Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Muziki wa Akapela "Tokeo Lililofikiwa kwa Kumjua Mungu" (Video Rasmi ya Muziki)

Hayuko katika upeo wa mbali, wala hajajificha juu mawinguni. Yuko kando yako, akiwa na mamlaka juu ya kila kitu chako, Yeye ni kila kitu ulicho nacho, na Yeye ni kitu pekee ulicho nacho.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Jumamosi, 2 Juni 2018

Kanisa la Mwenyezi Mungu | "Kuona Ni Kuamini" Haipaswi Kuaminiwa

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu | "Kuona Ni Kuamini" Haipaswi Kuaminiwa

                          Mji wa Zhengzhou, Mkoa wa Henan
Awali, nilipokuwa nikisikia watu wakitoa maoni juu ya kitu fulani, mara nyingi wangesema "kuona ni kuamini." Muda ulivyoendelea kupita, pia nilichukua huu kama msingi wa kuangalia mambo, na ilikuwa vivyo hivyo kuhusu maneno ya Mungu. Matokeo yake ni kwamba niliishia kutoweza kuamini maneno mengi ya Mungu ambayo hayakuwa yametimizwa. Kama wakati wangu uliotumiwa kumwamini Mungu ulipoongezeka, niliona maneno ya Mungu kwa viwango tofauti vya kutimizwa , nikaona ukweli wa mafanikio ya maneno ya Mungu na sikuwa tena na shaka juu ya chochote ambacho Mungu alisema. Nilidhani hii ilikuwa mimi kuwa na ufahamu kiasi wa uaminifu wa Mungu, na kwamba niliweza kuamini kwamba kila kitu ambacho Mungu alisema kilikuwa halisi.

Ijumaa, 1 Juni 2018

10. Usitafute Mbinu Mpya Unapomtumikia Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Kanisa

10. Usitafute Mbinu Mpya Unapomtumikia Mungu

Heyi   Mji wa Zhuanghe, Mkoa wa Liaoning
Nilikuwa nimepandishwa cheo tu kuchukua jukumu la kiongozi wa kanisa. Lakini baada ya kipindi cha kazi ngumu, sio tu kuwa kazi ya kiinjili ilikuwa bila uhai kiasi, lakini ndugu zangu wa kiume na wa kike katika timu ya kiinjili walikuwa pia wakiishi katika hali hasi na ya udhaifu. Nikiwa nimekabiliwa na hali hii, sikuweza tena kudhibiti hisia zangu. Ni vipi tena ningeweza kuiamsha kazi ya kiinjili? Baada ya kupiga ubongo wangu, hatimaye nilifikiria suluhisho zuri: Kama ningefanya sherehe ya kila mwezi kwa timu ya kiinjili na kuwachagua watu waliojipambanua na wahubiri wa kielelezo, yeyote ambaye angeshinda roho zaidi kwa ajili ya Mungu angepewa thawabu, na yeyote ambaye angeshinda roho chache angeonywa. Hili halingeisisimua shauku yao tu, lakini lingewainua ndugu wa kike na wa kiume waliokuwa hasi na dhaifu. Nilipofikiria hili, nilifurahishwa sana na hili "tendo langu la werevu". Niliwaza "Wakati huu kwa kweli nitamshangaza kila mtu."

Alhamisi, 31 Mei 2018

32. Kila Neno la Mungu ni Maonyesho ya Tabia Yake

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki

32. Kila Neno la Mungu ni Maonyesho ya Tabia Yake

Wakati wowote nilipoona maneno haya yaliyosemwa na Mungunilihisi kuwa na wasiwasi: “Kila sentensi Niliyoizungumza inaendeleza tabia ya Mungu. Mngefanya vizuri zaidi endapo mngetafakari kuhusu maneno Yangu kwa umakini, na kwa kweli mtafaidi pakubwa kutoka katika maneno haya.” Nilihisi kuwa na wasiwasi kwa sababu kuelewa tabia ya Mungu ni muhimu sana yote kwa ufahamu wa mwanadamu wa Mungu na kutafuta kumpenda na kumridhisha Yeye.

