Jaweni na Upendo kwa Ajili ya Mungu | Muziki wa Akapela "Yasifu Maisha Mapya"

Kristo wa siku za mwisho ameonekana, akifanya kazi na kuzungumza miongini mwa wanadamu. Neno lake hutuhukumu, kutuadibu na kututakasa, likituongoza kwenye njia sahihi ya maisha ya binadamu.

Muziki wa Akapela "Tokeo Lililofikiwa kwa Kumjua Mungu" (Video Rasmi ya Muziki)

Hayuko katika upeo wa mbali, wala hajajificha juu mawinguni. Yuko kando yako, akiwa na mamlaka juu ya kila kitu chako, Yeye ni kila kitu ulicho nacho, na Yeye ni kitu pekee ulicho nacho.

Mwabudu Mungu kwa Roho na Ukweli | “Sauti ya Moyo ya Kiumbe Aliyeumbwa” (Video za Kikristo)

Mungu wa vitendo na wa kweli, upendo ndani ya moyo wangu. Mimi ni vumbi lakini ninaweza kuona uso Wako. Ninawezaje kukosa kukuabudu?

Mungu ndiye Mwanzo na tena Mwisho | Kwaya ya Injili

Mungu ndiye Mwanzo (Mungu ndiye Mwanzo) na Mwisho (na Mwisho); ni Yeye Mwenyewe Anayetekeleza kazi Yake na hivyo lazima iwe Yeye Mwenyewe Anayemaliza enzi ya kale. Huo ndio ushahidi kuwa Yeye humshinda Shetani (humshinda Shetani) na huishinda dunia, ushahidi kuwa Yeye huishinda dunia.

Nampenda Mungu kwa Moyo Wangu Wote | "Nitampenda Mungu Milele" Video Rasmi ya Muziki

Nitakupa Wewe upendo wa kweli, na sitakuacha Usubiri. Mimi nitakupa Wewe upendo safi, na tafadhali furahia upendo wangu. Nitakupa Wewe upendo wangu wote, na kukuacha upate upendo wangu. Nitakupenda Wewe kwa wakati wote; kukuridhisha Wewe ni matamanio yangu.

Jumanne, 30 Aprili 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 68



Matamshi ya Mwenyezi MunguSura ya 68

Neno Langu linatekelezwa katika kila nchi, mahali, taifa na kikundi, na neno Langu linakamilishwa katika kila pembe wakati wowote. Maafa yanayotokea kila mahali si vita kati ya watu, wala si mapigano na silaha. Hakutakuwa na vita tena baadaye. Wote wako katika mfumbato Wangu. Wote watakabili hukumu Yangu na watadhoofika kati ya maafa. Acha wale wanaonipinga na wale wasioanza kushirikiana na Mimi wateseke uchungu wa maafa mbalimbali. Acha walie na kusaga meno yao hadi milele, na kubaki katika giza daima. Hawataendelea kuishi. 

Jumatatu, 29 Aprili 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 98

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 98

Mambo yote yatakuja juu ya kila mmoja wenu, na yatawawezesha kujua zaidi juu Yangu na kuwa na uhakika zaidi juu Yangu. Yatawawezesha kunijua, Mungu mmoja Mwenyewe, kunijua Mimi Mwenye uweza, kunijua Mimi Mungu Mwenyewe mwenye mwili. Baadaye, Nitatoka katika mwili, Nirudi Sayuni, Nirudi katika nchi nzuri ya Kanaani, ambayo ni makazi Yangu, ndiyo hatima Yangu, na ndio msingi ambao niliumba vitu vyote. Sasa hakuna yeyote kati yenu anayeelewa maana ya maneno ambayo Ninasema, hakuna mtu hata mmoja ambaye anaweza kuelewa maana ya maneno haya.

Jumapili, 28 Aprili 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 104

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 104

Watu, matukio na vitu vyote nje Yangu vitakufa na kuwakatika hali ya kutokuwepo, ilhali watu, matukio na vitu vyote vilivyo ndani Yangu vitapata kila kitu kutoka Kwangu na kuingia katika utukufu pamoja na Mimi, kuingia katika Mlima Wangu Sayuni, makazi Yangu, na kuishi pamoja kwa amani nami milele. Niliumba vitu vyote mwanzoni na Nitamaliza kazi Yangu mwishowe, na pia Nitatawala milele kama Mfalme. Katikati, pia Ninaongoza na kuutawala ulimwengu mzima. Hakuna anayeweza kuondoa mamlaka Yangu, kwani Mimi ni Mungu mmoja Mwenyewe, na pia Nina uwezo wa kupitisha mamlaka Yangu kwawazaliwa Wangu wa Kwanza, ili wazaliwa Wangu wa kwanza waweze kutawala kandokando Yangu.

