Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Muziki wa Akapela "Tokeo Lililofikiwa kwa Kumjua Mungu" (Video Rasmi ya Muziki)

Hayuko katika upeo wa mbali, wala hajajificha juu mawinguni. Yuko kando yako, akiwa na mamlaka juu ya kila kitu chako, Yeye ni kila kitu ulicho nacho, na Yeye ni kitu pekee ulicho nacho.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Jumanne, 20 Machi 2018

Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee X

Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee X

Jinsi Mungu Anavyotawala na Kuongoza Ulimwengu wa Kiroho

Mwenyezi Mungu alisema, Kwa ulimwengu yakinifu, watu wakikosa kuelewa vitu au jambo fulani, wanaweza kutafuta taarifa mwafaka, vinginevyo wanaweza kutumia njia mbalimbali kubaini asili ya habari kuvihusu. Lakini inapokuja kwa ulimwengu huu mwingine ambao tunauzungumzia leo—ulimwengu wa kiroho ulio nje ya ulimwengu yakinifu—watu hawana hasa mbinu au njia za kujifunzia chochote kuuhusu. Mbona Ninasema hivi? Kwa sababu, katika ulimwengu wa mwanadamu, kila kitu cha ulimwengu yakinifu hakijitengi na uwepo wa kimwili wa mwanadamu, na kwa sababu watu wanahisi kwamba kila kitu katika ulimwengu yakinifu hakitenganishwi na maisha yao ya kimwili na uhai wao wa kimwili, watu wengi wanafahamu tu kuhusu, au kuona, vitu yakinifu mbele ya macho yao, vitu vinavyoonekana kwao.

