Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Muziki wa Akapela "Tokeo Lililofikiwa kwa Kumjua Mungu" (Video Rasmi ya Muziki)

Hayuko katika upeo wa mbali, wala hajajificha juu mawinguni. Yuko kando yako, akiwa na mamlaka juu ya kila kitu chako, Yeye ni kila kitu ulicho nacho, na Yeye ni kitu pekee ulicho nacho.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Alhamisi, 28 Februari 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 8


Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 8

 Mungu anenapo neno Lake kutokana na mtazamo wa Roho, sauti Yake huelekezwa kwa wanadamu wote. Mungu anenapo neno Lake kutokana na mtazamo wa mwanadamu, sauti Yake huelekezwa kwa wote wafuatao uongozi wa Roho Wake. Mungu anenapo neno Lake kutokana na mtazamo wa nafsi ya tatu (kile ambacho watu hutaja kama mtazamaji), Anaonyesha neno Lake moja kwa moja kwa watu ili watu wamwone kama mtoa maoni, na huonekana kwamba kutoka kinywani Mwake hutoka mambo yasiyo na kikomo ambayo mwanadamu hayajui, mambo ambayo mwanadamu hawezi kuelewa.

Jumatano, 27 Februari 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Utendaji (2)


  Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Utendaji (2)


Katika nyakati zilizopita, watu walijifundisha wenyewe kuwa na Mungu na kuishi katikati ya roho kila wakati, ambao, ukilinganishwa na utendaji wa leo, ni mafundisho rahisi ya kiroho tu. Utendaji kama huu huja kabla ya kuingia kwa watu katika njia sahihi ya maisha, na ni mbinu ya juujuu zaidi na rahisi zaidi kati ya mbinu zote za utendaji. Ni utendaji wa hatua za mwanzoni kabisa za imani ya watu kwa Mungu. Ikiwa watu wataishi kila mara kwa utendaji huu, watakuwa na hisia nyingi sana, na hawataweza kuingia katika uzoefu ambao ni wa kina na wa kweli.

Jumanne, 26 Februari 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Kazi na Kuingia (3)


Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Kazi na Kuingia (3)


    Mungu amewaaminia wanadamu vitu vingi sana na Amezungumza bila kikomo juu ya kuingia kwao. Lakini kwa sababu ubora wa tabia ya watu ni duni mno, maneno mengi ya Mungu yameshindwa kuanza kustawi. Kuna sababu mbalimbali za huu ubora duni wa tabia, kama vile uharibifu wa mawazo na maadili ya binadamu, na kutokuwa na malezi mazuri; imani za usihiri zilizojaa moyoni mwa mwanadamu; mitindo ya maisha iliyopotoka ambayo imeweka maovu mengi katika sehemu ya ndani kabisa ya moyo wa mwanadamu;

Jumatatu, 25 Februari 2019

Neno la Mungu | Ni Lazima Wale Wanaofaa Kukamilishwa Wapitie Usafishaji

Kama unamwamini Mungu, ni lazima umtii Mungu, uweke ukweli katika vitendo na utimize wajibu wako wote. Zaidi ya hayo, ni lazima uelewe mambo unayopaswa kupitia. Ikiwa unapitia tu kushughulikiwa, kufundishwa nidhamu na hukumu, kama wewe unaweza tu kumfurahia Mungu, lakini huwezi kuhisi wakati Mungu anakufundisha nidhamu au kukushughulikia, hili halikubaliki. Labda katika wakati huu wa usafishaji unaweza kushikilia msimamo wako.

Jumapili, 24 Februari 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Hudumu kama Waisraeli Walivyofanya


Siku hizi watu wengi hawatilii maanani mafunzo yapi yanayopaswa kusomwa wakati wa upatano na wengine. Nimegundua kuwa wengi wenu hawawezi kujifunza mafunzo hata kidogo wakati wa ushirikiano na wengine. Wengi wenu mnashikilia maoni yenu mwenyewe, na wakati mnafanya kazi kanisani, unatoa maoni yako na yeye anatoa yake, moja uhusiano na mingine, bila kushirikiana kabisa. Mnajihusisha tu katika kutoa umaizi wenu wenyewe wa ndani, unaingia tu katika kuachilia huru “mizigo” ndani yenu, si kutafuta uzima hata kidogo.

