Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Muziki wa Akapela "Tokeo Lililofikiwa kwa Kumjua Mungu" (Video Rasmi ya Muziki)

Hayuko katika upeo wa mbali, wala hajajificha juu mawinguni. Yuko kando yako, akiwa na mamlaka juu ya kila kitu chako, Yeye ni kila kitu ulicho nacho, na Yeye ni kitu pekee ulicho nacho.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Jumatano, 9 Mei 2018

Umeme wa Mashariki | Siri Zilizofichwa Nyuma ya Ukimbizaji

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, ukweli

Umeme wa Mashariki | Siri Zilizofichwa Nyuma ya Ukimbizaji

Li Li     Mji wa Dezhou, Mkoa wa Shandong
Sio muda mrefu uliopita, nilitiwa moyo na Mungu na kupandiswa cheo kuwa mfanyakazi wa eneo. Siku moja, nilipokuwa nimekusanyika na wafanyakazi wenzangu, sikuweza kujizuia kufikiria mwenyewe: ni lazima nifanye vyema.

Jumanne, 8 Mei 2018

"Imani katika Mungu" (1) - Je, Utiifu kwa Wale Walio Madarakani Kweli ni Sawa na Utiifu kwa Mungu?

"Imani katika Mungu" (1) - Je, Utiifu kwa Wale Walio Madarakani Kweli ni Sawa na Utiifu kwa Mungu?

Utambulisho

Katika Biblia, Paulo alisema, "Acha kila nafsi itii mamlaka ya juu zaidi. Kwani hakuna mamlaka isipokuwa ya Mungu: mamlaka yaliyoko yameamriwa na Mungu. Yeyote yule anayepinga nguvu, anapinga amri ya Mungu: na yule anayepinga atapokea laana” (Warumi 13:1-2). Sisi waumini tunapaswa kuwatendea vipi wale walio madarakani? Je, utiifu kwa wale walio madarakani ni sawa na utiifu kwa Mungu kweli?
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Bwana Yesu
Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.

Umeme wa Mashariki | Niliupata Mwanga wa Kweli

Umeme wa Mashariki | Niliupata Mwanga wa Kweli


Qiuhe, Japani
Nilizaliwa katika familia ya Kikatoliki. Tangu nilipokuwa mdogo, nilihudhuria Misa kanisani na babu na bibi yangu. Kutokana na ushawishi wa mazingira yangu na imani yangu kwa Mungu, nilijifunza kuimba maandiko mengi tofauti na kufanya kaida mbalimbali za dini.
Mnamo 2009, niliwasili Japani ili kusoma. Wakati mmoja, katika chumba cha bweni cha mwanafunzi mwenzangu, kwa bahati nilikutana na kiongozi wa kikundi kidogo cha Kikristo aliyekuja kueneza injili. Nilifikiri: Waprotestanti na Wakatoliki humwamini Mungu mmoja. Wote wawili huamini katika Bwana Yesu. Matokeo yake, nilikubali mwaliko wa kiongozi huyo wa kundi ndogo kujiunga naye kanisani. Baada ya kusikiliza wachungaji wakihubiri na kusikia baadhi ya ndugu wa kiume na wa kike wakizungumza juu ya Biblia, nilipata ufahamu fulani juu ya maisha ya Bwana Yesu. Hili lilinisababisha niwe na imani zaidi katika Bwana. Hata hivyo, baada ya miezi michache, wachungaji na wahubiri walituomba kutoa zaka kila wiki. Pia, kila juma, tulipaswa kupeana vijitabu ili kueneza injili. Wakati mwingine, tulikuwa tumechoka kiasi kwamba tungesinzia wakati wa ibada ya Jumapili. Hatukuwa tena na utaratibu wa kawaida katika maisha yetu. Wakati huo, baadhi yetu tulifanya kazi na pia kusoma. Haikutubidi tu kutafuta pesa za kulipia masomo yetu, lakini pia tulihitaji fedha za gharama zetu za kila siku. Maisha yetu yalikuwa ni magumu sana tayari, lakini bado walitaka tuwape fedha zetu na nguvu zetu. Tulikuwa tunakabiliwa na shida nyingi sana na maumivu. Hatua kwa hatua, niligundua kwamba wachungaji na wahubiri hawakuwa kwa kweli watu waliomtumikia Bwana. Kwa kawaida, kwa kuwa walikuwa ndio wale ambao waliliongoza kanisa, wangepaswa kuwa wakitusaidia kukua katika maisha yetu ya kiroho. Hata hivyo, hawakuyajali maisha yetu. Hawakufikiria kabisa kuhusu matatizo yetu ya kivitendo. Badala yake, walitaka nguvu zetu na pesa zetu. Kila kitu walichokifanya kilikuwa ni cha kusaidia kupanua kanisa lao na kuimarisha hali zao na ushawishi wao. Kwa wakati huu, tulihisi kama tulikuwa tumedanganywa. Kwa hivyo, ndugu zangu kadhaa na mimi tuliliacha kanisa.
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Kanisa
Baada ya kuacha kanisa, nilipata kanisa moja Katoliki ambalo lilikuwa juu ya mlima. Watu katika kanisa hili walikuwa Wajapani Nilihudhuria Misa mara chache lakini nilihisi kuwa halikunifaidi kiroho. Zaidi ya hayo, ilikuwa vigumu kuhudhuria ushirika, kwa hiyo nililiacha kanisa hilo pia.