Jumamosi, 27 Aprili 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 65

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 65

Maneno Yangu daima yanaendeleza barabara, yaani yanaonyesha udhaifu wenu wa jaala, vinginevyo bado mgekuwa mnakokota visigino vyenyu, bila wazo la muda gani ulioko sasa. Fahamu hili! Mimi Hutumia njia ya upendo ili kuwaokoa. Bila kujali jinsi nyinyi mlivyo, bila shaka Nitakamilisha mambo ambayo Nimekubali bila kufanya kosa lolote. Je, Ninaweza, Mwenyezi Mungu Mwenye haki, kufanya kosa? Je, hiyo siyo dhana ya mtu? Niambieni, kila kitu Mimi Hufanya na kusema si kwa ajili yenu?

Ijumaa, 26 Aprili 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 97

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 97

Nitafanya kila mtu aone matendo Yangu ya ajabu na kusikia maneno Yangu ya hekima. Ni lazima iwe kila mtu na ni lazima iwe juu ya kila suala. Hii ni amri Yangu ya utawala na ni ghadhabu Yangu. Nitahusisha kila mtu na kila jambo ili watu wote kutoka mwisho mmoja wa ulimwengu hadi mwingine wataona kwa macho yao wenyewe, la sivyo Sitaacha kamwe. Ghadhabu Yangu imemwagwa kikamilifu na hakuna hata chembe imezuiwa. Inaelekezwa kwa kila mtu mmoja ambaye anakubali jina hili (hivi karibuni itageuzwa juu ya mataifa yote ya dunia). Na ghadhabu Yangu ni nini? Ni kali kiasi gani?

Alhamisi, 25 Aprili 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 100

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 100

Ninawachukia wale wote ambao hawajajaaliwa na kuchaguliwa na Mimi. Kwa hiyo ni lazima Niwafukuze watu hawa kutoka katika nyumba Yangu mmoja baada ya mwingine, hivyo hekalu Langu litakuwa takatifu na bila doa, nyumba Yangu itakuwa mpya daima na haitakuwa nzee kamwe, jina Langu takatifu litaenezwa milele na watu Wangu watakatifu watakuwa wapendwa Wangu. Aina hii ya mandhari, aina hii ya nyumba, aina hii ya ufalme ni lengo Langu, makao Yangu nayo ni msingi wa uumbaji Wangu wa vitu vyote. Hakuna mtu anayeweza kuyayumbisha au kuyabadilisha. Mimi mwenyewe na wana Wangu wapendwa tutaishi pamoja ndani yake na hakuna mtu atakayeruhusiwa kuyakanyaga, hakuna chochote kitakachoruhusiwa kuishi humo na hata zaidi hakuna kitu chochote kibaya kitakachoruhusiwa kutokea kamwe. Yote itakuwa sifa na kushangilia tu, yote yatakuwa mandhari ambayo mwanadamu hawezi kudhania.

Jumatano, 24 Aprili 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 120

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 120

Sayuni! Salamu! Sayuni! Ita kwa sauti! Nimerudi kwa ushindi, Nimerudi nikiwa mshindi! Watu wote! Harakisheni mpange foleni kwa utaratibu! Vitu vyote! Mtakuja kusimama kabisa, kwa sababu nafsi Yangu inaukabili ulimwengu mzima na nafsi Yangu inaonekana katika Mashariki ya dunia! Nani anayethubutu kutopiga magoti katika ibada? Nani anayethubutu kutosema kumhusu Mungu wa kweli? Nani anayethubutu kutoangalia juu kwa kumcha? Nani anayethubutu kutotoa sifa? Nani anayethubutu kutangaza kwa shangwe? Watu wangu wataisikia sauti Yangu, Wanangu watasalia ndani ya ufalme Wangu!