Jumatatu, 19 Machi 2018

Sura ya 88. Kulipa Gharama ili Kupata Ukweli ni Muhimu Sana

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki

Sura ya 88. Kulipa Gharama ili Kupata Ukweli ni Muhimu Sana

Mwenyezi Mungu alisema, rahisi kwa vijana kuendeleza kazi; wengi wao hawadumishi mwendo. Ni lazima moyo wako uwe mtulivu, lazima uweze kudumisha mwendo na uwe tayari kutumia muda kwake. Wengine hujiburudisha au kuwachezea wengine, lakini wewe unasema, "Siwezi, sina wakati. Biashara yangu ina shughuli sana. Nendeni mkajiburudishe.Ni lazima niipange biashara yangu.” Unaweza tu kufaulu kwa kushughulika na kujitolea kwa biashara yako. Kwa kweli, hukosi nguvu sasa, wala hukosi ujuzi wa kitaalamu. Ili kuboresha hali yako ya kitaaluma, unaweza kufanya baadhi ya utafiti na ujifunze. Ni yapi zaidi, una msingi huu, akili hii, ujuzi huu maalum; unachokosa kwa kweli ni kutumia wakati na nguvu. Vijana hujifunza kidogo kuhusu mambo ya kitaalamu na huelewa baadhi ya ujuzi, hivyo ni rahisi zaidi kwao kufaulu kuliko ilivyo kwa watu wazima? Nchi zinapomchagua raisi, kuna yeyote wa umri wa miaka 20 au 30 ambaye huchaguliwa? (La.) Mbona hivyo? Hawajahitimu vya kutosha katika uwanja wowote. Hawana tajriba ya kutosha, akili zao hazijakomaa, hawaoni mambo kwa upana; mambo kama ujasiri, umaizi, hekima au uwezo bado hayajakomaa. Zaidi ya hayo, kuna sababu kuu kwa nini mambo yako hivyo, watu wakiwa vijana, huwa na msukumo kuhusu mambo mengi. Na sababu nyingine ni kuwa, watu wakiwa vijana, kuna mambo mengi ulimwenguni ambayo bado hawajapitia au kukumbana nayo hapo awali, kwa hivyo mambo mengi yatakuwa yanawatia majaribuni na kuwavutia. Hilo ni kusema, ni vigumu sana kwa vijana kufaulu katika jambo lolote. Haijalishi kile ambacho umesoma, au kile ulichotaalimikia, ni vigumu kufaulu kwa chochote kizuri au muhimu, kuendeleza kazi, na majaribu ni mengi sana. Kwa jumla, watu katika umri wao wa miaka ya 50, 60, 70 au 80 huwa na tajriba nyingi sana za mambo ya ulimwengu na, kwa jumla, mtazamo wao wa ulimwengu uko imara. Wamepitia mambo katika ulimwengu wa nje kama vile ndoa, kushindwa na vikwazo, na aina zote za majaribu na vivutio, na wameyafaulu. Kwa watu wa umri wenu, karibu umri wa miaka 20, kuna mambo mengi sana katika ulimwengu wa nje ambayo ni maajabu kwenu; mnataka kupitia kila kitu, mnahisi kila kitu kikiwa kipya kwenu na mnapenda sana kujua kila kitu. Huna tajriba yake, hivyo daima iko katika akili yako, unahisi kwamba ulimwengu wa nje katika kupumbaza kwake kote sio lazima uwe mbaya hivyo, na sio lazima uwe wa kutisha sana. Hasa, ndani ya mazingira haya katika jamii, watu katika kikundi cha umri wenu hawana uwezo wa kutambua sawasawa mambo wanayosikia na kuona, na hawajui ni mambo yapi ambayo ni majaribu, au ni mambo yapi yatawaletea huzuni au kuwapotoza. Hivyo, kusema kiasi, vijana ni dhaifu sana kuliko watu wazima na wako katika hatari kuu sana. Kuna mambo machache ambayo watu katika kikundi hiki cha umri hufahamu katika mawazo yao, mambo machache ambayo mioyo yao huelewa na ambayo mioyo yao imejiandaa kwayo, na mambo mengi katika ulimwengu huu yako katika kiwango kisichojulikana na hayajulikani kwao, hivyo kuna mambo mengi ambayo kamwe hawawezi kuelewa kabla wawe na tajriba ya au wakumbane nayo, na kamwe hawawezi kujua mambo haya kwa hakika yanahusu nini. Hivyo, iwapo vijana wako katika mazingira ya kawaida, basi wataona ikiwa vigumu sana kusimama imara. Iwapo umeshawishika kwa miaka kadhaa kanisani, katika mazingira haya yaliyo na ukweli, kwa angalau miaka 8 au 10, basi moyo wako utakuwa umetulia na utakuwa umekita mizizi katika familia ya Mungu. Iwapo hutaweza kutuliza moyo wako katika aina hii ya mazingira, hata hivyo, basi utajipata katika shida na hatari kuu.
Kumwamini Mungu na kutekeleza wajibu wako ndiyo njia sahihi katika maisha, ndiyo sahihi kuchagua na, kwa huruma za Mungu, watu wana fursa hii ya kutekeleza wajibu wa binadamu aliyeumbwa. Kwa watu katika umri mchanga kama nyinyi ambao, inaweza kusemwa, mko katika upeo wa ujana wenu, ili kuweza kutekeleza wajibu wenu ni huruma za Mungu, na pia mnajaribu kushirikiana katika kufanya hivi. Lakini iwapo utadhibitiwa na kuzuiliwa kimakosa na baadhi ya masuala madogo, iwapo huwezi kuendelea kutekeleza wajibu wako na suala hili dogo liathiri wajibu wako, au labda lisumbue wajibu wako au hata kuutamatisha wajibu wako—hii haitakuwa aibu? Hii itakuwa sikitiko, aibu. Hivyo, ni lazima muombe pamoja mara kwa mara na mara nyingi kutulia; msifikirie kuhusu matatizo hayo ambayo hayawahusu au yale ambayo hampaswi kuwa mnafikiri kuyahusu sasa, na mfunge vipengele hivyo vya mioyo yenu. Mngali wachanga na wa miaka michache, kwa hivyo msiwe na wasiwasi sana wa kufikiri kuhusu mambo haya. Mambo makubwa maishani sio ndoa tu, kazi na matarajio ya siku sijazo, au kutulia na kuishi kwa amani. Wala kutokuwa na uvumilivu wa kupata nafasi yako katika jamii sio jambo la pekee. Haya sio mambo ya muhimu zaidi. Mambo muhimu zaidi ni yapi? Hapo awali, ndoa na mazishi yalikuwa mambo makubwa; mambo haya ndiyo makubwa sasa? (La.) Mambo makubwa zaidi ni yapi? (Kwanza, muiheshimu imani ya Mungu ndani yetu, na mtekeleze wajibu na shughuli ambazo binadamu aliyeumbwa anapaswa kutekeleza.) Hili ndilo azimio mnalopaswa kuwa nalo. Sasa mnamwamini Mungu na mnatekeleza wajibu wenu, hivyo maisha yenu yameanza kwa mwelekeo ulio sahihi. Hili ni kuu, na ni sahihi. Hivyo,ni nini mnachopaswa kufanya baada ya hili? Je, mnafahamu? (Weka msingi kwa njia ya kuingia katika maisha.) Hili ni sahihi. Weka misingi yako katika njia ya kutafuta ukweli, hakikisha lengo na mwelekeo wa maisha yako, uruhusu ukweli kuweka msingi katika moyo wako na, kwa njia hii, kwa hakika utakuwa mtu ambaye Mungu huchagua, mtu ambaye Mungu amejalia. Ni lazima kwanza muweke misingi. Misingi yenu sasa bado sio imara. Kamwe msijali kuhusu dhoruba, mpulizo kidogo wa upepo unaweza kuwatingisha wakati wowote, hivyo inaweza kusemwa kuwa bado hamjaweka misingi, na hii ni hatari sana. Wekeni lengo lenu la maisha, wekeni mwelekeo ambao mnatafuta, na muweke njia ambayo ni lazima muifuate katika maisha haya. Wekeni lengo hili na jambo kubwa katika maisha, tulieni kwa miaka, na mfanye kazi kwa bidii, tumieni, fanyeni juhudi na mlipe gharama ya suala husika na kwa lengo hili; msifikiri sasa kuhusu jambo lingine lolote. Mbona hampaswi kufikiri kuhusu jambo lingine lolote? Iwapo utaendelea kufikiri kuhusu mambo hayo mengine, basi suala husika halitakuwa jambo lako kuu, badala yake litakuwa la baadaye. Iwapo bado utaendelea kufikiri kuhusu kupata kazi, kupata pesa nyingi, kutajirika, kupata mahali thabiti pa usalama katika jamii, kupata nafasi yako mwenyewe, na pia kufikiri kuhusu kuolewa na kupata mume au mke, haya ni mambo makubwa mangapi? Na kisha unataka kufikiri kuhusu kupata ujuzi na uwezo katika siku sijazo, jinsi ya kuwa mtu aliyejitokeza, na unataka kusaidia na kukuza jamii katika siku zijazo na kuwapa wazazi wako maisha mazuri. Hutakuwa umechoka? Moyo wako ni mkubwa kiasi kipi? Je, mtu huwa na kiwango kipi cha nguvu katika maisha? Watu huwa na nguvu nyingi zaidi katika miaka yao mingapi, na ni miaka mingapi ambayo inaweza kuchukuliwa kuwa miaka yao bora zaidi? Katika maisha mazima ya mtu, wakati rahisi zaidi, wakati ambao nguvu yao husitawi zaidi, ni wakati ambapo wako katika miaka yao ya 20, na zaidi kabisa hadi umri wa miaka 40. Katika wakati huu, ni lazima mfahamu ukweli mnaopaswa kuelewa katika imani yenu kwa Mungu, na kisha muingie katika uhakika wa ukweli, mkubali hukumu na kuadibu kwa Mungu na mkubali kusafishwa na Mungu na majaribu—ni nini ambacho lazima mtimize kwa kufanya hivi? Hamtamkana Mungu hata hali iweje—hili ni la muhimu zaidi; kando na hili, haijalishi kitakachowavuta au kuwaburuta, au iwapo baadaye mtaolewa na kupata mume au mke, hamtakata tamaa kuhusu wajibu wenu na kukata tamaa kuhusu vitu ambavyo mwanadamu aliyeumbwa anapaswa kufanya; na zaidi ya hayo, iwapo wakati fulani katika siku sijazo Mungu hatawataka, bado mtaweza kuutafuta ukweli na kutafuta kutembea kwa njia ya kumcha Mungu na kuepuka uovu. Ni lazima mtie bidii kwa vipengele hivi; iwapo mtafanya hivyo, basi hamtaishi miaka hii bure.
