Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Muziki wa Akapela "Tokeo Lililofikiwa kwa Kumjua Mungu" (Video Rasmi ya Muziki)

Hayuko katika upeo wa mbali, wala hajajificha juu mawinguni. Yuko kando yako, akiwa na mamlaka juu ya kila kitu chako, Yeye ni kila kitu ulicho nacho, na Yeye ni kitu pekee ulicho nacho.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Jumatano, 24 Aprili 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 120

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 120

Sayuni! Salamu! Sayuni! Ita kwa sauti! Nimerudi kwa ushindi, Nimerudi nikiwa mshindi! Watu wote! Harakisheni mpange foleni kwa utaratibu! Vitu vyote! Mtakuja kusimama kabisa, kwa sababu nafsi Yangu inaukabili ulimwengu mzima na nafsi Yangu inaonekana katika Mashariki ya dunia! Nani anayethubutu kutopiga magoti katika ibada? Nani anayethubutu kutosema kumhusu Mungu wa kweli? Nani anayethubutu kutoangalia juu kwa kumcha? Nani anayethubutu kutotoa sifa? Nani anayethubutu kutangaza kwa shangwe? Watu wangu wataisikia sauti Yangu, Wanangu watasalia ndani ya ufalme Wangu!

Jumanne, 23 Aprili 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 114

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 114

Niliumba ulimwengu dunia; Nilitengeneza milima, mito, na vitu vyote; Niliunda miisho ya mifumo ya sayari; Niliwaongoza wana Wangu na watu Wangu; Niliamuru vitu na mambo yote. Sasa, Nitawaongoza wazaliwa Wangu wa kwanza warudi kwenye Mlima Wangu Sayuni, kurudi mahali ambapo Naishi, ambayo itakuwa hatua ya mwisho katika kazi Yangu. Yote ambayo Nimeyatenda (kila kitu kilichofanyika kutoka uumbaji mpaka sasa) yalikuwa kwa sababu ya hatua ya leo ya kazi Yangu, na zaidi ni kwa sababu ya utawala wa kesho, ufalme wa kesho, na kwa ajili ya Mimi na wazaliwa Wangu wa kwanza kuwa na furaha ya milele.

Jumatatu, 22 Aprili 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 14


Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 14


Katika enzi zote, hakuna mwanadamu ameingia katika ufalme na hivyo hakuna aliyefurahia neema ya Enzi ya Ufalme, hakuna aliyeona Mfalme wa ufalme. Ingawa chini ya nuru ya Roho Wangu watu wengi wametabiri uzuri wa ufalme, wanajua tu nje ya ufalme, sio umuhimu wa ndani. Leo, ufalme ujapo kuwepo rasmi duniani, binadamu wote bado hujui kinachopaswa kukamilishwa, ulimwengu ambao binadamu hatimaye ataletwa ndani, wakati wa Enzi ya Ufalme. Kuhusu haya, Naogopa watu wote wako katika hali ya mkanganyiko. Kwa sababu siku ya utambuzi kamili wa ufalme bado haijafika kabisa, wanadamu wote wamechanganyikiwa, hawawezi kuiona vizuri.

Jumapili, 21 Aprili 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 35

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 35

Nimeanza kutenda kazi Yangu kati ya wanadamu, kuwakubalia kuishi mkondo mmoja Nami. Nitakamilisha kazi Yangu nikiwa kati yao, maana wao ni vyombo Ninavyosimamia katika mpango Wangu wote wa usimamizi—na ni mapenzi Langu ili waweze kuwa watawala wa vitu vyote. Hivyo basi Naendelea kutembea kati ya wanadamu. Kadri wanadamu pamoja Nami tuingiavyo katika enzi ya sasa, Najihisi huru kabisa, kwa sababu, hatua Yangu ni ya haraka.