Jumanne, 23 Aprili 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 114

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 114

Niliumba ulimwengu dunia; Nilitengeneza milima, mito, na vitu vyote; Niliunda miisho ya mifumo ya sayari; Niliwaongoza wana Wangu na watu Wangu; Niliamuru vitu na mambo yote. Sasa, Nitawaongoza wazaliwa Wangu wa kwanza warudi kwenye Mlima Wangu Sayuni, kurudi mahali ambapo Naishi, ambayo itakuwa hatua ya mwisho katika kazi Yangu. Yote ambayo Nimeyatenda (kila kitu kilichofanyika kutoka uumbaji mpaka sasa) yalikuwa kwa sababu ya hatua ya leo ya kazi Yangu, na zaidi ni kwa sababu ya utawala wa kesho, ufalme wa kesho, na kwa ajili ya Mimi na wazaliwa Wangu wa kwanza kuwa na furaha ya milele.

Jumatatu, 22 Aprili 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 14


Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 14


Katika enzi zote, hakuna mwanadamu ameingia katika ufalme na hivyo hakuna aliyefurahia neema ya Enzi ya Ufalme, hakuna aliyeona Mfalme wa ufalme. Ingawa chini ya nuru ya Roho Wangu watu wengi wametabiri uzuri wa ufalme, wanajua tu nje ya ufalme, sio umuhimu wa ndani. Leo, ufalme ujapo kuwepo rasmi duniani, binadamu wote bado hujui kinachopaswa kukamilishwa, ulimwengu ambao binadamu hatimaye ataletwa ndani, wakati wa Enzi ya Ufalme. Kuhusu haya, Naogopa watu wote wako katika hali ya mkanganyiko. Kwa sababu siku ya utambuzi kamili wa ufalme bado haijafika kabisa, wanadamu wote wamechanganyikiwa, hawawezi kuiona vizuri.

Jumapili, 21 Aprili 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 35

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Sura ya 35

Nimeanza kutenda kazi Yangu kati ya wanadamu, kuwakubalia kuishi mkondo mmoja Nami. Nitakamilisha kazi Yangu nikiwa kati yao, maana wao ni vyombo Ninavyosimamia katika mpango Wangu wote wa usimamizi—na ni mapenzi Langu ili waweze kuwa watawala wa vitu vyote. Hivyo basi Naendelea kutembea kati ya wanadamu. Kadri wanadamu pamoja Nami tuingiavyo katika enzi ya sasa, Najihisi huru kabisa, kwa sababu, hatua Yangu ni ya haraka.

Jumamosi, 20 Aprili 2019

Wimbo wa Kuabudu | "Tabia ya Haki ya Mungu ni ya Pekee" | How to Know God


Wimbo wa Kuabudu | "Tabia ya Haki ya Mungu ni ya Pekee" | How to Know God
Mungu huonyesha tabia Yake ya haki kupitia mbinu na kanuni za kipekee,
haidhibitiwi na watu, matukio au vitu.
au kumshawishi Ajaribu njia tofauti.
Na hakuna awezaye kubadili dhana au mawazo Yake,
Mungu huhuku matendo na mawazo yote ya viumbe kwa tabia Yake ya haki.
Hii ndiyo asili ya kipekee ya tabia ya haki ya Muumba! Tabia Yake ya haki!
Na hakuna awezaye kubadili rehema au ghadhabu Yake.
Na kulingana na hili, Hutoa ghadhabu au kupeana rehema. Na ni kiini Chake tu kiwezacho kuamua njia hii.
hakuna awezaye kiuka au kushuku hili.
Hii ndiyo asili ya kipekee ya tabia ya haki ya Muumba! Tabia Yake ya haki! Tabia ya haki ya Mungu, takatifu na ya kipekee;
Hii ni asili ya kipekee ya tabia ya haki ya Muumba!
Hakuna awezaye kuimiliki, kiumbwacho au kisichoumbwa. Ghadhabu ya Mungu ni takatifu; haiwezi kukosewa. Rehema Yake pia yabeba asili hii. Tabia Yake ya haki!
Hii ndiyo asili ya kipekee ya tabia ya haki ya Muumba!
Hakuna mbadala wa Mungu katika Matendo Yake, kiumbwacho au kisichoumbwa. Wala hawezi kuuharibu Sodoma au kuuokoa Ninawi kama alivyofanya Mungu. Tabia Yake ya haki! Tabia Yake ya haki!