Jumamosi, 23 Februari 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Maana ya Kuwa Mwanadamu Halisi


Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Maana ya Kuwa Mwanadamu Halisi


Kumsimamia mwanadamu ndio Kazi Yangu, na ushindi Wangu dhidi yake ni kitu ambacho kilikuwa hata zaidi kimeshaamuliwa kabla Nilipoiumba dunia. Watu huenda hawajui kwamba Nitashinda kabisa katika siku za mwisho na pia huenda hawajui kwamba ushahidi Wangu kumshinda Shetani ni kuwashinda wale walio waasi miongoni mwa binadamu. Lakini, adui Yangu alipoungana katika vita na Mimi, Nilikuwa Nimeshamwambia kwamba Nitakuwa mshindi wa wale waliokuwa wamechukuliwa na Shetani na kufanywa watoto wake na watumishi wake waaminifu wanaoangalia nyumba yake.

Ijumaa, 22 Februari 2019

Neno la Mungu | "Kuonekana kwa Mungu Kumeleta Enzi Mpya"

Neno la Mungu | “Kuonekana kwa Mungu Kumeleta Enzi Mpya”

    
    Mwenyezi Mungu anasema, "Kuonekana kwa Mungu hurejelea kuwasili Kwake duniani kufanya kazi Yake. Akiwa na utambulisho na tabia Yake, na katika mbinu Yake ya asili, Yeye hushuka miongoni mwa wanadamu kufanya kazi ya kuanzisha enzi mpya na kukamilisha enzi nyingine. Kuonekana kwa aina hii si aina fulani ya sherehe. Si ishara, picha, muujiza, au ono kuu, na hata zaidi si mchakato fulani wa kidini. Ni ukweli halisi ambao waweza kushikwa na kuonekana.

Alhamisi, 21 Februari 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Kuhusu Uzoefu


Katika uzoefu wote wa Petro, alikumbana na mamia ya majaribio. Ingawa watu wa leo wanafahamu neno “jaribio,” wao huchanganyikiwa kuhusiana na maana yake ya kweli na hali. Mungu hutuliza azimio la watu, husafisha imani yao, na hukamilisha kila sehemu yao—na hii hufanikishwa kimsingi kupitia majaribio, ambayo pia ni kazi ya Roho Mtakatifu iliyofichwa. Inaonekana kama kwamba Mungu amewaacha watu, na kwa hivyo wasipokuwa waangalifu, watayaona majaribio haya kama majaribu ya Shetani.

Jumatano, 20 Februari 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Je, Wewe Ni Muumini wa Kweli wa Mungu?

Matamshi ya Mwenyezi Mungu  | Je, Wewe Ni Muumini wa Kweli wa Mungu?


Huenda ikawa safari yako ya imani katika Mungu imekuwa ndefu zaidi ya mwaka mmoja au miwili, na labda kwa maisha yako umestahimili ugumu mwingi miaka hii yote; au labda haujapitia ugumu na badala yake umepokea neema nyingi. Kuna uwezekano pia kuwa hujapitia ugumu wala kupokea neema, na badala yake umeishi maisha ya kawaida tu. Hiyo haijalishi, kwani wewe bado u mfuasi wa Mungu, kwa hivyo tushirikiane kuhusu mada ya kumfuata Mungu.

Jumanne, 19 Februari 2019

Neno la Mungu | Jinsi Hatua ya Pili ya Kazi ya Ushindi Huzaa Matunda


Neno la Mungu | Jinsi Hatua ya Pili ya Kazi ya Ushindi Huzaa Matunda


Hatua ya kazi ya watenda-huduma ni hatua ya kwanza ya kazi ya ushindi; kwa sasa hii ni hatua ya pili ya kazi ya ushindi. Kwa nini ukamilifu unajadiliwa katika kazi ya ushindi? Ni kuujenga msingi kwa ajili ya siku za baadaye—kwa sasa hii ni hatua ya mwisho katika kazi ya kushinda, na baada ya hii, kazi ya kuwakamilisha watu itaanza rasmi wakati watakuwa wanapitia dhiki kuu. Jambo la msingi sasa ni ushindi; hata hivyo, hii pia ni hatua ya kwanza ya kukamilisha, kukamilisha ufahamu na utii wa watu, ambayo kwa kweli bado yanajenga msingi wa kazi ya kushinda.