Na baadhi ya watu bado wamechanganyikiwa, wakiota siku yote. Wanasema, "Bado kuna muda mwingi kabla ya kazi ya Mungu kufika mwisho. Ni kawaida kula, kunywa, kuoa na kujitolea katika ndoa, na muwe au msiwe na mimi, haileti utofauti wowote." Ni kweli kwamba haileti utofauti wowote ukiwa au usipokuwa nao. Lakini kuna wakati ambao Mungu humuokoa mwanadamu, na wakati ambao ni wa kazi ya Mungu kufikia kikomo, kuna mtu mmoja tu ambaye anaweza kuokolewa; Yeye anamchukua tu mtu huyo mmoja na kuwaharibu wengine wote—hii ni tabia ya Mungu. Mtu hawezi kuitambua na hawezi kuielewa. Ni watu wangapi walikufa wakati wa Nuhu? Nuhu alikuwa akijenga safina kwa zaidi ya miaka 100, na watu hao wote hawakuwa wametubu. Mwishowe, Mungu alimuokoa Nuhu na familia yake tu ya watu wanane, na baada ya watu hawa wanane kuingia katika safina, ni nini basi kilichotendeka kwa wale wote waliobaki? (Wote waliangamia kabisa.) Wale katika ya wanadamu ambao wameshindwa kuokolewa ni wadudu na mchwa machoni pa Mungu. Huku Mungu akimuokoa mtu, tabia Yake ni yenye huruma, ya kupenda, na ya kuvumilia; lakini kazi ya Mungu ya kumuokoa mtu inapokamilika, Havumilii tena na Yeye huondoa uvumilivu wake, na ni ghadhabu na uadhama wake tu ambayo hubaki. Nyakati hizi mnazoishi sasa kwa kweli ni nyakati nzuri sana. Katika wakati huu ambao kazi ya Mungu ni muhimu zaidi, mko tu katika umri unaofaa, mliweza kuupata na nyote mnaweza kutekeleza wajibu wenu. Haijalishi ni taaluma gani mlizosomea, kile ambacho mmemudu au ni ujuzi upi maalum mlionao, kwa njia ya taaluma zenu wenyewe maalum mumekuja katika nyumba ya Mungu kutekeleza wajibu wenu. Hii ndiyo huruma ya Mungu na ni fursa ambayo haiji kila siku. Matendo ya Mungu hayapendelei yeyote. Ni Mwenye huruma kwako na Hukuruhusu kufurahia baraka hii, sio ili uweze kutosheleza mwili wako na sio ili uweze kuishi maisha ya kutosheka na kutofanya juhudi zozote za kuendelea. Haijalishi ni aina gani ya njia Mungu atakupa, haijalishi jinsi Alivyo mwenye huruma kwako, mwishowe ana mapenzi haya tu, ambayo ni wewe kuelewa ukweli, ili uweze kuyaelewa mapenzi yake na kuelewa ukweli katika mazingira haya ambayo yanafaa kwa ukuaji wako. Maneno ya Mungu na ukweli wa Mungu huletwa kwako na yanakuwa maisha yako, na unaweza kumtii na kumuogopa Mungu. Licha ya umri wako mchanga, azimio lako ni kuu, kama yalivyo maisha yako, shauku lako na moyo wako wa kumuogopa Mungu. Basi hili ni kuu, na Mungu ameridhika. Mungu angesema kuwa huruma Zake kwako si za bure. Mungu huvuna mavuno, huzaa matunda na huona matokeo pamoja na wewe; gharama ambayo Yeye hulipa si bure. Mungu anafurahi na ana raha kuona hilo. Huu ni ukuu na mpango wa Mungu, kwa hiyo ni jambo ambalo mtu anaweza kuchagua?
Gharama ambayo Mungu hulipia kila mmoja wenu haijakuwa tu miongo iliyopita tangu mzaliwe. Haijakuwa miongo hiyo tu. Kama Mungu anavyoona, umekuja katika ulimwengu huu mara nyingi na umepata mwili tena mara nyingi. Je, ni nani anayehusika na suala hili? (Mungu.) Mungu ndiye anayehusika nalo, hivyo unafahamu nini kulihusu? Hujui chochote kulihusu. Kila unapokuja ulimwenguni, Mungu hupanga kila kitu Yeye Mwenyewe. Hupanga miaka utakayoishi, aina ya familia utakayozaliwa ndani, utakapooa na kutulia katika ndoa, utakachofanya ulimwenguni, utakachotegemea kuishi, na Mungu hukufungulia njia ili uweze kukamilisha kazi yako katika maisha haya bila tatizo. Wakati unaofuata unapopewa jukumu ulimwenguni, Mungu hutimiza mipango Yake kwa ajili ya maisha yako kulingana na mipango unayopaswa kuwa nayo na ambayo anapaswa kukutengenezea. Hivi tu, Hukupangia mambo mara nyingi sana na, mwishowe, unazaliwa katika enzi hii ya siku za mwisho na unazaliwa katika aina hii ya familia, na Mungu anakuruhusu uende sambamba na kazi yake, umsikize Akizungumza na kuisikia sauti Yake, na hivyo umeishi hadi sasa. Hujui umekuja ulimwenguni mara ngapi, ni mara ngapi ambapo umbo lako limebadilika, umeishi katika familia ngapi, ni enzi ngapi na ni koo ngapi umepitia. Mkono wa Mungu umekushikilia kila mara na Mungu amekulinda kila mara. Ni kiwango gani cha juhudi ambacho Mungu anapaswa kutumia kwa mtu! Baadhi ya watu husema, "Nina umri wa miaka 60, hivyo Mungu ametumia miaka 60 kwangu, Amenitunza na kunilinda kwa miaka 60 na kudhibiti hatima yangu kwa miaka 60.” Je, hili si jambo la ujinga kusema? Si suala la maisha ya wakati mmoja tu ndio Mungu hudhibiti hatima ya mtu na kumtunza na kumlinda. Iwapo lingekuwa suala la maisha ya wakati mmoja, la kipindi kimoja tu cha maisha, basi Mungu hangekuwa Mungu na hangekuwa na aina hii ya mamlaka au uwezo, na haingesemwa kuwa Mungu hutawalavitu vyote, kuwa hutawala kila kitu. Juhudi ambazo Mungu hufanya na gharama ambayo huwa Anakulipia sio tu kupanga vitu ambavyo unafanya katika maisha haya. Yeye hutenda kwa mwoyo na hutenda kwa kutumia maisha Yake Mwenyewe kama gharama, Akiongoza kila mmoja na kupanga maisha yote ya kila mtu. Hivyo, tukizingatia juhudi ambazo Mungu hufanya na gharama ambayo Yeye hulipa kwa niaba ya mwanadamu, na pia ukweli wote na maisha ambayo Yeye humpa mtu, iwapo watu hawatatimiza wajibu wa mtu aliyeumbwa katika nyakati hizi za mwisho na iwapo hawatamrudia Muumbaji, basi haijalishi ni maisha mangapi au ni enzi ngapi watakazoishi, si wao ndio watakuwa wamepoteza? Je, si watakuwa hawastahili gharama ambayo Mungu huwalipia? Hawastahili kabisa gharama anayowalipia Mungu. Kwa hivyo, katika maisha haya—Sizungumzi kuhusu maisha yoyote yaliyopita, lakini katika maisha haya—iwapo kwa ajili ya kazi yako mwenyewe huwezi kuacha vitu unavyopenda au iwapo huwezi kuacha vitu hivi vya nje—vitu hivi vya raha na maisha ya familia—iwapo huwezi kuacha vitu hivi kwa ajili ya gharama ambayo Mungu hukulipia au kulipa upendo wa Mungu, basi hakuna jambo lolote zuri kukuhusu kabisa! Kwa kweli kila gharama unayolipa inastahili. Ikilinganishwa na gharama ambayo Mungu hulipa kwa niaba yako, kiwango hicho kidogo unachotoa au unachotumia hufikia kiwango kipi? Kuteseka kwako hafifu hufikia kiwango kipi? Je, unajua Mungu ameteseka kwa kiwango kipi? Kuteseka hafifu ambako huwa unavumilia hakufikii kiwango chochote. Zaidi ya hayo, sasa unatimiza wajibu wako na unapata ukweli, hivyo mwishowe ni wewe utakayekuwa umebaki. Wakati huu, haijalishi iwapo utateseka au kulipa gharama, kwa hakika unashirikiana na Mungu, na unafanya chochote ambacho Yeye hukwambia ufanye kwa kuyatii maneno Yake; tenda kulingana na maneno Yake, usimkaidi Mungu, na usifanye chochote kinachomhuzunisha Yeye. Unaposhirikiana na Yeye, ni lazima uteseke kwa kiasi fulani na uache baadhi ya vitu, kuacha na kutoa baadhi ya vitu—kuacha umaarufu na faida, vyeo, mali na raha za dunia, hata ndoa, kazi na matarajio yako ya baadaye ya kilimwengu. Je, Mungu anajua unapoacha vitu hivi? Je, Anaweza kuona? (Ndio.) Na Anapoona hili, Atafanya nini? (Mungu anapendezwa. Mungu anafurahi.) Mungu hachukui tu mtazamo, Yeye huchukua hatua, la sivyo, matakwa Yake kwa mwanadamu hayangekuwa na maana. Yeye hafurahi tu, Akisema, “Gharama Niliyolipa inaonyesha matokeo. Mtu huyu yuko tayari kushirikiana na Mimi na ana azimio hili. Nimempata mtu huyu.” Kama Mungu amefurahi, Ameridhika au Anahisi kufarijika, huwa hachukui tu aina moja ya mtazamo—huwa Anachukua hatua. Huruma za Mungu kwa mwanadamu, upendo Wake kwa mwanadamu, rehema Zake kwa mwanadamu zote sio aina ya mtazamo tu; ni ukweli. Ukweli gani? Mungu huyaweka maneno Yake ndani yako ili uweze kupata nuru dani mwako, ili uweze kuona kupendeza kwa Mungu, ili uweze kuona kabisa jinsi ulimwengu ulivyo, ili moyo wako uweze kuchangamshwa na hivyo uweze kuyaelewa maneno ya Mungu na uelewe ukweli. Basi, si umepata kile ambacho unapaswa kupata? Hii sio tu aina ya mtazamo wa Mungu, ni mtazamo tu? Je, umepata nini? (Ukweli.) Umepata kile ambacho ni cha thamani zaidi. Mungu anapoona kuwa ni vyema, huwa Anachukua mtazamo fulani. Wakati huohuo wa kuchukua mtazamo, Yeye pia Huchukua hatua, kama tu vile watu husema, “Huwezi tu kuchukua mtazamo, ni lazima pia uchukue hatua fulani ya kiutendaji.” Watu husema, "Siutaki. Sitaki chochote. Sitaki chochote cha Mungu." Na Mungu husema, “Haikubaliki. Ni lazima Nikupe zawadi—hiki ndicho unachostahili.” Hivyo unapata faida. Unapata nini? Unapata ukweli, unapata maisha, unapata maarifa ya Muumbaji—basi bado ungali mtupu ndani? Je, hujatajirishwa ndani yako? Na mara unapotajirishwa ndani, basi si unaishi maisha ya thamani?
