Jumatano, 6 Juni 2018

Umeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Kanisa

Umeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Wafuasi wengi wa Bwana Yesu Kristo husikia kuhusu Umeme wa Mashariki kutoka kwa wachungaji wao, wazee wa kanisa, au wahubiri, lakini kwa hakika hakuna mtu anayejua Umeme wa Mashariki ulitoka wapi. Linapokuja suala la asili ya Umeme wa Mashariki, kila mtu ana maoni yake mwenyewe: Watu wengine wanaamini kuwa ni dhehebu jipya tu katika Ukristo, wengine huitweza kuwa “uasi” au “dhehebu bovu.” Watu wana mawazo haya ya upuuzi kwa sababu hawajui kazi ya Mungu.
Kazi ya Mungu ni ya kuendelea daima. Mwanadamu haitambui kanuni kwamba kazi ya Mungu daima ni mpya na kamwe si nzee au kwamba lengo la kazi ya Mungu ni kumwokoa mwanadamu, na aidha, mwanadamu ana tabia ya kiburi na ya kishetani ambayo ni kaidi. Ndiyo maana kila mara Mungu anapoanza kazi mpya daima Yeye atakumbwa na kufuru, mateso, na shutuma kutoka kwa dunia ya kidini ambayo hushikilia kwa ukaidi njia ya zamani. Kwa mintarafu ya wale ambao huikubali kazi mpya ya Mungu na kueneza njia ya kweli, wao hulimbikizwa kila aina ya shutuma zisizo na msingi na majina machafu. Agano Jipya la Biblia liliandika ukweli huu: Ili kumwokoa mwanadamu kutoka kwa hatari ya kuadibiwa kwa ajili ya kutoweza kushika sheria, Mungu alipata mwili na kuanza kazi ya ukombozi katika Enzi ya Neema. Wakati huo, wakati Bwana Yesu alipokuwa akifanya kazi Yake Uyahudi akifanya miujiza mingi–kuwaponya wagonjwa na kufukuza pepo–Aliwafadhili watu kwa neema za ukarimu na Alionyesha ukweli mwingi, akifanya ya kutosha kuthibitisha kuwa Alikuwa kwa kweli na kabisa Mungu Mwenyewe, kwamba Alikuwa ni Masihi kama ilivyotabiriwa. Lakini wakuu wa makuhani wa Kiyahudi, na waandishi na Mafarisayo hawangeamini kwamba Alikuwa Masihi aliyesubiriwa kwa muda mrefu, na badala yake walimkashifu Yeye, wakamhukumu Yeye, na kuitia hatiani kazi ya Bwana Yesu kama “uasi” na “dhehebu.” Ilikuwa ni katika Nazareti ambapo Bwana Yesu alilelewa na kuanza kazi Yake, na ndiyo maana walimpa Yeye na wafuasi wake wote jina la “dhehebu la Wanazorayo,” na wakamlaumu Mtume Paulo kuwa kiongozi wa waasi (taz. Matendo 24: 5). Hili linatuambia nini? Ndugu zetu wa kiume na wa kike ambao wanaoamini katika Bwana, wanajua kwamba kazi Bwana Yesu huko Uyahudi ilifanyika kabisa kulingana na mpango wa usimamizi wa Mungu Mwenyewe ili kuanza Enzi ya Neema na kuanza kazi mpya ya kumkomboa mwanadamu. Bila kujali Myahudi ama mtu wa Mataifa, Mkereketwa au Msadukayo, mtu yeyote ambaye kwa kweli ana kiu ya, na kutafuta njia ya kweli anaweza kupata msamaha kwa kumfuata Bwana Yesu, Mungu aliye mmoja wa kweli. Mungu kamwe hakuhitaji wala Hakuwahi kuanzisha dhehebu lolote, shirika, au kundi la kidini, sembuse hili “dhehebu la Wanazorayo.” Kwa hiyo, uasi, yaani hili “dhehebu la Wanazorayo,” kwa kweli ni uvumi ulioundwa ili kumshambulia na kumsingizia Bwana Yesu na kuishutumu kazi Yake–uvumi uliobuniwa na wakuu wa makuhani na waandishi na Mafarisayo “waliomhudumia” Yehova Mungu hekaluni. Hatimaye, ilikuwa chini ya udanganyifu na udhibiti wa hawa “watu waliomhudumia Mungu” ambapo watu wote wa Kiyahudi walichukua Bwana Yesu na wakamsulubisha Yeye kwa msalaba, wakiikosea tabia ya Mungu na kupata adhabu ya Mungu, wakileta miaka 2000 ya uangamizaji kwa Israeli.
