Jumapili, 8 Julai 2018

Utangulizi

Utangulizi

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu

Sehemu hii ya maneno ya Mungu ina jumla ya vifungu vinne; vilionyeshwa na Kristo kati ya mwishoni mwa mwaka wa 1992 na 2005. Mengi ya maneno hayo yanategemezwa kwa rekodi kutoka kwa mahubiri na ushirika Wake wakati Alitembea katika makanisa. Maandiko haya hayajapitia mabadiliko yoyote, wala Kristo hajafanya mabadiliko yoyote. Mengine yanajumuisha maandishi kutoka kwa kalamu ya Kristo mwenyewe.  (Kristo anapoandika yote hufanywa wakati mmoja bila kusita ili kufikiri, hayajawahi kuhitaji mabadiliko hata kidogo, na yote ni maonyesho ya Roho. Hili haliwezi kushukiwa.) Hatujapanga haya kwa kutenganisha, lakini badala yake tumeyaweka pamoja katika taratibu yake ya asili kama yalivyoonyeshwa. Kwa njia hii tutaweza kuona hatua za Mungu za kazi kutoka kwa kile Alichosema, na kuelewa jinsi Anavyofanya kazi wakati wa kila awamu. Taratibu hii pia inaleta faida zaidi kwa ufahamu wa wanadamu wa hatua za kazi ya Mungu, na kwa ajili ya kujua hekima yake.
Sura za kwanza nane za "Njia" za "Maneno ya Mwana wa Adamu Mwenye Mwili Alipokuwa Akitembea Makanisani (I)" ni sehemu ndogo ya maneno ya Kristo jinsi Alivyo sawa miongoni mwa wanadamu. Takriban yanaonekana hayana mvuto, lakini kwa kweli yana ufahamu wa upendo wa Mungu na kujali Kwake wanadamu. Kabla ya haya Mungu alinena kutoka kwa mtazamo wa mbingu ya tatu, kwa hiyo umbali kati ya mwanadamu na Mungu ukawa mkubwa sana na watu hawakuthubutu kumkaribia Mungu, sembuse kuomba ruzuku ya Mungu kwa maisha yao. Kwa hiyo, katika "Njia," Mungu alinena kwa mwanadamu kama mwenzi na Akaonyesha mwelekeo wa njia ili uhusiano kati ya mwanadamu na Mungu upate tena hali yake ya asili, mwanadamu hakuwa na shaka tena kama Mungu alikuwa bado Anatumia mbinu ya kuzungumza, na hakukuwa tena na tishio la jaribio la mauti. Mungu alishuka kutoka mbingu ya tatu hadi duniani; mwanadamu alikuja mbele ya kiti cha enzi cha Mungu kutoka kwa ziwa la moto na kiberiti, akivua haraka kivuli cha kuwa mtendaji huduma, na akakubali rasmi ubatizo wa maneno ya Mungu kama ndama aliyezaliwa hivi karibuni. Ilikuwa kwa njia hii tu ndipo Mungu aliweza kukaa ubavuni mwa watu na kuzungumza nao, na kutekeleza kazi zaidi ya kuendeleza maisha. Kusudi la Mungu kujinyenyekeza kama mwanadamu ni kuwa karibu zaidi na wanadamu, kupunguza umbali kati ya mwanadamu na Mungu, kupata utambuzi na imani ya watu, na kuhamasisha ujasiri wao kufuata maisha na kumfuata Mungu. Mwishowe, sura nane za "Njia" ni funguo za Mungu zinazofungua milango ya mioyo ya watu; ni kidonge Chake cha dawa kilichopakwa sukari. Ni kwa njia hii pekee ndipo watu wanaweza kusikiliza kwa makini mafundisho na makaripio ya Mungu. Inaweza kusemwa kuwa ni baada ya hapo tu ndipo Mungu alianza rasmi kazi ya utoaji wa maisha na maonyesho ya ukweli katika hatua hii ya sasa ya kazi, na Aliendelea kunena: "Maoni Wanayopaswa Kushikilia Waumini" na "Juu ya Hatua za Kazi ya Mungu".... Je, namna hii haionyeshi hekima ya Mungu na nia Zake zenye ari? Hii ni ruzuku ya kwanza kabisa ya Kristo kwa ajili ya maisha, kwa hiyo ikilinganishwa na sehemu chache zifuatazo ukweli huo ni wa juu juu kwa kiasi fulani. Kanuni inayounga mkono hili ni rahisi sana: Mungu hutenda kazi kulingana na mahitaji ya wanadamu. Yeye huwa hatendi au kunena bila kufahamu; Mungu pekee ndiye Anaelewa kwa ukamilifu mahitaji ya wanadamu, na Yeye pekee ndiye Anayejali sana na Aliye na upendo kwa mwanadamu.