Jumatatu, 7 Mei 2018

Latest Gospel Movie Swahili "Siri ya Utauwa: Mfuatano" | Ufunuo Mpya Zaidi wa Roho Mtakatifu


Latest Gospel Movie Swahili "Siri ya Utauwa: Mfuatano" | Ufunuo Mpya Zaidi wa Roho Mtakatifu

Lin Bo'en ni mhubiri mzee ambaye amemwani Bwana kwa miongo mingi. Tangu alipomkubali Mwenyezi Mungu, Kristo wa siku za mwisho, alihukumiwa, akatengwa, na akafukuzwa kutoka kwa jumuiya ya kidini na wachungaji na wazee wa kanisa, nguvu zinazompinga Kristo. Lakini ingawa Lin Bo’en alishambuliwa, akahukumiwa na kusingiziwa, hakusita kwa woga. Badala yake, imani yake ikawa thabiti zaidi kuliko ilivyowahi kuwa, na hili lilimwongoza kufahamu hatimaye kwamba wachungaji na wazee wa kanisa wa ulimwengu wa dini walikuwa wakiigiza kwa udanganyifu sura adilifu. Wakati huo huo, alikuja kujua kwamba Kristo pekee ndiye ukweli, njia, na uzima, na Kristo pekee ndiye Anaweza kumwokoa na kumtakasa na kumkamilisha mwanadamu. Kwa ajili ya hili, aliamua kumfuata Kristo, kumshuhudia Kristo, na kufanya kila linalowezekana kufuatilia ukweli, kutafuta kuigeuza tabia yake ili aweze kuwa shahidi wa kweli wa Mungu. Mara tu Chama cha Kikomunisti cha Uchina kilipogundua kwamba Lin Bo’en aliachiliwa kutoka gerezani na hakuwa amebadilika, kwamba hakuwa ameikana imani yake hata kidogo na hata aliamini katika Umeme wa Mashariki, kwamba alienda kila mahali kushuhudia kwamba Bwana Yesu amerudi tena na kwamba Yeye ni Mwenyezi Mungu, CCP kilimworodhesha kama mtu wa kutakiwa na walienda kila mahali kumkamata. Lin Bo’en alilazimika kuiacha familia yake, na kila mahali aliposhuhudia kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho, aliweza kuwaongoza waumini wengi waaminifu, wa tabia njema kwa upande wa Mungu. Video hii inatoa maelezo ya hadithi ya kweli ya Lin Bo’en ya kueneza injili na kumshuhudia Mungu.