Jumatatu, 18 Februari 2019

Neno la Mungu | Sura ya 26

Neno la Mungu | Sura ya 26

Ni nani ameshinda nyumbani Kwangu? Ni nani amesimama kwa ajili Yangu? Ni nani ameteseka kwa ajili Yangu? Ni nani ameweka ahadi yake mbele Zangu? Ni nani amenifuata hadi leo lakini hajakuwa wa kutojali? Mbona wanadamu wote wana ubaridi na hawana hisia? Mbona binadamu ameniacha? Mbona mwanadamu amechoka na Mimi? Mbona hakuna joto katika ulimwengu wa mwanadamu? Nikiwa Zayuni, Nimeonja joto lililo mbinguni, na Nikiwa Zayuni Nimefurahia baraka iliyoko mbinguni.

Jumapili, 17 Februari 2019

Ishini Katika Upendo wa Mungu | "Wimbo wa Mapenzi Matamu" | Best Swahili Christian nyimbo za kuabudu


Ishini Katika Upendo wa Mungu | "Wimbo wa Mapenzi Matamu" | Best Swahili Christian nyimbo za kuabudu


Kinani mwa moyo wangu, ni mapenzi Yako. Ni matamu sana, nakaa karibu yako.
Kukutunza hukoleza moyo wangu; kukutumikia na mawazo yangu yote.
Kuongoza moyo wangu, ni mapenzi Yako; mimi hufuata nyayo zako za mapenzi.
Mimi hujisogeza kulingana na macho Yako; mapenzi yanaonyesha furaha ya moyo wangu.

Jumamosi, 16 Februari 2019

Neno la Mungu | Wale Waliokamilishwa Pekee Ndio Wanaoweza Kuishi Maisha Yenye Maana

Neno la Mungu | Wale Waliokamilishwa Pekee Ndio Wanaoweza Kuishi Maisha Yenye Maana

    Mwenyezi Mungu anasema, "Wale waliofanywa kuwa wakamilifu hawawezi tu kuwa watiifu baada ya kushindwa, lakini wanaweza pia kuwa na maarifa wa kazi ya hukumu, kubadilisha tabia yao na kumjua Mungu. Wanapitia njia ya kumpenda Mungu na wamejazwa na ukweli. Wanajua namna ya kupitia kazi ya Mungu, wanaweza kuteseka kwa ajili ya Mungu, na wanayo hiari zao wenyewe. Wale waliokamilishwa ni wale walio na ufahamu halisi wa ukweli kutokana na kupitia neno la Mungu. Wale walioshindwa ni wale wanaojua kuhusu ukweli lakini hawajakubali maana halisi ya ukweli."

Yaliyopendekezwa:  APP Programu ya Kanisa la Mwenyezi Mungu 

Ijumaa, 15 Februari 2019

Nyimbo za Injili | "Njia Yote Pamoja na Wewe" Mungu ni Upendo

Nyimbo za Injili | "Njia Yote Pamoja na Wewe" Mungu ni Upendo 


Nilikuwa kama mashua, ikielea baharini.
Ulinichagua, na mahali pazuri Uliniongoza.
Sasa katika familia Yako, nikipewa joto na upendo Wako,
nina amani kabisa.
Unanibariki, Unatoa maneno Yako ya hukumu.
Bado sijui jinsi ninavyokosa kuithamini neema Yako.
Kila mara nikiasi, kwa namna fulani nikiuumiza moyo Wako.

Alhamisi, 14 Februari 2019

Nyimbo za Kuabudu "Upendo wa Kweli wa Mungu" | Haleluya! Msifuni Mungu! (Korean Song Swahili Subtitle)


Nyimbo za Kuabudu | "Upendo wa Kweli wa Mungu" | Haleluya! Msifuni Mungu! (Korean Song Swahili Subtitles)


Leo naja mbele ya Mungu tena,
naona uso Wake wa kupendeza.
Leo naja mbele ya Mungu tena,
nimeacha siku zangu za zamani za kuzurura nyuma yangu.
Leo naja mbele ya Mungu tena,
kufurahia neno Lake kunanijaza na furaha.