Jumamosi, 20 Aprili 2019

Wimbo wa Kuabudu | "Tabia ya Haki ya Mungu ni ya Pekee" | How to Know God


Wimbo wa Kuabudu | "Tabia ya Haki ya Mungu ni ya Pekee" | How to Know God
Mungu huonyesha tabia Yake ya haki kupitia mbinu na kanuni za kipekee,
haidhibitiwi na watu, matukio au vitu.
au kumshawishi Ajaribu njia tofauti.
Na hakuna awezaye kubadili dhana au mawazo Yake,
Mungu huhuku matendo na mawazo yote ya viumbe kwa tabia Yake ya haki.
Hii ndiyo asili ya kipekee ya tabia ya haki ya Muumba! Tabia Yake ya haki!
Na hakuna awezaye kubadili rehema au ghadhabu Yake.
Na kulingana na hili, Hutoa ghadhabu au kupeana rehema. Na ni kiini Chake tu kiwezacho kuamua njia hii.
hakuna awezaye kiuka au kushuku hili.
Hii ndiyo asili ya kipekee ya tabia ya haki ya Muumba! Tabia Yake ya haki! Tabia ya haki ya Mungu, takatifu na ya kipekee;
Hii ni asili ya kipekee ya tabia ya haki ya Muumba!
Hakuna awezaye kuimiliki, kiumbwacho au kisichoumbwa. Ghadhabu ya Mungu ni takatifu; haiwezi kukosewa. Rehema Yake pia yabeba asili hii. Tabia Yake ya haki!
Hii ndiyo asili ya kipekee ya tabia ya haki ya Muumba!
Hakuna mbadala wa Mungu katika Matendo Yake, kiumbwacho au kisichoumbwa. Wala hawezi kuuharibu Sodoma au kuuokoa Ninawi kama alivyofanya Mungu. Tabia Yake ya haki! Tabia Yake ya haki!

 
kutoka katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

Kujua zaidi: Umeme wa Mashariki Hutoka wapi?  Sauti na maneno ya Roho Mtakatifu | "Ni Muhimu Sana Kuelewa Tabia ya Mungu"

Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III Mamlaka ya Mungu II” Sehemi ya Tatu

Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III Mamlaka ya Mungu II” Sehemi ya Tatu
Mwenyezi Mungu alisema, "Baada ya mtu kupita utoto na wakati wake wa kubaleghe na kwa utaratibu bila kuzuilika kufikia ukomavu, hatua inayofuata ni kwake yeye kuuaga kabisa ule ujana wake, kuwaaga wazazi wake, na kukabiliana na barabara iliyo mbele yake akiwa mtu mzima huru. Wakati huo[c] lazima wakabiliane na watu, matukio na mambo yote ambayo mtu mzima lazima apitie, na kukabiliana na viungo mbalimbali katika msururu wa hatima yake. Hii ndiyo awamu ya tatu ambayo lazima mtu apitie."

Kujua zaidi: Utangulizi wa programu ya Kanisa la Mwenyezi Mungu | Injili ya kurudi kwa Bwana Yesu . Umeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Ijumaa, 19 Aprili 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Ngurumo Saba Zatoa Sauti—Zikitabiri Kuwa Injili ya Ufalme Itaenea Kote Ulimwenguni

Matamshi ya Mwenyezi Mungu Ngurumo Saba Zatoa Sauti—Zikitabiri Kuwa Injili ya Ufalme Itaenea Kote Ulimwenguni

Mimi Naeneza kazi Yangu katika nchi za Mataifa. Utukufu Wangu unamulika kotekote ulimwenguni; mapenzi Yangu yamo katika wanadamu yakitawanyika hapa na pale, wote wakiongozwa kwa mkono Wangu na kufanya kazi ambayo Nimewapa. Kuanzia wakati huu kuendelea, Nimeingia katika enzi mpya, kuwaleta watu wote katika ulimwengu mwingine. Niliporudi katika “nchi Yangu,” Nilianza sehemu nyingine tena ya kazi katika mpango Wangu wa asili, ili mwanadamu aje kunijua zaidi. Nauchukua ulimwengu katika ukamilifu wake na kuona kwamba[a] ni wakati muafaka wa kazi Yangu, kwa hiyo Naharakisha mbele na nyuma kufanya kazi Yangu mpya ndani ya mwanadamu. Hii ni enzi mpya, hata hivyo, na Nimeleta kazi mpya ili Niwachukue watu wapya wengi zaidi katika enzi mpya na kuachana na wengi wa wale Nitakaowaondoa.

Jumatano, 17 Aprili 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Wote Wasiomjua Mungu Ndio Wanaompinga Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Kazi ya Mungu,kumjua mungu

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Wote Wasiomjua Mungu Ndio Wanaompinga Mungu

Kufahamu madhumuni ya kazi ya Mungu, athari inayotimizwa kwa mwanadamu, na mapenzi ya Mungu kwa mwanadamu, hiki ndicho kitu ambacho kila mwanadamu anayemfuata Mungu anapaswa kutimiza. Sasa wanachokosa watu wote ni ufahamu wa kazi ya Mungu. Mwanadamu haelewi wala kufahamu kabisa maana ya vitendo vya Mungu ndani ya mwanadamu, kazi yote ya Mungu, na mapenzi ya Mungu tangu kuumbwa kwa dunia. Huu upungufu hauonekani tu katika ulimwengu mzima wa kidini, lakini zaidi ya hayo kwa waumini wote wa Mungu.