Kwa njia hiyo, ili kumwezesha mwanadamu kuponyoka kutoka kwa mzunguko wa kutenda dhambi halafu kuzikiri na kisha kuendelea na dhambi tena, kabisa kulegeza tabia potovu ya Shetani, ili kuondoa asili yake ya dhambi na kufikia utakatifu, kwa kweli kupata wokovu wa Mungu, katika siku za mwisho Mungu mara nyingine tena amekuwa mwili na ameonyesha ukweli kuhukumu na kuadibu wanadamu wapotovu. Kwa kazi Yake mpya, Yeye anamtakasa na kumwokoa mwanadamu kikamilifu. Kupitia hukumu, kuadibu, majaribu, na usafishaji wa maneno ya Mungu, ndugu wa kiume na wa kike ambao hukubali injili ya Mungu ya siku za mwisho na ambao huenda sawa na kazi Yake mpya huona kwa dhahiri kwamba Mwenyezi Mungu ambaye huwapa ukweli huu katika siku za mwisho ndiye kurudi kwa Bwana Yesu na kutoka vina vya mioyo yao wao hushangilia na kutukuza, wakihisi kwa undani ukuu wa ajabu wa kuinuliwa juu na wa wokovu Wake. Kwa hiyo, kwa kurudisha upendo wa Mungu, kuwaruhusu hata watu wengi zaidi waweze kuzifuata nyayo za Mungu na kurudi nyumbani mwa Mungu, wanatoka na kuwaambia habari njema wale wote ambao wamekuwa wakisubiri kwa shauku kurudi kwa Bwana Yesu. Wanawaambia kwamba Bwana Yesu tayari amepata mwili tena na kurudi ulimwenguni, nchini China huko Mashariki, akimaliza Enzi ya Neema na kuleta Enzi ya Ufalme. Ameanza kazi mpya, ya juu sana ya kumhukumu na kumtakasa mwanadamu. Wanawaambia kuwa Mungu sasa amefanikisha sura ya 24 mstari wa 27 wa Injili ya Mathayo: “Kwa maana kama umeme utokavyo mashariki, na kumulika hata magharibi; hivyo ndivyo ujio wake Mwana wa Adamu utakavyokuwa.” Ukweli ambao Mungu aliuleta wakati huu ni wa juu zaidi kuliko kabla, kufichua mafumbo ya kazi Yake kutoka uumbaji hadi siku za mwisho, Akichukua ukweli wote wa utakaso na wokovu wa wanadamu na kuwafadhilia wanadamu na ndugu wa kiume na wa kike ambao kwa kweli humwamini Mungu, katika umati wanakuja kwa nuru. Na katika siku za mwisho wakati wa kazi ya Mungu ya mavuno ni mfupi, kasi ni ya upesi, na, kama pigo la umeme, katika muda wa zaidi ya miaka kumi tu injili ya ufalme ya Mungu imeenea sana katika China Bara na inakua kwa nchi zote na maeneo ya dunia. Na hata hivyo, wakikabiliwa na kazi mpya ya Mungu ambayo hailingani na dhana za mtu, wale watu wenye kiburi na wa kujidai kutoka kwa madhehebu mbalimbali ya kidini kwa ukaidi hushikilia njia za zamani. Wao ambao hawawezi kwenda sawa na kazi mpya ya Mungu huwa hawatafuti au kuchunguza njia ya kweli tu, lakini badala yake huhangaika juu ya unabii wa kibiblia kama unavyonenwa na ndugu wa kiume na wa kike ambao hushuhudia kazi ya Mungu ya siku za mwisho. Wao kufanya madai yasiyo na msingi, kulishutumu na kulikashifu Kanisa la Mwenyezi Mungu kuwa “Dhehebu la Umeme wa Mashariki.” Na kwa kila njia wao hufanya kabisa kama jamii za kidini za Kiyahudi zilivyofanya kabla, kuwashambulia, kuwakashifu, na kuwashutumu wanafunzi wa Bwana Yesu na mitume kama “dhehebu la Wanazorayo.” Kwamba wanaweza kupinga na kushambulia kazi ya Mungu ya siku za mwisho jinsi hii, kwamba wanaweza kuwakataza watu kuzifuata nyayo za Mungu na kuitii kazi Yake, si hilo ni sawa kabisa kama Mafarisayo walivyompinga na kumshutumu Kristo kabla? Si kiini cha vitendo hivi ni hasa kuuchukia ukweli na kumkufuru Roho Mtakatifu?
