Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Muziki wa Akapela "Tokeo Lililofikiwa kwa Kumjua Mungu" (Video Rasmi ya Muziki)

Hayuko katika upeo wa mbali, wala hajajificha juu mawinguni. Yuko kando yako, akiwa na mamlaka juu ya kila kitu chako, Yeye ni kila kitu ulicho nacho, na Yeye ni kitu pekee ulicho nacho.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo imani-katika-Mungu. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo imani-katika-Mungu. Onyesha machapisho yote

Jumatatu, 8 Aprili 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Kazi na Kuingia (10)

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Kazi na Kuingia (10)


Kwa wanadamu kuendelea mbele kiasi hiki ni hali isiyo na kigezo. Kazi ya Mungu na kuingia kwa mwanadamu vinaendelea bega kwa bega, na hivyo kazi ya Mungu, pia, ni tukio kubwa lisilo na kifani. Kuingia kwa mwanadamu hadi sasa ni ajabu ambayo kamwe haijawahi kufikiriwa na mwanadamu. Kazi ya Mungu imefikia upeo wake—na, kufuatia, “kuingia” kwa mwanadamu[1] pia kumefikia kilele chake. Mungu amejishusha kwa kadiri Anavyoweza, na kamwe Hajawahi kuwalalamikia wanadamu au vitu vyote katika ulimwengu.

Jumapili, 7 Aprili 2019

Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee X Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (IV)”



Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee X Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (IV)”
Mwenyezi Mungu alisema, "Kwa kweli, Mungu hana mahitaji sana kwa wanadamu—au angalau, hana mahitaji kama watu wanavyodhani. Bila matamshi ya Mungu, au udhihirishaji wowote wa tabia Yake, matendo, au maneno, basi kumjua Mungu kungekuwa kugumu sana kwenu, kwa sababu watu wangelazimika kukisia nia ya Mungu na mapenzi Yake, kitu ambacho ni kigumu sana kwao. Lakini kutokana na hatua ya mwisho ya Kazi Yake, Mungu amenena maneno mengi, kufanya kiwango kikubwa cha kazi, na kufanya mahitaji mengi kwa wanadamu. Katika maneno Yake, na kiwango kikubwa cha kazi Yake, amejulisha watu anachokipenda, anachokichukia, na wanafaa kuwa aina gani ya watu. Baada ya kuelewa vitu hivi, ndani ya nyoyo watu wanafaa kuwa na maelezo sahihi ya mahitaji ya Mungu, kwa kuwa hawamwabudu tena yule Mungu asiye yakini, au kumfuata Mungu katika ukosefu uyakini na udhahania na utupu; badala yake, watu wanaweza kusikia maneno ya Mungu, wanaweza kuelewa viwango vya mahitaji ya Mungu, na kuvifikia, na Mungu hutumia lugha ya wanadamu kuwaambia watu yale yote wanafaa kujua na kulewa. Leo, kama watu hawafahamu mahitaji ya Mungu kwao, kile Mungu alicho, kwa nini wanamwamini Mungu, na jinsi wanafaa kumwamini Mungu na jinsi wanavyojichukulia mbele Zake, basi kuna shida hapa. Sasa hivi tu kila mmoja wenu amezungumza kuhusu kipengele kimoja; mnafahamu kuhusu mambo fulani, yawe ni mambo mahususi au ya jumla—lakini Ningependa kuwaambia mahitaji ya Mungu ya kweli, kamili, na mahususi kwa wanadamu. Ni maneno machache tu, na rahisi sana. Yawezekana tayari mnayajua haya maneno. Mahitaji sahihi ya Mungu kwa wanadamu na wale ambao wanamfuata ni kama ifuatavyo. Mungu anahitaji mambo matano kutoka kwa wale wanaomfuata; imani ya kweli, ufuasi wenye uaminifu, utiifu kamili, ufahamu wa kweli na heshima za kutoka moyoni.
Katika mambo haya matano, Mungu anahitaji kuwa watu wasimshuku tena, wala kumfuata wakitumia fikira zao au mitazamo ikosayo uyakini na iliyo dhahania; Ni lazima wamfuate Mungu bila fikira au dhana zozote. Mungu anahitaji kuwa wote wanaomfuata wafanye hivyo kwa uaminifu, sio kwa shingo upande au bila kujizatiti. Mungu anapokupa mahitaji yoyote, au kukujaribu, kukuhukumu, kukushughulikia na kukupogoa, au kukuadhibu na kukuangamiza, unapaswa kuwa mtiifu kabisa Kwake. Hufai kuuliza kilichosababisha, au kuweka masharti, au hata uongee kuhusu sababu. Utiifu wako lazima uwe usio na shaka. Kumjua Mungu ni kipengele ambacho watu wengi wanakosea. Mara kwa mara wanamlazimishia Mungu misemo, matamshi, na maneno ambayo hayahusiani na Yeye, wakiamini kuwa haya maneno ndiyo ya kweli kuhusu kumfahamu Mungu. Kumbe hawajui kuwa hii misemo, ambayo inatoka kwa fikira za watu, ung'amuzi wao, na busara zao, havina uhusiano wowote na kiini cha Mungu. Na kwa hiyo, Ninataka kukwambia kuwa, katika ufahamu wa watu unaotamaniwa na Mungu, Mungu haulizi tu kwamba umtambue Mungu na maneno Yake, lakini kuwa ufahamu wako juu ya Mungu ni sahihi. Hata kama unaweza kusema sentensi moja tu, au una ufahamu mdogo tu, huu ufahamu mdogo ni sahihi na wa kweli, na unalingana na kiini cha Mungu Mwenyewe. Kwa kuwa Mungu hapendi sifa na wao kumtukuza Yeye kwa hali isiyo halisi na yenye nia mbaya. Zaidi ya hayo, Anachukia watu wanapomchukulia kama hewa. Anachukia ambapo, wakati wa majadiliano juu ya mada kuhusu Mungu, watu wanazungumza kimzaha, wakiongea kwa hiari bila ya kujali, wakiongea wapendavyo; zaidi ya hayo, anawachukia wale wanaojifanya wanamjua Mungu, na wanaringa kuhusu ufahamu wa Mungu, wakijadili mada kuhusu Mungu bila mipaka au kipimo. La mwisho Kati ya yale mahitaji matano lilikuwa ni kumheshimu Mungu kutoka moyoni. Hili ndilo hitaji kuu la Mungu kwa wale wote wanaomfuata. Wakati mtu ana ufahamu wa kweli na sahihi kumhusu Mungu, anaweza kumheshimu Mungu na kuepuka maovu. Heshima hii hutoka ndani ya moyo wake, ni ya hiari, na sio kwa sababu Mungu amemshurutisha. Mungu hataki utoe zawadi ya mwelekeo wowote wa kupendeza, au tabia, au mienendo ya nje Kwake; badala yake, anataka kwamba umheshimu na umwogope kutoka ndani ya moyo wako. Heshima hii inaafikiwa kutokana na mabadiliko katika tabia ya maisha yako, kwa sababu una ufahamu juu ya Mungu, kwa sababu unaelewa matendo ya Mungu, kwa sababu ya uelewa wako wa kiini cha Mungu, na kwa sababu umetambua ukweli kuwa wewe ni mmoja wa viumbe wa Mungu. Na kwa hiyo, nia yangu ya kutumia neno “kutoka moyoni” kwa kurejelea heshima hapa ni kwamba wanadamu waelewe kuwa heshima ya watu kwa Mungu inapaswa kutoka ndani ya mioyo yao.
Sasa yafikirie hayo matakwa matano: kuna yeyote kati yenu anaweza kupata matatu ya kwanza? Ambapo Ninamaanisha uaminifu wa kweli, ufuasi wenye uaminifu, na utiifu kamili. Kuna wowote kati yenu wanaoweza mambo haya? Najua Nikisema yote matano, basi bila kuuliza hapatakuwa na hata mmoja kati yenu anayeweza—lakini nimeyapunguza hadi matatu. Tafakari kama umeyapata au la. Je, “uaminifu wa kweli” ni rahisi kuupata? (La, sio rahisi.) Sio rahisi, kwa kuwa mara nyingi watu humtilia Mungu mashaka. Na, je, “ufuasi wenye uaminifu”? Huu “uaminifu” una maana gani? (Sio kwa shingo upande ila kwa moyo wote.) Sio kwa shingo upande ila kwa moyo wote. Mmegonga ndipo! Kwa hiyo, je, mna uwezo wa kupata hili hitaji? Inabidi mjitahidi zaidi—siyo? Kwa sasa bado hamjapata hili hitaji. Kuhusu “utiifu kamili”—je, mmepata hilo? (Hapana.) Bado hamjapata hilo, pia. Mara nyingi nyinyi si watiifu na ni waasi, mara nyingi hamsikilizi, au kupenda kutii, au kutaka kusikia. Haya ndiyo mahitaji matatu ya msingi wanayopata watu baada ya kuingia katika maisha yao, na bado hamjayapata. Kwa hiyo, kwa wakati huu, mna uwezo mkubwa? Leo, baada ya kunisikia nikisema maneno haya, mna wasiwasi? (Ndiyo.) Ni sawa kuwa mna wasiwasi—. Msiwe na wasiwasi Ninahisi wasiwasi kwa niaba yenu. Sitakwenda katika mahitaji hayo mengine mawili; bila shaka, hakuna anayeweza kuyafikia. Mna shauku. Kwa hivyo mmebaini malengo yenu? Malengo yapi, kuelekeza upande gani, mnapaswa kuyafuata, na kujitolea jitihada zenu? Mna lengo? (Ndiyo.) Lengo lenu ni lipi? (Kuutafuta ukweli, kuutafuta ufahamu wa Mungu katika maneno Yake, na kwa hakika kupata heshima na utiifu kwa Mungu.) Hebu niongee waziwazi: mnapofikia mahitaji haya matano, mtakuwa mmemridhisha Mungu. Kila mojawapo ni ishara, ishara ya watu wakiingia katika maisha wakiwa wamefikia ukomavu, na lengo la mwisho la hii. Hata kama Ningechukua moja kati ya mahitaji na kuongea kwa kina kulihusu na kinachohitajika, haiwezi kuwa rahisi kupata; ni lazima mpitie kiwango fulani cha matatizo na kufanya kiasi fulani cha juhudi. Na ni aina gani ya mawazo mnapaswa kuwa nayo? Yanapaswa kuwa sawa na yale ya mgonjwa wa saratani anayesubiri kwenda kwenye meza ya upasuaji. Na ni kwa nini Ninasema haya? Kama ungependa kumwamini Mungu, na kumpata Mungu na kupata ridhaa Yake, basi kama hutapitia katika kiasi fulani cha shida, au kufanya kiwango fulani cha juhudi, hutaweza kupata vitu hivi. Umesikia mahubiri mengi, lakini kuyasikia hakumaanishi kuwa haya mahubiri ni yako; ni lazima uyachukue na kuyageuza yawe kitu ambacho ni chako, ni lazima uyasimilishe maishani mwako, na kuyaleta katika uwepo wako, ukiyaruhusu maneno na mahubiri haya yakuongoze katika maisha yako, na kuleta dhamana na maana ya uhai katika maisha yako—na hivyo basi itakuwa ni thamani kuwa uliyasikia maneno haya. Kama maneno haya Ninayoyanena hayaleti mabadiliko yoyote katika maisha yenu, au thamani yoyote katika uwepo wako, basi hakuna haja ya kuyasikiliza. Mnaelewa haya, ndiyo? Baada ya kuelewa haya, basi kilichobaki ni juu yenu wenyewe. Ni lazima mfanye kazi! Ni lazima muwe na bidii katika kila jambo! Msiwe huku na kule—wakati unapita upesi! Wengi wenu wameamini kwa zaidi ya miaka kumi. Tazama nyuma kwa hii miaka zaidi ya kumi ya imani katika Mungu: Umenufaika kiasi gani? Na mmesalia na miongo mingapi ya haya maisha? Sio mirefu. Sahau kuhusu iwapo kazi ya Mungu inakusubiri, iwapo Amekuachia nafasi, iwapo Atafanya kazi ile ile tena; usizungumze kuhusu hili. Unaweza kurudisha nyuma miaka yako kumi iliyopita? Kwa kila siku inayopita, na kila hatua unayochukua, siku ambazo unazo hupunguzwa kwa siku moja. Muda haumsubiri mwanadamu yeyote! Utanufaika tu kutokana na imani kwa Mungu kama utaichukulia kama kitu kikubwa zaidi maishani mwako, muhimu zaidi kuliko chakula, mavazi, au kitu kingine chochote! Kama huwa unaamini tu unapokuwa na wakati, na huwezi kutoa umakini wako wote kwa imani yako, kama siku zote umetatizwa na vurugu, basi hutafaidi chochote. Unaelewa hili, ndio? Tutaishia hapa kwa leo. Tuonane wakati ujao! (Shukrani kwa Mungu!)"


kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili


Kujua zaidi: Umeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Jumatano, 20 Februari 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Je, Wewe Ni Muumini wa Kweli wa Mungu?

Matamshi ya Mwenyezi Mungu  | Je, Wewe Ni Muumini wa Kweli wa Mungu?


Huenda ikawa safari yako ya imani katika Mungu imekuwa ndefu zaidi ya mwaka mmoja au miwili, na labda kwa maisha yako umestahimili ugumu mwingi miaka hii yote; au labda haujapitia ugumu na badala yake umepokea neema nyingi. Kuna uwezekano pia kuwa hujapitia ugumu wala kupokea neema, na badala yake umeishi maisha ya kawaida tu. Hiyo haijalishi, kwani wewe bado u mfuasi wa Mungu, kwa hivyo tushirikiane kuhusu mada ya kumfuata Mungu.

Alhamisi, 31 Januari 2019

Kanisa la Mwenyezi Mung|7. Roho Ya Majivuno Kabla ya Kuanguka

Kanisa la Mwenyezi Mung | 7. Roho Ya Majivuno Kabla ya Kuanguka

Baixue Mji wa Shenyang

Kwa sababu ya mahitaji ya kazi, nilihamishiwa hadi sehemu nyingine ya kazi. Wakati huo, nilikuwa na shukurani sana kwa Mungu. Nilihisi kwamba nilikuwa ninapungukiwa sana, lakini kwa njia ya ukuzwaji mtakatifu na Mungu, nilipewa nafasi ya kutimiza wajibu wangu katika eneo la kazi la ajabu hivyo. Niliweka nadhiri kwa Mungu moyoni mwangu: Ningefanya lote ninaloweza kumlipa Mungu.

Jumapili, 6 Januari 2019

5. Imani Katika Mungu Haipasi Kuwa kwa ajili ya Kutafuta Amani na Baraka Pekee.

Sura ya 7 Vipengele Kadhaa Vingine vya Ukweli Ambao ni wa Kiwango cha Chini Ambao Unafaa Kueleweka na Waumini Wapya
5. Imani Katika Mungu Haipasi Kuwa kwa ajili ya Kutafuta Amani na Baraka Pekee.


Maneno Husika ya Mungu:
Leo, lazima uwe katika njia sahihi kwani unaamini katika Mungu wa vitendo. Kwa kuwa una imani katika Mungu, hupaswi tu kutafuta baraka, lakini pia kutafuta kumpenda Mungu na kumjua Mungu. Kupitia kwa kupata nuru kutoka Kwake na harakati yako mwenyewe, unaweza kula na kunywa neno Lake, kukuza ufahamu wa kweli kuhusu Mungu, na kuwa na upendo wa kweli kwa Mungu unaotoka moyoni mwako. 