Jumanne, 16 Aprili 2019

“Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee X Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (IV)” Sehemu ya Tatu


“Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee X Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (IV)” Sehemu ya Tatu

3. Mzunguko wa Uhai na Mauti wa Watu Wanaomfuata Mungu

Baada ya hayo, hebu tuzungumzie mzunguko wa uhai na mauti wa wale wanaomfuata Mungu. Hili linawahusu, hivyo kuweni makini. Kwanza, fikiria kuhusu ni makundi gani ambamo watu wanaomfuata Mungu wanaweza kugawika. (Wateule wa Mungu na watendaji huduma.) Kuna mawili: wateule wa Mungu na watendaji huduma. Kwanza tutazungumza kuhusu wateule wa Mungu, ambao ni wachache. “Wateule wa Mungu” inarejelea nini?

Jumatatu, 15 Aprili 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Tabia Yako Ni Duni Sana!




Kanisa la Mwenyezi Mungu,Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki

Matamshi ya Mwenyezi MunguTabia Yako Ni Duni Sana!

Ninyi nyote mmeketi katika viti vya kifahari, mkiwafundisha wale wa vizazi vijana ambao ni wa aina yenu, ukiwafanya waketi nawe. Je, mngekosaje kujua kwamba wale “watoto” wenu walikuwa tayari hawana pumzi, na kwamba hawakuwa na kazi Yangu zamani? Utukufu Wangu huangaza kutoka nchi ya Mashariki hadi nchi ya Magharibi, lakini wakati utukufu Wangu huenea mpaka mwisho wa dunia na wakati unapoanza kuinuka na kuangaza, Nitaondoa utukufu wa Mashariki na kuuletea Magharibi ili kwamba watu hawa wa giza katika Mashariki ambao wameniacha Mimi watakuwa bila mwanga unaong’aa kuanzia hapo kwendelea. Wakati huo, mtaishi katika bonde la kivuli. Ingawa watu leo ni wazuri mara mia zaidi kuliko awali, bado hawawezi kuyatosheleza mahitaji Yangu, na bado wao si ushahidi mtukufu Kwangu. 

Jumapili, 14 Aprili 2019

Wimbo wa Kuabudu | "Sifa kwa Maisha Mapya katika Ufalme" | Watu wa Mungu Humsifu na Kumwabudu Mungu


Wimbo wa Kuabudu | "Sifa kwa Maisha Mapya katika Ufalme" | Watu wa Mungu Humsifu na Kumwabudu Mungu

Tumesikia sauti ya Mungu na kurudi nyumbani Kwake.
Mikutanoni tunakula na kunywa maneno ya Mungu, tunahudhuria karamu.
Sisi tunaaga huzuni na vifungo vyetu, tunaishi maisha mapya.
Tunapofungua mioyo yetu katika ushirika wa kweli, mioyo yetu inaangazwa sana.
Maneno ya Mungu yako nasi kila siku, tunastarehe ndani yake.
Tunaondolewa vizuizi na ubaguzi wetu, tunaishi ndani ya upendo wa Mungu.
Tunatafakari, kufikiri maneno ya Mungu, Roho Mtakatifu anatuangazia.
Tunaelewa moyo wa Mungu, sisi si hasi tena.

Ijumaa, 12 Aprili 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Umuhimu wa Kuukoa Uzao wa Moabu

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Umuhimu wa Kuukoa Uzao wa Moabu

Katika miaka hii miwili hadi mitatu ya kazi, kile kilichopaswa kutimizwa katika kazi ya hukumu iliyofanyika juu yenu kimetimizwa kimsingi. Watu wengi wamesahau matarajio na kudura yao ya baadaye. Hata hivyo, inapotajwa kuwa ninyi ni uzao wa Moabu, wengi wenu huchukizwa sana—nyuso zenu hubadilika, vinywa vyenu hupinda, na macho yenu hukodolea. Hamuwezi kabisa kuamini kwamba ninyi ni uzao wa Moabu.