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki

Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee IV

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki

Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee IV

Utakatifu wa Mungu (I)

Mwenyezi Mungu alisema, Tumekuwa na ushirika wa ziada wa mamlaka ya Mungu leo, na hatutazungumza kuhusu haki ya Mungu sasa hivi. Leo tutazungumza kuhusu mada nzima mpya—utakatifu wa Mungu. Utakatifu wa Mungu pia ni kipengele kingine cha kiini cha kipekee cha Mungu, hivyo kuna umuhimu mkubwa wa kushiriki mada hii hapa. 

Jumapili, 6 Mei 2018

Umeme wa Mashariki | Uso halisi wa Mtu Anayedaiwa Kuwa Mtu Mzuri

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, hukumu

Umeme wa Mashariki | Uso halisi wa Mtu Anayedaiwa Kuwa Mtu Mzuri

Kemu     Jiji la Zhumadian, Mkoa wa Henan
Katika mawazo yangu mwenyewe, daima nimejifikiria kuwa na ubinadamu mzuri. Nimefikiria hivi kwa sababu, majirani zangu mara nyingi walinisifu mbele ya wazazi wangu kwa kuwa mwenye busara na wa kuijali familia yetu; wakisema kuwa mimi nilikuwa kipenzi cha wazazi wangu. 

Mimi Sistahili Kumwona Kristo

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, ukweli

Mimi Sistahili Kumwona Kristo

Huanbao    Mji wa Dalian, Mkoa wa Liaoning
Tangu kwanza nianze kumwamini Mwenyezi Mungu, daima nimewapenda wale ndugu wa kiume na wa kike ambao wanaweza kupokea huduma ya kibinafsi ya Kristo, ambao wanaweza kusikia mahubiri Yake kwa masikio yao wenyewe.

Jumamosi, 5 Mei 2018

Latest Swahili Gospel Movie "Kusubiri" | Bwana Yesu Kristo Ameonekana Kufanya Kazi Yake

Latest Swahili Gospel Movie "Kusubiri" | Bwana Yesu Kristo Ameonekana Kufanya Kazi Yake

Yang Hou'en ni mchungaji katika kanisa la nyumbani Uchina. Pamoja na babake Yang Shoudao, wamemngoja Bwana Yesu ashuke kutoka mawinguni na kuwachukua juu hadi katika ufalme wa mbinguni. Kwa ajili ya hili, walimfanyia Bwana kazi kwa bidii, walishikilia imara jina Lake, na kuamini kuwa yeyote ambaye sio Bwana Yesu ashukaye mawinguni ni Kristo wa uongo. Na hivyo, waliposikia habari kuhusu kuja mara ya pili kwa Bwana, hawakuisikiliza wala kuikubali. Walidhani ni bora kukesha na kungoja. …Wakiendelea kungoja kwa kimyakimya, binamu wa Yang Hou'en, Li Jiayin alikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho, na kueneza injili kwao. Baada ya majadiliano makali sana, Yang Hou'en hatimaye alielewa maana ya kweli ya “kukesha na kuomba,” na aliiweza kuona kuwa maneno ya Mwenyezi Mungu ni ukweli, njia, uzima, na hii ni sauti ya Bwana, na Mwenyezi Mungu ni kuja kwa mara ya pili kwa Bwana Yesu ambaye walikuwa wamemngoja kwa miaka mingi sana …
Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Bwana Yesu