Ayubu aliomba ng'ombe na kondoo waliokuwa kote milimani, au utajiri mkubwa wa familia? (La.) Aliomba nini? Kumcha Mungu na kujiepusha na uovu. Kulingana na Mungu, Mungu alisema kwamba aliona ni vyema, na basi mwishowe Alifanya nini? Je, Alinena maneno hayo machache tu na kisha huo ukawa mwisho? Mungu alichukua hatua; Alichukua hatua gani? Mungu alimtuma Shetani kumjaribu Ayubu, na kuchukua ng'ombe na kondoo wake waliokuwa kote milimani, mali na vitu vyake, watoto wake na wafanyakazi wake, na haya yalikuwa majaribio ya Mungu kwa Ayubu. Mungu alitaka nini kwa kumfanya Ayubu kupitia majaribio haya? Mungu alitaka ushuhuda wa Ayubu. Na Mungu alimpa Ayubu nini wakati huo? Watu wanafikiri, “Mungu alimpa Ayubu nini wakati huo? Ng'ombe na kondoo wake wote walichukuliwa. Hakumpa Ayubu chochote.” Hapa kuna kitu alichopewa Ayubu, na kulikuwa na zawadi, na bado hakuna anayeweza kuona wazi zawadi ambayo Mungu alimpa Ayubu. Mungu alitaka ushuhuda wa Ayubu hivyo Mungu alimpa Ayubu zawadi ya fursa; Hii ilikuwa fursa gani? Ilikuwa Ayubu awe na ushuhuda wa Mungu mbele ya Shetani na mbele ya wanadamu wote, kuwa shahidi kwa ukweli kwamba Ayubu alimcha Mungu na kujiepusha na uovu, na kuwa shahidi kwamba Ayubu alikuwa mkamilifu na mwaminifu. Hiki ndicho Mungu alimpa Ayubu? Iwapo Mungu hakumpa Ayubu fursa hii, Shetani angethubutu kusonga dhidi yake? Hakika Shetani hangethubutu, na hii ni hakika asilimia 100. Na iwapo Shetani hangethubutu kumjaribu, bado Ayubu angekuwa na fursa hii? Hangekuwa na fursa hii. Hivyo, Mungu alimpa Ayubu aina hii ya fursa ili kuthibitisha kwa umati kuwa njia aliyoifuata Ayubu—njia ya kumcha Mungu na kujiepusha na uovu—ilikuwa njia sahihi, kwamba ilikuwa inakubalika kwa Mungu na kwamba Ayubu alikuwa mtu mwaminifu na mkamilifu. Umati uliona haya yote, Mungu aliona haya, na Ayubu alichukua fursa hii na hakumsikitisha Mungu; alikuwa shahidi wa Mungu, alimpiga Shetani, akamshinda Shetani na Mungu aliona kwamba ilikuwa vyema. Hivyo, mwishowe, Mungu alimpa Ayubu chochote kama zawadi? (Ndio.) Ni nini kilichokuwa zawadi ya pili ya Ayubu kutoka kwa Mungu? Mungu alisema kwamba Ayubu alimcha Mungu na kujiepusha na uovu na alikubaliwa na Mungu, kwamba Ayubu alikuwa shahidi wa Mungu mbele ya Shetani, na kuwa kila alichoamini kilikuwa kizuri, na Mungu alipendezwa na kufurahi, na Alichukua aina hii ya mtazamo. Je, Mungu hakuchukua hatua nyingine zaidi baada ya kuuchukua mtazamo huu? Mungu alifanya nini? Hamkifahamu sana kitabu cha Ayubu. Ni katika hali zipi ambapo Ayubu alisema, “Nimesikia habari zako kwa kusikia kwa masikio: lakini sasa macho yangu yanakuona” (Ayubu 42:5)? (Baada ya Mungu kunena na yeye.) Mungu alinena na yeye na kufichua mgongo Wake kwa Ayubu. Je, hii haikuwa zawadi ya Ayubu kutoka kwa Mungu? Kuna yeyote ambaye alikuwa amewahi kumuona Mungu kabla ya Ayubu? Hakuna aliyekuwa ameiona nafsi halisi ya Mungu hapo awali, ikijumuisha mgongo wa Mungu. Ayubu aliuona mgongo wa Mungu na kuisikia sauti yake, na hiki si kitu ambacho mtu aliyeumbwa hutamani sana kukipata? Ayubu alipata hili, hivyo mnamuonea wivu? (Ndio.) Ni vigumu kupata hili, sivyo? Hivyo ni vipi ambavyo mtu anaweza kupata fursa hii, huruma hii na zawadi hii? Ni lazima uwe na ushuhuda wa Mungu; Ni lazima uwe shahidi wa Mungu miongoni mwa majaribu ya Shetani, ni lazima utembee katika njia ya kumcha Mungu na kujiepusha na uovu na ni lazima usimame mbele za Mungu na umfanye kusema kuwa Anachoona ni chema na umfanye Apendezwe na kufurahi. Anapoona kuwa kila unachofanya ni kizuri na ushuhuda wako ni mzuri, Anaposema umekamilika, kuwa wewe ni mtu anayetafuta ukweli, basi utapata haya yote. Baada ya Ayubu kuuona mgongo wa Yehova, zawadi ya Mungu iliishia pale? Mungu alifanya nini baada ya hayo? Alimbariki Ayubu na mali nyingi zaidi kuliko aliyokuwa nayo hapo mbeleni, sivyo? Hivyo ni kusema, alikuwa mwenye mali kuliko mbeleni. Sema kwanza alikuwa kama milionea, hivyo sasa alikuwa labda zaidi ya bilionea. Unaona, kwa mtu anayemcha Mungu na kujiepusha na uovu, kuwa bilionea ni kitu rahisi kutimiza. Hizi ndizo huruma za Mungu!
Kile ambacho Mungu humpa mwanadamu huzidi kile ambacho anaomba au kutamani, lakini iwapo utapenda kupata zawadi inayozidi unachoomba au kutamani, basi lazima uifuate njia ya Mungu. Sio suala rahisi kuifuata njia ya Mungu—ni lazima ulipe gharama. Hata hivyo, gharama hii hailipwi bure—unafidiwa. Watu hufikiri kila mara kuwa Mungu huchukua tu aina ya mtazamo kwao, kuwa Hafanyi chochote, lakini Yeye tu hukaa mahali pamoja kila wakati, Akichunguza na kutazama. Hivi ndivyo ilivyo kweli? La, sivyo. Mungu ni kama mzazi kwa mwanadamu. Unawasikiliza wazazi wako, unakuwa na tabia njema, unatekeleza wajibu wako mzuri, na unateseka sana kutembea katika njia sahihi. Kwa hiyo hilo huwafanya wazazi wako kuhisi vipi? Mioyo yao huvunjika kwa upendo, na wangetoa maisha yao kwa ajili yako ili kupunguza kuteseka kwako, kukufanya ule vyema, uvae nguo nzuri na ujifurahishe. Hawataki uteseke kutokana na umaskini wowote. Huu ndio moyo walio nao wazazi wako. Na ikilinganishwa na hii, moyo wa Mungu unaweza kuwa hata mwema zaidi, wa kupendeza zaidi, mzuri zaidi. Moyo wa Mungu hauwezi kuwa chini ya hii. Kuhusu kikundi chenu cha umri, je, hamuwezi kushukuru kwa ajili ya baadhi ya vitu vingine vizuri ambavyo wazazi wenu huwafanyia? Kwa hiyo zaidi ya yote, tumia utunzaji wa wazazi wako kwako kuushukuru moyo wa Mungu. Kwa mfano wakati wewe ni mgonjwa na unalala kitandani, wazazi wako huhisi vipi? Hawahisi kwenda kazini, na iwapo huwezi kula pia wao hawawezi. Kabla ya wewe kuweza kutembea au kutambaa, walikushikilia kila usiku. Wakati ambapo hungeweza kula hata chembe cha chakula, walikulisha kutoka kwa kinywa chao wenyewe; hii ndiyo aina ya moyo walio nao. Ulipokua na kuweza kutembea, kila wakati walikuwa wakiogopa kwamba ungegongwa na vitu. Ulipofanya hivyo, mioyo yao ilivunjika kwa upendo, na wangekusugua pale ulipogongwa na kupigapiga sakafu na kukubembeleza. Iwapo ulilia, mioyo yao ilivunjika. Iwapo uliteseka kutokana na kosa lolote, wangekuwa tayari mara moja kupigana vita vyako. Unapokua na wanakuona ukiteseka, au wakuone ukiwa umechoka kutoka kazini, wako na hamu ya kukaa na wewe siku yote, bila kula au kunywa chochote wao wenyewe, kuwa karibu na wewe na kukupikia, kufua nguo zako, kukutumikia, kuwa mjakazi wako, kutuliza mateso yako, na hata kutamani kuwa wangeteseka kwa niaba yako; huu ndio moyo walio nao. Na iwapo wazazi wanaweza kuwa hivi kwa watoto wao, basi Mungu anaweza kuwa zaidi vipi kwa wanadamu? Mungu anaweza tu kuwa mkubwa zaidi, halisi zaidi. Hawezi kuwa chini ya jinsi wazazi walivyo kwa watoto wao, kwani kwa kawaida kutakuwa na vitu kwa watu ambavyo watu wengine hawawezi kuvishughulikia, ilhali Mungu hushughulikia watu kwa kila njia iwezekanayo. Wazazi wako walikuzaa na hukuchukulia kama mwili na damu yao wenyewe. Wanakupenda, wanakutunza na kukulinda sana. Kwa hiyo Niambie, mwanadamu ni nani kwa Mungu, kama mwanadamu aliumbwa kwa mikono Yake Mwenyewe? Mtu ni mwili na damu ya Mungu Mwenyewe. Ingawa si kama hali ya mtu pale ambapo watoto wameunganishwa na wazazi wao kupitia kuzaliwa kwa mwili na damu na kwamba Mungu hutumia mkono Wake kumuumba mwanadamu, ni kwamba Mungu anapumua pumzi Yake ndani ya mwanadamu, na Anaweka matarajio Yake kwa mwanadamu. Hili ni kusema, mwanadamu amepewa matumaini ya Mungu, Mungu ana matakwa kwa mwanadamu na Huweka imani Yake kwake. Sio suala rahisi sana kwa kuwa Mungu anamuumba mwanadamu na kupumua pumzi Yake ndani ya mwanadamu, na kwa hali yoyote Mungu ni Mwenye uwezo sana, kwa hiyo iwapo Hakutaka wanadamu hawa, basi Angeumba wengine tu. Baada ya kuwaumba wanadamu, Aliwaweka katika moyo Wake. Wanadamu ni nyama na damu Yake na ni wenza Wake; pia wao ndio walioaminiwa na wanaobeba matumaini yote ya Mungu katika mpango Wake wa usimamizi, na mwishowe Anataka kuona matumaini na kupata matokeo kutoka kwa wanadamu. Kwa kuzingatia dhana hii, jaribuni kuthamini matakwa na mapenzi ya Mungu, na basi hamtakuwa na kuthamini kwa kina zaidi)? Hebu tuchukue mfano. Ili kumweka mtoto wao shuleni na kujipatia sifa, mtoto wao anaposoma, wazazi wako hapo kando yake wakimfukuta, kisha kumpa shira, kisha faluda ya mayai iliyotiwa mvuke, kisha kukwaruza mwasho wake, kisha kuwakanda. Hawajui cha kufanya kwa matokeo bora. Mioyo yao huwa naye kila wakati, na ulimwengu wao humzunguka. Ulimwengu wa wazazi wako hukuzunguka, na je, hawaweki matarajio kwako na kukuamini na matumaini yao? Iwapo huwasikilizi na huwatii kila wakati, je, hawahuzuniki? Je, hawasikitiki? Hivyo basi, kwa kutumia wazo hili, fikiria kuhusu moyo wa Mungu. Mungu huona wanadamu na, haijalishi jinsi ulivyo mzee, nyote ni watoto machoni pa Mungu. Unasema una miaka 80 na Mungu anasema wewe bado ni mtoto. Unasema una miaka 20 na Mungu anasema wewe hata ni mtoto zaidi. Mungu hatofautishi kati ya umri; machoni Pake wanadamu wote ni wachanga, wote ni watoto, na hivi ndivyo Yeye huwachukulia wanadamu. Kwa hivyo, machoni pake, wewe ni mwili na damu Yake, mwenzi Wake. Kwa hiyo unawezaje kustahili kuwa mwili na damu Yake, mwenza Wake, muwe watu wanaopendeza roho Yake na kumridhisha? Je, hili si swali ambalo wanadamu wanastahili kulizingatia na kulitafakari?
Mungu huchukulia wanadamu kuwa mwili na damu Yake, kama wenza Wake, kama wanaobeba gharama iliyo na uchungu ambayo Mungu hulipa, hivyo Mungu ana moyo wa aina gani? Mungu ana hali gani ya akili na Mungu ana aina gani ya mtazamo kwa watu hawa ili Aweze kuwa na kiwango hiki cha uhusiano nao? Mungu ana moyo gani Anapokuwa na kiwango hiki cha uhusiano? Je, watu wanaweza kuuthamini kikamilifu? Mtu anaweza kusema, “Sijamuona Mungu, na siwezi nikatambua chochote ambacho Mungu amenifanyia katika maisha yangu machache yaliyopita.” Lakini unaishi sasa, kwa hiyo unaweza kutambua mwongozo wa Mungu na gharama Anayokulipia sasa? Unaweza kuelewa hili? (Ndio.) Ni sawa iwapo unaweza kuelewa hili, na hili linathibitisha kuwa wewe si mjinga. Inatosha kuweza kuyaelewa haya yote, na inastahili kabisa kuacha kila kitu na kumfuata Mungu.

