Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Muziki wa Akapela "Tokeo Lililofikiwa kwa Kumjua Mungu" (Video Rasmi ya Muziki)

Hayuko katika upeo wa mbali, wala hajajificha juu mawinguni. Yuko kando yako, akiwa na mamlaka juu ya kila kitu chako, Yeye ni kila kitu ulicho nacho, na Yeye ni kitu pekee ulicho nacho.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Mateso. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Mateso. Onyesha machapisho yote

Alhamisi, 24 Januari 2019

Ushuhuda wa Washindi | 2. Nguvu ya Maisha Ambayo Haiwezi Kuzimwa Kamwe

Ushuhuda wa Washindi | 2. Nguvu ya Maisha Ambayo Haiwezi Kuzimwa Kamwe

Dong Mei, Mkoa wa Henan


Mimi ni mtu wa kawaida. Niliishi maisha ya kawaida. Kama wengi wanaotamani sana mwanga, nilijaribu njia nyingi kutafuta maana ya kweli ya uwepo wa wanadamu, nikijaribu kuyapa maisha yangu umuhimu zaidi. Mwishowe, juhudi zangu zote zilikuwa bure. Lakini baada ya kuwa na bahati ya kutosha kukubali kazi ya Mwenyezi Mungu ya siku za mwisho, mabadiliko ya muujiza yalitokea katika maisha yangu.

Jumapili, 16 Desemba 2018

"Utamu katika Shida" (VI): Kufunua Ukweli wa Sera ya CCP juu ya Dini Iliyofunikwa na Katiba Yake

Utamu katika Shida” - Ukweli wa Sera ya CCP juu ya Dini Iliyofunikwa na Katiba Yake 

Katiba ya serikali ya Kikomunisti ya Kichina hutamka dhahiri juu ya uhuru wa dini na ibada, lakini kwa siri kuna ukandamizaji wa jeuri na mashambulizi kwa dini na ibada. Wafuasi wa Kristo wanasingiziwa kuwa wahalifu wakubwa wa kitaifa na mbinu za mapinduzi zinachukuliwa ili kuwakandamiza, kuwazuilia, kuwatesa na hata kuwaua kwa ukatili.

Jumatano, 28 Novemba 2018

95. Kuinuka Kupitia Ukandamizaji wa Giza

Umeme wa Mashariki | 95. Kuinuka Kupitia Ukandamizaji wa Giza

imani,maombi,Mateso-ya-Kidini,maneno-ya-Mungu

Mo Zhijian Mkoa wa Guangdong

Nilizaliwa katika eneo maskini, la mbali lenye milima ambako tumefukiza na kumwabudu Budha kwa vizazi vingi. Kuna hekalu za Budha sehemu hiyo kote ambako familia zote zingekwenda kuchoma uvumba; hakuna mtu yeyote aliyewahi kumwamini Mungu kamwe. Katika mwaka wa 1995, mimi na mke wangu tulikuwa katika sehemu nyingine ya nchi ambapo tulimwamini Bwana Yesu; baada ya sisi kurudi tulianza kushiriki injili na idadi ya watu ambao waliikubali ilikua polepole hadi watu zaidi ya 100.

Jumanne, 27 Novemba 2018

94. Majonzi Yalivutia Upendo Wangu kwa Mungu

94. Majonzi Yalivutia Upendo Wangu kwa Mungu

upendo-wa-Mungu,neno-la-Mungu,Mateso,ukatili,
Meng Yong Mkoa wa Shanxi


Mimi kwa asili ni mtu mwaminifu, ikiwa ndiyo maana nimekuwa nikidhulumiwa daima na watu wengine. Kwa sababu hiyo, nimeonja dharau ya ulimwengu wa mwanadamu na nilihisi maisha yangu yakiwa matupu na bila maana. Baada ya mimi kuanza kumwamini Mwenyezi Mungu, kupitia kusoma maneno ya Mungu na kuishi maisha ya kanisa, nilifurahia ari na shangwe katika moyo wangu ambazo sikuwahi kamwe kuzihisi kabla. Kuona ndugu wa kiume na wa kike wa Kanisa la Mwenyezi Mungu wakipendana wenyewe kwa wenyewe kama familia kulinifanya nitambue kwamba Mungu peke yake ndiye mwenye haki, na kwamba ni katika Kanisa la Mwenyezi Mungu tu kuliko na mwanga. 

Ijumaa, 16 Novemba 2018

Swahili Christian Video "Mazungumzo" (6): Jinsi Wakristo Wanavyojibu "Chambo cha Familia" cha CCP

 Swahili Christian Video "Mazungumzo" (6): Jinsi Wakristo Wanavyojibu "Chambo cha Familia" cha CCP


Wakati ambapo CCP hakipati mafanikio katika jitihada zake za kuwalazimisha Wakristo kumtelekeza Mungukupitia mateso yao ya ukatili na kutia kasumba, wao kisha huzitumia familia zao kama chambo kuwajaribu. Wakiwa wamekabiliwa na mbinu hizi duni,Wakristo husimamaje imara na haki, wakizikanusha? Na wao hutoa onyo gani?

Jumapili, 4 Machi 2018

Mbinu ya Chama cha Kikomunisti cha China ya Kuwashurutisha Wakristo kwa Kutishia Familia Zao

Mbinu ya Chama cha Kikomunisti cha China ya Kuwashurutisha Wakristo kwa Kutishia Familia Zao

Ili kuwashurutisha Wakristo kulighilibu kanisa, wamsaliti Mungu na kuharibu nafasi zao za kuokolewa na Mungu, Chama cha Kikomunisti cha China kwa ufidhuli kinawatishia wanafamilia wa Wakristo na kutumia hisia za familia za Wakristo kuwashurutisha kumsaliti Mungu. Je, njama za Chama cha Kikomunisti cha China zinaweza kuendelea? Katika mapambano haya kati ya mema na mabaya, Wakristo watawezaje kumtegemea Mungu ili kushinda majaribu ya Shetani na kusimama imara na kuwa na ushuhuda kwa Mungu?
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, ushuhuda
Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.