Ijumaa, 4 Mei 2018

64. Huku Ni Kuweka Ukweli Katika Vitendo

Kanisa la Mwenyezi Mungu, ushuhuda, Umeme wa Mashariki

64. Huku Ni Kuweka Ukweli Katika Vitendo

Fan Xing    Mji wa Zhumadian, Mkoa wa Henan
Katika siku za nyuma, nilikuwa nimeunganishwa na dada mmoja kufanya kazi kwa wajibu fulani. Kwa sababu nilikuwa na majisifu na mwenye kiburi na sikutafuta ukweli, nilikuwa na mawazo kiasi ya kabla kuhusu dada huyu ambayo niliweka moyoni mwangu daima na sikuzungumza waziwazi naye. Tulipotengana, sikuwa nimeingia katika ukweli wa uhusiano wa kufanya kazi wenye kuridhisha. Baadaye, kanisa lilinipangia kufanya kazi na dada mwingine nami nikaweka azimio mbele ya Mungu: Kuanzia sasa kuendelea, sitatembea katika njia za kufeli. Nimejifunza mafundisho yangu na hivyo kwa sasa wakati huu bila shaka nitakuwa na mawasiliano ya wazi zaidi na dada huyu na kufikia uhusiano wa kufanya kazi wenye kuridhisha.
Kila wakati kulikuwa na mgongano au pengo kati yetu tulipokuwa tukifanya wajibu wetu pamoja, ningechukua fursa ya kwanza kuwasiliana na dada na kuzungumza kwa dhati. Ningemwuliza ni vipengele vipi nilikuwa nikifanya kwa njia isiyofaa. Dada huyo kisha angeonyesha kuwa nilikuwa na kiburi na mwenye majisifu na kwamba siku zote ningekataa mitazamo yake katika mawasiliano yetu. Alisema wakati mwingine ningeonyesha hali zake na kumpachika jina bila haki, na kwamba wakati wa mikusanyiko, nilifanya maamuzi yote kuhusu kusoma neno la Mungu. Nilikubali kwa kichwa mambo haya yote dada alisema juu yangu. Nilidhani: "Kwa kuwa unasema mimi nina kiburi, basi nitazungumza kwa unyenyekevu zaidi kuanzia sasa na kuendelea na kuzingatia kwa makini hasa kuzungumza kwa hekima na busara. Ikiwa nitatambua matatizo yoyote unayo, basi nitayadunisha wakati ninapoyataja. Ikiwa hutayatambua, basi sitayazungumzia. Wakati wa mikusanyiko, nitakula na kunywa chochote utakachoniambia nikule na ninywe, na nitasikia kila kitu unachosema. Si hili litatatua kila suala?" Baada ya haya, nilianza kuweka hili katika vitendo. Kabla ya kuzungumza, ningefikiri vile ningeweza kuepuka kukana wazo la dada. Wakati mitazamo yetu hayakulingana pamoja, ningekubali kushindwa na mtazamo wake na kutekeleza wazo lake. Nilipomwona dada akifanya jambo kwa njia isiyo sahihi, singemfafanulia kwa waziwazi. Lakini baada ya kipindi cha muda cha kutenda kwa namna hii, niligundua kuwa itikadi yangu ya "nyima mwili na weka ukweli katika matendo" haikuwa imebadilisha uhusiano wetu hata kidogo. Badala yake, iliimarisha mawazo yake yaliyotungwa kabla kunihusu. Kwa kuona matokeo hayo, nilihisi nimekosewa. Niliwaza: "Tayari nimejitahidi kadri niwezavyo kuweka ukweli katika matendo, mbona haifanyi kazi? Dada huyu si rahisi kupatana na yeye, hana wepesi wa kuhisi hata kidogo. "Kwa hiyo, nilizama katika uhasi na moyo wangu ukahuzunika sana.