Jumatano, 28 Novemba 2018

95. Kuinuka Kupitia Ukandamizaji wa Giza

Umeme wa Mashariki | 95. Kuinuka Kupitia Ukandamizaji wa Giza

imani,maombi,Mateso-ya-Kidini,maneno-ya-Mungu

Mo Zhijian Mkoa wa Guangdong

Nilizaliwa katika eneo maskini, la mbali lenye milima ambako tumefukiza na kumwabudu Budha kwa vizazi vingi. Kuna hekalu za Budha sehemu hiyo kote ambako familia zote zingekwenda kuchoma uvumba; hakuna mtu yeyote aliyewahi kumwamini Mungu kamwe. Katika mwaka wa 1995, mimi na mke wangu tulikuwa katika sehemu nyingine ya nchi ambapo tulimwamini Bwana Yesu; baada ya sisi kurudi tulianza kushiriki injili na idadi ya watu ambao waliikubali ilikua polepole hadi watu zaidi ya 100.

Jumamosi, 19 Mei 2018

Umeme wa Mashariki | Vitabu vya Shetani Vinaweza Kutulisha Sumu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, ukweli

Umeme wa Mashariki |  Vitabu vya Shetani Vinaweza Kutulisha Sumu

Peihe    Jiji la Xianning, Mkoa wa Hubei
Daima niliamini kwamba mimi na mume wangu tulipitia maisha yetu "na nyuso zetu kwa mchanga na migongo yetu kwa jua" kwa sababu hatukusoma vya kutosha tulipokuwa vijana, na kwa sababu hatukuwa na elimu. 

Jumatano, 16 Mei 2018

"Imani katika Mungu" (6) - Imani ya Kweli katika Mungu Inamaanisha Nini?


"Imani katika Mungu" (6) - Imani ya Kweli katika Mungu Inamaanisha Nini?

Utambulisho

Watu wengi wanaamini kwamba imani katika Mungu ni imani katika Biblia, na kwamba kumfanyia Bwana kazi kwa bidii ni uhalisi wa kuamini katika Mungu. Hakuna mtu katika ulimwengu wa dini ana uwezo wa kuelewa kabisa imani ya kweli katika Mungu ina maana gani. Mwenyezi Mungu anasema, “‘Imani katika Mungu’ inamaanisha kuamini kuwa kuna Mungu; hii ndiyo dhana rahisi zaidi ya imani katika Mungu. Zaidi ya hayo, kuamini kuwa kuna Mungu sio sawa na kuamini katika Mungu kwa ukweli; bali, ni hali ya imani sahili ikiwa na vipengee vya uzito vya kidini. Imani ya kweli katika Mungu ina maana kupitia maneno na kazi ya Mungu kwa msingi wa imani kuwa Mungu ndiye mkuu juu ya vitu vyote. Kwa hivyo mtakuwa huru kutokana na tabia yenu ya upotovu, mtatimiza hamu ya Mungu, na mtapata kumjua Mungu. Ni kwa kupitia safari ya aina hii tu ndio mnaweza kusemekana kuwa mnaamini katika Mungu." ( Neno Laonekana katika Mwili).
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu

Soma Zaidi: Kujua Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Jumanne, 15 Mei 2018

"Imani katika Mungu" (5) - Je, Kufanya Kazi kwa Bidii kwa ajili ya Bwana ni Uhalisi wa Imani katika Bwana?


"Imani katika Mungu" (5) - Je, Kufanya Kazi kwa Bidii kwa ajili ya Bwana ni Uhalisi wa Imani katika Bwana?

Utambulisho

Waumini wengi huamini kwamba mradi tunalilinda jina la Bwana, kuomba mara kwa mara, kusoma Biblia na kuwa na mikutano, na mradi sisi huyaacha vitu, hutumia rasilmali na kufanya kazi kwa bidii kwa ajili ya Bwana, basi hii ni imani ya kweli katika Bwana, na tutaweza kunyakuliwa hadi katika ufalme wa mbinguni Bwana atakaporudi. Je, aina hii ya mtazamo ni sahihi? Wengi wataniita siku hiyo, Bwana, Bwana, hatujafanya unabii kwa jina lako? na kwa jina lako kutoa pepo? na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Halafu nitasema wazi kwao, Sikuwajua nyinyi kamwe: ondokeni mbele yangu, nyinyi watenda maovu." (Mathayo 7: 22-23). Mwenyezi Mungu anasema, "Sijali jinsi kazi yako ya bidii ni ya kutunukiwa, jinsi sifa zako ni za kuvutia, jinsi unanifuata Mimi kwa karibu, jinsi una umashuhuri, au jinsi umeendeleza mwelekeo wako; mradi hujafanya kile Ninachodai, kamwe hutaweza kushinda sifa Zangu." (Neno Laonekana katika Mwili).
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, wokovu
Soma Zaidi: Kujua Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Jumatano, 9 Mei 2018

"Imani katika Mungu" (2) - Je, Njia Inayoshutumiwa na CCP na Miongoni mwa Watu wa Dini Siyo Njia ya kweli?


"Imani katika Mungu" (2) - Je, Njia Inayoshutumiwa na CCP na Miongoni mwa Watu wa Dini Siyo Njia ya kweli?

Utambulisho
Watu wengi hutafuta na kuchunguza njia ya kweli pasipo kutegemeza vitendo hivi katika maneno na kazi ya Mungu. Badala yake, wao hufuata mitindo ya ulimwengu wa dini na wanaamini kwamba kile ambacho serikali ya kikomunisti ya China na ulimwengu wa dini inalaani sio njia ya kweli—je, hii ni njia sahihi ya kuelekea? Biblia inasema, “dunia nzima hukaa ndani ya maovu."(1 Yohana 5:19). “Hiki ni kizazi kiovu” (Luka 11:29). Hivyo inaweza kuonekana kwamba mifumo ya kisiasa ya kukana Mungu na ulimwengu wa dini hakika utakana na kuishutumu njia ya kweli. Wakati ambapo Bwana Yesu alifanya kazi Yake katika Enzi ya Neema, serikali ya Kiyahudi na ya Kirumi zilimpinga na kumtia hatiani kwa hasira, na mwishowe Bwana Yesu alisulubishwa msalabani. Je, si huu ni ukweli wa hali? Mwenyezi Mungu anapokuja kufanya kazi Yake katika siku za mwisho, Anapitia uasi mkali na shutuma ya serikali ya China na ulimwengu wa dini. Hili linaonyesha nini? Je, si hili linastahili sisi kulitafakari?
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki
Soma Zaidi: Kujua Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Jumanne, 8 Mei 2018

"Imani katika Mungu" (1) - Je, Utiifu kwa Wale Walio Madarakani Kweli ni Sawa na Utiifu kwa Mungu?

"Imani katika Mungu" (1) - Je, Utiifu kwa Wale Walio Madarakani Kweli ni Sawa na Utiifu kwa Mungu?

Utambulisho

Katika Biblia, Paulo alisema, "Acha kila nafsi itii mamlaka ya juu zaidi. Kwani hakuna mamlaka isipokuwa ya Mungu: mamlaka yaliyoko yameamriwa na Mungu. Yeyote yule anayepinga nguvu, anapinga amri ya Mungu: na yule anayepinga atapokea laana” (Warumi 13:1-2). Sisi waumini tunapaswa kuwatendea vipi wale walio madarakani? Je, utiifu kwa wale walio madarakani ni sawa na utiifu kwa Mungu kweli?
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Bwana Yesu
Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.

Jumatano, 18 Aprili 2018

Umeme wa Mashariki | Vigezo vya Mtu Mwema Kwa Dhati

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, upendo wa Mungu

Umeme wa Mashariki | Vigezo vya Mtu Mwema Kwa Dhati

Moran   Mji wa Linyi, Mkoa wa Shandong
Tangu nilipokuwa mtoto, siku zote nilishikiza umuhimu mkubwa kwa jinsi watu wengine walivyoniona na ukadiriaji wao kwangu. Ili niweze kupata sifa kutoka kwa wengine kwa kila kitu nilichokifanya, sikubishana na yeyote asilani wakati wowote kitu chochote kilichoibuka, ili kuepuka kuharibu picha nzuri watu wengine walikuwa nayo kwangu. 