Umeme wa Mashariki | Mwokozi Amerudi Tayari Juu ya “Wingu Jeupe”

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki

Umeme wa Mashariki | Mwokozi Amerudi Tayari Juu ya “Wingu Jeupe”

Kwa maelfu kadhaa ya miaka, mwanadamu ametamani kuweza kushuhudia kufika kwa Mwokozi. Mwanadamu ametamani kumtazama Yesu Mwokozi katika wingu jeupe Anaposhuka, yeye binafsi, kati ya wale ambao wamengoja na kumtamani kwa maelfu ya miaka. Mwanadamu ametamani Mwokozi arejee na kuungana na watu, yaani, ili Yesu Mwokozi Arudi kwa watu ambao wamekuwa mbali Naye kwa maelfu ya miaka. Na mwanadamu anatumaini kuwa Atatekeleza tena kazi ya ukombozi Aliyoifanya kati ya Wayahudi, Atakuwa na huruma na mwenye upendo kwa mwanadamu, Atasamehe dhambi za mwanadamu, kuchukua dhambi za mwanadamu, na hata kuchukua makosa yote ya mwanadamu na kumkomboa mwanadamu kutoka kwa dhambi. Wanatamani Yesu Mwokozi Awe Alivyokuwa hapo awali—Mwokozi Ambaye Anapendeka, wa kirafiki na heshima, Asiye na hasira kwa mwanadamu, na Asiyemrudi mwanadamu. Mwokozi huyu Anasamehe na kubeba dhambi zote za mwanadamu, na hata kufa msalabani tena kwa ajili ya mwanadamu. Tangu Yesu Aondoke, wafuasi waliomfuata, na watakatifu wote waliookolewa kwa sababu ya jina Lake, wamekuwa wakimtamani mno na kumngoja. Wale wote waliookolewa na neema ya Yesu Kristo katika Enzi ya Neema wamekuwa wakiitamani siku hiyo ya furaha katika siku za mwisho, wakati ambapo Yesu Mwokozi Anawasili juu ya wingu jeupe na kuonekana kati ya mwanadamu. Bila shaka, haya pia ni mapenzi ya wale wote wanaolikubali jina la Yesu Mwokozi leo. Ulimwenguni kote, wale wote wanaojua kuhusu wokovu wa Yesu Mwokozi wamekuwa wakingoja kwa hamu kurejea ghafla kwa Yesu Kristo, kutimiza maneno ya Yesu Akiwa duniani: “Nitarejea tu jinsi Nilivyoondoka”. Mwanadamu anaamini kuwa, kufuatia kusulubishwa na kufufuka, Yesu Alirudi mbinguni juu ya wingu jeupe, na kuchukua mahali Pake katika mkono wa kulia wa Yule Aliye Juu. Vilevile, mwanadamu anatazamia kuwa Yesu Atashuka, tena juu ya wingu jeupe (wingu hili linarejelea lile wingu ambalo Yesu Alipaa juu yake Aliporudi mbinguni), miongoni mwa wale ambao wamemtamani mno kwa maelfu ya miaka, na kuwa Atachukua mwonekano na mavazi ya Wayahudi. Baada ya kumwonekania mwanadamu, Atafadhili chakula kwa sababu yao, na kufanya maji ya uzima kuwamwagika kwa ajili yao, na Ataishi miongoni mwa wanadamu, Akiwa amejawa na neema na upendo, Akiwa hai na wa hakika. Na mengine. Ilhali Yesu Mwokozi hakufanya haya; Alitenda kinyume cha yale ambayo mwanadamu alikuwa anatazamia. Hakurejea kati ya wale ambao walikuwa wametamani kurejea Kwake, na hakutokea kwa wanadamu wote Akitumia wingu jeupe. Amerejea tayari, lakini mwanadamu hamjui, na kubaki mjinga kuhusu kurejea Kwake. Mwanadamu anamngoja tu bila mwelekeo, bila kujua kuwa ameshuka tayari juu ya wingu jeupe (wingu ambalo ni Roho Yake, maneno Yake, na tabia Yake yote na yale yote ambayo Yeye ni), na sasa yuko kati ya kikundi cha washindi ambacho Atakitengeneza katika siku za mwisho. Mwanadamu hafahamu haya: Ingawa Mwokozi Mtakatifu Yesu Amejawa na upendo na mapenzi kwa mwanadamu, Atafanya kazi vipi katika “hekalu” ambalo limejaa uchafu na roho wasio safi? Ingawa mwanadamu amekuwa akingoja kufika Kwake, Atawaonekania vipi wale wanaokula mwili wa wale wasio na haki, kunywa damu ya wasio na haki, kuvaa mavazi ya wasio na haki, wanaomwamini lakini hawamfahamu, na wanaompokonya kila wakati? Mwanadamu anajua tu kuwa Yesu Mwokozi Amejawa na upendo na huruma, na ni sadaka ya dhambi iliyojawa na ukombozi. Lakini mwanadamu hana habari kwamba Yeye pia ni Mungu Mwenyewe, ambaye Amejawa na haki, utukufu, ghadhabu, na hukumu, na kuwa na mamlaka na kujawa na hadhi. Kwa hivyo ingawa mwanadamu anayo hamu na kutamani kurudi kwa Mkombozi, na hata Mbingu inaguswa na maombi ya mwanadamu, Yesu Mwokozi hawaonekanii wale wanaomwamini ilhali hawamfahamu.
“Yehova” ni jina ambalo Nilichukua wakati wa kazi Yangu kule Uyahudi, na linamaanisha Mungu wa Wayahudi (Wateule wa Mungu) Anayeweza kumhurumia mwanadamu, kumlaani mwanadamu, na kuyaongoza maisha ya mwanadamu. Lina maana Mungu Anayemiliki nguvu kuu na Amejawa na hekima. “Yesu” ni Imanueli, na lina maana sadaka ya dhambi iliyojawa na upendo, Amejawa na huruma, na Anamkomboa mwanadamu. Alifanya kazi ya Enzi ya Neema, na Anawakilisha Enzi ya Neema, na Anaweza tu kuwakilisha sehemu moja tu ya mpango wa usimamizi. Hivyo ni kusema, Yehova pekee ndiye Mungu wa watu wa Uyahudi waliochaguliwa, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, Mungu wa Yakobo, Mungu wa Musa na Mungu wa Wayahudi wote. Na sasa katika enzi hii, Wayahudi wote isipokuwa kabila la Uyahudi wanamwabudu Yehova. Wanatoa kafara Kwake kwa madhabahu, na kumtumikia wakivaa mavazi ya kikuhani hekaluni. Wanachotumainia ni kuonekana tena kwa Yehova. Yesu pekee ndiye Mkombozi wa wanadamu. Yeye ni sadaka ya dhambi ambayo ilimkomboa mwanadamu kutoka kwa dhambi. Ambayo ni kusema, jina la Yesu lilitoka katika Enzi ya Neema, na kuwepo kwa ajili ya kazi ya wokovu katika Enzi ya Neema. Jina la Yesu liliwepo ili kuwezesha watu wa Enzi ya Neema kuzaliwa upya na kuokolewa, na ni jina mahsusi la wokovu wa binadamu wote. Kwa hivyo jina Yesu linawakilisha kazi ya wokovu, na kuashiria Enzi ya Neema. Jina Yehova ni jina mahsusi la Wayahudi walioishi chini ya sheria. Katika kila enzi na kila hatua ya kazi, jina Langu haliwi bila msingi, lakini lina umuhimu wakilishi: Kila jina linawakilisha enzi moja. “Yehova” Anawakilisha Enzi ya Sheria, na ni jina la heshima kwa Mungu Aliyeabudiwa na Wayahudi. “Yesu” Anawakilisha Enzi ya Neema, na ni jina la Mungu wa wale wote waliokombolewa katika Enzi ya Neema. Iwapo mwanadamu bado anatamani kufika kwa Yesu Mwokozi katika siku za mwisho, na bado anatarajia Afike na picha Aliyokuwa nayo kule Uyahudi, basi mpango wote wa usimamizi wa miaka elfu sita ungekoma katika Enzi ya Ukombozi, na usingeweza kuendelea zaidi. Siku za mwisho, hata zaidi, zisingeweza kufika, na enzi isingefikishwa kikomo. Hii ni kwa sababu Yesu Mwokozi ni wa ukombozi na wokovu wa mwanadamu peke yake. Nilichukua jina la Yesu kwa sababu ya watenda dhambi wote katika Enzi ya Neema, na silo jina ambalo nitatumia kuleta wanadamu wote kufika kikomo. Ingawa Yehova, Yesu, na Masiha yote yanawakilisha Roho Wangu, majina haya yanaashiria wakati tofauti katika mpango Wangu wa usimamizi, na hayauwakilishi ukamilifu Wangu. Majina wanayoniita watu duniani hayawezi kueleza tabia Yangu nzima na yote Niliyo. Ni majina tu ambayo Ninaitwa katika enzi tofauti. Kwa hivyo, enzi ya mwisho—enzi ya siku za mwisho—itakapofika, jina langu litabadilika tena. Sitaitwa Yehova, au Yesu, na wala sio Masiha, lakini nitaitwa Mwenyezi Mungu Mwenyewe mwenye nguvu, na chini ya jina hili Nitaleta enzi nzima kufikia tamati. Nilijulikana kama Yehova wakati mmoja. Niliitwa pia Masiha, na watu wakaniita Yesu Mwokozi pia wakati mmoja kwa sababu walinipenda na kuniheshimu. Lakini leo Mimi sio Yehova au Yesu Ambaye watu walimfahamu nyakati zilizopita—Mimi ni Mungu Ambaye Amerejea katika siku za mwisho, Mungu Ambaye ataleta enzi kufika mwisho. Mimi ni Mungu Mwenyewe Ambaye Anainuka katika kingo za dunia, Nimejawa na tabia Yangu nzima, na Nimejawa na mamlaka, heshima na utukufu. Watu hawajawahi kushirikiana na Mimi, hawajawahi kunifahamu, na wamekosa ufahamu kuhusu tabia Yangu. Tangu uumbaji wa dunia hadi leo, hapana hata mtu mmoja ambaye Ameniona. Huyu ni Mungu Ambaye ametokea kwa mwanadamu katika siku za mwisho lakini Amejificha kati ya mwanadamu. Anaishi kati ya mwanadamu, wa kweli na halisi, kama jua iwakayo na moto unaochoma, Aliyejaa nguvu na kujawa mamlaka. Hakuna hata mtu mmoja au kitu ambacho hakitahukumiwa na maneno Yangu, wala mtu hata mmoja au kitu ambacho hakitatakaswa kupitia moto unaowaka. Hatimaye, mataifa yote yatabarikiwa kwa sababu ya maneno Yangu, na pia kupasuliwa kwa vipande kwa sababu ya maneno Yangu. Kwa njia hii, watu wote katika siku za mwisho wataona kuwa Mimi ndiye Mwokozi Aliyerejea, Mimi ndiye Mungu Mwenyezi Ambaye Ninatamalaki juu ya binadamu wote, na Nilikuwa sadaka ya dhambi kwa mwanadamu wakati mmoja, lakini katika siku za mwisho Ninakuwa pia miale ya Jua Linalochoma vitu vyote, na pia Jua la haki Linalofichua vitu vyote. Hivyo ndivyo ilivyo kazi Yangu ya siku za mwisho. Nilichukua jina hili na Ninamiliki tabia hii ili watu wote wapate kuona kuwa Mimi ni Mungu mwenye haki, na Mimi ni jua linachoma, na moto unaowaka. Ni hivyo ili watu wote waniabudu, Mungu pekee wa kweli, na ili waone uso Wangu wa kweli: Mimi sio tu Mungu wa Wayahudi, wala Mimi sio Mkombozi tu—Mimi ni Mungu wa viumbe vyote katika mbingu na dunia na bahari.
Mwokozi Atakapofika katika siku za mwisho, kama Angeitwa Yesu bado, na kuzaliwa mara nyingine Uyahudi, na kufanya kazi Yake Uyahudi, basi hii ingeonyesha kuwa Niliumba Wayahudi peke yao na kuwakomboa Wayahudi peke yao, na kuwa sina uhusiano wowote na Mataifa. Je, hii haitakuwa kinyume cha maneno Yangu kwamba “Mimi ni Bwana Aliyeumba mbingu na nchi na vitu vyote”? Nilitokea Uyahudi kufanya kazi Yangu kati ya Mataifa kwa sababu Mimi sio tu Mungu wa Wayahudi, ila Mungu wa viumbe vyote. Ninaonekana kati ya Mataifa katika siku za mwisho kwa sababu Mimi sio tu Yehova, Mungu wa Wayahudi, lakini, zaidi, kwa sababu Mimi ni Muumba wa wote Niliowachagua kati ya Mataifa. Sikuumba Uyahudi pekee, Misri, na Lebanoni, bali Niliumba pia Mataifa yote mbali na Israeli. Na kwa sababu ya hii, Mimi ni Bwana wa viumbe vyote. Nilitumia tu Uyahudi kama hatua ya kwanza ya kazi Yangu, Nikatumia Uyahudi na Galilaya kama ngome ya kazi Yangu ya ukombozi, na kutumia Mataifa kama msingi ambao Nitaleta enzi nzima kufika mwisho. Nilifanya hatua mbili za kazi kule Uyahudi (hatua mbili za kazi za Enzi ya Sheria na Enzi ya Neema), na Nimekuwa Nikitekeleza zaidi hatua mbili za kazi (Enzi ya Neema na Enzi ya Ufalme) katika nchi nyingine nje ya Uyahudi. Kati ya Mataifa Nitafanya kazi ya kutamalaki, na hivyo kukamilisha enzi. Mwanadamu Akiniita Yesu Kristo kila wakati, lakini hajui kuwa nimeanza enzi mpya katika siku za mwisho na Nimeanza kazi mpya, na mwanadamu akingoja kwa hamu kufika kwa Yesu Mwokozi, basi Nitawaita watu kama hao watu wasioniamini. Ni watu ambao hawanijui, na imani yao Kwangu ni bandia. Watu hao wanaweza kushuhudia kufika kwa Yesu Mwokozi kutoka mbinguni? Wanachongoja sio kufika Kwangu, bali ni kufika kwa Mfalme wa Wayahudi. Hawatamani maangamizo Yangu ya dunia hii nzee yenye uchafu, badala yake, wanatamani kurudi kwa Yesu mara ya pili, ambapo watakombolewa; wanamtazamia Yesu kumkomboa binadamu mara nyingine kutoka kwa hii dunia iliyochafuliwa na isiyo na haki. Watu hao watakuwa vipi wale wanaokamilisha kazi Yangu katika siku za mwisho? Tamaa ya mwanadamu haina uwezo wa kufikia matakwa Yangu ama kutimiza kazi Yangu, kwani mwanadamu hutamani tu au kuenzi kazi ambayo Nimefanya hapo awali, na hawajui kuwa Mimi ni Mungu Mwenyewe ambaye ni mpya kila siku na hawi mzee. Mwanadamu anajua tu kuwa Mimi ni Yehova, na Yesu, na hana ufahamu kuwa Mimi ni Mwisho, Yule Ambaye Ataleta binadamu kufika mwisho. Yale ambayo mwanadamu anatamani na kujua ni ya dhana yake mwenyewe, na ni yale tu ambayo anaweza kuyaona na macho yake mwenyewe. Hayako sambamba na kazi Ninayofanya, bali kwa mvurugano nayo. Kama kazi Yangu ingefanywa kulingana na mawazo ya mwanadamu, basi ingefika mwisho lini? Mwanadamu angeingia mapumziko lini? Na Ningewezaje kuingia katika siku ya saba, siku ya Sabato? Nafanya kazi kulingana na mpango Wangu, kulingana na lengo Langu, na sio kulingana na nia ya mwanadamu.
wa Mashariki
kutoka kwa Neno Laonekana katika Mwili
Kujua zaidi: Kuhusu Kanisa la Mwenyezi Mungu

Jumapili, 18 Machi 2018

Upendo wa Mungu | "Kama Nisingeokolewa na Mungu" | Swahili Gospel Music Video

Upendo wa Mungu | "Kama Nisingeokolewa na Mungu" | Swahili Gospel Music Video

Kama nisingeokolewa na Mungu, ningekuwa bado nazurura ulimwenguni humu,
nikipambana kwa bidii na maumivu katika dhambi; kila siku huwa ya taabu isiyo na tarajio.
Kama nisingeokolewa na Mungu, bado ningekuwa nimepondwa chini ya miguu ya shetani,
kama nimenaswa katika dhambi na starehe zake, bila kujua maisha yangu yangekuwaje.
Kama nisingeokolewa na Mungu, nisingekuwa na baraka zangu leo,
wala kujua kwa nini sisi tuendelee kuishi ama maana ya maisha yetu.
Kama nisingeokolewa na Mungu, bado ningekuwa nimechanganywa kuhusu imani yangu,
nikiwa ningali katika nafasi tupu nikisukuma siku, bila kujua imani yangu iwe kwa nani.
Hatimaye nimeelewa mikono ya upendo ya Mungu imeshika yangu safarini.
Sitaweza kwenda na kupotea njia kwa sababu niko kwa mwendo huu mwangavu kukaa.
Hatimaye nimeelewa dhamira ya Mungu, yenye ari kwa mtu.
Fikra danganyifu kuondolewa kabisa, nitampa Mungu mwili wangu na roho yangu.
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Kanisa
Kama nisingeokolewa na Mungu, nisingekuwa na baraka zangu hapa leo,
wala kujua kwa nini sisi tuendelee kuishi ama maana ya maisha yetu.
Kama nisingeokolewa na Mungu, bado ningekuwa nimechanganywa kuhusu imani yangu,
nikiwa ningali katika nafasi tupu nikisukuma siku, bila kujua imani yangu iwe kwa nani.
Hatimaye nimeelewa mkono wa upendo wa Mungu umeushika wangu safarini.
Sitaweza kwenda na kupotea njia kwa sababu niko kwa mwendo huu mwangavu kukaa.
Hatimaye nimeelewa dhamira ya Mungu, yenye ari kwa mtu.
Fikra danganyifu kuondolewa kabisa, nitampa Mungu mwili wangu na roho yangu.

kutoka kwa Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya
Utukufu wote Uwe kwa Mwenyezi Mungu!

