Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Muziki wa Akapela "Tokeo Lililofikiwa kwa Kumjua Mungu" (Video Rasmi ya Muziki)

Hayuko katika upeo wa mbali, wala hajajificha juu mawinguni. Yuko kando yako, akiwa na mamlaka juu ya kila kitu chako, Yeye ni kila kitu ulicho nacho, na Yeye ni kitu pekee ulicho nacho.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Jumatano, 16 Mei 2018

"Imani katika Mungu" (6) - Imani ya Kweli katika Mungu Inamaanisha Nini?


"Imani katika Mungu" (6) - Imani ya Kweli katika Mungu Inamaanisha Nini?

Utambulisho

Watu wengi wanaamini kwamba imani katika Mungu ni imani katika Biblia, na kwamba kumfanyia Bwana kazi kwa bidii ni uhalisi wa kuamini katika Mungu. Hakuna mtu katika ulimwengu wa dini ana uwezo wa kuelewa kabisa imani ya kweli katika Mungu ina maana gani. Mwenyezi Mungu anasema, “‘Imani katika Mungu’ inamaanisha kuamini kuwa kuna Mungu; hii ndiyo dhana rahisi zaidi ya imani katika Mungu. Zaidi ya hayo, kuamini kuwa kuna Mungu sio sawa na kuamini katika Mungu kwa ukweli; bali, ni hali ya imani sahili ikiwa na vipengee vya uzito vya kidini. Imani ya kweli katika Mungu ina maana kupitia maneno na kazi ya Mungu kwa msingi wa imani kuwa Mungu ndiye mkuu juu ya vitu vyote. Kwa hivyo mtakuwa huru kutokana na tabia yenu ya upotovu, mtatimiza hamu ya Mungu, na mtapata kumjua Mungu. Ni kwa kupitia safari ya aina hii tu ndio mnaweza kusemekana kuwa mnaamini katika Mungu." ( Neno Laonekana katika Mwili).
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi Mungu

Soma Zaidi: Kujua Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Jumanne, 15 Mei 2018

39. Kutumia Neno la Mungu Kama Kioo

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, hukumu

39. Kutumia Neno la Mungu Kama Kioo

Wu Xia    Mji wa Linyi , Mkoa wa Shandong
Baada ya kuikubali kazi hii na kula na kunywa neno la Mungu, ilikuwa dhahiri kwangu kwamba ni muhimu sana kwamba mimi nijifahamu. Kwa hiyo, nilipokuwa nikila na kunywa neno la Mungu, nilihakikisha nimejithibitisha tena dhidi ya neno ambalo Mungu humfichua mwanadamu. Katika hali nyingi, niliweza kutambua kasoro zangu na upungufu.

"Imani katika Mungu" (5) - Je, Kufanya Kazi kwa Bidii kwa ajili ya Bwana ni Uhalisi wa Imani katika Bwana?


"Imani katika Mungu" (5) - Je, Kufanya Kazi kwa Bidii kwa ajili ya Bwana ni Uhalisi wa Imani katika Bwana?

Utambulisho

Waumini wengi huamini kwamba mradi tunalilinda jina la Bwana, kuomba mara kwa mara, kusoma Biblia na kuwa na mikutano, na mradi sisi huyaacha vitu, hutumia rasilmali na kufanya kazi kwa bidii kwa ajili ya Bwana, basi hii ni imani ya kweli katika Bwana, na tutaweza kunyakuliwa hadi katika ufalme wa mbinguni Bwana atakaporudi. Je, aina hii ya mtazamo ni sahihi? Wengi wataniita siku hiyo, Bwana, Bwana, hatujafanya unabii kwa jina lako? na kwa jina lako kutoa pepo? na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Halafu nitasema wazi kwao, Sikuwajua nyinyi kamwe: ondokeni mbele yangu, nyinyi watenda maovu." (Mathayo 7: 22-23). Mwenyezi Mungu anasema, "Sijali jinsi kazi yako ya bidii ni ya kutunukiwa, jinsi sifa zako ni za kuvutia, jinsi unanifuata Mimi kwa karibu, jinsi una umashuhuri, au jinsi umeendeleza mwelekeo wako; mradi hujafanya kile Ninachodai, kamwe hutaweza kushinda sifa Zangu." (Neno Laonekana katika Mwili).
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, wokovu
Soma Zaidi: Kujua Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Jumatatu, 14 Mei 2018

Umeme wa Mashariki | Ufafanuzi wa Tamko la Kumi na Sita

Umeme wa Mashariki | Ufafanuzi wa Tamko la Kumi na Sita

Mwenyezi Mungu alisema, Kwa watu, Mungu ni mkuu mno, mwenye utele mno, wa ajabu mno, Asiyeeleweka mno; machoni pao, maneno ya Mungu hupaa juu, na huonekana kama kazi bora sana ya ulimwengu. Lakini kwa vile watu wana kasoro nyingi sana, na akili zao ni za kawaida sana,