"Kazi na Kuingia" (1 hadi 10) ni maneno ya Mungu yanayoingia katika awamu nyingine mpya, kwa hiyo tumeanza na sura hizi kumi na baada ya hayo, yalisababisha "Maneno ya Mwana wa Adamu Mwenye Mwili Alipokuwa Akitembea Makanisani (II)." Katika awamu hiyo, Mungu alitoa matakwa ya kina zaidi kwa kundi Lake la wafuasi, ambayo yalijumuisha ufahamu kuhusu mitindo ya maisha ya watu, mahitaji kuhusu ubora wa tabia yao, na kadhalika. Na kwa sababu watu hao walikuwa tayari wamedhamiria mioyo yao kwa uthabiti kumfuata Mungu na hawakuwa na shaka kuhusu utambulisho na asili ya Mungu, Alianza kuwachukulia kwa urasmi wale waliomfuata kama familia Yake Mwenyewe na Akashirikiana nao katika ushirika, ukweli wa ndani kuhusu kazi ya Mungu tangu uumbaji wa dunia mpaka sasa. Pia Alifichua ukweli kuhusu Biblia, na hata zaidi, Aliwaruhusu kuelewa umuhimu wa kweli wa Mungu kupata mwili. Watu wanaweza kuelewa vizuri zaidi asili ya Mungu na asili ya kazi Yake kutoka kwa maneno haya, na zaidi ya hayo, watatambua kwamba kile watu wamepata kwa njia ya wokovu wa Mungu kimepita kile kilichopatikana na manabii na mitume kotekote katika enzi. Kutoka kila mstari wa maneno ya Mungu, unaweza kupitia kila chembe ya hekima Yake pamoja na upendo na utunzaji Wake mwangalifu. Wakati Akielezea maneno haya, pia Aliwafichulia watu waziwazi fikira zao za awali, makosa, mambo ambayo hawakuwa wamefikiria hapo awali, na hata njia zao za baadaye moja moja. Labda hii ni hisi finyu ya upendo ambayo watu wanaweza kupitia! Hata hivyo, Mungu tayari amempa mwanadamu kile anachohitaji na kile ambacho ameomba—Hajaficha na Hajatoa madai hasa.
Sura maalum chache katika sehemu hii ni maneno Yake kuhusu Biblia. Hili ni kwa sababu Biblia ilifuata miaka elfu kadhaa ya historia ya wanadamu na watu wote wanaichukulia kama Mungu kiasi kwamba watu walio katika siku za mwisho wanambadilisha Mungu na Biblia. Hiki ni kitu ambacho Mungu anachukia sana. Kwa hiyo katika wakati wake wa ziada, Alilazimika kubainisha hadithi ya ndani na asili ya Biblia. La sivyo, Biblia bado ingeweza kuchukua nafasi ya Mungu katika mioyo ya watu na wangeweza kuhukumu na kupima matendo ya Mungu kutegemezwa kwa maneno yaliyo katika Biblia. Maelezo ya Mungu ya asili, uundaji, na hitilafu za Biblia bila shaka sio kukataa kuwepo kwake, wala sio kuishutumu Biblia. Badala yake, ni kutoa ufafanuzi wa busara na wa kufaa, kurejesha sura ya asili ya Biblia, na kurekebisha kuelewa visivyo kwa watu kuhusu Biblia ili watu wote wawe na mtazamo sahihi kuihusu, wasiiabudu tena, na wasipotee tena—wao huchukulia kimakosa imani yao kwa Biblia isiyoweza kutambua kama kumwamini na kumwabudu Mungu, na hata hawathubutu kukabiliana na usuli wake wa kweli na upungufu wake. Baada ya kila mtu kuwa na ufahamu halisi wa Biblia ataweza kuiweka kando bila kusita na kuyakubali maneno mapya ya Mungu kwa ujasiri. Hili ni lengo la Mungu katika sura hizi kadhaa. Ukweli ambao Mungu anataka kuwaambia watu hapa ni kwamba hakuna nadharia au ukweli unaoweza kuchukua nafasi ya kazi ya Mungu ya sasa au maneno, na hakuna kitu ambacho kinaweza kuchukua nafasi ya Mungu. Ikiwa watu hawawezi kuondoa wavu wa Biblia, hawataweza kuja mbele ya Mungu kamwe. Ikiwa wanataka kuja mbele ya Mungu, lazima kwanza watakase mioyo yao kutokana na chochote ambacho kinaweza kuchukua nafasi Yake—hivi Mungu ataridhika. Ingawa Mungu anaelezea tu Biblia hapa, usisahau kwamba kuna mambo mengine mengi yenye makosa ambayo watu huabudu kwa hakika mbali na Biblia, na vitu pekee ambavyo hawaabudu ni vile ambavyo hutoka kwa Mungu kweli. Mungu hutumia tu Biblia kama mfano kumkumbusha kila mtu asishike njia mbaya na asivuke mipaka tena na kuingia katika kuchanganyikiwa wakati anamwamini Mungu na kukubali maneno Yake.
Maneno ambayo Mungu hutoa yanaanzia juujuu na kuwa ya kina. Kwa hivyo, Anachosema kinaendelea kuzidi kutoka kwa tabia na matendo ya nje ya watu hadi kwa tabia zao potovu, na kutoka hapo kinaenda zaidi kumulika mashubaka ya ndani zaidi ya nafsi za watu—asili yao. Katika wakati ambapo "Maneno ya Mwana wa Adamu Mwenye Mwili Alipokuwa Akitembea Makanisani (III)" ilionyeshwa, matamko ya Mungu yanasisitiza asili na utambulisho wa mwanadamu, na maana ya mwanadamu halisi—huu ukweli wa kina zaidi na maswali muhimu kuhusu kuingia kwa watu katika maisha. Bila shaka, kukumbuka ukweli ambao Mungu anampa mwanadamu katika "Maneno ya Mwana wa Adamu Mwenye Mwili Alipokuwa Akitembea Makanisani (I)," kwa ulinganishi, "Maneno ya Mwana wa Adamu Mwenye Mwili Alipokuwa Akitembea Makanisani (III)" ni ya maana sana hasa. Sehemu hii inashughulikia njia ya baadaye ya watu na jinsi wanaweza kukamilishwa; inashughulikia hatima ya baadaye ya wanadamu pamoja na maneno kuhusu Mungu na mwanadamu kuingia katika pumziko pamoja. (Inaweza kusemwa kuwa hadi sasa, haya ndiyo maneno ambayo Mungu amemwonyesha mwanadamu kuhusu asili yake, misheni yake, na hatima yake ambayo ni rahisi sana kuelewa.) Mungu hutumaini kwamba wale ambao wanayasoma maneno haya ni wale waliotoka kwa fikira na mawazo ya binadamu, na ambao wanaweza kuwa na ufahamu halisi wa kila neno Lake ndani ya mioyo yao. Anatarajia hata zaidi kwamba wote wanaosoma maneno haya wanaweza kuyachukulia maneno Yake kama ukweli, njia, na uzima, na kwamba wasimtendee Mungu bila uzito au kumdanganya. Watu wakisoma maneno haya kwa mtazamo wa kumchunguza au kumsoma Mungu, basi umuhimu wake wote umewapotea. Ni wale tu wanaofuata ukweli, waliodhamiria mioyo yao kumfuata Mungu, na hawana shaka hata kidogo Kwake ndio wanastahili kuyakubali maneno haya.
"Maneno ya Mwana wa Adamu Mwenye Mwili Alipokuwa Akitembea Makanisani (IV)" ni aina nyingine ya maneno matakatifu yanayofuata baada ya "Matamshi ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima." Fungu hili linajumuisha ushawishi, mafundisho, na ufunuo wa Mungu kwa watu wote katika madhehebu ya Kikristo, kama vile: "Utakapouona Mwili wa Kiroho wa Yesu ndio Utakuwa Wakati Ambao Mungu Ametengeneza Upya Mbingu na Dunia," "Wale Ambao Hawalingani na Kristo Hakika Ni Wapinzani wa Mungu." Pia ni pamoja na matakwa maalum zaidi aliyonayo Mungu kwa wanadamu, kama vile: "Unapaswa Kufanya Matendo Mema ya Kutosha Ili Uandae Mwisho Wako wa Safari," "Maonyo Matatu," "Dhambi Zitampeleka Mwanadamu Jahanamu." Hali nyingi zinazungumziwa kama vile ufunuo na hukumu kwa aina zote za watu na maneno kuhusu jinsi ya kumjua Mungu. Inaweza kusemwa kwamba sehemu hii ni kiini cha hukumu ya Mungu kwa wanadamu. Kile kisichosahaulika ni kwamba wakati Mungu alipokuwa karibu kumaliza kazi Yake, Alifunua kilicho ndani ya kina cha watu—usaliti. Lengo Lake ni kuwafanya watu wajue ukweli huu mwishowe na kuuwasha moto ndani ya sehemu za kina za mioyo yao: Haijalishi umekuwa mfuasi wake kwa muda gani—asili yako bado ni kumsaliti Mungu. Yaani, ni asili ya watu kumsaliti Mungu kwa sababu watu hawana ukomavu kamili katika maisha yao, wana mabadiliko yanayohusiana tu katika tabia. Ingawa sura hizi mbili, "Usaliti (1)" na "Usaliti (2)," zinatoa pigo kwa watu, hizo kweli ni maonyo ya Mungu yenye uaminifu na karimu zaidi kwa watu. Angalau kabisa, wakati watu wanaridhika mno na wanajipenda, baada ya kusoma sura hizi mbili, uovu wao wenyewe utazuiwa na watatulia. kupitia kwa sura hizi mbili Mungu anawakumbusha watu wote kwamba haijalishi vile maisha yako yalivyo mapevu, jinsi uzoefu wako ulivyo mkubwa, jinsi imani yako ilivyo, na haijalishi ulikozaliwa na unakokwenda, asili yako ya kumsaliti Mungu inaweza kutokea wakati wowote na mahali popote. Kile Mungu anataka kumwambia kila mtu ni hiki: Kumsaliti Mungu ni asili ya binadamu. Bila shaka kusudi la Mungu katika kuonyesha sura hizi mbili sio kupata visingizio vya kuwaondosha au kuwashutumu wanadamu, lakini ni kuwafanya wawe na ufahamu zaidi kuhusu asili yao wenyewe na hivyo waishi kwa makini zaidi mbele ya Mungu wakati wote ili kupata uongozi Wake, wakiepuka kupoteza uwepo Wake na kuingia kwenye njia isiyoweza kurudi nyuma tena. Sura hizi mbili ni kengele ya onyo kwa wale wote wanaomfuata Mungu. Tunatarajia watu wanaweza kuelewa nia zenye ari za Mungu. Hata hivyo, maneno haya yote ni ukweli usiopingika, kwa hiyo mbona mwanadamu hubishana kuhusu yalionyeshwa na Mungu wakati gani na vipi? Kama Mungu angenyamaza na mambo haya yote na Akakosa kuyasema lakini Akangoja mpaka watu wadhani ni wakati unaofaa, wakati haungekuwa umechelewa? Wakati unaofaa zaidi ungekuwa gani?