Jumatano, 11 Aprili 2018

Umeme wa Mashariki | Kupenya Ukungu ili Kuona Mwanga

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Kanisa

Umeme wa Mashariki | Kupenya Ukungu ili Kuona Mwanga

Faith China
Mimi ni mfanyakazi wa kawaida. Mwishoni mwa Novemba, 2013, mfanyakazi mwenza aliona kwamba mke wangu na mimi tungefanya kelele nyingi sana juu ya vitu vidogo, kwamba kila siku tulikuwa na wasiwasi na huzuni, hivyo alipitisha kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku mwisho kwetu. 

Ijumaa, 6 Aprili 2018

Kuhusu Biblia (4)

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki

Kuhusu Biblia (4)

Mwenyezi Mungu alisema, Watu wengi wanaamini kwamba kuelewa na kuwa na uwezo wa kufasiri Biblia ni sawa na kutafuta njia ya kweli—lakini, kimsingi, je, vitu ni rahisi sana? Hakuna anayejua uhalisia wa Biblia: kwamba si kitu chochote zaidi ya rekodi ya kihistoria ya kazi ya Mungu, na agano la hatua mbili zilizopita za kazi ya Mungu, na haikupatii ufahamu wa malengo ya kazi ya Mungu.

Jumanne, 3 Aprili 2018

Umeme wa Mashariki | Dibaji

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki
Mwenyezi Mungu alisema, Ingawa watu wengi wanaamini katika Mungu, ni wachache wanaoelewa ni nini maana ya imani katika Mungu, na ni nini wanachopaswa kufanya ili waupendeze moyo wa Mungu. Hii ni kwa sababu, hata ingawa watu wengi wanalifahamu neno “Mungu” na mafungu ya maneno kama “kazi ya Mungu”, hawamjui Mungu, na kwa kiwango cha chini zaidi hawaijui kazi ya Mungu.

Jumatatu, 2 Aprili 2018

Umeme wa Mashariki | Maonyo Matatu

Umeme wa Mashariki | Maonyo Matatu

Mwenyezi Mungu alisema, Kama muumini wa Mungu, hufai kuwa watiifu kwa yeyote mwingine isipokuwa Yeye katika mambo yote na mjilinganishe na moyo Wake katika mambo yote. Hata hivyo, ingawa wote huelewa mafundisho haya, ukweli huu wa kimsingi ulio wazi kabisa kwa binadamu hauwezi kuonekana kuwa kujumuishwa kwao kikamilifu, kutokana na ugumu wao, kama vile hali yao ya kutojua, upuzi, au ufisadi. Kwa hivyo, kabla ya kuuamua mwisho wenu, Ninafaa kuwaambia kwanza baadhi ya mambo, ambayo ni yenye umuhimu mkubwa sana kwenu.