Umeme wa Mashariki | 38. Siri Niliyoishikilia kwa Kina Ndani ya Moyo Wangu


Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mungu

Umeme wa Mashariki | 38. Siri Niliyoishikilia kwa Kina Ndani ya Moyo Wangu

Wuzhi    Mji wa Linyi, Mkoa wa Shandong
Katika majira ya kuchipua ya mwaka wa 2006, nilinyang'anywa cheo changu kama kiongozi na nikarudishwa nilikotoka kwa sababu nilifikiriwa kuwa "bwana ndiyo" sana. Niliporejea mara ya kwanza, nilitumbukia ndani ya kikalibu cha mateso na maumivu makubwa. Sikuwahi kufikiri kwamba baada ya miaka mingi ya uongozi mambo yangeharibika kwa sababu ya kuwa "bwana ndiyo." Huu ulikuwa ndio mwisho kwangu, nilidhani, kila mtu aliyenijua angejua juu ya kushindwa kwangu na ningefanywa kama mfano mbaya katika kanisa. Ningewezaje kukabiliana na wengine baada ya haya yote?

Jumatano, 30 Mei 2018

Umeme wa Mashariki | Kuna Furaha Kubwa Katika Uaminifu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, ukweli


Umeme wa Mashariki
| Kuna Furaha Kubwa Katika Uaminifu

Gan'en    Mji wa Hefei, Mkoa wa Anhui
Katika maisha yangu, siku zote nimeongozwa na msemo, "Mtu hapaswi kuwa na moyo wa kuwadhuru wengine, lakini lazima awe macho ili asidhuriwe" katika uingiliano wa kijamii. Kamwe huwa siwaridhii wengine imani yangu kwa urahisi. Daima nimehisi kuwa katika hali ambapo hujui nia za kweli ya mtu, hupaswi kuonyesha nia yako punde sana. Kwa hiyo, inatosha kuweka mtazamo wa amani—kwa njia hii unajilinda na utafikiriwa na wenzako wa rika kama "mtu mzuri."

Jumanne, 29 Mei 2018

Kanisa la Mwenyezi Mungu | 52. Jitiishe Mwenyewe ili Kufundisha Wengine Nidhamu

Kanisa-la-Mwenyezi-Mungu, ndugu-na-dada, ushuhuda

Kanisa la Mwenyezi Mungu | 52. Jitiishe Mwenyewe ili Kufundisha Wengine NidhamuXiaoyan    Jiji la Xinyang, Mkoa wa Henan

Nilikuwa na ubia wa kazi wa karibu na dada mmoja mzee katika masuala ya jumla. Baada ya kufanya kazi naye kwa muda fulani, nikamwona kuwa mzembe katika kazi yake na kwamba hakukubali ukweli. Kikwelikweli, nilikata kauli kumhusu. Hatua kwa hatua, uhusiano wa kawaida kati yetu ulipotea, hatukuweza kupatana vizuri, na hatukuweza kuwa mbia katika kazi. Nilihisi kuwa lilikuwa ni kosa lake hasa kwamba uhusiano wetu ulifikia kiwango hiki, na hivyo nilijaribu kufikiria njia za aina zote za kuzungumza naye ili apate kujijua. Lakini majaribu yangu yote ya kuzungumza naye yalikuwa bure au hata kuwa na athari za mkabala. Hatimaye tukaachana, kama masuala yetu hayajatatuliwa. Hili lilinifanya kuamini hata zaidi kuwa hakuwa mtu ambaye hukubali ukweli. Baada ya hapo, kanisa lilinipangia kukaa na familia mwenyeji tofauti. Baada ya muda mfupi, niligundua matatizo mengi pia yalikuwa na ndugu wa kiume na wa kike wa familia mwenyeji, na mimi tena "nikajitahidi" kuwasiliana nao, lakini jitihada zangu zote hazikufaa, na wakaanza kuwa na chuki dhidi yangu. Nikiwa nimekabiliwa na hali hizi, nilikuwa na wasiwasi sana na kukanganyika: Mbona wYesuatu ninaokutana nao hawakubali ukweli? Mpaka siku moja, nikapata chanzo cha tatizo wakati nilipotatizika kazini.