Katika sehemu hizi nne Mungu anatumia mbinu na mitazamo mingi. Kwa mfano, wakati mwingine Anatumia dhihaka, na wakati mwingine Anatumia njia ya kutoa na kufundisha moja kwa moja; wakati mwingine Anatumia mifano, na wakati mwingine Anatumia makaripio makali. Kwa jumla, kuna aina zote za mbinu tofauti, na lengo ni kuhudumia hali mbalimbali na tamaa za watu. Mtazamo ambao Ananena kutokana nao unabadilika na mbinu tofauti au maudhui ya kile Anachosema. Kwa mfano, wakati mwingine Anasema, "Mimi," yaani, Anazungumza na watu kwa mtazamo wa Mungu Mwenyewe. Wakati mwingine Anazungumza kutoka kwa nafsi ya tatu, akisema "Mungu" ni hii au hiyo, na kuna nyakati nyingine ambazo Anazungumza kwa mtazamo wa mwanadamu. Haijalishi Anazungumza kwa mtazamo gani, hauwezi kubadilisha asili Yake. Hiyo ni kwa sababu haijalishi jinsi Anavyozungumza, kile Anachoonyesha yote ni asili ya Mungu Mwenyewe—yote ni ukweli, na ni kile ambacho wanadamu wanahitaji.

Soma Zaidi: Kuhusu Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki Hutoka wapi

0 评论:

Chapisha Maoni