Jumapili, 13 Mei 2018

46. Maana halisi ya "Uasi dhidi ya Mungu"

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, ukweli

46. Maana halisi ya "Uasi dhidi ya Mungu"

Zhang Jun    Mji wa Shenyang, Mkoa wa Liaoning
Katika siku za nyuma, niliamini kuwa "uasi dhidi ya Mungu" ilimaanisha kumsaliti Mungu, kuacha kanisa, au kuutelekeza wajibu wa mtu. Nilidhani tabia hizi hufanyiza uasi. Kwa hiyo, wakati wowote niliposikia kuhusu watu wakihusika katika tabia hizo, ningejikumbusha kwamba sipaswi kuasi dhidi ya Mungu kama walivyofanya. Aidha, nilikuwa mwangalifu katika jitihada zangu zote na nilishikilia kazi zote nilizopewa na kanisa. 

"Imani katika Mungu" (4) - Je, Kuamini katika Biblia ni Sawa na Kuamini katika Bwana?


"Imani katika Mungu" (4) - Je, Kuamini katika Biblia ni Sawa na Kuamini katika Bwana?

Utambulisho

Watu wengi zaidi katika ulimwengu wa dini huamini kwamba Biblia ni kanuni ya Ukristo, kwamba mtu lazima ashikilie Biblia na kuweka msingi wa imani yake katika Bwana kwenye Biblia kabisa, na kwamba mtu hawezi kuitwa muumini akipotoka kutoka kwenye Biblia. Hivyo imani katika Bwana na imani katika Biblia ni sawa? Uhusiano kati ya Biblia na Bwana ni upi hasa? Bwana Yesu aliwakaripia Mafarisayo wakati fulani kwa maneno haya, "Tafuta katika maandiko; kwa kuwa ndani yake mnadhani kuwa mna uzima wa milele: na hayo ndiyo yananishuhudia. Nanyi hamtakuja Kwangu, kwamba mpate uhai." (Yohana 5:39-40). Biblia ni ushuhuda wa Mungu tu, lakini haina uzima wa milele. Mungu pekee ndiye ukweli, njia na uzima. Kwa hivyo, tuiangalie Biblia vipi kwa njia ambayo inakubaliana na mapenzi ya Bwana?

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki


Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.



Jumamosi, 12 Mei 2018

34. Kupata Ahueni kwa Njia ya Kumwamini Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, ukweli

34. Kupata Ahueni kwa Njia ya Kumwamini Mungu

Zhuanbian     Mji wa Shanghai

Ingawa nilikuwa nikimfuata Mungu kwa miaka mingi, nilikuwa karibu sijafanya maendeleo yoyote na kuingia kwangu katika maisha, na hii ilinifanya nihisi kuwa na wasiwasi sana. Hasa wakati niliposikia rekodi ya mahubiri juu ya kuingia kwa maisha, na kusikia mtu aliyetumiwa na Roho Mtakatifu akizungumza na ndugu wa kiume na wa kike waliokuwepo na kusikiliza mahubiri, nilihisi nikiwa nimejawa na wasiwasi nikimsikia akisema jambo kama hili, "Nyinyi sasa mnamwamini Mungu na mmeonja uzuri wa ukimbizaji wa ukweli. Nyinyi mmeanza kuingia kwa njia sahihi na mmejaa imani katika ukimbizaji wenu wa wokovu."

Ijumaa, 11 Mei 2018

Umeme wa Mashariki | Ni Nini Ambacho Kimeidanganya Roho Yangu?

Umeme wa Mashariki  | Ni Nini Ambacho Kimeidanganya Roho Yangu?

Xu Lei     Mji wa Zaozhuang, Mkoa wa Shandong
Siku moja nilipokea taarifa juu ya mkutano. Kwa kawaida hili ni tukio la kufurahisha, lakini mara tu nilipofikiria jinsi kazi yangu hivi karibuni ilikuwa machafuko kabisa, sikuweza kujizuia kuhisi wasiwasi. Kama mkuu wangu angejua jinsi sikuwa nimemaliza kazi yoyote yangu, bila shaka angehitaji kunishughulikia, na huenda hata kunibadilisha na mwingine kazini. Ningefanya nini basi?

"Imani katika Mungu" (3) - Je, Kazi ya Mungu na Kuonekana kwa Mungu Kunaleta Nini katika Jamii ya Dini?

"Imani katika Mungu" (3) - Je, Kazi ya Mungu na Kuonekana kwa Mungu Kunaleta Nini katika Jamii ya Dini?