Jumatano, 13 Februari 2019

Filamu za Injili | “Siri ya Utauwa” (3) - Siri ya Kupata Mwili kwa Mungu


Filamu za Injili | “Siri ya Utauwa” (3) - Siri ya Kupata Mwili kwa Mungu


     Katika Enzi ya Neema, Mungu alipata mwili na akawa Bwana Yesu aliyekuja kuwakomboa wanadamu, na Mafarisayo wa Kiyahudi wakasema kwamba Bwana Yesu alikuwa mwanadamu tu. Katika siku za mwisho, Mungu amepata mwili na amekuwa Mwenyezi Mungu ambaye Amekuja kufanya kazi Yake ya hukumu, wachungaji na wazee wa kanisa wa ulimwengu wa kidini pia wanasema kwamba Mwenyezi Mungu ni mwanadamu tu, kwa hiyo tatizo ni lipi hapa? Kwa upande wa nje, Mungu mwenye mwili Anaonekana kuwa mtu wa kawaida. Lakini ndani Roho wa Mungu anaishi ndani Yake; Anaweza kuonyesha ukweli, kuonyesha sauti ya Mungu na kufanya kazi ya Mungu, kwa hiyo Mungu mwenye mwili ni mwanadamu, au ni Mungu?

Jumanne, 12 Februari 2019

Gospel Movie Clip “Siri ya Utauwa” (4) - Mungu Mwenye Mwili pekee Ndiye Anaweza Kufanya Kazi ya Hukumu Katika Siku za Mwisho



Umeme wa Mashariki unashuhudia kwamba Mungu amepata mwili katika siku za mwisho kufanya kazi ya hukumu Mwenyewe. Lakini kazi ya Mungu katika Enzi ya Sheria ilifanywa kwa kumtumia Musa. Kwa hiyo kazi ya Mungu ya hukumu katika siku za mwisho haiwezi kufanywa kwa namna hiyo hiyo, kwa kuwatumia watu? Kwa nini Mungu anahitaji kupata mwili na kuifanya Mwenyewe? Mwenyezi Mungu asema, "Kazi ya hukumu ni kazi ya Mungu Mwenyewe, kwa hivyo lazima ifanywe na Mungu Mwenyewe kwa kawaida; haiwezi kufanywa na mwanadamu kwa niaba Yake. Kwa sababu hukumu ni kumshinda mwanadamu kupitia ukweli, hakuna shaka kuwa Mungu bado Anaonekana kama kiumbe aliyepata mwili kufanya kazi hii miongoni mwa wanadamu" (Neno Laonekana katika Mwili).

Jumatatu, 11 Februari 2019

Maneno ya Roho Mtakatifu | “Kazi ya Mungu na Utendaji wa Mwanadamu” (Sehemu ya Kwanza)



Maneno ya Roho Mtakatifu | “Kazi ya Mungu na Utendaji wa Mwanadamu” (Sehemu ya Kwanza)


    Mwenyezi Mungu anasema, "Katika kila aina ya kazi ya Mungu kuna maono yanayofahamika na mwanadamu; maono yanayofuatwa na matarajio mwafaka ya Mungu kwa mwanadamu. Bila haya maono kama msingi, mwanadamu hawezi kuwa na uwezo wa utendaji na pia hangeweza kumfuata Mungu bila kuyumbayumba. Ikiwa mwanadamu hamjui Mungu au hayaelewi mapenzi ya Mungu, basi yote ayafanyayo ni bure na yasiyoweza kukubalika na Mungu.

Jumapili, 10 Februari 2019

Neno la Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III Mamlaka ya Mungu (II)” Sehemu ya Saba


Neno la Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III Mamlaka ya Mungu (II)” Sehemu ya Saba


Maneno ya Mungu katika video hii ni kutoka kitabu “Neno Laonekana katika Mwili”.

