Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Muziki wa Akapela "Tokeo Lililofikiwa kwa Kumjua Mungu" (Video Rasmi ya Muziki)

Hayuko katika upeo wa mbali, wala hajajificha juu mawinguni. Yuko kando yako, akiwa na mamlaka juu ya kila kitu chako, Yeye ni kila kitu ulicho nacho, na Yeye ni kitu pekee ulicho nacho.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo imani-ya-kidini. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo imani-ya-kidini. Onyesha machapisho yote

Alhamisi, 24 Januari 2019

Ushuhuda wa Washindi | 2. Nguvu ya Maisha Ambayo Haiwezi Kuzimwa Kamwe

Ushuhuda wa Washindi | 2. Nguvu ya Maisha Ambayo Haiwezi Kuzimwa Kamwe

Dong Mei, Mkoa wa Henan


Mimi ni mtu wa kawaida. Niliishi maisha ya kawaida. Kama wengi wanaotamani sana mwanga, nilijaribu njia nyingi kutafuta maana ya kweli ya uwepo wa wanadamu, nikijaribu kuyapa maisha yangu umuhimu zaidi. Mwishowe, juhudi zangu zote zilikuwa bure. Lakini baada ya kuwa na bahati ya kutosha kukubali kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho, mabadiliko ya muujiza yalitokea katika maisha yangu.

Jumatatu, 24 Desemba 2018

"Utamu katika Shida" (II): Kwa Nini Chama cha Kikomunisti cha China Kwa Hasira Kinakandamiza na Kutesa Imani ya Kidini?

Umeme wa Mashariki | "Utamu katika Shida" (II): Kwa Nini Chama cha Kikomunisti cha China Kwa Hasira Kinakandamiza na Kutesa Imani ya Kidini?


Chama cha Kikomunisti cha China wakati huu wote kimewakandamiza kwa hasira, kuwashambulia na kupiga marufuku imani za kidini. Wanawachukulia Wakristo kama wahalifu wakuu wa taifa. Hawasiti kutumia njia za mapinduzi kukandamiza, kukamata, kutesa na hata kuwachinja. 

Jumapili, 16 Desemba 2018

"Utamu katika Shida" (VI): Kufunua Ukweli wa Sera ya CCP juu ya Dini Iliyofunikwa na Katiba Yake

Utamu katika Shida” - Ukweli wa Sera ya CCP juu ya Dini Iliyofunikwa na Katiba Yake 

Katiba ya serikali ya Kikomunisti ya Kichina hutamka dhahiri juu ya uhuru wa dini na ibada, lakini kwa siri kuna ukandamizaji wa jeuri na mashambulizi kwa dini na ibada. Wafuasi wa Kristo wanasingiziwa kuwa wahalifu wakubwa wa kitaifa na mbinu za mapinduzi zinachukuliwa ili kuwakandamiza, kuwazuilia, kuwatesa na hata kuwaua kwa ukatili.

Alhamisi, 30 Agosti 2018

Swahili Gospel Movie Clip "Kutoka kwa Enzi Hububujika Maji ya Uzima" (2) - Mbona Kuna Ukiwa Ulioenea Pote katika Ulimwengu wa Dini?


Swahili Gospel Movie Clip "Kutoka kwa Enzi Hububujika Maji ya Uzima" (2) - Mbona Kuna Ukiwa Ulioenea Pote katika Ulimwengu wa Dini?

Dunia nzima ya dini kwa sasa inapitia njaa kubwa, hawapo tena pamoja na kazi ya Roho Mtakatifu au uwepo wa Bwana, wanafanya mambo maovu zaidi na zaidi na imani na huruma ya waumini inadhoofika na kuwa baridi. Aidha, maafa yanazidi kuwa mabaya zaidi na zaidi kote duniani, unabii kwamba Bwana angerudi katika siku za mwisho tayari umetimia. Hivyo, tunawezaje kutatua chanzo cha ukiwa wa makanisa kwa njia ambayo inawaruhusu wale ambao kweli wanaamini katika Mungu, ambao wanatamani kuonekana kwa Mungu kwa mara nyingine tena waje mbele za Mungu na kutembea kwenye njia ya wokovu? Hii video fupi itachunguza pamoja nawe jinsi ya kutatua tatizo hili la ukiwa wa makanisa.