Siku moja, kiongozi mmoja alitujia kukagua kazi yetu na kuuliza jinsi hali zetu zilivyokuwa wakati wa kipindi hiki. Kisha nikaeleza vile hali yangu ilivyokuwa. Baada ya kusikiliza, kiongozi huyo alisema: "Hii mbinu yako haiweki ukweli katika matendo. Wewe ni mchafu ndani. Unatenda hivi kwa madhumuni yako mwenyewe na hautendi kulingana na ukweli." Baada ya haya, tulisoma vifungu viwili vya maneno ya Mungu. Mungu alisema: “Upande wa nje, inaonekana kana kwamba unatia ukweli katika vitendo, lakini kwa kweli, hali ya matendo yako haionyeshi kwamba unatia ukweli katika vitendo. Kuna watu wengi walio na mienendo fulani ya nje, wanaoamini ‘Ninatia ukweli katika vitendo…,’ Lakini Mungu asema: ‘Sitambui kwamba unatia ukweli katika vitendo.’ Hii ni nini? Hii ni aina ya mwenendo. Kusema kweli, unaweza kuhukumiwa kwa hilo; halitasifiwa, halitakumbukwa. Hata kusema kweli zaidi, katika kulichangua hili, unafanya uovu, mwenendo wako unampinga Mungu. Kutoka nje, hukatizi, husumbui, huharibu chochote, au kukiuka ukweli wowote. Inaonekana kile ambacho unafanya ni chenye mantiki na cha maana, lakini unafanya uovu na kumpinga Mungu. Kwa hivyo unapaswa kutegemea chanzo jinsi Mungu amehitaji, kuona kama kuna badiliko katika tabia yako au kama umetia ukweli katika vitendo. Haihusu kukubali mawazo na maoni ya mwanadamu, au kwa hiari zako mwenyewe. Badala yake, ni Mungu ndiye husema kama unakubali mapenzi Yake; ni Mungu ambaye husema kama matendo yako yana ukweli na kama yanafikia viwango Vyake au la. Kujipima dhidi ya matakwa ya Mungu ndiyo njia sahihi tu” (“Unachopaswa Kujua Kuhusu Kuigeuza Tabia Yako” katika Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo). “Mawazo ya binadamu kwa kawaida yanaonekana mazuri na sahihi kwa watu na yanaonekana kama hayakiuki ukweli kwa kiasi kikubwa. Watu wanahisi kwamba kufanya kwa jinsi hii ni kuweka kweli katika matendo, wanahisi kwamba kufanya kwa jinsi hii ni kumtii Mungu. Kwa kweli, watu hawamtafuti Mungu hakika na kumwomba Mungu kuhusu hili. Hawajitahidi kufanya vizuri kuridhisha mapenzi ya Mungu wala hawajitahidi kufanya vizuri kulingana na mahitaji Yake. Hawana hali hii ya kweli, na hawana hamu kama hiyo. Hili ndilo kosa kubwa zaidi ambalo watu hufanya katika matendo yao, kwa sababu unamwamini Mungu, lakini Mungu hayupo moyoni mwako. Hii sio dhambi vipi? Huku sio kujidanganya mwenyewe vipi? Ni athari gani kuamini jinsi hii kutakuwa nayo? Uko wapi umuhimu wa matendo ya kumwamini Mungu?” (“Kutafuta Mapenzi ya Mungu na Kuuweka Ukweli Katika Vitendo Kwa Kiasi Kikubwa Zaidi Iwezekanavyo” katika Kumbukumbu za Maongezi ya Kristo). Nilijaribu kuelewa maneno yake Mungu na kuyalinganisha na hali yangu inayodaiwa kuwa "kuweka ukweli katika matendo." Moyo wangu ulichangamka. Hivyo, njia niliyokuwa nikifanya mambo haikukusudiwa kukidhi Mungu. Ilikusudiwa kulinda hadhi yangu bure. Niliogopa kiongozi huyo angesema asili yangu ilikuwa na dosari, kwamba sikutafuta ukweli, na kuwa sikufanya kazi vyema na yeyote. Aidha, nilifikiri ilikuwa ni kisingizio cha kurahisisha uhusiano wangu na dada na kujinasua kwa aibu na uchungu uliosababishwa na mgogoro huo. Nilidhani ingekomboa ile taswira ambayo watu wengine walikuwa nayo kunihusu na kuwaruhusu kuona kuwa nilikuwa nimebadilika. Inaweza kuonekana kuwa kile kilichodaiwa kuwa "kuweka ukweli katika matendo" kwangu kilikuwa kwa madhumuni yangu