Maudhui ya video hii:
Hakuna Anayeweza Kubadilisha Hoja Kwamba Mungu Anashikilia Ukuu juu ya Hatima ya Binadamu
Mtazamo na Matendo Bora ya Mtu Anayependa Kujinyenyekeza katika Mamlaka ya Mungu
Kumkubali Mungu kama Bwana Wenu wa Kipekee Ndiyo Hatua ya Kwanza katika Kutimiza Wokovu

Baadhi ya Makala: Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee V Utakatifu wa Mungu (II)” Sehemu ya Kwanza"

Jumamosi, 9 Februari 2019

nyimbo za injili | Toa Akili na Mwili ili Kutimiza Agizo la Mungu


Nyimbo za InjiliToa Akili na Mwili ili Kutimiza Agizo la Mungu

I
Kama washiriki wa jamii ya wanadamu,
Kama wafuasi wa Kristo wa dhati,
ni wajibu wetu, ni jukumu letu
kutoa akili zetu na miili yetu
kwa kutimiza agizo la Mungu.
Kwa maana asili yetu yote ilitoka kwa Mungu,
na twaishi, kwa ajili ya ukuu Wake.
Kwa maana asili yetu, ilitoka kwa Mungu,
na twaishi, kwa ajili ya ukuu Wake.

Ijumaa, 8 Februari 2019

Matamshi ya Mungu | “Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo ya Kazi Yake” Sehemu ya Tatu

Matamshi ya Mungu | “Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo ya Kazi Yake” Sehemu ya Tatu

Namna Ambavyo Mungu Huanzisha Matokeo Ya Binadamu na Kiwango Ambacho Hutumia Kuasisi Matokeo ya Binadamu

Kabla ya kuwa na mitazamo au hitimisho zako binafsi, unafaa kwanza kuelewa mwelekeo wa Mungu kwako, kile ambacho Mungu anafikiria, na kuamua kama kufikiria kwako ni sahihi au la. Mungu hajawahi kutumia vipimo vya muda katika kuasisi matokeo ya mtu, na Hajawahi kutumia kiwango cha mateso yaliyovumiliwa na mtu katika kuasisi matokeo yake.

Alhamisi, 7 Februari 2019

Imani za Kimsingi za Kanisa la Mwenyezi Mungu

Imani za Kimsingi za Kanisa la Mwenyezi Mungu


(1) Mafundisho ya Kanisa la Mwenyezi Mungu

Mafundisho ya Ukristo yanatoka kwa Biblia, na mafundisho ya Kanisa la Mwenyezi Mungu yanatoka kwa ukweli wote ulioonyeshwa na Mungu tangu wakati wa uumbaji wakati wa kazi ya Enzi ya Sheria, Enzi ya Neema, na Enzi ya Ufalme. Hiyo ni kusema, Agano la Kale, Agano Jipya, na Biblia ya Enzi ya Ufalme–Neno Laonekana Katika Mwili–zilizoonyeshwa Bwana Yesu aliyekurudi wa siku za mwisho, Mwenyezi Mungu, ni imani za msingi na mafundisho ya Kanisa la Mwenyezi Mungu.

Jumatano, 6 Februari 2019

Je, Kanisa la Mwenyezi Mungu Lina Malengo Yapi?

Je, Kanisa la Mwenyezi Mungu Lina Malengo Yapi?

     Kanisa la Mwenyezi Mungu hunyunyizia na kuwaongoza waumini wake kwa mujibu kamili wa maneno ya Mungu katika Biblia na Neno Laonekana Katika Mwili yanayoonyeshwa na Mwenyezi Mungu, ili kwamba kila muumini anaweza, chini ya uongozi, utolewaji, unyunyiziwaji, na uongozwaji wa maneno ya Mwenyezi Mungu, kuelewa ukweli wote katika maneno ya Mungu, kumiliki mtazamo sahihi juu ya maisha na maadili, kuwa na malengo sahihi ya kufuatilia, kufuata njia ya Mungu, kushikilia maagizo ya Mungu, kumtukuza Mungu kwa kuwa nuru na chumvi ya dunia, na kusifiwa na Mungu, na kuwa na sifa kamili kurithi ahadi za Mungu.