Jumatatu, 19 Machi 2018

Sura ya 88. Kulipa Gharama ili Kupata Ukweli ni Muhimu Sana

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki

Sura ya 88. Kulipa Gharama ili Kupata Ukweli ni Muhimu Sana

Mwenyezi Mungu alisema, rahisi kwa vijana kuendeleza kazi; wengi wao hawadumishi mwendo. Ni lazima moyo wako uwe mtulivu, lazima uweze kudumisha mwendo na uwe tayari kutumia muda kwake. Wengine hujiburudisha au kuwachezea wengine, lakini wewe unasema, "Siwezi, sina wakati. Biashara yangu ina shughuli sana. Nendeni mkajiburudishe.Ni lazima niipange biashara yangu.” Unaweza tu kufaulu kwa kushughulika na kujitolea kwa biashara yako. Kwa kweli, hukosi nguvu sasa, wala hukosi ujuzi wa kitaalamu. Ili kuboresha hali yako ya kitaaluma, unaweza kufanya baadhi ya utafiti na ujifunze. Ni yapi zaidi, una msingi huu, akili hii, ujuzi huu maalum; unachokosa kwa kweli ni kutumia wakati na nguvu. Vijana hujifunza kidogo kuhusu mambo ya kitaalamu na huelewa baadhi ya ujuzi, hivyo ni rahisi zaidi kwao kufaulu kuliko ilivyo kwa watu wazima? Nchi zinapomchagua raisi, kuna yeyote wa umri wa miaka 20 au 30 ambaye huchaguliwa? (La.) Mbona hivyo? Hawajahitimu vya kutosha katika uwanja wowote. Hawana tajriba ya kutosha, akili zao hazijakomaa, hawaoni mambo kwa upana; mambo kama ujasiri, umaizi, hekima au uwezo bado hayajakomaa. Zaidi ya hayo, kuna sababu kuu kwa nini mambo yako hivyo, watu wakiwa vijana, huwa na msukumo kuhusu mambo mengi. Na sababu nyingine ni kuwa, watu wakiwa vijana, kuna mambo mengi ulimwenguni ambayo bado hawajapitia au kukumbana nayo hapo awali, kwa hivyo mambo mengi yatakuwa yanawatia majaribuni na kuwavutia. Hilo ni kusema, ni vigumu sana kwa vijana kufaulu katika jambo lolote. Haijalishi kile ambacho umesoma, au kile ulichotaalimikia, ni vigumu kufaulu kwa chochote kizuri au muhimu, kuendeleza kazi, na majaribu ni mengi sana. Kwa jumla, watu katika umri wao wa miaka ya 50, 60, 70 au 80 huwa na tajriba nyingi sana za mambo ya ulimwengu na, kwa jumla, mtazamo wao wa ulimwengu uko imara. Wamepitia mambo katika ulimwengu wa nje kama vile ndoa, kushindwa na vikwazo, na aina zote za majaribu na vivutio, na wameyafaulu. Kwa watu wa umri wenu, karibu umri wa miaka 20, kuna mambo mengi sana katika ulimwengu wa nje ambayo ni maajabu kwenu; mnataka kupitia kila kitu, mnahisi kila kitu kikiwa kipya kwenu na mnapenda sana kujua kila kitu. Huna tajriba yake, hivyo daima iko katika akili yako, unahisi kwamba ulimwengu wa nje katika kupumbaza kwake kote sio lazima uwe mbaya hivyo, na sio lazima uwe wa kutisha sana. Hasa, ndani ya mazingira haya katika jamii, watu katika kikundi cha umri wenu hawana uwezo wa kutambua sawasawa mambo wanayosikia na kuona, na hawajui ni mambo yapi ambayo ni majaribu, au ni mambo yapi yatawaletea huzuni au kuwapotoza. Hivyo, kusema kiasi, vijana ni dhaifu sana kuliko watu wazima na wako katika hatari kuu sana. Kuna mambo machache ambayo watu katika kikundi hiki cha umri hufahamu katika mawazo yao, mambo machache ambayo mioyo yao huelewa na ambayo mioyo yao imejiandaa kwayo, na mambo mengi katika ulimwengu huu yako katika kiwango kisichojulikana na hayajulikani kwao, hivyo kuna mambo mengi ambayo kamwe hawawezi kuelewa kabla wawe na tajriba ya au wakumbane nayo, na kamwe hawawezi kujua mambo haya kwa hakika yanahusu nini. Hivyo, iwapo vijana wako katika mazingira ya kawaida, basi wataona ikiwa vigumu sana kusimama imara. Iwapo umeshawishika kwa miaka kadhaa kanisani, katika mazingira haya yaliyo na ukweli, kwa angalau miaka 8 au 10, basi moyo wako utakuwa umetulia na utakuwa umekita mizizi katika familia ya Mungu. Iwapo hutaweza kutuliza moyo wako katika aina hii ya mazingira, hata hivyo, basi utajipata katika shida na hatari kuu.
Kumwamini Mungu na kutekeleza wajibu wako ndiyo njia sahihi katika maisha, ndiyo sahihi kuchagua na, kwa huruma za Mungu, watu wana fursa hii ya kutekeleza wajibu wa binadamu aliyeumbwa. Kwa watu katika umri mchanga kama nyinyi ambao, inaweza kusemwa, mko katika upeo wa ujana wenu, ili kuweza kutekeleza wajibu wenu ni huruma za Mungu, na pia mnajaribu kushirikiana katika kufanya hivi. Lakini iwapo utadhibitiwa na kuzuiliwa kimakosa na baadhi ya masuala madogo, iwapo huwezi kuendelea kutekeleza wajibu wako na suala hili dogo liathiri wajibu wako, au labda lisumbue wajibu wako au hata kuutamatisha wajibu wako—hii haitakuwa aibu? Hii itakuwa sikitiko, aibu. Hivyo, ni lazima muombe pamoja mara kwa mara na mara nyingi kutulia; msifikirie kuhusu matatizo hayo ambayo hayawahusu au yale ambayo hampaswi kuwa mnafikiri kuyahusu sasa, na mfunge vipengele hivyo vya mioyo yenu. Mngali wachanga na wa miaka michache, kwa hivyo msiwe na wasiwasi sana wa kufikiri kuhusu mambo haya. Mambo makubwa maishani sio ndoa tu, kazi na matarajio ya siku sijazo, au kutulia na kuishi kwa amani. Wala kutokuwa na uvumilivu wa kupata nafasi yako katika jamii sio jambo la pekee. Haya sio mambo ya muhimu zaidi. Mambo muhimu zaidi ni yapi? Hapo awali, ndoa na mazishi yalikuwa mambo makubwa; mambo haya ndiyo makubwa sasa? (La.) Mambo makubwa zaidi ni yapi? (Kwanza, muiheshimu imani ya Mungu ndani yetu, na mtekeleze wajibu na shughuli ambazo binadamu aliyeumbwa anapaswa kutekeleza.) Hili ndilo azimio mnalopaswa kuwa nalo. Sasa mnamwamini Mungu na mnatekeleza wajibu wenu, hivyo maisha yenu yameanza kwa mwelekeo ulio sahihi. Hili ni kuu, na ni sahihi. Hivyo,ni nini mnachopaswa kufanya baada ya hili? Je, mnafahamu? (Weka msingi kwa njia ya kuingia katika maisha.) Hili ni sahihi. Weka misingi yako katika njia ya kutafuta ukweli, hakikisha lengo na mwelekeo wa maisha yako, uruhusu ukweli kuweka msingi katika moyo wako na, kwa njia hii, kwa hakika utakuwa mtu ambaye Mungu huchagua, mtu ambaye Mungu amejalia. Ni lazima kwanza muweke misingi. Misingi yenu sasa bado sio imara. Kamwe msijali kuhusu dhoruba, mpulizo kidogo wa upepo unaweza kuwatingisha wakati wowote, hivyo inaweza kusemwa kuwa bado hamjaweka misingi, na hii ni hatari sana. Wekeni lengo lenu la maisha, wekeni mwelekeo ambao mnatafuta, na muweke njia ambayo ni lazima muifuate katika maisha haya. Wekeni lengo hili na jambo kubwa katika maisha, tulieni kwa miaka, na mfanye kazi kwa bidii, tumieni, fanyeni juhudi na mlipe gharama ya suala husika na kwa lengo hili; msifikiri sasa kuhusu jambo lingine lolote. Mbona hampaswi kufikiri kuhusu jambo lingine lolote? Iwapo utaendelea kufikiri kuhusu mambo hayo mengine, basi suala husika halitakuwa jambo lako kuu, badala yake litakuwa la baadaye. Iwapo bado utaendelea kufikiri kuhusu kupata kazi, kupata pesa nyingi, kutajirika, kupata mahali thabiti pa usalama katika jamii, kupata nafasi yako mwenyewe, na pia kufikiri kuhusu kuolewa na kupata mume au mke, haya ni mambo makubwa mangapi? Na kisha unataka kufikiri kuhusu kupata ujuzi na uwezo katika siku sijazo, jinsi ya kuwa mtu aliyejitokeza, na unataka