 
kutoka katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

Kujua zaidi: Umeme wa Mashariki Hutoka wapi?  Sauti na maneno ya Roho Mtakatifu | "Ni Muhimu Sana Kuelewa Tabia ya Mungu"

Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III Mamlaka ya Mungu II” Sehemi ya Tatu

Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee III Mamlaka ya Mungu II” Sehemi ya Tatu
Mwenyezi Mungu alisema, "Baada ya mtu kupita utoto na wakati wake wa kubaleghe na kwa utaratibu bila kuzuilika kufikia ukomavu, hatua inayofuata ni kwake yeye kuuaga kabisa ule ujana wake, kuwaaga wazazi wake, na kukabiliana na barabara iliyo mbele yake akiwa mtu mzima huru. Wakati huo[c] lazima wakabiliane na watu, matukio na mambo yote ambayo mtu mzima lazima apitie, na kukabiliana na viungo mbalimbali katika msururu wa hatima yake. Hii ndiyo awamu ya tatu ambayo lazima mtu apitie."

Kujua zaidi: Utangulizi wa programu ya Kanisa la Mwenyezi Mungu | Injili ya kurudi kwa Bwana Yesu . Umeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Ijumaa, 19 Aprili 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Ngurumo Saba Zatoa Sauti—Zikitabiri Kuwa Injili ya Ufalme Itaenea Kote Ulimwenguni

Matamshi ya Mwenyezi Mungu Ngurumo Saba Zatoa Sauti—Zikitabiri Kuwa Injili ya Ufalme Itaenea Kote Ulimwenguni

Mimi Naeneza kazi Yangu katika nchi za Mataifa. Utukufu Wangu unamulika kotekote ulimwenguni; mapenzi Yangu yamo katika wanadamu yakitawanyika hapa na pale, wote wakiongozwa kwa mkono Wangu na kufanya kazi ambayo Nimewapa. Kuanzia wakati huu kuendelea, Nimeingia katika enzi mpya, kuwaleta watu wote katika ulimwengu mwingine. Niliporudi katika “nchi Yangu,” Nilianza sehemu nyingine tena ya kazi katika mpango Wangu wa asili, ili mwanadamu aje kunijua zaidi. Nauchukua ulimwengu katika ukamilifu wake na kuona kwamba[a] ni wakati muafaka wa kazi Yangu, kwa hiyo Naharakisha mbele na nyuma kufanya kazi Yangu mpya ndani ya mwanadamu. Hii ni enzi mpya, hata hivyo, na Nimeleta kazi mpya ili Niwachukue watu wapya wengi zaidi katika enzi mpya na kuachana na wengi wa wale Nitakaowaondoa.

Jumatano, 17 Aprili 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Wote Wasiomjua Mungu Ndio Wanaompinga Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Kazi ya Mungu,kumjua mungu

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Wote Wasiomjua Mungu Ndio Wanaompinga Mungu

Kufahamu madhumuni ya kazi ya Mungu, athari inayotimizwa kwa mwanadamu, na mapenzi ya Mungu kwa mwanadamu, hiki ndicho kitu ambacho kila mwanadamu anayemfuata Mungu anapaswa kutimiza. Sasa wanachokosa watu wote ni ufahamu wa kazi ya Mungu. Mwanadamu haelewi wala kufahamu kabisa maana ya vitendo vya Mungu ndani ya mwanadamu, kazi yote ya Mungu, na mapenzi ya Mungu tangu kuumbwa kwa dunia. Huu upungufu hauonekani tu katika ulimwengu mzima wa kidini, lakini zaidi ya hayo kwa waumini wote wa Mungu.

Jumanne, 16 Aprili 2019

“Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee X Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (IV)” Sehemu ya Tatu


“Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee X Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (IV)” Sehemu ya Tatu

3. Mzunguko wa Uhai na Mauti wa Watu Wanaomfuata Mungu

Baada ya hayo, hebu tuzungumzie mzunguko wa uhai na mauti wa wale wanaomfuata Mungu. Hili linawahusu, hivyo kuweni makini. Kwanza, fikiria kuhusu ni makundi gani ambamo watu wanaomfuata Mungu wanaweza kugawika. (Wateule wa Mungu na watendaji huduma.) Kuna mawili: wateule wa Mungu na watendaji huduma. Kwanza tutazungumza kuhusu wateule wa Mungu, ambao ni wachache. “Wateule wa Mungu” inarejelea nini?