mwenyewe. Yote yalitendwa mbele ya wengine na hayakuanzishwa kwa msingi wa kutafuta kumridhisha Mungu. Sikujidharau na kwa kweli kuunyima mwili kwa sababu sikuwa na ufahamu wa asili yangu ya majisifu na kiburi. Katika kutafakari juu ya kufanya kazi na dada, ni kwa sababu sikutambua asili yangu ya kujisifu na kiburi, na kwa sababu nilijiheshimu na nilikuwa nafikiri kila wakati kuwa nilikuwa bora zaidi kuliko wengine nilipozungumza, bila kujua nilikuwa nimesimama kwenye kiweko nikidunisha wengine. Wakati wa kushughulikia mambo, nilipenda kuwa msimamizi; nilifanya mambo kwa njia yangu mwenyewe, na kamwe sikuwahi kutafuta maoni ya watu wengine. Wakati dada alipoonyesha haya matatizo niliyokuwa nayo, sikutafuta ukweli uliofanana ili kuchambua na kuelewa hali ya asili yangu. Hata zaidi, sikutafuta jinsi ninapaswa kuiweka katika vitendo kulingana na mahitaji ya Mungu na kwa mujibu wa ukweli. Nilibadili tu matendo machache ya nje, nikifikiria kuwa kwa kuwa niliacha kufanya mambo ambayo yalikuwa mabaya, nilikuwa nikiweka ukweli katika matendo. Kwa kweli, kila kitu nilichokuwa nikifanya kilikuwa ukweli kulingana na mawazo yangu mwenyewe. Vyote vilikuwa ni vitendo vya nje na havikuwa na chochote kuhusu neno la Mungu. Mungu hangetambua kuwa nilikuwa nikiweka ukweli katika matendo. Kwa sababu sikuwa natenda kulingana na mahitaji ya Mungu na sikuwa natenda kwa mujibu wa ukweli, na kila kitu nilichofanya kilifanyika ili kukidhi tamaa zangu za kibinafsi na kufikia malengo yangu mwenyewe, kwa hiyo matendo yangu yalikuwa mabaya machoni pa Mungu; ilikuwa kumpinga Mungu.
Baada ya kutambua hili, niliunganisha neno la Mungu kwa makusudi ili nipate kuelewa asili yangu potovu katika maisha. Wakati nilionyesha upotovu wangu au nilipotambua kuwa hali yangu haikuwa sahihi, nilifichua waziwazi nafasi yangu na nikaichunguza na kutafuta chanzo kulingana na neno la Mungu. Nilipofanya hili, kunena kwangu na matendo yangu yakawa ya kawaida, na nilijua nafasi ambao nilipaswa kusimama. Nikawa na heshima kwa watu na kutii kwa uvumilivu. Kuunyima mwili kukawa sio kugumu sana na tukaweza kuwa mawasiliano ya dhati. Ushirikiano wetu ulikuwa umekuwa wa kuridhisha tena zaidi kuliko siku za nyuma.
Kupitia uzoefu huu, nimepata kuelewa kwamba kuweka ukweli katika vitendo lazima kuwekwe kwa msingi wa neno la Mungu na lazima kuanzishwe kwa kanuni za kweli. Mtu akiacha neno la Mungu, basi kila kitu kinakuwa kitendo cha nje, yaani, kuweka ukweli wa mawazo yao wenyewe katika matendo. Hata ikiwa ningefanya mambo vizuri na kwa usahihi, bado haingechukuliwa kama kuweka ukweli katika vitendo, na hata zaidi haingeleta mabadiliko kwa tabia ya maisha yangu. Kuanzia sasa kuendelea, bila kujali ni nini ninachofanya, nataka maneno ya Mungu kuwa kanuni za matendo yangu na kuweka neno la Mungu kikamilifu katika vitendo ili mwenendo wangu utalingana na ukweli na mapenzi ya Mungu na kupata kuridhika kwa Mungu. Utukufu wote Uwe kwa Mwenyezi Mungu!
kutoka kwa Ushuhuda wa Kuipitia Hukumu ya Kristo
Kujua zaidi: Kuhusu Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Alhamisi, 3 Mei 2018