kusaidia na kukuza jamii katika siku zijazo na kuwapa wazazi wako maisha mazuri. Hutakuwa umechoka? Moyo wako ni mkubwa kiasi kipi? Je, mtu huwa na kiwango kipi cha nguvu katika maisha? Watu huwa na nguvu nyingi zaidi katika miaka yao mingapi, na ni miaka mingapi ambayo inaweza kuchukuliwa kuwa miaka yao bora zaidi? Katika maisha mazima ya mtu, wakati rahisi zaidi, wakati ambao nguvu yao husitawi zaidi, ni wakati ambapo wako katika miaka yao ya 20, na zaidi kabisa hadi umri wa miaka 40. Katika wakati huu, ni lazima mfahamu ukweli mnaopaswa kuelewa katika imani yenu kwa Mungu, na kisha muingie katika uhakika wa ukweli, mkubali hukumu na kuadibu kwa Mungu na mkubali kusafishwa na Mungu na majaribu—ni nini ambacho lazima mtimize kwa kufanya hivi? Hamtamkana Mungu hata hali iweje—hili ni la muhimu zaidi; kando na hili, haijalishi kitakachowavuta au kuwaburuta, au iwapo baadaye mtaolewa na kupata mume au mke, hamtakata tamaa kuhusu wajibu wenu na kukata tamaa kuhusu vitu ambavyo mwanadamu aliyeumbwa anapaswa kufanya; na zaidi ya hayo, iwapo wakati fulani katika siku sijazo Mungu hatawataka, bado mtaweza kuutafuta ukweli na kutafuta kutembea kwa njia ya kumcha Mungu na kuepuka uovu. Ni lazima mtie bidii kwa vipengele hivi; iwapo mtafanya hivyo, basi hamtaishi miaka hii bure.
Na baadhi ya watu bado wamechanganyikiwa, wakiota siku yote. Wanasema, "Bado kuna muda mwingi kabla ya kazi ya Mungu kufika mwisho. Ni kawaida kula, kunywa, kuoa na kujitolea katika ndoa, na muwe au msiwe na mimi, haileti utofauti wowote." Ni kweli kwamba haileti utofauti wowote ukiwa au usipokuwa nao. Lakini kuna wakati ambao Mungu humuokoa mwanadamu, na wakati ambao ni wa kazi ya Mungu kufikia kikomo, kuna mtu mmoja tu ambaye anaweza kuokolewa; Yeye anamchukua tu mtu huyo mmoja na kuwaharibu wengine wote—hii ni tabia ya Mungu. Mtu hawezi kuitambua na hawezi kuielewa. Ni watu wangapi walikufa wakati wa Nuhu? Nuhu alikuwa akijenga safina kwa zaidi ya miaka 100, na watu hao wote hawakuwa wametubu. Mwishowe, Mungu alimuokoa Nuhu na familia yake tu ya watu wanane, na baada ya watu hawa wanane kuingia katika safina, ni nini basi kilichotendeka kwa wale wote waliobaki? (Wote waliangamia kabisa.) Wale katika ya wanadamu ambao wameshindwa kuokolewa ni wadudu na mchwa machoni pa Mungu. Huku Mungu akimuokoa mtu, tabia Yake ni yenye huruma, ya kupenda, na ya kuvumilia; lakini kazi ya Mungu ya kumuokoa mtu inapokamilika, Havumilii tena na Yeye huondoa uvumilivu wake, na ni ghadhabu na uadhama wake tu ambayo hubaki. Nyakati hizi mnazoishi sasa kwa kweli ni nyakati nzuri sana. Katika wakati huu ambao kazi ya Mungu ni muhimu zaidi, mko tu katika umri unaofaa, mliweza kuupata na nyote mnaweza kutekeleza wajibu wenu. Haijalishi ni taaluma gani mlizosomea, kile ambacho mmemudu au ni ujuzi upi maalum mlionao, kwa njia ya taaluma zenu wenyewe maalum mumekuja katika nyumba ya Mungu kutekeleza wajibu wenu. Hii ndiyo huruma ya Mungu na ni fursa ambayo haiji kila siku. Matendo ya Mungu hayapendelei yeyote. Ni Mwenye huruma kwako na Hukuruhusu kufurahia baraka hii, sio ili uweze kutosheleza mwili wako na sio ili uweze kuishi maisha ya kutosheka na kutofanya juhudi zozote za kuendelea. Haijalishi ni aina gani ya njia Mungu atakupa, haijalishi jinsi Alivyo mwenye huruma kwako, mwishowe ana mapenzi haya tu, ambayo ni wewe kuelewa ukweli, ili uweze kuyaelewa mapenzi yake na kuelewa ukweli katika mazingira haya ambayo yanafaa kwa ukuaji wako. Maneno ya Mungu na ukweli wa Mungu huletwa kwako na yanakuwa maisha yako, na unaweza kumtii na kumuogopa Mungu. Licha ya umri wako mchanga, azimio lako ni kuu, kama yalivyo maisha yako, shauku lako na moyo wako wa kumuogopa Mungu. Basi hili ni kuu, na Mungu ameridhika. Mungu angesema kuwa huruma Zake kwako si za bure. Mungu huvuna mavuno, huzaa matunda na huona matokeo pamoja na wewe; gharama ambayo Yeye hulipa si bure. Mungu anafurahi na ana raha kuona hilo. Huu ni ukuu na mpango wa Mungu, kwa hiyo ni jambo ambalo mtu anaweza kuchagua?
Gharama ambayo Mungu hulipia kila mmoja wenu haijakuwa tu miongo iliyopita tangu mzaliwe. Haijakuwa miongo hiyo tu. Kama Mungu anavyoona, umekuja katika ulimwengu huu mara nyingi na umepata mwili tena mara nyingi. Je, ni nani anayehusika na suala hili? (Mungu.) Mungu ndiye anayehusika nalo, hivyo unafahamu nini kulihusu? Hujui chochote kulihusu. Kila unapokuja ulimwenguni, Mungu hupanga kila kitu Yeye Mwenyewe. Hupanga miaka utakayoishi, aina ya familia utakayozaliwa ndani, utakapooa na kutulia katika ndoa, utakachofanya ulimwenguni, utakachotegemea kuishi, na Mungu hukufungulia njia ili uweze kukamilisha kazi yako katika maisha haya bila tatizo. Wakati unaofuata unapopewa jukumu ulimwenguni, Mungu hutimiza mipango Yake kwa ajili ya maisha yako kulingana na mipango unayopaswa kuwa nayo na ambayo anapaswa kukutengenezea. Hivi tu, Hukupangia mambo mara nyingi sana na, mwishowe, unazaliwa katika enzi hii ya siku za mwisho na unazaliwa katika aina hii ya familia, na Mungu anakuruhusu uende sambamba na kazi yake, umsikize Akizungumza na kuisikia sauti Yake, na hivyo umeishi hadi sasa. Hujui umekuja ulimwenguni mara ngapi, ni mara ngapi ambapo umbo lako limebadilika, umeishi katika familia ngapi, ni enzi ngapi na ni koo ngapi umepitia. Mkono wa Mungu umekushikilia kila mara na Mungu amekulinda kila mara. Ni kiwango gani cha juhudi ambacho Mungu anapaswa kutumia kwa mtu! Baadhi ya watu husema, "Nina umri wa miaka 60, hivyo Mungu ametumia miaka 60 kwangu, Amenitunza na kunilinda kwa miaka 60 na kudhibiti hatima yangu kwa miaka 60.” Je, hili si jambo la ujinga kusema? Si suala la maisha ya wakati mmoja tu ndio Mungu hudhibiti hatima ya mtu na kumtunza na kumlinda. Iwapo lingekuwa suala la maisha ya wakati mmoja, la kipindi kimoja tu cha maisha, basi Mungu hangekuwa Mungu na hangekuwa na aina hii ya mamlaka au uwezo, na haingesemwa kuwa Mungu hutawalavitu vyote, kuwa hutawala kila kitu. Juhudi ambazo Mungu hufanya na gharama ambayo huwa Anakulipia sio tu kupanga vitu ambavyo unafanya katika maisha haya. Yeye hutenda kwa mwoyo na hutenda kwa kutumia maisha Yake Mwenyewe kama gharama, Akiongoza kila mmoja na kupanga maisha yote ya kila mtu. Hivyo, tukizingatia juhudi ambazo Mungu hufanya na gharama ambayo Yeye hulipa kwa niaba ya mwanadamu, na pia ukweli wote na maisha ambayo Yeye humpa mtu, iwapo watu hawatatimiza wajibu wa mtu aliyeumbwa katika nyakati hizi za mwisho na iwapo hawatamrudia Muumbaji, basi haijalishi ni maisha mangapi au ni enzi ngapi watakazoishi, si wao ndio watakuwa wamepoteza? Je, si watakuwa hawastahili gharama ambayo Mungu huwalipia? Hawastahili kabisa gharama anayowalipia Mungu. Kwa hivyo, katika maisha haya—Sizungumzi kuhusu maisha yoyote yaliyopita, lakini katika maisha haya—iwapo kwa ajili ya kazi yako mwenyewe huwezi kuacha vitu unavyopenda au iwapo huwezi kuacha vitu hivi vya nje—vitu