Jumatano, 19 Desemba 2018

25. Umuhimu wa Uratibu Katika Huduma

Umeme wa Mashariki |  25. Umuhimu wa Uratibu Katika Huduma

Mungu,Kristo,ukweli,Kanisa,

Mei Jie Jijini Jinan, Mkoani Shandong

Baada ya kubadilisha uongozi wa kanisa kurudi kwa ule wa asili, ubia uliwekwa kwa kila ngazi ya kiongozi katika nyumba ya Mungu. Wakati huo, nilifikiri kwamba huu ulikuwa mpangilio mzuri. Nilikuwa wa ubora wa tabia wa chini na nilikuwa na kazi nyingi; kwa kweli nilihitaji mbia wa kunisaidia kukamilisha kila aina ya kazi katika eneo langu.
Kwa hiyo, mimi na dada aliyekuwa mbia wangu tulianza kufanya kazi ya uchungaji katika kanisa pamoja. Lakini polepole, nikaona kuwa hakuwa akifanya kila aina ya vitu kulingana na mapenzi yangu, na upinzani ulianza moyoni mwangu: Ingawa mimi ni mwenye shughuli nyingi kiasi ninapofanya kazi mwenyewe, ni sawa, na kupangia mbia kweli kutakuwa mabishano. Ikiwa nitamruhusu kufanya kazi fulani na sio bora, basi afadhali niifanye mwenyewe. Nisipomruhusu afanye kazi hiyo, haidhuru, yeye ni mbia wangu. ... Kwa hiyo, upinzani zaidi ulikua moyoni mwangu, hadi wakati mmoja, sikuweza kuuzuia tena na nikamsirikia: "Unawezaje kuwa mjinga kiasi hicho? Umekuwa kiongozi kwa miaka mingi, inawezekanaje bado hufanyi kazi nzuri? Kwa nini huwezi kamwe kuelewa, au kujibu? ... " Baada ya kumaliza, nilihisi vibaya, mwenye hatia sana. Nilifikiria moyoni: Je, hali yangu si sahihi? Kwa hiyo nilikuja mbele ya Mungu kwa kuomba, na kuona maneno ya Mungu yaliyosema: “Leo mahitaji ya nyinyi kufanya kazi pamoja kwa upatanifu ni sawa na jinsi Yehova alivyowataka Waisraeli kumtumikia. Vinginevyo, tamatisha tu huduma yenu. Kwa sababu nyinyi ni watu wanaomtumikia Mungu moja kwa moja, kwa kiwango cha chini zaidi mnapaswa kuweza kuwa waaminifu na watiifu katika huduma yenu, na lazima muweze wa kujifunza masomo kwa njia ya vitendo. … Hata hamjifunzi au kuingia katika somo la matendo kama hilo, na bado mnazungumza juu ya kumtumikia Mungu! … Ikiwa ninyi watu ambao mnaratibu kufanya kazi katika makanisa hamjifunzi kutoka kwa kila mmoja, na kuwasiliana, kufidia mapungufu ya kila mmoja, mnaweza kujifunza masomo kutoka wapi? Mnapokutana na chochote, mnapaswa kushirikiana na kila mmoja, ili maisha yenu yaweze kufaidika” (“Hudumu kama Waisraeli Walivyofanya” katika Neno Laonekana katika Mwili). Kisha nikaona mambo haya katika ushirika wa mtu huyu: "Kuna watu wengine ambao hawawezi kushirikiana na mtu mwingine wanapotekeleza wajibu wao. Hakuna mtu anayeweza kuwakaribia; hii inaonyesha kiburi na majivuno yao, kuwa hawana hisia yoyote ya kibinadamu, hawajijui wenyewe, na wanawadharau wengine. Je, si hili ni la kuhurumiwa? Tabia ya mwanadamu wa aina hii haibadiliki hata kidogo, na si rahisi kusema kama anaweza kuokolewa na Mungu. Watu ambao wanajijua kwa kweli wanaweza kuwatendea watu wengine kwa usahihi bila kuwakosoa sana. Wanaweza pia kuwasaidia na kuwafadhili wengine kwa