Jumatatu, 15 Aprili 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Tabia Yako Ni Duni Sana!




Kanisa la Mwenyezi Mungu,Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki

Matamshi ya Mwenyezi MunguTabia Yako Ni Duni Sana!

Ninyi nyote mmeketi katika viti vya kifahari, mkiwafundisha wale wa vizazi vijana ambao ni wa aina yenu, ukiwafanya waketi nawe. Je, mngekosaje kujua kwamba wale “watoto” wenu walikuwa tayari hawana pumzi, na kwamba hawakuwa na kazi Yangu zamani? Utukufu Wangu huangaza kutoka nchi ya Mashariki hadi nchi ya Magharibi, lakini wakati utukufu Wangu huenea mpaka mwisho wa dunia na wakati unapoanza kuinuka na kuangaza, Nitaondoa utukufu wa Mashariki na kuuletea Magharibi ili kwamba watu hawa wa giza katika Mashariki ambao wameniacha Mimi watakuwa bila mwanga unaong’aa kuanzia hapo kwendelea. Wakati huo, mtaishi katika bonde la kivuli. Ingawa watu leo ni wazuri mara mia zaidi kuliko awali, bado hawawezi kuyatosheleza mahitaji Yangu, na bado wao si ushahidi mtukufu Kwangu. 

Jumapili, 14 Aprili 2019

Wimbo wa Kuabudu | "Sifa kwa Maisha Mapya katika Ufalme" | Watu wa Mungu Humsifu na Kumwabudu Mungu


Wimbo wa Kuabudu | "Sifa kwa Maisha Mapya katika Ufalme" | Watu wa Mungu Humsifu na Kumwabudu Mungu

Tumesikia sauti ya Mungu na kurudi nyumbani Kwake.
Mikutanoni tunakula na kunywa maneno ya Mungu, tunahudhuria karamu.
Sisi tunaaga huzuni na vifungo vyetu, tunaishi maisha mapya.
Tunapofungua mioyo yetu katika ushirika wa kweli, mioyo yetu inaangazwa sana.
Maneno ya Mungu yako nasi kila siku, tunastarehe ndani yake.
Tunaondolewa vizuizi na ubaguzi wetu, tunaishi ndani ya upendo wa Mungu.
Tunatafakari, kufikiri maneno ya Mungu, Roho Mtakatifu anatuangazia.
Tunaelewa moyo wa Mungu, sisi si hasi tena.

Ijumaa, 12 Aprili 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Umuhimu wa Kuukoa Uzao wa Moabu

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Umuhimu wa Kuukoa Uzao wa Moabu

Katika miaka hii miwili hadi mitatu ya kazi, kile kilichopaswa kutimizwa katika kazi ya hukumu iliyofanyika juu yenu kimetimizwa kimsingi. Watu wengi wamesahau matarajio na kudura yao ya baadaye. Hata hivyo, inapotajwa kuwa ninyi ni uzao wa Moabu, wengi wenu huchukizwa sana—nyuso zenu hubadilika, vinywa vyenu hupinda, na macho yenu hukodolea. Hamuwezi kabisa kuamini kwamba ninyi ni uzao wa Moabu. 

Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee II Tabia ya Haki ya Mungu” Sehemu ya Pili



Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee II Tabia ya Haki ya Mungu” Sehemu ya Pili


Ingawaje Hasira ya Mungu ni Fiche na Haijulikani kwa Binadamu, Haivumilii Kosa Lolote

Namna Mungu alivyoshughulikia binadamu wote wa ujinga na kutojua ulitokana kimsingi na huruma na uvumilivu. Hasira yake, kwa upande mwingine, imefichwa kwenye wingi mkubwa mno wa muda na wa mambo; haijulikani kwa binadamu. Kutokana na hayo, ni vigumu sana kwa binadamu kumwona Mungu akionyesha hasira Yake, na ni vigumu pia kuelewa hasira Yake. Kwa hivyo, binadamu huchukulia hasira ya Mungu kuwa ndogo. Wakati binadamu anakabiliwa na kazi ya mwisho ya Mungu na hatua ya kuvumilia na kusamehe binadamu—yaani, wakati onyesho la mwisho la Mungu la huruma na onyo Lake la mwisho linapowafikia—kama bado wangali wanatumia mbinu zile kumpinga Mungu na hawafanyi jitihada zozote za kutubu, kurekebisha njia zao au kukubali huruma Yake, Mungu hataweza tena kuwapatia uvumilivu na subira yake.

