Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Muziki wa Akapela "Tokeo Lililofikiwa kwa Kumjua Mungu" (Video Rasmi ya Muziki)

Hayuko katika upeo wa mbali, wala hajajificha juu mawinguni. Yuko kando yako, akiwa na mamlaka juu ya kila kitu chako, Yeye ni kila kitu ulicho nacho, na Yeye ni kitu pekee ulicho nacho.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Jumatatu, 24 Juni 2019

Neno la Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VII Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (I)” Sehemu ya Tatu


Neno la Mungu |  “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VII Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (I)” Sehemu ya Tatu

Mwenyezi Mungu

anasema, “Mungu aliumba vitu vyote kuhusiana, kupatana na kutegemeana. Alitumia njia hii na kanuni hizi kudumisha kuendelea kuishi na uwepo wa vitu vyote na kwa njia hii binadamu ameishi kwa utulivu na kwa amani na amekua na kuzaliana kutoka kizazi kimoja hadi kingine katika mazingira haya hai hadi siku ya leo. Yaani, Mungu anaweka uwiano katika mazingira ya asili.

Jumapili, 23 Juni 2019

Maneno ya Mungu | Sura ya 43

Maneno ya Mungu | Sura ya 43

Je, Sijawakumbusha? Msiwe wenye hofu; ninyi hamjanisikiliza tu, watu wasio na fikira ninyi! Je, mtaweza kuuelewa moyo Wangu lini? Kila siku kuna nuru mpya, kila siku kuna mwanga mpya. Ni mara ngapi mmeuelewa kwa ajili yenu wenyewe? Je, Sijawaambia Mwenyewe? Bado ninyi ni wa kukaa tu kama wadudu ambao watasonga tu wanaposukumwa, lakini hamwezi kuchukua hatua ya kushirikiana na Mimi, kuufikiria mzigo Wangu. 

Jumamosi, 22 Juni 2019

Sauti ya Mungu | Sura ya 42


Sauti ya Mungu | Sura ya 42

Jinsi gani matendo ya Mwenyezi Mungu yalivyo makuu! Jinsi ilivyo ya ajabu! Jinsi ilivyo ya kushangaza! Tarumbeta saba zinatoa sauti, ngurumo saba zinatolewa, bakuli saba zinamwangwa—hii itadhihirika wazi mara moja na hakuwezi kuwa na shaka. Upendo wa Mungu huja juu yetu kila siku na ni Mwenyezi Mungu pekee Anayeweza kutuokoa; kama tunakabiliwa na bahati mbaya au kupokea baraka ni kwa sababu Yake kabisa, na sisi wanadamu hatuna njia ya kuamua hili. 

Ijumaa, 21 Juni 2019

Maneno ya Mungu | Sura ya 41


Maneno ya Mungu | Sura ya 41

Kuhusu shida zinazoibuka kanisani, usiwe na mashaka mengi. Kanisa linapojengwa haiwezekani kuepuka makosa, lakini usiwe na wasiwasi unapokabiliwa na shida hizo; kuwa mtulivu na makini. Sijawaambia hivyo? Omba Kwangu mara nyingi, na Nitakuonyesha kwa wazi nia Zangu. Kanisa ni moyo Wangu na ni lengo Langu la msingi, Nawezaje kutolipenda? Usiogope, mambo kama haya yanapotendeka kanisani, yote yanaruhusiwa na Mimi.

Alhamisi, 20 Juni 2019

Maneno ya Mungu | Sura ya 40


Maneno ya Mungu | Sura ya 40

Kwa nini ninyi ni wa mwendo wa polepole? Kwa nini hamsikii? Makumbusho kadhaa hayajawazindua; hili linanihuzunisha. Kwa kweli Sipendi kuwaona wanangu namna hii. Moyo Wangu unawezaje kustahimili hili? Ah! Lazima Niwafundishe kwa mkono Wangu mwenyewe. Mwendo Wangu unaendelea kuwa wa kasi. Wanangu! Inukeni haraka na mshirikiane na Mimi. Nani wanajitumia kwa dhati kwa ajili Yangu sasa? Ni nani anayeweza kujitolea kikamilifu bila malalamiko hata kidogo? Daima ninyi ni wenye kutosikia na wapumbavu! 

Jumatano, 19 Juni 2019

Sauti ya Mungu | Sura ya 39

Sauti ya Mungu | Sura ya 39

    Fungua macho yako na uangalie na unaweza kuona nguvu Zangu kuu kila mahali! Unaweza kuwa na uhakika na Mimi kila mahali. Ulimwengu na anga unaeneza nguvu Zangu kuu. Maneno ambayo Nimenena yametimia katika ongezeko la joto la hali ya hewa, mabadiliko ya hali ya hewa, vioja vya watu, ulemavu wa elimumwendo ya kijamii, na udanganyifu wa mioyo ya watu. Jua linakuwa jeupe na mwezi unakuwa mwekundu; Yote yako katika machafuko. Je, bado huoni haya? 