ustahamilivu, kuwafanya watu wahisi kuwa ni mahabubu na wapendwa; wanaweza kuwa na mahusiano yanayofaa na wengine. Wao ni watu wenye ubinadamu, na watu wenye ubinadamu tu ndio wana moyo wa ibada kwa Mungu, wanaweza kuishi kwa upatanisho na wengine, na kutekeleza wajibu wao vya kutosha" ("Wakati wa Kutimiza Wajibu wa Mtu Matokeo ya Mwisho ya Mwanadamu Yanaonekana "katika Rekodi za Maongezi ya Kristo Pamoja na Viongozi na Wafanyakazi wa Kanisa). Yakiwekwa pamoja na yale maneno ya Mungu na haya kutoka kwa ushirika wa yule mtu, nilijichunguza kwa makini na kuona kuwa sikuwa nimeelewa mapenzi ya Mungu katika nyumba ya Mungu kupanga wabia kwa ngazi zote za viongozi. Hata zaidi, sikuwa nimeweka katika matendo au kuingia katika ukweli wa uratibu patanifu. Sababu moja ya nyumba ya Mungu kupanga wabia kwa ajili yetu ilikuwa ni kwa sababu ubora wetu wa tabia ulikuwa wa chini sana, na ufahamu wetu wa vipengele vyote vya ukweli ulikuwa finyu sana. Hatungeweza kuikabili kazi yote kanisani pekee yetu. Kwa msaada wa mbia, tungeweza kukamilisha kazi ya kanisa vyema zaidi na pia kuepuka upinzani dhidi ya Mungu kupitia kufanya kazi pekee yetu, kufanya chochote tulichotaka, na kutegemea mapenzi yetu wenyewe katika huduma yetu kwa Mungu. Sababu nyingine ilikuwa ili tungeweza kufanya mazoezi bora zaidi ya kuingia katika ukweli wa ubinadamu wa kawaida, ili tungeweza kuwa na ushirika wa pande mbili na wabia, na kujifunza kutoka kwa kila mmoja. Hili ni la manufaa makubwa kwa kazi ya kanisa pamoja na uingiaji wa maisha yetu ya kibinafsi. Hii ilinifanya nione kuwa ushirikiano patanifu katika huduma yetu ni ya muhimu sana kwa kazi ya kanisa na uingiaji wa maisha yetu ya kibinafsi! Lakini sikuwa nimetafuta mapenzi ya Mungu hata kidogo kwa hili. Sikuwa makini kwa masomo ya utendaji ambayo ningeweza kujifunza kupitia uratibu huu. Nilifanya kazi naye tu kwa kutotaka kwa sababu ya utaratibu wa kanisa, na mara tu dada huyu hakufanya mambo machache vizuri, nilimkemea na kupatwa na hasira. Daima nilihisi kuwa hakuwa na uwezo kama nilivyokuwa nao mimi, na sikuona uwezo wake na faida. Hata nikapinga utaratibu wa kanisa. Kwa kweli nilikuwa mwenye kiburi sana, nisiyejijua, na sikuwa na ubinadamu wa kawaida hata kidogo au mantiki, na hata zaidi sikuwa na moyo wa uchaji kwa Mungu kabisa, na sikustahili kutoa huduma mbele ya Mungu.
Ee Mungu! Ufunuo wako uliniwezesha kutambua kutoweza kwangu kuratibu kwa upatano, kiburi changu na upande wangu wa kusikitisha katika huduma Kwako. Kuanzia siku hii na kuendelea mbele, niko tayari kudumisha moyo wa uchaji Kwako, kutojitetea tena, na katika vitu vyote kusisitiza maslahi ya kanisa. Katika uratibu wa huduma nitawasaidia wengine na kujifunza kutoka kwa wengine. Nitalenga kuingia kwangu mwenyewe katika ukweli, na kutafuta hivi karibuni kuwa mtu mwenye ukweli na ubinadamu ambaye ni wa kufaa kukutumiwa na Wewe.
Utukufu wote Uwe kwa Mwenyezi Mung.

0 评论:

Chapisha Maoni