hivi vya raha na maisha ya familia—iwapo huwezi kuacha vitu hivi kwa ajili ya gharama ambayo Mungu hukulipia au kulipa upendo wa Mungu, basi hakuna jambo lolote zuri kukuhusu kabisa! Kwa kweli kila gharama unayolipa inastahili. Ikilinganishwa na gharama ambayo Mungu hulipa kwa niaba yako, kiwango hicho kidogo unachotoa au unachotumia hufikia kiwango kipi? Kuteseka kwako hafifu hufikia kiwango kipi? Je, unajua Mungu ameteseka kwa kiwango kipi? Kuteseka hafifu ambako huwa unavumilia hakufikii kiwango chochote. Zaidi ya hayo, sasa unatimiza wajibu wako na unapata ukweli, hivyo mwishowe ni wewe utakayekuwa umebaki. Wakati huu, haijalishi iwapo utateseka au kulipa gharama, kwa hakika unashirikiana na Mungu, na unafanya chochote ambacho Yeye hukwambia ufanye kwa kuyatii maneno Yake; tenda kulingana na maneno Yake, usimkaidi Mungu, na usifanye chochote kinachomhuzunisha Yeye. Unaposhirikiana na Yeye, ni lazima uteseke kwa kiasi fulani na uache baadhi ya vitu, kuacha na kutoa baadhi ya vitu—kuacha umaarufu na faida, vyeo, mali na raha za dunia, hata ndoa, kazi na matarajio yako ya baadaye ya kilimwengu. Je, Mungu anajua unapoacha vitu hivi? Je, Anaweza kuona? (Ndio.) Na Anapoona hili, Atafanya nini? (Mungu anapendezwa. Mungu anafurahi.) Mungu hachukui tu mtazamo, Yeye huchukua hatua, la sivyo, matakwa Yake kwa mwanadamu hayangekuwa na maana. Yeye hafurahi tu, Akisema, “Gharama Niliyolipa inaonyesha matokeo. Mtu huyu yuko tayari kushirikiana na Mimi na ana azimio hili. Nimempata mtu huyu.” Kama Mungu amefurahi, Ameridhika au Anahisi kufarijika, huwa hachukui tu aina moja ya mtazamo—huwa Anachukua hatua. Huruma za Mungu kwa mwanadamu, upendo Wake kwa mwanadamu, rehema Zake kwa mwanadamu zote sio aina ya mtazamo tu; ni ukweli. Ukweli gani? Mungu huyaweka maneno Yake ndani yako ili uweze kupata nuru dani mwako, ili uweze kuona kupendeza kwa Mungu, ili uweze kuona kabisa jinsi ulimwengu ulivyo, ili moyo wako uweze kuchangamshwa na hivyo uweze kuyaelewa maneno ya Mungu na uelewe ukweli. Basi, si umepata kile ambacho unapaswa kupata? Hii sio tu aina ya mtazamo wa Mungu, ni mtazamo tu? Je, umepata nini? (Ukweli.) Umepata kile ambacho ni cha thamani zaidi. Mungu anapoona kuwa ni vyema, huwa Anachukua mtazamo fulani. Wakati huohuo wa kuchukua mtazamo, Yeye pia Huchukua hatua, kama tu vile watu husema, “Huwezi tu kuchukua mtazamo, ni lazima pia uchukue hatua fulani ya kiutendaji.” Watu husema, "Siutaki. Sitaki chochote. Sitaki chochote cha Mungu." Na Mungu husema, “Haikubaliki. Ni lazima Nikupe zawadi—hiki ndicho unachostahili.” Hivyo unapata faida. Unapata nini? Unapata ukweli, unapata maisha, unapata maarifa ya Muumbaji—basi bado ungali mtupu ndani? Je, hujatajirishwa ndani yako? Na mara unapotajirishwa ndani, basi si unaishi maisha ya thamani?
Ayubu aliomba ng'ombe na kondoo waliokuwa kote milimani, au utajiri mkubwa wa familia? (La.) Aliomba nini? Kumcha Mungu na kujiepusha na uovu. Kulingana na Mungu, Mungu alisema kwamba aliona ni vyema, na basi mwishowe Alifanya nini? Je, Alinena maneno hayo machache tu na kisha huo ukawa mwisho? Mungu alichukua hatua; Alichukua hatua gani? Mungu alimtuma Shetani kumjaribu Ayubu, na kuchukua ng'ombe na kondoo wake waliokuwa kote milimani, mali na vitu vyake, watoto wake na wafanyakazi wake, na haya yalikuwa majaribio ya Mungu kwa Ayubu. Mungu alitaka nini kwa kumfanya Ayubu kupitia majaribio haya? Mungu alitaka ushuhuda wa Ayubu. Na Mungu alimpa Ayubu nini wakati huo? Watu wanafikiri, “Mungu alimpa Ayubu nini wakati huo? Ng'ombe na kondoo wake wote walichukuliwa. Hakumpa Ayubu chochote.” Hapa kuna kitu alichopewa Ayubu, na kulikuwa na zawadi, na bado hakuna anayeweza kuona wazi zawadi ambayo Mungu alimpa Ayubu. Mungu alitaka ushuhuda wa Ayubu hivyo Mungu alimpa Ayubu zawadi ya fursa; Hii ilikuwa fursa gani? Ilikuwa Ayubu awe na ushuhuda wa Mungu mbele ya Shetani na mbele ya wanadamu wote, kuwa shahidi kwa ukweli kwamba Ayubu alimcha Mungu na kujiepusha na uovu, na kuwa shahidi kwamba Ayubu alikuwa mkamilifu na mwaminifu. Hiki ndicho Mungu alimpa Ayubu? Iwapo Mungu hakumpa Ayubu fursa hii, Shetani angethubutu kusonga dhidi yake? Hakika Shetani hangethubutu, na hii ni hakika asilimia 100. Na iwapo Shetani hangethubutu kumjaribu, bado Ayubu angekuwa na fursa hii? Hangekuwa na fursa hii. Hivyo, Mungu alimpa Ayubu aina hii ya fursa ili kuthibitisha kwa umati kuwa njia aliyoifuata Ayubu—njia ya kumcha Mungu na kujiepusha na uovu—ilikuwa njia sahihi, kwamba ilikuwa inakubalika kwa Mungu na kwamba Ayubu alikuwa mtu mwaminifu na mkamilifu. Umati uliona haya yote, Mungu aliona haya, na Ayubu alichukua fursa hii na hakumsikitisha Mungu; alikuwa shahidi wa Mungu, alimpiga Shetani, akamshinda Shetani na Mungu aliona kwamba ilikuwa vyema. Hivyo, mwishowe, Mungu alimpa Ayubu chochote kama zawadi? (Ndio.) Ni nini kilichokuwa zawadi ya pili ya Ayubu kutoka kwa Mungu? Mungu alisema kwamba Ayubu alimcha Mungu na kujiepusha na uovu na alikubaliwa na Mungu, kwamba Ayubu alikuwa shahidi wa Mungu mbele ya Shetani, na kuwa kila alichoamini kilikuwa kizuri, na Mungu alipendezwa na kufurahi, na Alichukua aina hii ya mtazamo. Je, Mungu hakuchukua hatua nyingine zaidi baada ya kuuchukua mtazamo huu? Mungu alifanya nini? Hamkifahamu sana kitabu cha Ayubu. Ni katika hali zipi ambapo Ayubu alisema, “Nimesikia habari zako kwa kusikia kwa masikio: lakini sasa macho yangu yanakuona” (Ayubu 42:5)? (Baada ya Mungu kunena na yeye.) Mungu alinena na yeye na kufichua mgongo Wake kwa Ayubu. Je, hii haikuwa zawadi ya Ayubu kutoka kwa Mungu? Kuna yeyote ambaye alikuwa amewahi kumuona Mungu kabla ya Ayubu? Hakuna aliyekuwa ameiona nafsi halisi ya Mungu hapo awali, ikijumuisha mgongo wa Mungu. Ayubu aliuona mgongo wa Mungu na kuisikia sauti yake, na hiki si kitu ambacho mtu aliyeumbwa hutamani sana kukipata? Ayubu alipata hili, hivyo mnamuonea wivu? (Ndio.) Ni vigumu kupata hili, sivyo? Hivyo ni vipi ambavyo mtu anaweza kupata fursa hii, huruma hii na zawadi hii? Ni lazima uwe na ushuhuda wa Mungu; Ni lazima uwe shahidi wa Mungu miongoni mwa majaribu ya Shetani, ni lazima utembee katika njia ya kumcha Mungu na kujiepusha na uovu na ni lazima usimame mbele za Mungu na umfanye kusema kuwa Anachoona ni chema na umfanye Apendezwe na kufurahi. Anapoona kuwa kila unachofanya ni kizuri na ushuhuda wako ni mzuri, Anaposema umekamilika, kuwa wewe ni mtu anayetafuta ukweli, basi utapata haya yote. Baada ya Ayubu kuuona mgongo wa Yehova, zawadi ya Mungu iliishia pale? Mungu alifanya nini baada ya hayo? Alimbariki Ayubu na mali nyingi zaidi kuliko aliyokuwa nayo hapo mbeleni, sivyo? Hivyo ni kusema, alikuwa mwenye mali kuliko mbeleni. Sema kwanza alikuwa kama milionea, hivyo sasa alikuwa labda zaidi ya bilionea. Unaona, kwa mtu anayemcha Mungu na kujiepusha na uovu, kuwa bilionea ni kitu rahisi kutimiza. Hizi ndizo huruma za Mungu!