Alhamisi, 11 Aprili 2019

Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VII” Sehemu ya Kwanza



Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VII” Sehemu ya Kwanza



Mhutasari wa Mamlaka ya Mungu, Tabia ya Haki ya Mungu, na Utakatifu wa Mungu
Mnapomaliza maombi yenu, je, mioyo yenu inahisi utulivu katika uwepo wa Mungu? (Ndiyo.) Ikiwa moyo wa mtu unaweza kutulizwa, ataweza kusikia na kuelewa neno la Mungu na ataweza kusikia na kuuelewa ukweli. Ikiwa moyo wako hauwezi kutulizwa, ikiwa moyo wako siku zote unayoyoma, au siku zote unafikiria juu ya mambo mengine, utaathiri kuja kwako pamoja kusikia neno la Mungu. Sasa, ni kitu gani cha msingi tunachokijadili wakati huu? Hebu sote turudi nyuma kidogo katika hoja kuu. Kuhusiana na kumjua Mungu Mwenyewe, yule wa kipekee, sehemu ya kwanza tuliyoijadili ni ipi? (Mamlaka ya Mungu.) Ya pili ilikuwa ni ipi? (Tabia ya haki ya Mungu.) Na ya tatu? (Utakatifu wa Mungu.) Tumejadili mara ngapi kuhusu mamlaka ya Mungu?

Jumatano, 10 Aprili 2019

Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee V Utakatifu wa Mungu II” Sehemu ya Nne



Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee V Utakatifu wa Mungu (II)” Sehemu ya Nne
Mwenyezi Mungu anasema, “Kuelewa kiini cha Mungu na kujua kiini cha Mungu kinapeana msaada usioweza kupimika kwa kuingia kwa watu katika maisha. Natumai kwamba hamtapuuza haya ama kuyaona kama mchezo; kwa sababu kumjua Mungu ni msingi muhimu na msingi wa imani ya mwanadamu kwa Mungu na ufuatiliaji wa mwanadamu wa ukweli na wokovu na kitu ambacho hakifai kuachiliwa. Iwapo mwanadamu anamwamini Mungu lakini hamjui Mungu, na iwapo mwanadamu anaishi miongoni mwa baadhi ya barua na mafundisho ya kidini, hutawahi kufikia wokovu hata kama utatenda na kuishi kulingana na maana ya juujuu ya ukweli. Hiyo ni kusema, iwapo imani yako kwa Mungu haitokani na kumjua, basi imani yako haimaanishi chochote.”

kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Kujua zaidi:  Umeme wa Mashariki Hutoka wapi? . Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | “Kumjua Mungu Ndiyo Njia ya Kumcha Mungu na Kuepuka Maovu

Jumanne, 9 Aprili 2019

Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | "Kutazama Kuonekana kwa Mungu katika Hukumu na Kuadibu Kwake"



Matamshi ya Kristo wa Siku za Mwisho | "Kutazama Kuonekana kwa Mungu katika Hukumu na Kuadibu Kwake"