Chochote Mungu Asemacho Ndiyo Hukumu Hasa ya Mwanadamu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, hukumu

Chochote Mungu Asemacho Ndiyo Hukumu Hasa ya Mwanadamu



Xunqiu    Mji wa Nanyang, Mkoa wa Henan
Nilikuwa nikidhani kwamba Mungu alimhukumu na kumuadibu mwanadamu wakati tu Alipoufichua upotovu wa asili wa mwanadamu au alipoeleza maneno mkali ambayo yaliuhukumu mwisho wa mwanadamu. Ilikuwa ni baadaye kabisa tu ambapo tukio moja liliponiongoza kutambua kwamba hata maneno mapole ya Mungu pia yalikuwa ni hukumu na kuadibu Kwake. Niligundua kuwa kila neno Alilolisema Mungu ni hukumu Yake kwa mwanadamu.
Hivi karibuni, dada mzee wa familia ya mwenyeji alipata kuhusika na hisia za kimwili, na kwa sababu hiyo aliteseka sana. Niliwasiliana naye kwa karibu mara kadhaa, lakini ilionekana kuwa bure.

Jumatano, 2 Mei 2018

Umeme wa Mashariki | Kuvunja Pingu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, hukumu

Umeme wa Mashariki | Kuvunja Pingu

Zhenxi Jijini Zhenzhou, Mkoani Hena
Miaka kumi iliyopita, nikiendeshwa na asili yangu ya kiburi, sikuweza kamwe kutii kikamilifu mipangilio ya kanisa. Ningetii ikiwa ilinifaa, lakini iwapo haingenifaa ningechagua iwapo ningetii au la. Hili lilisababisha kukiuka sana mipangilio ya kazi wakati wa kutimiza wajibu wangu. Nilifanya jambo langu mwenyewe na kuichukiza tabia ya Mungu, na hivyo baada ya hapo nilitumwa nyumbani.

Jumanne, 1 Mei 2018

New Swahili Gospel Movie "Siri ya Utauwa" | Bwana Yesu Kristo Atarudi Vipi?


New Swahili Gospel Movie "Siri ya Utauwa" | Bwana Yesu Kristo Atarudi Vipi?

Lin Bo'en alikuwa mzee wa kanisa katika kanisa la nyumbani Uchina. Wakati wa miaka yake yote kama muumini, alihisi kwamba ameheshimiwa kuteseka kwa ajili ya Bwana, na alithamini kumfahamu na kumpata Bwana Yesu Kristo zaidi ya kitu kingine chochote duniani. Siku moja ya jaala, alienda nje kuhubiri na akasikia habari fulani za kushtua: Bwana Yesu amerudi katika mwili, na Yeye ni Kristo wa siku za mwisho—Mwenyezi Mungu! Lin Bo'en alikanganyikiwa. Wakati Bwana atarudi, Anatakiwa kushuka na mawingu, kwa hiyo angejipatiaje mwili na kufanya kazi Yake kwa siri? Ni siri gani zilifichwa katika kupata mwili kwa Mungu? Ikiwa Bwana amerudi kweli, kwa nini hatujanyakuliwa? … Mjadala mkali sana unajitokeza kati ya Lin Bo'en na wafanyakazi wenzake na wahubiri kutoka kwa Kanisa la Mwenyezi Mungu … Je, hatimaye wataweza kuelewa kwamba Mwenyezi Mungu ni kurudi kwa Bwana Yesu, kuonekana kwa Mungu katika mwili?

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki
Soma Zaidi:  Umeme wa Mashariki Hutoka wapi?