani Wewe daima; kukupenda Wewe hufurahisha moyo wangu kila siku. Ee mpenzi moyoni mwangu! Nimekupa mapenzi yangu yote. Moyo wangu hukutamani Wewe daima; kukupenda Wewe hufurahisha moyo wangu kila siku. Ee mpenzi moyoni mwangu! Nimekupa mapenzi yangu yote.
kutoka kwa Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Tenzi,
Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.
Kauli Maalum: Uzalishaji huu wa video ulitengenezwa kama mradi usio wa faida na Kanisa la Mwenyezi Mungu. Wahusika wanaoonekana katika uzalishaji huu wanafanya kwa msingi wa kutotafuta faida, na hawajalipwa kwa njia yoyote. Video hii isisambazwe kwa mtu mwingine kwa minajili ya faida, na ni matumaini yetu kwamba kila mtu atashiriki kuigawa na kuisambaza hadharani. Wakati unapoisambaza, tafadhali sisitiza chanzo chake. Bila ridhaa ya Kanisa la Mwenyezi Mungu, hakuna shirika, kundi la kijamii, au mtu binafsi anayeweza kubadilisha au kuhudhurisha visivyo maudhui ya video hii.