Jumanne, 5 Februari 2019

Kanisa la Mwenyezi Mungu | 2. Utangulizi Mfupi Kuhusu Usuli wa Kuonekana kwa Kazi ya Kristo wa Siku za Mwisho Nchini China


    China ni nchi ambamo joka kubwa jekundu hukaa, na ni mahali ambapo pamempinga na kumshutumu Mungu zaidi sana katika historia. China ni kama ngome ya mapepo na gereza linalodhibitiwa na shetani, lisilopenyeka na lisiloingilika. Zaidi ya hayo, utawala wa joka kubwa jekundu husimama ukilinda katika ngazi zote na umeanzisha ulinzi katika kila kaya. Matokeo yake, hakuna mahali pagumu zaidi ya hapa kueneza injili ya Mungu na kufanya kazi ya Mungu.

Jumatatu, 4 Februari 2019

Ushuhuda wa Maisha | 11. Kiini cha Ulipizaji Kisasi wa Mtu Binafsi

Ushuhuda wa Maisha | 11. Kiini cha Ulipizaji Kisasi wa Mtu Binafsi

Zhou Li Mji wa Xintai, Mkoa wa Shandong

     Wakati fulani kitambo, tulihitaji kuzichora wilaya katika eneo letu, na kwa msingi wa kanuni zetu kwa ajili ya uteuzi wa viongozi, kulikuwa na ndugu mmoja wa kiume aliyekuwa mtaradhia mzuri kiasi. Nilitayarisha kumpandisha cheo hadi kuwa kiongozi wa wilaya. Siku moja nilipokuwa nikizungumza na ndugu huyu, alitaja kwamba alihisi kuwa nilikuwa mwenye nguvu sana katika kazi yangu, mkali sana, na kwamba katika mkusanyiko pamoja nami hapakuwa na furaha nyingi .... Niliposikia jambo hili, nilihisi kuwa nilikuwa nimedunishwa. Nilihisi vibaya sana; mara moja nikakuza maoni fulani ya ndugu huyu, na sikukusudia tena kumpandisha cheo kuwa kiongozi wa wilaya.

Jumapili, 3 Februari 2019

Ushuhuda wa Maisha | 6. Huduma ya Aina Hii Kwa Hakika Ni Ya Kudharauliwa

Ushuhuda wa Maisha | 6. Huduma ya Aina Hii Kwa Hakika Ni Ya Kudharauliwa


Ding Ning Mji wa Heze, Mkoa wa Shandong

     Katika siku chache zilizopita, kanisa limepanga mabadiliko katika kazi yangu. Nilipopokea wajibu huu mpya, niliwaza, "Ninahitaji kuchukua fursa hii ya mwisho kuita mkutano na ndugu zangu wa kiume na wa kike, niongee nao wazi juu ya mambo, na niwaache na picha nzuri." Kwa hiyo, nilikutana na mashemasi kadhaa, na kufikia mwisho wa wakati wetu pamoja, nikasema, "Nimeulizwa kuondoka hapa na kuenda kwa kazi tofauti.

Jumamosi, 2 Februari 2019

Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | ""Je, Wajua? Mungu Amefanya Jambo Kubwa Miongoni Mwa Wanadamu"""


Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | "Je, Wajua? Mungu Amefanya Jambo Kubwa Miongoni Mwa Wanadamu"


  Mwenyezi Mungu anasema, "Bila kazi ya Yesu, mwanadamu hangeweza kushuka chini kutoka msalabani, lakini bila kupata mwili siku hii, wale wanaoshuka chini kutoka msalabani hawangewahi kusifiwa na Mungu ama kuingia katika enzi mpya. Bila kuja kwa huyu mwanadamu wa kawaida, basi hamngeweza kuwa na hii fursa ama kustahiki kuona uso wa ukweli wa Mungu, kwani nyinyi nyote ni wale ambao wangepaswa kuangamizwa kitambo sana. Kwa sababu ya kuja kwa Mungu mwenye mwili kwa mara ya pili, Mungu amewasamehe na kuwaonyesha huruma. Bila kujali, maneno ambayo lazima Niwaachie mwishowe ni haya: Huyu mwanadamu wa kawaida, ambaye ni Mungu mwenye mwili, ni wa umuhimu sana kwenu. Hili ndilo jambo kubwa ambalo Mungu tayari Amefanya miongoni mwa wanadamu."