Jumapili, 27 Mei 2018

Ni Muhimu Sana Kuanzisha Uhusiano wa Kufaa na Mungu

Ni Muhimu Sana Kuanzisha Uhusiano wa Kufaa na Mung


Watu wanaamini katika Mungu, wanampenda Mungu, na kumkidhi Mungu kwa kugusa Roho wa Mungu kwa moyo wao, hivyo kupata ridhaa ya Mungu; na wakati wanajihusisha na maneno ya Mungu kwa moyo wao, kwa hivyo wanasisimuliwa na Roho wa Mungu. Ikiwa unataka kufikia maisha ya kawaida ya kiroho na kuanzisha uhusiano wa kawaida na Mungu, lazima kwanza uutoe moyo wako kwa Mungu, na uuweke moyo wako uwe mtulivu mbele za Mungu. Baada tu ya kuutoa moyo wako mzima katika Mungu ndipo utaweza kuwa na maisha ya kawaida ya kiroho hatua kwa hatua. Kama, kwa imani yao katika Mungu, watu hawautoi moyo wao kwa Mungu, ikiwa moyo wao hauko katika Mungu, na wala hawauchukulii mzigo wa Mungu kama wao wenyewe, basi kila kitu wanachofanya ni kumdanganya Mungu, nayo ni matendo ya watu wa kidini, wasioweza kuipokea sifa ya Mungu. Mungu hawezi kupata kitu chochote kutoka kwa aina hii ya mtu; aina hii ya mtu anaweza tu kutumika kama foili[a] kwa kazi ya Mungu, kama pambo katika nyumba ya Mungu, kuchukua nafasi, naye hana manufaa—Mungu hamtumii aina hii ya mtu.

Umeme wa Mashariki 56. Filosofia ya Shetani Inanasa na Kuharibu


Umeme wa Mashariki 56. Filosofia ya Shetani Inanasa na Kuharibu


Wu You    Mji wa Hechi, Mkoa wa Guangxi
Wakati fulani uliopita, kanisa lilinipangia kuishi na familia mwenyeji kwa sababu za kazi. Wakati nilipofanya ushirika kwanza na ndugu wa kiume na wa kike wa familia hii mwenyeji, walisema, "Tunaogopa sana kuomba katika ushirika. Tunajua cha kusema tunaposali peke yetu, lakini linapokuja suala la kuomba wakati wa ushirika, hatujui hasa cha kusema." Niliposikia hili, nilijiwazia, "Tusiposali wakati wa ushirika hatutaweza kupokea kazi ya Roho Mtakatifu, na mawasiliano hayatakuwa na ufanisi. Ni lazima tuombe!" Lakini hata hivyo nikafikiria tena, nikifikiri kuwa kama kwa kweli waliogopa kuomba, si wangetunga maoni kunihusu kama ningesisitiza kwamba waombe? Ili kutimiza wajibu wangu katika kuhariri makala, ningehitaji kukaa na familia mwenyeji kwa muda mrefu. Na je kama wangetunga maoni kunihusu na hawakutaka kunikaribisha kwa sababu sikukubaliana na matakwa yao? Nadhani ni lazima nikubaliane na matakwa yao.

Jumamosi, 26 Mei 2018

Kanisa la Mwenyezi Mungu | 55. Njia ya Pekee ya Kuepuka Maafa

55. Njia ya Pekee ya Kuepuka Maafa




Kanisa la Mwenyezi Mungu, Biblia, neema
Chaotuo    Mji wa Xiaogan, Mkoa wa Hubei
Tangu tetemeko la ardhi la Sichuan, daima nimekuwa na hofu na wasiwasi kwamba siku moja huenda nikakumbwa na maafa. Hasa kwa vile nimeona maafa yakiongezeka, na matetemeko ya ardhi yakiwa ya mara kwa mara, hofu yangu ya maangamizi imekuwa hata wazi zaidi. Matokeo yake ni kuwa, mimi hutumia siku nzima nikitafakari ni tahadhari gani ambazo napaswa kuchukua ili kujilinda iwapo tetemeko la ardhi litazuka.