Kama Mwenyezi Mungu hangesema neno Lake na kufunua mafumbo, basi hatungeelewa kwa kweli kamwe ni nini maana na unabii “Kwa maana kama umeme utokavyo mashariki, na kumulika hata magharibi.” Mwenyezi Mungu anasema: “Watu wote wanapotilia maanani, wakati vitu vyote vinafanywa upya na kuhuishwa, wakati kila mtu anamtii Mungu bila shaka, na yuko tayari kubeba jukumu zito la mzigo wa Mungu—hapa ndipo wakati umeme wa mashariki unatoka, ukiangaza yote kutoka Mashariki hadi Magharibi, ukiyatisha yote ya ulimwengu na ujaji wa mwanga huu; na wakati huu, Mungu tena huanza maisha Yake mapya. … Ambayo ni kusema, katika Mashariki ya dunia, kutoka wakati ushuhuda kwa Mungu Mwenyewe huanza, hadi wakati Yeye huanza kufanya kazi, mpaka wakati uungu huanza kushika madaraka makuu pande zote duniani—huu ni mwale unaong’aa wa umeme wa mashariki, ambao daima umemulika kwa ulimwengu mzima. Wakati ambapo nchi duniani zinakuwa ulimwengu wa Kristo ndio wakati ambapo ulimwengu mzima unatiwa nuru. Sasa ndio wakati ambapo umeme wa mashariki unatoka: Mungu mwenye mwili Anaanza kufanya kazi, na, zaidi ya hayo, Anaongea moja kwa moja katika uungu. Inaweza kusemwa kwamba Mungu anapoanza kuongea duniani ni wakati ambapo umeme wa mashariki unatoka. Kwa usahihi zaidi, wakati ambapo maji ya uhai yanatiririka kutoka katika kiti cha enzi—wakati ambapo matamshi kutoka katika kiti cha enzi huanza—bila shaka ni wakati ambapo matamshi ya Roho wa mara saba huanza kirasmi” (“Ufafanuzi wa Tamko la Kumi na Mbili” katika Neno Laonekana katika Mwili). “Kotekote katika ulimwengu Ninafanya kazi Yangu, na katika Mashariki, mashambulio ya radi yanapiga bila kukoma, yakitingisha madhehebu yote na vikundi. Ni sauti Yangu ndiyo imewaleta watu katika wakati wa sasa. Nitawasababisha watu wote kushindwa na sauti Yangu, kuingia katika mkondo huu, na kunyenyekea mbele Yangu, kwa maana Nilijirudishia utukufu Wangu kutoka duniani kote zamani na Nikautoa upya Mashariki. Ni nani asiyetamani kuuona utukufu Wangu? Ni nani asiyesubiri kwa hamu kurudi Kwangu? Ni nani asiye na kiu cha kuonekana Kwangu tena? Ni nani asiyetamani kuona kupendeza Kwangu? Ni nani hangetaka kuja kwenye nuru? Ni nani hangeuona utajiri wa Kanaani? Ni nani hangoji kwa hamu kurudi kwa Mkombozi? Ni nani asiyempenda kwa dhati Mwenyezi Mkuu? Sauti Yangu itaenea kotekote duniani; Ningependa, kuwazungumzia maneno mengi zaidi wateule wangu, Nikiwatazama. Nanena maneno Yangu kwa ulimwengu wote na kwa wanadamu, kama radi yenye nguvu inayotingisha milima na mito. Hivyo maneno yaliyo kinywani Mwangu yamekuwa hazina ya mwanadamu, na watu wote wanayahifadhi maneno Yangu kwa upendo mkubwa. Umeme wa radi unaangaza kutoka Mashariki mpaka Magharibi. Maneno Yangu ni kiasi kwamba mwanadamu huchukia kuyaacha na pia huyaona kama yasiyoeleweka, lakini zaidi ya yote mwanadamu huyafurahia. Kama mtoto mchanga aliyezaliwa hivi karibuni, wanadamu wote wana uchangamfu na furaha, wakisherehekea kuja Kwangu. Kwa njia ya sauti Yangu, Nitawaleta watu wote mbele Yangu. Tangu hapo, Nitaingia rasmi katika jamii ya wanadamu ili waje kuniabudu. Kwa utukufu Ninaoutoa