Utambulisho


Kila wakati ambapo Mungu anakuwa mwili na kuonekana ili kufanya kazi Yake, nguvu za uovu za Shetani hupinga na kulaani njia ya kweli kwa ghadhabu. Kwa njia hii, vita vinatokea ndani ya dunia ya kiroho ambavyo hugawanya na kufunua ulimwengu wa dini. Bwana Yesu alisema, “Msifikiri kwamba nimekuja kuleta amani duniani: sikuja kuleta amani, bali upanga”(Mathayo 10:34). Wakati ambapo Bwana Yesu alionekana na kufanya kazi katika Enzi ya Neema, dini ya Kiyahudi iligawanyika katika vikundi vingi. Sasa kwa kuonekana kwa Mwenyezi Mungu na kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho, ulimwengu wa dini unapatwa na mfichuo mkubwa; ngano na magugu mwitu, kondoo na mbuzi, wanawali wenye busara na wanawali wapumbavu, na watumishi wazuri na watumishi wabaya —wote wanafunuliwa, kila mmoja na aina yake. Hekima ya Mungu na maajabu kweli ni ya kina sana!
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki

Soma Zaidi: Kujua Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Alhamisi, 10 Mei 2018

Umeme wa Mashariki | Mateso na Maafa Yalinisaidia Kukua

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, ushuhuda

Umeme wa Mashariki |  Mateso na Maafa Yalinisaidia Kukua

Baituo     Mji wa Dezhou, Mkoa wa Shandong
Kabla, nilijua tu kwamba hekima ya Mungu ilitumiwa kwa msingi wa njama za Shetani, kwamba Mungu ni Mungu mwenye hekima na kwamba Shetani milele atakuwa adui mshinde wa Mungu katika nadharia, lakini sikuwa na ufahamu au maarifa ya jambo hili kutegemeza uzoefu halisi. Baadaye, ni ndani tu ya mazingira yaliyopangwa na Mungu nilipopata uzoefu halisi wa kipengele hiki cha kweli.
Nilikuwa kwa mkutano fulani alasiri moja, wakati ghafla mwenzi wa kiongozi wa wilaya alikimbia kwangu kwa haraka na kusema, "Mama yako amechukuliwa na joka kubwa jekundu.

Umeme wa Mashariki | Niko Tayari Kukubali Usimamizi wa Wote

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, hukumu

 Umeme wa Mashariki | Niko Tayari Kukubali Usimamizi wa Wote

Xianshang     Mji wa Jinzhong, Mkoa wa Shanxi
Muda mfupi uliopita, kila wakati niliposikia kwamba wahubiri wa wilaya walikuwa wakija kwa kanisa letu, ningehisi kutaharaki kiasi. Sikufichua hisia zangu kwa nje, lakini moyo wangu ulijaa upinzani wa siri.

Jumatano, 9 Mei 2018

"Imani katika Mungu" (2) - Je, Njia Inayoshutumiwa na CCP na Miongoni mwa Watu wa Dini Siyo Njia ya kweli?


"Imani katika Mungu" (2) - Je, Njia Inayoshutumiwa na CCP na Miongoni mwa Watu wa Dini Siyo Njia ya kweli?

Utambulisho
Watu wengi hutafuta na kuchunguza njia ya kweli pasipo kutegemeza vitendo hivi katika maneno na kazi ya Mungu. Badala yake, wao hufuata mitindo ya ulimwengu wa dini na wanaamini kwamba kile ambacho serikali ya kikomunisti ya China na ulimwengu wa dini inalaani sio njia ya kweli—je, hii ni njia sahihi ya kuelekea? Biblia inasema, “dunia nzima hukaa ndani ya maovu."(1 Yohana 5:19). “Hiki ni kizazi kiovu” (Luka 11:29). Hivyo inaweza kuonekana kwamba mifumo ya kisiasa ya kukana Mungu na ulimwengu wa dini hakika utakana na kuishutumu njia ya kweli. Wakati ambapo Bwana Yesu alifanya kazi Yake katika Enzi ya Neema, serikali ya Kiyahudi na ya Kirumi zilimpinga na kumtia hatiani kwa hasira, na mwishowe Bwana Yesu alisulubishwa msalabani. Je, si huu ni ukweli wa hali? Mwenyezi Mungu anapokuja kufanya kazi Yake katika siku za mwisho, Anapitia uasi mkali na shutuma ya serikali ya China na ulimwengu wa dini. Hili linaonyesha nini? Je, si hili linastahili sisi kulitafakari?
Kanisa la Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki
Soma Zaidi: Kujua Kanisa la Mwenyezi MunguUmeme wa Mashariki Hutoka wapi?