Jumamosi, 17 Machi 2018

Umeme wa Mashariki | Tafuteni Maana ya Maisha - "Kwa Ajili ya Nani Mtu Aishi" (Video Rasmi ya Muziki)

Umeme wa Mashariki | Tafuteni Maana ya Maisha - "Kwa Ajili ya Nani Mtu Aishi" (Video Rasmi ya Muziki)

Kwa Ajili ya Nani Mtu Aishi
Haikuwa wazi ni kwa ajili ya nani mtu anapaswa kuishi. Sasa nina jibu kwa hilo.
Nilikuwa naishi tu kwa ajili yangu mwenyewe, kutafuta hadhi tu na umaarufu.
Maombi kwa Mungu yaliyojaa maneno mema, lakini nikishikilia njia zangu mwenyewe katika maisha halisi.Imani juu ya msingi wa kesho na majaliwa, sina ukweli au uhalisi.
Mila na sheria, zikifungia imani yangu; sikubaki na kitu ila utupu.
Kushindwa kuishi kama binadamu, sistahili upendo wa Mungu kwa ajili yangu.

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, hukumu
Moyo wangu umeamshwa sasa, ukiniambia ni lazima nilipe upendo wa Mungu.
Najichukia kwa kuwa sikuwa na dhamira, kutomtii Mungu na kuvunja moyo wake.
Kamwe sijawahi kuutunza moyo wa Mungu; kamwe sikuwahi kujishughulisha na maneno Yake.Bila dhamiri, kutokuwa na hisi, ni jinsi gani naweza kuorodheshwa kama mtu?
Hukumu ya Mungu hunifanya nione, nilikuwa nimepotoshwa na Shetani kabisa.
Maovu, dunia hii, iliyojaa mitego, Ukweli ndio muumini lazima achague.
Ee Mungu mpenzi, Unanipenda sana, kufanya kila Unaloweza kunifanya niokolewe.
Kile Ulichonifanyia, nitakiweka kwa kumbukumbu! Kamwe sitasahau milele.
Utunzaji wa moyo wa Mungu, hayo ni mapenzi yangu yote. Nina kusudio la kufuata ukweli.
Najishughulisha kugharimia rasilmali kwa ajili ya Mungu, kujitoa mwenyewe kulipa upendo wake,kujitoa mwenyewe kulipa upendo wake.
kutoka kwa Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya
Utukufu wote Uwe kwa Mwenyezi Mungu!

Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe II

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki

Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe II

Mwenyezi Mungu alisema, Kwenye mkutano  mwisho tuliweza kuzungumzia mada muhimu sana. Je, wakumbuka mada hiyo ilikuwa kuhusu nini? Hebu Niirudie. Mada ya ushirika wetu wa mwisho ilikuwa: Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe. Je, mada hii ni muhimu kwako? Ni sehemu gani katika mada hii ni muhimu kwako? Kazi ya Mungu, tabia ya Mungu, au Mungu Mwenyewe? Ni sehemu ipi inakuvutia zaidi? Ni sehemu ipi unayotaka kusikiliza kuhusu zaidi? Najua ni vigumu kwako wewe kulijibu swali hilo, kwa sababu tabia ya Mungu inaweza kuonekana katika kila kipengele cha kazi Yake, na tabia Yake inafichuliwa katika kazi Yake siku zote na pahali pote, na, kutokana na hayo, inawakilisha Mungu Mwenyewe; kwenye mpango wa usimamizi wa ujumla wa Mungu, kazi ya Mungu, tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe vyote hivi haviwezi kutenganishwa.
Maudhui ya ushirika wetu wa mwisho kuhusu kazi ya Mungu yaliweza kuangazia mambo yaliyofanyika kitambo kwenye Biblia. Maudhui hayo yote yalikuwa hadithi kuhusu binadamu na Mungu, na yalimfanyikia binadamu na wakati huohuo yakahusisha kushiriki na maonyesho ya Mungu, hivyo basi hadithi hizi zinashikilia thamani na umuhimu mkubwa katika kujua Mungu. Baada tu ya kuumba ubinadamu, Mungu Alianza kujihusisha na binadamu na kuzungumza na binadamu, na tabia yake ikaanza kuonyeshwa kwa binadamu. Kwa maneno mengine, tangu Mungu alipojihusisha kwanza na mwanadamu, Alianza kuujuza umma kuhusu binadamu, bila kusita, kiini Chake halisi na kile Anacho na alicho. Licha ya kama watu wa awali au watu wa leo wanaweza kuona au kuelewa kiini hicho, kwa ufupi Mungu anamzungumzia mwanadamu na kufanya kazi miongoni mwa binadamu, Akifichua tabia Yake na Akionyesha kiini Chake —jambo ambalo ni ukweli, na lisilopingika na mtu yeyote. Hii inamaanisha pia kwamba tabia ya Mungu, kiini cha Mungu, na kile Anacho na alicho vyote vinatolewa daima na kufichuliwa huku naye Akifanya kazi na kujihusisha na binadamu. Hajawahi kusetiri au kumfichia binadamu chochote, lakini badala yake anatangaza kwa umma na kuachilia tabia Yake binafsi bila ya kuficha chochote. Hivyo basi, Mungu anatumai kwamba binadamu anaweza kumjua Yeye na kuielewa tabia Yake na kiini chake. Hapendi binadamu kuchukulia tabia Yake na kiini Chake kuwa mafumbo ya milele, wala Hataki mwanadamu kumchukulia Mungu kama fumbo lisiloweza kutatuliwa. Mpaka tu pale ambapo mwanadamu atakapomjua Mungu ndipo binadamu atakapojua njia ya kufuata na kuweza kuukubali mwongozo wa Mungu, na mwanadamu tu kama huyu ndiye anayeweza kuishi kwa kweli katika utawala wa Mungu, na kuishi katika mwangaza, na kuishi katikati ya baraka za Mungu.
Maneno na tabia iliyowasilishwa mbele na kufichuliwa na Mungu inawakilisha mapenzi Yake, na pia inawakilisha kiini Chake halisi. Wakati Mungu anapojihusisha na binadamu, haijalishi ni nini Anachosema au kufanya, au tabia gani Anayofichua, na haijalishi ni nini binadamu anaona kuhusu kiini cha Mungu na kile Anacho na alicho, vyote vinawasilisha mapenzi ya Mungu kwa binadamu. Licha ya kiwango ambacho binadamu anaweza kutambua, kufahamu, au kuelewa, vyote hivi vinawakilisha mapenzi ya Mungu—mapenzi ya Mungu kwa binadamu. Hii ni zaidi ya shaka! Mapenzi ya Mungu kwa binadamu ni vile Anavyohitaji watu kuwa, kile Anachohitaji wao kufanya, namna Anavyohitaji wao kuishi, na vile Anavyowahitaji kuweza kukamilisha kutimia kwa mapenzi ya Mungu. Je, mambo haya hayawezi kutenganishwa na kiini cha Mungu? Kwa maneno mengine, Mungu huwasilisha mbele tabia Yake na vyote Alivyo navyo na kile ambacho Mungu ni wakati huohuo Akimtolea madai binadamu. Hakuna uongo, hakuna kusingizia, hakuna ufichaji, na wala hakuna kupiga chuku. Ilhali kwa nini binadamu hawezi kujua na kwa nini hajawahi kuweza kutambua waziwazi tabia ya Mungu? Na kwa nini hajawahi kutambua mapenzi ya Mungu? Kile ambacho kimefichuliwa na kuwasilishwa mbele na Mungu ndicho kile Mungu anacho Mwenyewe na maana yake , na kinaonyesha kila kipengele cha tabia Yake ya kweli—hivyo kwa nini binadamu hawezi kuona? Kwa nini binadamu hana uwezo wa kuwa na maarifa ya kina? Kunayo sababu muhimu ya haya. Na sababu yenyewe ni ipi? Tangu wakati wa uumbaji, binadamu hajawahi kumchukulia Mungu kama Mungu. Kwenye nyakati zile za mwanzo kabisa, haikujalisha ni nini Mungu alifanya kuhusiana na binadamu, yule binadamu ambaye ndiye tu alikuwa ameumbwa, binadamu alimchukulia yeye kuwa mwandani wake tu na wala si zaidi ya hapo, kama mtu wa kutegemewa, na hakuwa na maarifa yoyote wala uelewa wa Mungu. Hivi ni kusema, hakujua kwamba kile kilichowasilishwa mbele na Kiumbe huyu—Kiumbe huyu ambaye yeye alitegemea na kumwona kuwa mwandani wake—alikuwa kiini cha Mungu, na wala hakujua kwamba Kiumbe huyu ndiye anayetawala viumbe wote. Nikisema kwa urahisi, watu wa wakati huo hawakuwa na maarifa hata kidogo kumhusu Mungu. Hawakujua kwamba mbingu na nchi na mambo yote yalikuwa yameumbwa na Yeye na wala hawakujua ni wapi Alipotokea, na, zaidi hawakujua Yeye Alikuwa nani. Bila shaka, wakati huo Mungu hakumhitaji binadamu kumjua Yeye au kumfahamu Yeye au kuelewa kila kitu Alichofanya, au kufahamishwa kuhusu mapenzi Yake, kwani hizi zilikuwa nyakati za mapema zaidi baada ya uumbwaji wa mwanadamu. Wakati Mungu alipoanza matayarisho ya kazi ya Enzi ya Sheria, Mungu alifanya mambo fulani kwa binadamu na pia Akaanza kutolea binadamu madai fulani, Akimwambia namna ya kutolea Mungu sadaka na namna ya kumwabudu. Ni wakati huo ndipo binadamu alipopata mawazo machache mepesi kuhusu Mungu, ni hapo tu ndipo alipojua tofauti kati ya binadamu na Mungu na kwamba Mungu Ndiye aliyewaumba wanadamu. Wakati binadamu alipojua kwamba Mungu alikuwa Mungu na binadamu alikuwa binadamu kukawa umbali fulani kati ya Yeye na Mungu , bado Mungu hakuhitaji kwamba binadamu awe na maarifa makuu au uelewa wa kina kumhusu Yeye. Hivyo basi, Mungu anayatoa mahitaji tofauti kwa binadamu kutokana na awamu na hali za kazi Yake. Unaona nini katika haya? Ni kipengele kipi cha tabia ya Mungu unayoitambua? Je, Mungu ni wa kweli? Yale mahitaji ambayo Mungu anampa binadamu yanastahili? Kwenye nyakati za mapema kabisa kufuatia uumbaji wa wanadamu na Mungu, wakati ambao Mungu alikuwa bado hajatekeleza kazi ya ushindi na utimilifu wa binadamu, na Alikuwa hata bado hajaongea yale maneno mengi sana kwake, Alihitaji kidogo sana kutoka kwa binadamu. Licha ya kile ambacho binadamu alifanya na namna alivyotenda—hata kama alifanya mambo fulani yaliyomkosea Mungu—Mungu alimsamehe hayo yote, na akayapuuza. Kwa sababu Mungu Alijua kile Alichokuwa Amempa binadamu, na Alijua kile kilichokuwa ndani ya binadamu, basi Alijua kiwango cha mahitaji ambayo anafaa kudai kutoka kwa binadamu. Ingawaje kiwango cha mahitaji Yake kilikuwa cha chini sana wakati huo, hii haimaanishi kwamba tabia Yake haikuwa kuu, au kwamba hekima na uweza Wake yalikuwa si yoyote ila maneno matupu. Kwa binadamu, kunayo njia moja tu ya kujua tabia ya Mungu na Mungu Mwenyewe: kwa kufuata hatua za kazi ya usimamizi ya Mungu na wokovu wa mwanadamu, na kuyakubali maneno ambayo Mungu anaongea akiyaelekeza kwa mwanadamu. Kujua kile Mungu anacho na alicho, na kujua tabia ya Mungu, bado binadamu angemuuliza Mungu kumwonyesha ubinafsi Wake halisi? Binadamu hatafanya hivyo, na hathubutu kufanya hivyo, kwa kuweza kuifahamu tabia ya Mungu na kile Anacho na alicho, tayari binadamu atakuwa amemwona Mungu Mwenyewe wa kweli, na atakuwa tayari ameona ubinafsi Wake halisi. Haya ndiyo matokeo yasiyoepukika.
Kazi na mpango wa Mungu ulipokuwa ukiendelea mbele bila kusia, na baada ya Mungu kuanzisha agano la upinde wa mvua na binadamu kama ishara kwamba Hangewahi tena kuuangamiza ulimwengu kwa kutumia gharika, Mungu alikuwa na tamanio lililokuwa likiongezeka na kumsukuma kuwapata wale ambao wangeweza kuwa katika akili moja na Yeye. Hivyo, pia, Alikuwa na tamanio lenye udharura zaidi wa kupata wale waliokuwa na uwezo wa kutekeleza mapenzi Yake duniani, na, isitoshe, kupata kundi la watu ambao wangeweza kuwa huru dhidi ya nguvu za giza, na kutoweza kuwa watumwa wa Shetani, na kuweza kuwa na ushuhuda kwake Yeye duniani. Kupata kundi la watu kama hawa kulikuwa ni tamanio la Mungu kwa muda mrefu, Alichokuwa akisubiria tangu wakati wa uumbaji. Hivyo basi, licha ya matumizi ya gharika na Mungu ili kuuangamiza ulimwengu, au agano Lake na binadamu, mapenzi ya Mungu, hali yake ya akili, mpango, na matumaini yote yalibakia yaleyale. Kile Alichotaka kufanya, ambacho Alikuwa ametamani kwa muda mrefu kabla ya uumbaji, kilikuwa kupata wale walio miongoni mwa wanadamu ambao Alitamani kuwapata—Kupata watu wa kundi hili ambao walioweza kufahamu na kujua tabia Yake, na kuyaelewa mapenzi Yake, kundi ambalo lingeweza kumwabudu Yeye. Watu kwenye kundi kama hili wanaweza kweli kuwa na ushuhuda kwake, na wao ndio, yaweza kusemekana, wasiri Wake.
Leo, hebu tuendelee kuzifuata nyayo za Mungu na kufuata nyayo za kazi Yake, ili tuweze kufichua fikira na mawazo ya Mungu, na kila kitu kinachomhusu Mungu, vyote ambavyo “vimehifadhiwa kwenye ghala” kwa muda mrefu. Kupitia mambo haya tutajua hatimaye tabia ya Mungu, kukielewa kiini cha Mungu, tutamruhusu Mungu kuingia kwenye mioyo yetu, na kila mmoja wetu ataweza kukaribia Mungu kwa utaratibu, na kupunguza umbali wetu na Mungu.
Sehemu ya kile tulichozungumzia wakati wa mwisho ilihusiana na kwa nini Mungu alianzisha agano na binadamu. Wakati huu, tutakuwa na ushirika kuhusu vifungo vya maandiko zilizo hapa chini. Hebu tuanze kwa kuyasoma maandiko.
Ibrahimu
1. Mungu Amwahidi Ibrahimu Mwana
(Mwa 17:15-17) Mungu akamwambia Abrahamu, na Sarai mkeo, hutamwita jina lake Sarai, kwa kuwa jina lake litakuwa Sara. Nami nitambariki, na pia nitakupa mwana kutoka kwake: naam, Nitambariki, na yeye atakuwa mama wa mataifa; na wafalme wa za watu watatoka kwake. Kisha Abrahamu akaanguka kifudifudi, akacheka, akasema moyoni, Je, mtoto atazaliwa kwa mtu wa umri aliye namiaka mia moja? Na Sara, aliye na umri wa miaka tisini, atazaa?” Kwa maneno mengine wanandoa hawa wazee walikuwa na umri mwingi sana wa kupata watoto. Naye Ibrahimu alifanya nini baada ya Mungu Kumwahidi? Aliuangukia uso wake akicheka, na kujiambia, “Je, mtoto atazaliwa kwa mtu wa umri aliye na miaka mia moja?” Ibrahimu aliamini kwamba haikuwezekana—hivi alimaanisha kwamba alisadiki ahadi ya Mungu kwake haikuwa chochote ila mzaha. Kutoka mtazamo wa binadamu, ahadi isingeweza kutimizika na binadamu, na vilevile isingeweza kutimizika na Mungu na ilikuwa haiwezekani kwa Mungu. Pengine, kwa Ibrahimu, ahadi hii ilikuwa ya kuchekesha. Mungu alimuumba binadamu, lakini yaonekana kwamba hajui kwamba mtu aliyezeeka sana hawezi kupata watoto; Anafikiria kwamba Anaweza kuniruhusu kupata mtoto, Anasema kwamba atanipa mtoto—kwa kweli hilo haliwezekani!. Na hivyo, Ibrahimu akaangukia uso wake na kucheka, akijifikiria yeye mwenyewe: Haiwezekani—Mungu anafanya mzaha na mimi, hili haliwezi kuwa kweli. Hakutilia maanani maneno yake Mungu. Hivyo, katika macho ya Mungu, Ibrahimu alikuwa binadamu wa aina gani? (Mwenye haki) Ni wapi ulipojifunza kwamba alikuwa mwenye haki? Wewe unafikiria kwamba wale wote ambao Mungu anawaita ni wenye haki, na watimilifu, na watu wanaotembea na Mungu. Wewe unashikilia mafundisho ya dini! Lazima uone waziwazi kwamba wakati Mungu anapomfasili mtu, Hafanyi hivyo kiholela. Hapa, Mungu hakusema kwamba Ibrahimu alikuwa mwenye haki. Katika moyo Wake, Mungu anavyo viwango vya kupima kila mtu. Ingawaje Mungu hakusema ni mtu wa aina gani ambaye Ibrahamu alikuwa, kwa mujibu wa mwenendo wake, Ibrahimu alikuwa na imani ya aina gani kwake Mungu? Ilikuwa ya kidhahania kidogo? Au alikuwa mwenye imani kuu? La, hakuwa! Kicheko na fikira zake zilionyesha yeye alikuwa nani, hivyo imani yako kwamba alikuwa mwenye haki ni ndoto ya kufikiria kwako, ni matumizi yasiyo na mwelekeo ya mafundisho ya dini, usiopaswa. Je, Mungu alikiona kicheko cha Ibrahimu na maonyesho yake madogo, [a] Alijua kuyahusu? Mungu alijua. Lakini Mungu angebadilisha kile Alichokuwa ameamua kufanya? La! Wakati Mungu alipopangilia na kuamua kwamba Angemchagua binadamu huyu, suala hilo lilikuwa tayari limekamilishwa. Si fikira za binadamu wala mwenendo wake ungemshawishi au kuhitilafiana na Mungu hata chembe; Mungu Asingebadilisha kiholela mpango Wake, wala Asingebadilisha au kuharibu mpango Wake kwa sababu ya mwenendo wa binadamu, hali ambayo ingekuwa ujinga. Nini, basi, kimeandikwa katika Mwanzo 17:21-22? “Lakini agano langu Nitalifanya imara na Isaka, ambaye Sara atakuzalia wakati kama huu mwaka ujao. Na akaacha kuzungumza naye, na Mungu akapanda kutoka kwa Ibrahimu.” Mungu hakutilia maanani hata chembe kile Ibrahimu alichofikiria au kusema. Na sababu ya kutotilia maanani Kwake ni gani? Kutotilia maanani kwake kulikuwa kwa sababu, wakati huo Mungu hakuhitaji kwamba mwanadamu awe mwenye imani kuu au kwamba aweze kuwa na maarifa kuu kuhusu Mungu, au, vilevile, aweze kuelewa kile kilichofanywa na kusemwa na Mungu. Hivyo, hakuhitaji kwamba binadamu aelewe kabisa kile Alichoamua kufanya, au watu Alioamua kuchagua, au kanuni za vitendo Vyake, kwani kimo cha binadamu hakikutosha tu. Wakati huo, Mungu alichukulia kile ambacho Ibrahimu alifanya na vyovyote alivyojiendesha yeye mwenyewe kuwa kawaida. Hakushutumu, au kukemea, lakini alisema tu: “Sara atakuzalia Isaka wakati huu uliopangwa mwaka ujao.” Kwa Mungu, baada Yake kuyatangaza maneno haya, suala hili hatimaye lilikuwa kweli hatua kwa hatua; katika macho ya Mungu, kile ambacho kilikuwa kikamilishwe na mpango Wake kilikuwa tayari kimetimizwa. Baada ya kuikamilisha mipangilio ya hayo, Mungu aliondoka. Kile binadamu hufanya au kufikiria, kile binadamu huelewa, mipango ya binadamu—hakuna chochote kati ya hivi vyote kinacho uhusiano wowote na Mungu. Kila kitu hufanyika kulingana na mpango wa Mungu, kikiendana na nyakati na awamu zilizowekwa na Mungu. Hivyo ndivyo kanuni ya kazi ya Mungu inavyoenda. Mungu haingilii kati chochote kile binadamu anafikiria au kujua, ilhali Haachi mpango Wake, wala kuacha kazi Yake kwa sababu binadamu hasadiki wala kuelewa. Kweli hizi hivyo basi zinakamilishwa kulingana na mpango na fikira za Mungu. Hivi ndivyo hasa tunavyoona kwenye Biblia: Mungu Alisababisha Isaka kuzaliwa wakati ule Aliokuwa amepanga. Je, kweli zinathibitisha kwamba tabia na mwenendo wa binadamu vilizuia kazi ya Mungu? Havikuzuia kazi ya Mungu! Je, imani ndogo ya binadamu kwa Mungu, na dhana zake na fikira kumhusu Mungu viliweza kuathiri kazi ya Mungu? La, havikuathiri! Hata kidogo! Mpango wa usimamizi wa Mungu hauathiriwi na binadamu, suala, au mazingira yoyote. Kila kitu Anachoamua kufanya kitakamilika na kukamilishwa kwa wakati na kulingana na mpango Wake, na kazi Yake haiwezi kutatizwa na binadamu yeyote. Mungu hatilii maanani baadhi ya ujinga na kutojua kwa binadamu, na hata Hupuuza upinzani na dhana fulani za binadamu Kwake; badala yake, Anafanya kazi ambayo lazima Afanye bila ya kusita. Hii ni tabia ya Mungu na ni onyesho la kudura Yake.