Umeme wa Mashariki | 58. Wivu, Ugonjwa Sugu Wa Kiroho

58. Wivu, Ugonjwa Sugu Wa Kiroho

Kanisa la Mwenyezi Mungu, siku za mwisho, hukumu
He Jiejing    Jiji la Hezhou, Mkoa wa Guangxi
Dada mmoja na mimi tuliunganishwa ili tusahihishe makala pamoja. Tulipokuwa tukikutana, nilitambua kuwa haikujalisha kama ilikuwa ni kuimba, kucheza ngoma, kupokea neno la Mungu, au kuwasiliana ukweli, huyu dada alikuwabora kuniliko katika kila kipengele. Ndugu wa kiume na wa kike wa familia mwenyeji wote walimpenda na wangezungumza naye. Kwa sababu ya hili, moyo wangu ulikuwa na wasiwasi sana na nilihisi kama nilikosa kuthaminiwa—hata kufikia kiasi kwamba nilifikiri kuwa mradi alikuwa huko, hakukuwa na nafasi yangu. Moyoni mwangu nilianza kuhisi kuchoshwa naye na kutotaka kuandamana naye katika kutimiza wajibu wetu. Nilitumaini kwamba angeondoka ili kwamba ndugu wa kiume na wa kike wangenipenda na kuniheshimu sana.
Siku moja, kiongozi alituzuru. Huyu dada aliomba kuhamishiwa kwa kazi tofauti kwa sababu ya usafishwaji wa jazba aliokuwa akiupitia ambao ulikuwa ukifanya hali yake kuwa hasi. Baada ya kusikia akisema hivi, nikawa na msisimko mno. Niliwaza: Nilikuwa nikitumaini daima ya kwamba ungeenda. Ukienda, basi nitayaondokea mashaka yangu. Kwa hiyo, nilikuwa na shauku ya kiongozi huyu kumpa kazi nyingine mara moja. Hata hivyo, mambo yaliniendea kinyume na matarajio na kiongozi hakukosa tu kumpa kazi mpya, lakini kwa uvumilivu aliwasiliana naye ukweli na kumsaidia kubadilisha hali yake. Nilipoona hayo, nilihisi kuwa na wasiwasi hasa, na nikatumaini hata zaidi kuwa huyu dada angeondoka. Nikafikiri: Ni lini nitaweza kuyaondokea mashaka haya kama haendi wakati huu? Hapana, ni lazima nifikirie njia ya kumfanya aondoke haraka. Kwa hiyo, nilitumia fursa wakati huyu dada hakuwepo ili kumpa kiongozi maelezo zaidi, nikisema: "Mara nyingi yeye huwa na usafishwaji wa jazba ambao humzuia kulenga kusahihisha makala. Sasa amepoteza kazi ya Roho Mtakatifu na hawezi kusahihisha makala. Tayari imeathiri kazi ya kanisa ya kuhariri na kukusanya makala. Ni heri umpe kazi mpya. Dada X ni bora kwa kuandika makala, unaweza kumchagua kusahihiisha makala hayo. Anaweza kuwa na thamani bora ya kukuza kuliko dada niliyewekwa naye." Mara tu nilipomaliza kusema hili, neno la Mungu liliingia ndani yangu likinishutumu: “Wanadamu dhalimu, wakatili! Kufumba macho na kula njama, kusukumana, kung’ang’ania sifa na mali, kuuana—haya yote yataisha lini? Mungu Amezungumza maelfu na mamia ya maneno, ilhali hakuna hata mmoja ambaye amejifahamu. … Ni wangapi wasiobagua na kuonea wengine wakiwa na nia ya kudumisha hali yao?” (“Waovu Lazima Waadhibiwe” katika Neno Laonekana katika Mwili). Katika kukabiliana na maneno ya hukumu ya Mungu, nilihisi kama Mungu alikuwa akinikaripia kwa ukali uso kwauso. Kwa ghafla nilianza kutetemeka kwa hofu na sikuweza kujizuia kuhisi woga kwamaneno ambayo nilikuwa tu nimeyasema. Si mimi ni kama watu wanaofichuliwa na neno la Mungu ambao “kuonea wengine wakiwa na nia ya kudumisha hali yao”? Nilipoona kwamba dada niliyekuwa nikifanya kazi naye alikuwa bora zaidi kuniliko katika kila kipengele na kwamba ndugu wa kiume na wa kike wote walimpenda, nilikuwa na wivu moyoni mwangu. Nilikuwa nimechoshwa naye, nikambagua, na kutarajia kuwa angeondoka hivi karibuni ili kwamba ningeyaondokea mashaka yangu. Ili kuwafanya ndugu wa kiume na wa kike kunisikiliza ili kwamba ningejisikia kama nilikuwa na hadhi nikiwa nao, nilitumia hali mbaya ya dada huyu kwa manufaa yangu na kumsengenya kwa kiongozi kwakisingizio cha kulinda maslahi ya kanisa. Lilikuwa jaribio langu la bure la kutumia kiongozi kumwondoa yule dada kabisa. Mwenendo wangu ulifunua kabisa sura yangu ya kweli na kufichua kwamba nilikuwa nyoka muovu na mwenye nia mbaya, kwamba kweli nilikuwa mtoto wa joka kubwa jekundu! Ili kubuni udikteta, joka kubwa jekundu hutumia njia yoyote muhimu ili kuwaondoa wapinzani kabisa. Ili kuwa kiini cha ndugu zangu wa kiume na wa kike na kuwafanya watake kuwa karibu nami, kwa hila niliwaondoa kabisa wale ambao hawakuwa na faida kwangu. Joka kubwa jekundu lina wivu kwa wale walio wakubwa kuliliko na huwaangamiza wale wenye malengo mema. Mimi pia nilikuwa na wivu kwa dada huyu kwa sababu alikuwa bora zaidi kuniliko katika kila kipengele na nilitumia mbinu za kusikitisha kumwondoa kabisa. Joka kubwa jekundu huwahukumu na kuwaua watu kwamatilaba yake mwenyewe. Ili kupata matilaba yangu mwenyewe, kwa makusudi nilitia chumvi mambo kumhusu dada huyu. Mwenendo wangu ulikuwa sawa na ule wa joka kubwa jekundu; nilikuwa tu mwenye kiburi, mwovu, na mbaya mno. Kanisa lilikuwa limetupangia kufanya kazi pamoja ili tuweze kusaidia na kuauniana, ili tuweze kufanya kazi nzuri kwa moyo na akili moja ili kumpendeza Mungu. Ilikuwapia ili tuweze kutumia nguvu zetu ili kufidia udhaifu wa mwingine ili tuweze kuelewana kupata ukweli zaidi na kubadilisha tabia yetu. Lakini sikuwa na ufahamu wamapenzi ya Mungu hata kwa kiwango kidogo. Nilipoona huyu dada alikuwa katika hali mbaya, sio tu kuwa sikutegemea upendo kumsaidia, lakini pia nilitarajia abadilishwe kwa haraka ili kuilinda nafasi yangu. Mimi kwa kweli ni mbaya sana. Tabia yangu imeharibiwa sana. Sikuwa na upendo ambao mtu wa kawaida anapaswakuwa nao. Nilikuwa nimepoteza ubinadamu wangu kabisa kiasi kwamba ningetumia njia yoyote ili kufanikisha malengo yangu mwenyewe. Kama sitaharakisha na kutubu, ni lazima hatimaye niangamizwe pamoja na joka kubwa jekundu.
Asante Mungu! Hukumu Yako na kuadibu vimeniamsha wakati ufaao kunifanya nione kwamba mwenendo wangu ulikuwa sawa na ule wa joka kubwa jekundu na kwamba mimi kwa kweli ni mtoto wa joka kubwa jekundu kwa jina na kwa vitendo. Hili limenisababisha niidharau asili ya Shetani ambayo iko ndani yangu. Kuanzia wakati huu kwendelea, nitageuka kutoka kwa asili ya Shetani iliyo ndani yangu. Sitajipignia mwenyewe tena. Natumaini kufanya kazi vyema na dada huyu ili kutimiza wajibu wetu na kumridhisha Mungu. Nitakuwa tayari zaidi kutafuta ukweli na kutupa sumu ya joka kubwa jekundu, na hivyo kuishi kama mtu halisi ili kumfariji Mungu!
kutoka kwa Ushuhuda wa Kuipitia Hukumu ya Kristo
Soma Zaidi: Kujua Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?