na maneno yaliyo kinywani Mwangu, Nitawafanya watu wote kuja mbele Yangu na kuona kwamba umeme unaangaza kutoka Mashariki … Kwani Nimeshafufuka kitambo, na Nimeondoka miongoni mwa wanadamu, na kisha Nimeonekana tena miongoni mwa wanadamu Nikiwa na utukufu. Mimi ndiye Niliyeabudiwa enzi nyingi kabla ya wakati huu, na pia Mimi ni ‘mtoto mchanga’ Aliyeachwa na Israeli enzi nyingi kabla ya wakati huu. Zaidi ya hayo, Mimi ndiye Mwenyezi Mungu mwenye utukufu wote wa enzi hii!” (“Ngurumo Saba Zatoa Sauti— Zikitabiri Kuwa Injili ya Ufalme Itaenea Kote Ulimwenguni” katika Neno Laonekana katika Mwili). Kutokana na maneno ya Mwenyezi Mungu tunaona kuwa kazi ya Mungu na neno la siku za mwisho ni umeme ambao huangaza kutoka Mashariki. “Umeme” ni mwanga mkubwa, kumaanisha neno la Mungu, njia ya Mungu ya hukumu na kuadibu katika siku za mwisho. Kifungu “utokavyo mashariki” kinamaanisha hutoka China, na “kumulika hata magharibi” kikimaanisha kuwasili katika nchi za Magharibi. Mwisho, “hivyo ndivyo ujio wake Mwana wa Adamu utakavyokuwa” kinahusu Mungu kupata mwili na kwanza akijifichua Mwenyewe na kuanza kazi Yake nchini China katika Mashariki. Huko Analifanya kundi la watu ambao kwa kweli wanamjua Mungu, na wao ni washindi kama ilivyotabiriwa katika Kitabu cha Ufunuo. Kisha kupitia watu hawa, injili ya siku za mwisho itaenea Magharibi, ili kila mmoja atapokea wokovu wa Mungu wa siku ya mwisho. Hili limefanikishwa sasa na ni ukweli ambao unaweza kuonekana na kila mtu! Umeme wa Mashariki (yaani, kazi ya Mungu ya hukumu katika siku za mwisho nchini China) unaweza kuturuhusu tupokee upendo wote na wokovu ambao Mungu humfadhilia mwanadamu, unaweza kuturuhusu tuujue uso wa kweli wa Mungu, na husababisha ndani yetu uchaji na ibada ya kweli ya Mungu. Kama tu pigo la umeme, neno la Mungu humpa mwanadamu mwanga na matumaini. Wale wote ambao huukubali umeme wa Mashariki–kazi ya Mungu ya siku za mwisho–wote wanaweza kulishuhudia jambo hili.
Sasa, mnaposoma hili, naamini nyinyi nyote mna jibu dhahiri kwa swali la ni nini asili ya Umeme wa Mashariki. Mungu ni Muumba wa mbingu na nchi na vitu vyote. Kwa sababu mtu alipotoshwa na Shetani, Mungu alianza kazi Yake ya kumwokoa mwanadamu. Mungu anataka kuwafanya watu wote katika ulimwengu kuyaona matendo Yake, kwamba dini zote zitakuwa moja, zikimwabudu Muumba. Kisha Atawaruhusu wale wote watafutao kuonekana kwa Mungu na kufuata nyayo Zake kufanikisha usafi na kufikia wokovu. Atawachukua watu hawa ambao wanaupendeza moyo wa Mungu katika ufalme kupumzika na Yeye. Kwa hiyo, kila mmoja wa ndugu zetu wa kiume na wa kike ambao kweli wanaamini katika Mungu na kwa shauku hungoja kurudi kwa Bwana Yesu lazima waweke dhana zao za kidini kando na kuchunguza njia ya kweli. Usitilie maanani uvumi, kupinga njia ya kweli kwa upofu, kwa kuwa itaishia katika kuupoteza wokovu wa Mungu katika siku za mwisho. Ni lazima tufanye hima kufuata hatua za kazi ya Mungu, kufuata nyayo za Mungu kwa karibu. Hii ndiyo njia ya pekee ambayo kwayo tunaweza kupata wokovu Wake hatimaye na kuletwa na Mungu katika ufalme Wake.

0 评论:

Chapisha Maoni