    Soma Zaidi: Kuhusu Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Jumapili, 26 Agosti 2018

Filamu za Kikristo "Chama Hakijamaliza Kuzungumza" | Concrete Proof of the CCP Persecuting Christians


Filamu za Kikristo "Chama Hakijamaliza Kuzungumza" | Concrete Proof of the CCP Persecuting Christians

Li Ming’ai ni Mkristo nchini China Bara. Yeye ni mwanamke mwadilifu ambaye anawaheshimu wakweze, humsaidia mumewe na kumuelimisha mtoto wake, na ana familia ya furaha na patanifu. Katika China, ambako ukanaji Mungu unatawala, hata hivyo, serikali ya Kikomunisti ya China daima huwakamata na kuwatesa ovyo ovyo watu wanaomwamini Mungu. Katika mwaka wa 2006, Li Ming'ai alikamatwa na kutozwa faini kwa sababu ya imani yake kwa Mungu. Baada ya Li Ming'ai kurudi nyumbani, polisi wa Kikomunisti wa China daima walimtisha na kumwogofya yeye na familia yake, na walijaribu kumzuia Li Ming'ai kuendeleza imani yake kwa Mungu. Siku moja, Li Ming'ai alipokuwa mbali na nyumbani akifanya mkutano, aliripotiwa na mtoa habari. Polisi walikwenda nyumbani kwa Li Ming'ai wakijaribu kumkamata. Alilazimika kuondoka nyumbani, na tangu wakati huo kwendelea, maisha ya Li Ming'ai ya kujificha kutoka mahali pamoja hadi pengine na kukimbia kutoka nyumbani yalianza. Polisi wa Kikomunisti wa China bado hawakuachana naye, daima wakiichunga nyumbani yake, na kusubiri fursa ya kumkamata. Jioni moja, Li Min’gai ananyemelea nyumbani kwa familia yake, lakini karibu mara moja polisi wanaharakisha kumkamata. Kwa bahati nzuri mtu fulani anamwonya, na Li Ming'ai anaepuka maafa.

Miaka mitatu baadaye, wakati Li Ming'ai anaendeleza imani yake na kufanya kazi yake mbali na nyumbani, anafuatwa na kukamatwa na polisi wa Kikomunisti wa China. Polisi wa Kikomunisti wa China wanatekeleza mateso na maudhi ya kikatili kwa Li Ming'ai , na kutumia upendo wa familia kujaribu kumshawishi. Wanatumia vitisho kama vile kumnyima mtoto wake haki ya kuhudhuria shule, na kuzuia upatikanaji wa kazi baadaye katika serikali ili mtoto aweze kujaribu kumlazimisha kuiacha imani yake kwa Mungu, kuwasaliti viongozi katika kanisa, na kutangaza fedha za kanisa. Wakati huu, Li Mingai anamwomba Mungu na kuweka imani yake kwa Mungu. Katika neno la Mungu anapata nuru na mwongozo. Anavumilia mateso na maudhi na polisi wa Kikomunisti wa China, anazitambua mbinu za Shetani, na kuamua kutomsaliti Mungu. Anakuwa shahidi kwa udhabiti kwa Mungu. Masaili ya Polisi wa Kikomunisti wa China hayazai matunda, na wao wanakasirika kwa aibu. Wanamwongoza Li Mingai akiwa amevaa nguo za mfungwa kwa nyumba yake ya kijijini, wakimtembeza ili wote wamuone. Wanafanya hivi ili kumdhalilisha, na kisha kujaribu kuwafanya jamaa zake wamshawishi kumsaliti Mungu, na kulisaliti kanisa. Li Ming’ai anaghadhibishwa sana na jinsi Wakomunisti wa China wanavyoona kuwa matatizo ya familia yake ni kwa sababu ya imani yake kwa Mungu. Akiwa amejaa hasira ya kudhulumiwa, Li Ming'ai kwa ghadhabu anafichua ukweli wa uovu wa jinsi serikali ya Kikomunisti ya China huwakamata na kuwatesa Wakristo. Anasema kuwa mwangamizi halisi wa familia za Wakristo ni serikali ya Kikomunisti ya China, ambayo ndiyo mhalifu mkuu wa jinai ambaye huwaletea watu kila aina za majanga. Kwa hiyo anawapa ushinde kikamilifu na kwa aibu Wakomunisti wa China.

    Tufuate : Kanisa la Mwenyezi Mungu, Neno la Mwenyezi mungu

Jumapili, 1 Julai 2018

Swahili Christian Movie | Nyendo za Mateso ya Kidini | "Kukaribia Hatari na Kurudi"


Swahili Christian Movie | Nyendo za Mateso ya Kidini | "Kukaribia Hatari na Kurudi"

    Tangu kilipokuja mamlakani katika China Bara mnamo mwaka wa 1949, Chama Cha Kikomunisti cha China kimekuwa hakikomi katika mateso yake kwa imani ya kidini. Kwa wayowayo kimewashika na kuwaua Wakristo, kuwafukuza na kuwadhulumu wamishonari wanaofanya kazi nchini China, wakachukua ngawira na kuchoma nakala nyingi za Biblia, wakafunga kabisa na kubomoa majengo ya kanisa, na bila mafanikio wakajaribu kukomesha makanisa yote ya nyumbani.