1. Mwenyezi Mungu Amenipa Fursa ya Pili Katika Maisha

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mungu


1. Mwenyezi Mungu Amenipa Fursa ya Pili Katika Maisha

Agosti 15, 2012Ndugu wawili wa kawaida, Beijing
 Julai 21, mwaka wa 2012 ilikuwa siku isiyosahaulika sana kwangu, pamoja na kuwa siku muhimu zaidi ya maisha yangu.
   Siku hiyo, mvua kubwa ilikuwa ikinyesha katika Wilaya ya Fangshan jijini Beijing—ilikuwa kubwa kuliko yoyote iliyowahi kuonekana pale katika miaka sitini na mmoja. Muda mfupi baada ya saa 10 jioni, nilitoka nje mtaani ili kuangalia na nikaona kuwa maji yalikuwa kila mahali. Gari la familia yetu lilikuwa tayari limeelea, na sababu ya pekee gari hilo kutosombwa na mkondo wa maji ilikuwa kwamba lilizuiwa na kitu mbele yake kilicholizuia kusonga.

Ijumaa, 25 Mei 2018

4. Bila Ya Wokovu wa Mungu, Singeweza Kuwa Hapa Leo

4. Bila Ya Wokovu wa Mungu, Singeweza Kuwa Hapa Leo

Kanisa la Mwenyezi Mungu, maombi, wokovu
Zhang Jin, Beijing
Agosti 16, 2012
   Mimi ni dada mzee mwenye miguu miwili yenye kasoro. Hata wakati hali ya hewa ni nzuri nje, nina shida kutembea, lakini wakati maji ya mafuriko yalipokuwa karibu kunimeza, Mungu aliniruhusu kutoroka hatari kimiujiza.