Kile ambacho Mungu humpa mwanadamu huzidi kile ambacho anaomba au kutamani, lakini iwapo utapenda kupata zawadi inayozidi unachoomba au kutamani, basi lazima uifuate njia ya Mungu. Sio suala rahisi kuifuata njia ya Mungu—ni lazima ulipe gharama. Hata hivyo, gharama hii hailipwi bure—unafidiwa. Watu hufikiri kila mara kuwa Mungu huchukua tu aina ya mtazamo kwao, kuwa Hafanyi chochote, lakini Yeye tu hukaa mahali pamoja kila wakati, Akichunguza na kutazama. Hivi ndivyo ilivyo kweli? La, sivyo. Mungu ni kama mzazi kwa mwanadamu. Unawasikiliza wazazi wako, unakuwa na tabia njema, unatekeleza wajibu wako mzuri, na unateseka sana kutembea katika njia sahihi. Kwa hiyo hilo huwafanya wazazi wako kuhisi vipi? Mioyo yao huvunjika kwa upendo, na wangetoa maisha yao kwa ajili yako ili kupunguza kuteseka kwako, kukufanya ule vyema, uvae nguo nzuri na ujifurahishe. Hawataki uteseke kutokana na umaskini wowote. Huu ndio moyo walio nao wazazi wako. Na ikilinganishwa na hii, moyo wa Mungu unaweza kuwa hata mwema zaidi, wa kupendeza zaidi, mzuri zaidi. Moyo wa Mungu hauwezi kuwa chini ya hii. Kuhusu kikundi chenu cha umri, je, hamuwezi kushukuru kwa ajili ya baadhi ya vitu vingine vizuri ambavyo wazazi wenu huwafanyia? Kwa hiyo zaidi ya yote, tumia utunzaji wa wazazi wako kwako kuushukuru moyo wa Mungu. Kwa mfano wakati wewe ni mgonjwa na unalala kitandani, wazazi wako huhisi vipi? Hawahisi kwenda kazini, na iwapo huwezi kula pia wao hawawezi. Kabla ya wewe kuweza kutembea au kutambaa, walikushikilia kila usiku. Wakati ambapo hungeweza kula hata chembe cha chakula, walikulisha kutoka kwa kinywa chao wenyewe; hii ndiyo aina ya moyo walio nao. Ulipokua na kuweza kutembea, kila wakati walikuwa wakiogopa kwamba ungegongwa na vitu. Ulipofanya hivyo, mioyo yao ilivunjika kwa upendo, na wangekusugua pale ulipogongwa na kupigapiga sakafu na kukubembeleza. Iwapo ulilia, mioyo yao ilivunjika. Iwapo uliteseka kutokana na kosa lolote, wangekuwa tayari mara moja kupigana vita vyako. Unapokua na wanakuona ukiteseka, au wakuone ukiwa umechoka kutoka kazini, wako na hamu ya kukaa na wewe siku yote, bila kula au kunywa chochote wao wenyewe, kuwa karibu na wewe na kukupikia, kufua nguo zako, kukutumikia, kuwa mjakazi wako, kutuliza mateso yako, na hata kutamani kuwa wangeteseka kwa niaba yako; huu ndio moyo walio nao. Na iwapo wazazi wanaweza kuwa hivi kwa watoto wao, basi Mungu anaweza kuwa zaidi vipi kwa wanadamu? Mungu anaweza tu kuwa mkubwa zaidi, halisi zaidi. Hawezi kuwa chini ya jinsi wazazi walivyo kwa watoto wao, kwani kwa kawaida kutakuwa na vitu kwa watu ambavyo watu wengine hawawezi kuvishughulikia, ilhali Mungu hushughulikia watu kwa kila njia iwezekanayo. Wazazi wako walikuzaa na hukuchukulia kama mwili na damu yao wenyewe. Wanakupenda, wanakutunza na kukulinda sana. Kwa hiyo Niambie, mwanadamu ni nani kwa Mungu, kama mwanadamu aliumbwa kwa mikono Yake Mwenyewe? Mtu ni mwili na damu ya Mungu Mwenyewe. Ingawa si kama hali ya mtu pale ambapo watoto wameunganishwa na wazazi wao kupitia kuzaliwa kwa mwili na damu na kwamba Mungu hutumia mkono Wake kumuumba mwanadamu, ni kwamba Mungu anapumua pumzi Yake ndani ya mwanadamu, na Anaweka matarajio Yake kwa mwanadamu. Hili ni kusema, mwanadamu amepewa matumaini ya Mungu, Mungu ana matakwa kwa mwanadamu na Huweka imani Yake kwake. Sio suala rahisi sana kwa kuwa Mungu anamuumba mwanadamu na kupumua pumzi Yake ndani ya mwanadamu, na kwa hali yoyote Mungu ni Mwenye uwezo sana, kwa hiyo iwapo Hakutaka wanadamu hawa, basi Angeumba wengine tu. Baada ya kuwaumba wanadamu, Aliwaweka katika moyo Wake. Wanadamu ni nyama na damu Yake na ni wenza Wake; pia wao ndio walioaminiwa na wanaobeba matumaini yote ya Mungu katika mpango Wake wa usimamizi, na mwishowe Anataka kuona matumaini na kupata matokeo kutoka kwa wanadamu. Kwa kuzingatia dhana hii, jaribuni kuthamini matakwa na mapenzi ya Mungu, na basi hamtakuwa na kuthamini kwa kina zaidi)? Hebu tuchukue mfano. Ili kumweka mtoto wao shuleni na kujipatia sifa, mtoto wao anaposoma, wazazi wako hapo kando yake wakimfukuta, kisha kumpa shira, kisha faluda ya mayai iliyotiwa mvuke, kisha kukwaruza mwasho wake, kisha kuwakanda. Hawajui cha kufanya kwa matokeo bora. Mioyo yao huwa naye kila wakati, na ulimwengu wao humzunguka. Ulimwengu wa wazazi wako hukuzunguka, na je, hawaweki matarajio kwako na kukuamini na matumaini yao? Iwapo huwasikilizi na huwatii kila wakati, je, hawahuzuniki? Je, hawasikitiki? Hivyo basi, kwa kutumia wazo hili, fikiria kuhusu moyo wa Mungu. Mungu huona wanadamu na, haijalishi jinsi ulivyo mzee, nyote ni watoto machoni pa Mungu. Unasema una miaka 80 na Mungu anasema wewe bado ni mtoto. Unasema una miaka 20 na Mungu anasema wewe hata ni mtoto zaidi. Mungu hatofautishi kati ya umri; machoni Pake wanadamu wote ni wachanga, wote ni watoto, na hivi ndivyo Yeye huwachukulia wanadamu. Kwa hivyo, machoni pake, wewe ni mwili na damu Yake, mwenzi Wake. Kwa hiyo unawezaje kustahili kuwa mwili na damu Yake, mwenza Wake, muwe watu wanaopendeza roho Yake na kumridhisha? Je, hili si swali ambalo wanadamu wanastahili kulizingatia na kulitafakari?
Mungu huchukulia wanadamu kuwa mwili na damu Yake, kama wenza Wake, kama wanaobeba gharama iliyo na uchungu ambayo Mungu hulipa, hivyo Mungu ana moyo wa aina gani? Mungu ana hali gani ya akili na Mungu ana aina gani ya mtazamo kwa watu hawa ili Aweze kuwa na kiwango hiki cha uhusiano nao? Mungu ana moyo gani Anapokuwa na kiwango hiki cha uhusiano? Je, watu wanaweza kuuthamini kikamilifu? Mtu anaweza kusema, “Sijamuona Mungu, na siwezi nikatambua chochote ambacho Mungu amenifanyia katika maisha yangu machache yaliyopita.” Lakini unaishi sasa, kwa hiyo unaweza kutambua mwongozo wa Mungu na gharama Anayokulipia sasa? Unaweza kuelewa hili? (Ndio.) Ni sawa iwapo unaweza kuelewa hili, na hili linathibitisha kuwa wewe si mjinga. Inatosha kuweza kuyaelewa haya yote, na inastahili kabisa kuacha kila kitu na kumfuata Mungu.

Jumatano, 20 Desemba 2017

Katika Imani Yako kwa Mungu Unapaswa Kumtii Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu,

Katika Imani Yako kwa Mungu Unapaswa Kumtii Mungu

Mwenyezi Mungu alisema, Kwa nini unamwamini Mungu? Watu wengi wanafadhaishwa na swali hili. Siku zote wana mitazamo tofauti kuhusu Mungu wa vitendo na Mungu wa mbinguni, jambo linaloonyesha kwamba wanamwamini Mungu sio ili wamtii, bali kupata manufaa fulani, au kuepuka mateso ya janga. Wakati huo tu ndipo wanakuwa watii kwa kiasi fulani, lakini utii wao ni wa masharti, ni kwa ajili ya matarajio yao wenyewe, na kushinikiziwa. Hivyo: kwa nini unamwamini Mungu? Ikiwa ni kwa ajili ya matarajio yako tu, na majaliwa yako, basi ni bora zaidi usingeamini. Imani kama hii ni kujidanganya, kujihakikishia, na kujishukuru. Kama imani yako haijajengwa katika msingi wa utii kwa Mungu, basi hatimaye utaadhibiwa kwa kumpinga Mungu.