Kazi ya Usimamizi wa Mungu na Wokovu wa Mwanadamu Yaanza kwa Sadaka ya Isaka ilivyotolewa na Ibrahimu

Baada ya kumpa mtoto Ibrahimu, maneno ambayo Mungu alikuwa ametamka kwa Ibrahimu yakawa yametimizwa. Hii haimaanishi kwamba mpango wa Mungu ulifikia mwisho hapa; kinyume cha mambo ni kwamba, mpango wa ajabu wa Mungu wa usimamizi na wokovu wa mwanadamu ndipo ulikuwa tu umeanza, na baraka Yake ya mwana kwa Ibrahimu ilikuwa tu ni utangulizi wa mpango wa usimamizi Wake kwa ujumla. Wakati huo, ni nani aliyejua kwamba vita vya Mungu na Shetani vilikuwa vimeanza kimya kimya wakati Ibrahimu alipomtoa Isaka?

Mungu Hajali Kama Binadamu Ni Mjinga—Anahitaji Tu Binadamu Awe Mkweli

Kisha, hebu tuangalie kile Mungu alimfanyia Ibrahimu. Ukiangalia Mwanzo 22:2, Mungu alimtolea Ibrahimu amri ifuatayo: “Naye akasema, Umchukue mwanao, mwanao wa pekee, umpendaye, Isaka, uende mpaka nchi ya Moria; na huko umtoe sadaka ya kuteketezwa huko juu ya mlima mmojawapo Nitakaokuambia.” Maana ya Mungu ilikuwa wazi: Alikuwa akimwambia Ibrahimu amtoe mtoto wake wa pekee Isaka, ambaye alimpenda, kwa minajili ya sadaka ya kuteketezwa. Tukiiangalia amri ya Mungu leo, je ingali inakinzana na dhana za binadamu? Ndiyo! Kile alichokifanya Mungu wakati huo ni kinyume sana na dhana za binadamu na hakieleweki kwa binadamu. Katika dhana zao, watu husadiki yafuatayo: Wakati binadamu hakusadiki, na akafikiria ni jambo lisilowezekana, Mungu Alimpa mwana, na baada ya kupata mtoto, Mungu alimwomba amtoe mwana wake—haiwezekani! Mungu kwa hakika alinuia kufanya nini? Kusudio halisi la Mungu lilikuwa nini? Alimpa Ibrahimu mtoto bila masharti yoyote, ilhali pia Alimwomba Ibrahimu aweze kutoa bila masharti. Maji yalikuwa yamezidi unga? Katika mtazamo wa mtu wa pembeni, hapa maji hayakuwa tu yamezidi unga lakini pia ilikuwa kwa kiasi fulani hali ya “kuunda tatizo pasipo na tatizo” Lakini Ibrahimu mwenyewe hakusadiki kwamba Mungu alikuwa akihitaji mengi sana. Ingawaje alikuwa na wasiwasi fulani, na alimshuku kidogo Mungu, alikuwa tayari bado kumtoa mtoto wake. Wakati huu, ni nini unachoona ambacho kinathibitisha kuwa Ibrahimu alikuwa radhi kumtoa mtoto wake? Ni nini kinazungumzwa kwenye sentensi hizi? Maandishi asilia yanaelezea yafuatayo: “Abrahamu akaondoka alfajiri, akatandika punda wake, akachukua vijana wawili pamoja naye, na Isaka mwanawe, akachanja kuni kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa, akaondoka, akaenda hadi mahali alipoambiwa na Mungu.” (Mwa 22:3). “Wakafika mahali pale alipoambiwa na Mungu; Abrahamu akajenga madhabahu huko, akazipanga kuni tayari, na akamfunga Isaka mwanawe, na akamweka juu ya madhabahu juu ya zile kuni. Abrahamu akanyosha mkono wake, akakichukua kisu ili amchinje mwanawe.” (Mwa 22:9-10). Wakati Ibrahimu alipounyosha mkono wake, na kukichukua kisu ili kumwua mtoto wake, Mungu aliviona vitendo vyake? Naam aliviona. Mchakato wote—kuanzia mwanzo, wakati Mungu alipomwomba Ibrahimu kumtoa Isaka, hadi pale ambapo Ibrahimu alikiinua kisu chake ili kumwua mtoto wake—hilo lilionyesha Mungu moyo wa Ibrahimu, na haijalishi kuhusu ujinga wake wa awali, kutojua kwake, na kutomwelewa Mungu kwake, wakati huo moyo wa Ibrahimu kwa Mungu ulikuwa kweli, na wenye uaminifu, na kwa kweli alikuwa akienda kumrudisha Isaka, mtoto aliyepewa yeye na Mungu, ili arudi kwa Mungu. Ndani yake, Mungu aliuona utiifu—utiifu uleule ambao Yeye Alitamani.
Kwa binadamu, Mungu hufanya mengi yasiyoeleweka na yaliyo ya ajabu. Wakati Mungu anapotaka kupangilia mtu, mpango huu mara nyingi unakinzana na dhana za binadamu, na huwa haueleweki kwa binadamu huyo, ilhali ni ukosefu wa mwafaka huu na kutofahamu ndiyo majaribio ya Mungu na mtihani wake kwa binadamu. Ibrahimu, huku haya yakiendelea, aliweza kuonyesha utiifu kwa Mungu uliokuwa ndani yake, jambo ambalo ndilo lililokuwa sharti muhimu zaidi la yeye kuweza kushibisha mahitaji ya Mungu. Hapo tu, wakati Ibrahimu alipoweza kutii mahitaji ya Mungu, alipomtoa Isaka ndipo Mungu Alipohisi kwa kweli utulivu na kukubaliwa na Mungu—kwa Ibrahimu, ambaye Alikuwa amemchagua. Hapo tu ndipo Mungu alipokuwa na hakika kwamba mtu huyu Aliyekuwa amemchagua Yeye alikuwa kiongozi muhimu ambaye angetekeleza ahadi Yake na mpango Wake wa usimamizi wa baadaye. Ingawaje lilikuwa tu jaribio na mtihani, Mungu alihisi furaha, Alihisi upendo wa binadamu kwake Yeye, na Alihisi akiwa ametulizwa na binadamu kwa mara ya kwanza. Wakati huu ambao Ibrahimu alipokiinua kisu chake ili kumwua Isaka, Mungu alimsimamisha? Mungu hakumruhusu Ibrahimu kumpa Isaka, kwani Mungu hakuwa na nia yoyote ya kumtoa uhai Isaka. Hivyo, Mungu alimsimamisha Ibrahimu kwa wakati mwafaka. Kwake Mungu, utiifu wa Ibrahimu ulikuwa tayari umepita mtihani, kile alichofanya kilitosha, naye Mungu tayari alikuwa ameona matokeo ya kile Alichokuwa amenuia kufanya. Je, matokeo haya yalimtosheleza Mungu? Yaweza kusemekana kwamba matokeo haya yalimtosheleza Mungu na kwamba ndiyo ambayo Mungu alitaka, na ndiyo ambayo Mungu alikuwa ametamani kuyaona. Je, hili ni kweli? Ingawaje, katika miktadha tofauti, Mungu anatumia njia tofauti za kupima kila mtu. Kwa Ibrahimu Mungu aliona kile Alichotaka, Aliona kwamba moyo wa Ibrahimu ulikuwa wa kweli, na kwamba utiifu wake haukuwa na masharti na ilikuwa hali hii hasa ya “kutokuwa na masharti” ambayo Mungu alitamani. Watu mara nyingi husema, tayari nimetoa hii, tayari nimeachana na ile—kwa nini bado Mungu hajatosheka na mimi? Kwa nini Anaendelea kuniweka katika majaribio? Kwa nini Anaendelea kunijaribu? Hii yaonyesha ukweli mmoja: Mungu bado hajauona moyo wako, na bado hajapata moyo wako. Hivi ni kusema, Hajauona uaminifu kama wakati ule ambao Ibrahimu aliweza kukiinua kisu chake ili kumuua mtoto wake kwa mkono wake mwenyewe na kumtoa kwa Mungu. Bado Hajauona utiifu wako usio na masharti, na hajatulizwa na wewe. Ni jambo la kiasili, hivyo basi, kwamba Mungu anaendelea kukujaribu. Je, haya si kweli? Tutaachia hapa kwa mada hii. Halafu, tutasoma “Ahadi ya Mungu kwa Ibrahimu.”
3. Ahadi ya Mungu kwa Ibrahimu
(Mwa 22:16-18) … Nimeapa kwa nafsi yangu, akasema BWANA, kwa kuwa umetenda jambo hili, wala hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee: Kwamba katika kubariki Nitakubariki, na katika kuzidisha Nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulio kwenye ukanda wa pwani; na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao; na katika uzao wako mataifa yote ya dunia watabarikiwa; kwa sababu umeitii sauti yangu.
Huu ni ukamilifu wa maelezo ya baraka za Mungu kwa Ibrahimu. Ingawaje ni fupi, maudhui yake ni mengi: Yanajumuisha sababu ya, na usuli wa, zawadi ya Mungu kwa Ibrahimu, na kile ambacho Alimpa Ibrahimu. Unao pia mhemko wa furaha na msisimko Aliotumia Mungu kutamka maneno haya, , pamoja na udharura wa tamanio Lake la kupata wale wanaoweza kusikiliza maneno Yake. Katika haya, tunaona upendo wa Mungu kwa, na wema Wake kwa, wale wanaotii maneno Yake na kufuata amri Zake. Hivyo, pia, tunaiona gharama Anayolipia ili kupata watu, na utunzaji na fikira Anazotumia kuweza kuwapata. Zaidi ya hayo, kifungu hicho, kilicho na maneno “Nimeapa kwa nafsi yangu,” kinatupa hali ya nguvu ya machungu na maumivu Aliyoyapitia Mungu, na Mungu pekee, usiri wa kazi hii ya mpango wa usimamizi. Ni kifungu cha kuchokonoa fikira, na kile ambacho kilikuwa na umuhimu maalum kwa, na ilikuwa na athari nyingi ajabu kwa wale waliokuja baadaye.
kutoka kwa Mwendelezo wa Neno Laonekana katika Mwili 

Juni 13, 2014

Ijumaa, 16 Machi 2018

Umeme wa Mashariki | Ufafanuzi wa Tamko la Kwanza

Umeme wa Mashariki | Ufafanuzi wa Tamko la Kwanza

Mwenyezi Mungu alisema, Kama tu Mungu alivyosema, “Hakuna anayeweza kuelewa mzizi wa maneno Yangu, wala kusudi la maneno haya.” Kama Isingekuwa uongozi wa Roho wa Mungu, kama isingekuwa kwa majilio ya maneno Yake, wote wangeangamia chini ya kuadibu Kwake. Ni kwa nini Mungu humjaribu mwanadamu kwa muda mrefu hivyo? Na kwa muda mrefu kama miezi mitano? Hili ndilo wazo la kulenga la ushirika wetu na vilevile wazo kuu katika hekima ya Mungu.