Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Muziki wa Akapela "Tokeo Lililofikiwa kwa Kumjua Mungu" (Video Rasmi ya Muziki)

Hayuko katika upeo wa mbali, wala hajajificha juu mawinguni. Yuko kando yako, akiwa na mamlaka juu ya kila kitu chako, Yeye ni kila kitu ulicho nacho, na Yeye ni kitu pekee ulicho nacho.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo ushahidi. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo ushahidi. Onyesha machapisho yote

Jumapili, 1 Julai 2018

Swahili Christian Movie | Nyendo za Mateso ya Kidini | "Kukaribia Hatari na Kurudi"


Swahili Christian Movie | Nyendo za Mateso ya Kidini | "Kukaribia Hatari na Kurudi"

    Tangu kilipokuja mamlakani katika China Bara mnamo mwaka wa 1949, Chama Cha Kikomunisti cha China kimekuwa hakikomi katika mateso yake kwa imani ya kidini. Kwa wayowayo kimewashika na kuwaua Wakristo, kuwafukuza na kuwadhulumu wamishonari wanaofanya kazi nchini China, wakachukua ngawira na kuchoma nakala nyingi za Biblia, wakafunga kabisa na kubomoa majengo ya kanisa, na bila mafanikio wakajaribu kukomesha makanisa yote ya nyumbani.

Mateso-ya-Kidini, ukatili, imani-ya-kidini,

     Filamu hii ni masimulizi ya uzoefu wa kweli wa mateso katika mikono ya Chama Cha Kikomunisti cha China yaliyopitiwa na Chen Wenzhong, Mkristo wa Kichina. Chen Wenzhong alikuwa na mafanikio katika kazi yake na alikuwa na familia nzuri na yenye furaha, lakini kwa sababu alimwamini Mungu na kutekeleza wajibu wake, akawa mtu aliyetakiwa na CCP. Alilazimika kuondoka nyumbani na alikuwa mkimbizi kwa zaidi ya miaka kumi. Ili kupata habari za mahali alikokuwa, polisi wa CCP daima waliifuatia, kuitishia, na kuiogofya familia yake, na hata hawangemhurumia mwanawe mdogo wa kiume, Xiaoyu. Hatimaye, walimlazimisha Xiaoyu kutenda kitendo ambacho hangekiepuka …

Yaliyopendekezwa: Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki Mwenyezi Mungu

Jumamosi, 3 Februari 2018

Swahili Christian Testimony Video "Katikati ya Majira ya Baridi"


Swahili Christian Testimony Video "Katikati ya Majira ya Baridi"

Jina lake ni Xiao Li. Ameamini katika Mungu kwa zaidi ya muongo mmoja. Katika majira ya baridi ya mwaka wa 2012, alikamatwa na polisi wa Kikomunisti wa China katika mkutano. Wakati wa mahojiano, polisi walimshawishi, kumtisha, kumpiga na kumtesa tena na tena katika majaribio yao ya kumshawishi ili amsaliti Mungu kwa kufichua walipokuwa viongozi na fedha za kanisa. Hasa katika usiku mmoja baridi sana wakati ambapo halijoto ilikuwa nyuzi ishirini chini ya sifuri, alivuliwa nguo kwa nguvu akawa uchi, akaroweshwa maji ya barafu, akashtuliwa kwa umeme kwenye viungo vyake vya uzazi, na kunyweshwa maji ya haradali kwa nguvu na polisi... Alikuwa amepitia mateso ya kikatili na fedheha isiyowazika. Wakati wa mahojiano, alihisi kuumizwa na kudhalilishwa. Alimwomba Mungu bila tumaini muda baada ya muda. Neno la Mungu lilimpa nuru na mwongozo wa wakati wa kufaa. Kwa imani na nguvu aliyopata kutoka kwa neno la Mungu, alishinda mateso makali na maangamizi ya kishetani na akatoa ushuhuda mzuri sana wa kuenea pote. Kama maua ya plamu ya majira ya baridi, yeye alionyeshwa nguvu thabiti kwa kusitawi kwa fahari katikati ya dhiki kali, akitoa kumbukumbu ya kupendeza sana...
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, maombi

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.

Ijumaa, 26 Januari 2018

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Wewe U Mwaminifu kwa Nani?

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Wewe U Mwaminifu kwa Nani?

Mwenyezi Mungu alisema, Kila siku unayoiishi sasa ni ya maana sana na muhimu sana kwa hatima yako na majaliwa yako, kwa hivyo unapaswa kufurahia kila ulicho nacho na kila dakika inayopita. Unapaswa kutumia muda wako vizuri ili uweze kujinufaisha, ili usije kuishi maisha haya bure. Pengine unajihisi kukanganyikiwa unaojiuliza ni kwa nini Ninazungumza maneno haya. Kwa kweli, Sijapendezwa na matendo ya yeyote kati yenu.