Jumanne, 18 Juni 2019

Maneno ya Mungu | Sura ya 38


Maneno ya Mungu | Sura ya 38

Si kwamba imani yako ni nzuri au safi, lakini badala yake, kazi Yangu ni ya ajabu! Kila kitu ni kwa sababu ya rehema Zangu! Hupaswi kuwa na tabia potovu ya ubinafsi au kiburi hata kidogo, vinginevyo kazi Yangu kwako haitaendelea. Lazima uelewe wazi kwamba iwapo watu wanaanguka au kusimama imara si kwa sababu yao, ni kwa sababu Yangu. Leo, kama huelewi vizuri hatua hii, hutaweza kuingia katika ufalme!

Jumatatu, 17 Juni 2019

Neno la Mungu | “Kujua Hatua Tatu za Kazi ya Mungu Ndiyo Njia ya Kumjua Mungu” Sehemu ya Pili


Neno la Mungu | “Kujua Hatua Tatu za Kazi ya Mungu Ndiyo Njia ya Kumjua Mungu” Sehemu ya Pili

Mwenyezi Mungu anasema, “Hatua tatu za kazi ndizo kiini cha usimamizi mzima wa Mungu, na ndani yazo zimeelezwa tabia ya Mungu na kile Alicho. Wale wasiojua kuhusu hatua tatu za kazi ya Mungu hawana uwezo wa kutambua jinsi Mungu anavyoonyesha tabia Yake, wala hawajui hekima ya kazi ya Mungu, na wanasalia kutojua njia nyingi Anazomwokoa mwanadamu, na mapenzi Yake kwa wanadamu wote.

Jumapili, 16 Juni 2019

Maneno ya Mungu | Sura ya 36


Maneno ya MunguSura ya 36

Mwenyezi Mungu wa kweli, Mfalme katika kiti cha enzi, hutawala ulimwengu mzima, Anakabiliana na mataifa yote na watu wote, kila kitu chini ya mbingu hung’aa kwa utukufu wa Mungu. Viumbe vyote hai katika miisho ya ulimwengu vitaona. Milima, mito, maziwa, ardhi, bahari na viumbe vyote viishivyo, katika nuru ya uso wa Mungu wa kweli wamefungua mapazia yao, kuhuishwa, kama kuamka kutoka kwa ndoto, kuchipuka kwa kuvunja uchafu!

Jumamosi, 15 Juni 2019

Sauti ya Mungu | Sura ya 35


Sauti ya Mungu | Sura ya 35

Ngurumo saba zinatoka kwenye kiti cha enzi, zinautikisa ulimwengu, zinageuza mbingu na ardhi, na zinavuma angani! Sauti hiyo inapenya sana kiasi kwamba watu hawawezi kuepuka wala kujificha. Nuru ya ghafla ya umeme na sauti ya radi zinatumwa mbele, zikiiangusha chini mbingu na ardhi papo hapo, na watu wamekaribia kufa. Kisha, dhoruba ya mvua kali inafagia ulimwengu wote kwa kasi ya umeme, ikianguka kutoka angani! 

Ijumaa, 14 Juni 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 34


Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 34

Mwenyezi Mungu ni mwenye nguvu zote , mwenye kutimiliza yote na Mungu wa kweli kabisa! Habebi tu nyota saba, ana Roho saba, ana macho saba, anafungua mihuri saba na kufungua hati ya kukunja yenye maandishi, lakini zaidi ya hayo Yeye anaendesha mapigo saba na vikasa saba na kufungua radi saba; zamani za kale Yeye alipiga vinumbi saba! Vitu vyote vilivyoumbwa na kufanywa kuwa kamili na Yeye vinapaswa kumsifu, kumpa adhama na kutukuza kiti Chake cha enzi.

Alhamisi, 13 Juni 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 33


Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 33

Ufalme Wangu unawahitaji wale ambao ni waaminifu, wasio wanafiki, na wasio wadanganyifu. Je, si watu wenye moyo safi na waaminifu duniani hawapendwi na watu? Mimi ni kinyume kabisa cha jinsi ilivyo. Inakubalika kwa watu waaminifu kuja Kwangu; Nafurahia mtu wa aina hii, pia Ninamhitaji mtu wa aina hii. Hii ni haki Yangu hasa. Watu wengine ni wajinga; hawawezi kuhisi kazi ya Roho Mtakatifu na hawawezi kuyaelewa mapenzi Yangu.