Mateso-ya-Kidini, ukatili, imani-ya-kidini,

     Filamu hii ni masimulizi ya uzoefu wa kweli wa mateso katika mikono ya Chama Cha Kikomunisti cha China yaliyopitiwa na Chen Wenzhong, Mkristo wa Kichina. Chen Wenzhong alikuwa na mafanikio katika kazi yake na alikuwa na familia nzuri na yenye furaha, lakini kwa sababu alimwamini Mungu na kutekeleza wajibu wake, akawa mtu aliyetakiwa na CCP. Alilazimika kuondoka nyumbani na alikuwa mkimbizi kwa zaidi ya miaka kumi. Ili kupata habari za mahali alikokuwa, polisi wa CCP daima waliifuatia, kuitishia, na kuiogofya familia yake, na hata hawangemhurumia mwanawe mdogo wa kiume, Xiaoyu. Hatimaye, walimlazimisha Xiaoyu kutenda kitendo ambacho hangekiepuka …

Yaliyopendekezwa: Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki Mwenyezi Mungu

Jumanne, 6 Machi 2018

Swahili Christian Testimony Video "Utamu katika Shida" | Mungu Ndiye Nguvu Wangu

Swahili Christian Testimony Video "Utamu katika Shida" | Mungu Ndiye Nguvu Wangu

Han Lu ni kiongozi wa Kanisa la Mwenyezi Mungu katika China bara. Ameamini katika Mungu kwa zaidi ya muongo mmoja na amepitia kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho. Anaelewa baadhi ya ukweli na anajua kwamba ni kupitia tu Kristo wa siku za mwisho, Mwenyezi Mungu, ndiyo mwanadamu ataweza kuwekwa huru kutoka dhambini na kuishi maisha yenye maana. Ametupa mbali kila kitu kumfuata Mwenyezi Mungu, na ametembea huku na huku na kushuhudia kuonekana kwa Mungu na kazi katika siku za mwisho. Hata hivyo, nchini China ambako chama cha kisiasa kikanamungu cha CCP kiko mamlakani, hakuna uhuru wa imani ya dini kwa vyovyote. Serikali ya CCP imetoa hati za siri ikipiga marufuku kabisa makanisa yote ya nyumbani, na wamewakamata kwa hasira na kuwatesa Wakristo. Han Lu na wengine walichunguzwa na kufuatwa na maafisa wa polisi wa CCP, ambayo ilisababisha kukamatwa kwao. Maafisa hao wa polisi wa CCP wamemtesa kikatili Han Lu kujaribu kuliibia kanisa mali lake na kuwashika wakuu zaidi wa kanisa, na pia wametumia uvumi na uongo kumtia kasumba, wakatumia familia yake kujaribu kumshurutisha, na njia zingine za kudharauliwa kujaribu kumtishia katika jaribio la kumshurutisha amkane Mungu na kumsaliti Mungu. … Katika uchungu na udhaifu wake, Han Lu amemtegemea Mungu na kumwomba Mungu, na chini ya uongozi wa neno la Mungu, ameweza kubaini ujanja wote wa Shetani. Ameweza kustahimili mahojiano mengi chini ya mateso na ameweza kwa nguvu kukana uvumi na uongo kadhaa wa CCP. Ndani ya mazingira machungu ya utesaji wa CCP, ushuhuda wa kupendeza na wa nguvu umefanywa …
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki,maombi

Kujua zaidi:  Umeme wa Mashariki

Jumapili, 4 Machi 2018

Kwa Nini Chama cha Kikomunisti cha China Kwa Hasira Kinakandamiza na Kutesa Imani ya Kidini?

Kwa Nini Chama cha Kikomunisti cha China Kwa Hasira Kinakandamiza na Kutesa Imani ya Kidini?


Chama cha Kikomunisti cha China wakati huu wote kimewakandamiza kwa hasira, kuwashambulia na kupiga marufuku imani za kidini. Wanawachukulia Wakristo kama wahalifu wakuu wa taifa. Hawasiti kutumia njia za mapinduzi kukandamiza, kukamata, kutesa na hata kuwachinja. Sababu zao za kufanya mambo haya ni nini? Wale wanaoamini katika Mungu wanamheshimu Mungu kama mkuu. Wanamcha Mungu na wanalenga kutafuta ukweli na kutembea njia sahihi ya maisha. Kwa nini Chama cha Kikomunisti cha China kiwachukulie Wakristo kama maadui? Kwa nini hawalingani na watu wanaoamini katika Mungu? Video hii itachunguza sababu kwa nini Chama cha Kikomunisti cha China kinatesa imani ya kidini.
Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.

Jumamosi, 3 Machi 2018

"Ivunje Laana" (5) - Je, Wachungaji na Wazee wa Kanisa wa Ulimwengu wa Dini Wanateuliwa na Bwana Kweli?

"Ivunje Laana" (5) - Je, Wachungaji na Wazee wa Kanisa wa Ulimwengu wa Dini Wanateuliwa na Bwana Kweli?

Mungu mwenyewe hutoa ushuhuda kwa kila mtu Anayemteua na kumtumia. Angalau, wote hupokea uthibitisho wa kazi ya Roho Mtakatifu, huonyesha matunda ya kazi ya Roho Mtakatifu, na wanaweza kuwasaidia watu wa Mungu waliochaguliwa kupokea utoaji wa maisha na uchungaji wa kweli. Kwa sababu Mungu ni mwenye haki na mtakatifu, kila mtu Anayemteua na kumtumia lazima alingane na mapenzi ya Mungu. Wachungaji na wazee wa kanisa katika kutoka ulimwengu wa kidini hawana neno la Mungu kama ushuhuda, na pia hawana uthibitisho wa kazi ya Roho Mtakatifu. Hivyo, wachungaji na wazee wa kanisa ndani ya ulimwengu wa kidini wangewezaje kuchaguliwa na kutumiwa na Mungu binafsi?
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Kanisa

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.

Ijumaa, 2 Machi 2018

Swahili Gospel Movie | “Ivunje Laana” Movie Clip: Je, Imani katika Biblia ni Sawa na Imani katika Bwana?

Swahili Gospel Movie | "Ivunje Laana" Movie Clip: Je, Imani katika Biblia ni Sawa na Imani katika Bwana?


Wachungaji wengi sana na wazee wa kanisa wa ulimwengu wa kidini huamini kwamba Biblia inamwakilisha Bwana, na kwamba kuamini katika Bwana ni kuamini katika Biblia, na kuamini katika Biblia ni kuamini katika Bwana. Wao huamini kwamba mtu akiachana na Biblia basi hawezi kuitwa muumini, na kwamba mtu anaweza kuokolewa na anaweza kuingia katika ufalme wa mbinguni almradi ashikilie Biblia. Je, Bibilia inaweza kweli kumwakilisha Bwana? Je, uhusiano kati ya Biblia na Bwana ni upi hasa? Bwana Yesu alisema, "Tafuta katika maandiko; kwa kuwa ndani yake mnadhani kuwa mna uzima wa milele: na hayo ndiyo yananishuhudia. Nanyi hamtakuja Kwangu, kwamba mpate uhai" (Yohana 5:39-40). Mwenyezi Mungu alisema, "Hata hivyo, kipi ni kikubwa? Mungu au Biblia? Kwa nini ni lazima kazi ya Mungu iwe kulingana na Biblia? Je, inaweza kuwa kwamba Mungu hana haki ya kuwa juu ya Biblia? Je, Mungu hawezi kujitenga na Biblia na kufanya kazi nyingine? Kwa nini Yesu na wanafunzi Wake hawakutunza Sabato? … Unapaswa kujua ni kipi kilitangulia, Mungu au Biblia! Kuwa Bwana wa Sabato, je, Asingeweza pia kuwa Bwana wa Biblia?" (Neno Laonekana katika Mwili)
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Biblia

Alhamisi, 8 Februari 2018

Umeme wa Mashariki | Njia ya Huduma ya Kidini lazima Ipigwe Marufuku

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki

Umeme wa Mashariki | Njia ya Huduma ya Kidini lazima Ipigwe Marufuku

Mwenyezi Mungu alisema, Tangu mwanzo wa kazi Yake katika ulimwengu mzima, Mungu ameamulia kabla watu wengi kumhudumia Yeye, wakiwemo watu kutoka kila nyanja ya maisha. Kusudio Lake ni kutimiza mapenzi Yake Mwenyewe na kuhakikisha kwamba kazi Yake hapa ulimwenguni imetimia. Hili ndilo kusudio la Mungu katika kuwachagua watu wa kumhudumia Yeye. Kila mtu anayehudumia Mungu lazima aelewe mapenzi haya ya Mungu. 

Jumatatu, 29 Januari 2018

Kumwamini Mungu Lazima Kulenge Uhalisi, Si Tamaduni za Kidini

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki

Kumwamini Mungu Lazima Kulenge Uhalisi, Si Tamaduni za Kidini

 Je, ni desturi ngapi za kidini unazozizingatia? Ni mara ngapi wewe umeasi dhidi ya neno la Mungu na kwenda kwa njia yako mwenyewe? Ni mara ngapi wewe umetia katika vitendo neno la Mungu kwa sababu wewe kwa kweli unajali mizigo Aliyobeba na unatafuta kutimiza mapenzi Yake?