Mwenyezi Mungu anasema, “Hakuna mtu mbali na Yeye anayeweza kujua mawazo yetu yote, au kufahamu asili yetu na kiini chetu kwa dhahiri na ukamilifu, ama kuhukumu uasi na upotovu wa binadamu, ama kusema nasi na kufanya kazi kati yetu kama hivi kwa niaba ya Mungu aliye mbinguni. Hakuna mtu isipokuwa Yeye ambaye amepewa mamlaka, hekima, na heshima ya Mungu; tabia ya Mungu na kile Mungu Anacho na alicho yanatoka, kwa ukamilifu wao, ndani Yake. Hakuna mtu mbali na Yeye ambaye anaweza kutuonyesha njia na kutuletea mwangaza. Hakuna yeyote ila Yeye anayeweza kutufichulia siri ambazo Mungu hajatufunulia tangu uumbaji hadi leo. Hamna yeyote isipokuwa Yeye ambaye anaweza kutuokoa kutokana na utumwa wa Shetani na tabia yetu potovu. Yeye humwakilisha Mungu. Yeye huonyesha moyo wa ndani zaidi wa Mungu, ushawishi wa Mungu, na maneno ya hukumu ya Mungu kwa wanadamu wote. Ameanzisha enzi mpya, nyakati mpya, na kuleta mbingu na nchi mpya na kazi mpya, na ametuletea matumaini, akimaliza maisha ambayo tuliishi katika hali isiyo dhahiri, na kuwezesha nafsi yetu nzima kuona njia ya wokovu kwa udhahiri kamili. Ameshinda ubinadamu wetu wote, na kupata mioyo yetu. Tangu wakati huo na kuendelea, akili zetu zimepata ufahamu, na nafsi zetu huonekana kufufuka: Huyu mwanadamu wa kawaida asiyekuwa na umuhimu, ambaye huishi kati yetu na ambaye amekataliwa na sisi zamani—Je, huyu si ni Bwana Yesu, ambaye daima huwa kwa mawazo yetu, tukiwa tumeamka au kuota, na ambaye tunamtamani usiku na mchana? Ni Yeye! Ni Yeye kweli! Yeye ni Mungu wetu! Yeye ndiye ukweli, njia, na uzima! Yeye ametuwezesha kuishi tena na kuona nuru, na amekomesha mioyo yetu kuhangaika. Tumerudi nyumbani mwa Mungu, tumerejea mbele ya kiti Chake cha enzi, tuko uso kwa uso pamoja na Yeye, tumeshuhudia uso Wake, na tumeona njia iliyo mbele.”
kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Jumatatu, 8 Aprili 2019

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Kazi na Kuingia (10)

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki

Matamshi ya Mwenyezi Mungu | Kazi na Kuingia (10)


Kwa wanadamu kuendelea mbele kiasi hiki ni hali isiyo na kigezo. Kazi ya Mungu na kuingia kwa mwanadamu vinaendelea bega kwa bega, na hivyo kazi ya Mungu, pia, ni tukio kubwa lisilo na kifani. Kuingia kwa mwanadamu hadi sasa ni ajabu ambayo kamwe haijawahi kufikiriwa na mwanadamu. Kazi ya Mungu imefikia upeo wake—na, kufuatia, “kuingia” kwa mwanadamu[1] pia kumefikia kilele chake. Mungu amejishusha kwa kadiri Anavyoweza, na kamwe Hajawahi kuwalalamikia wanadamu au vitu vyote katika ulimwengu.

Jumapili, 7 Aprili 2019

Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee X Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (IV)”



Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee X Mungu ni Chanzo cha Uhai kwa Vitu Vyote (IV)”
Mwenyezi Mungu alisema, "Kwa kweli, Mungu hana mahitaji sana kwa wanadamu—au angalau, hana mahitaji kama watu wanavyodhani. Bila matamshi ya Mungu, au udhihirishaji wowote wa tabia Yake, matendo, au maneno, basi kumjua Mungu kungekuwa kugumu sana kwenu, kwa sababu watu wangelazimika kukisia nia ya Mungu na mapenzi Yake, kitu ambacho ni kigumu sana kwao. Lakini kutokana na hatua ya mwisho ya Kazi Yake, Mungu amenena maneno mengi, kufanya kiwango kikubwa cha kazi, na kufanya mahitaji mengi kwa wanadamu. Katika maneno Yake, na kiwango kikubwa cha kazi Yake, amejulisha watu anachokipenda, anachokichukia, na wanafaa kuwa aina gani ya watu. Baada ya kuelewa vitu hivi, ndani ya nyoyo watu wanafaa kuwa na maelezo sahihi ya mahitaji ya Mungu, kwa kuwa hawamwabudu tena yule Mungu asiye yakini, au kumfuata Mungu katika ukosefu uyakini na udhahania na utupu; badala yake, watu wanaweza kusikia maneno ya Mungu, wanaweza kuelewa viwango vya mahitaji ya Mungu, na kuvifikia, na Mungu hutumia lugha ya wanadamu kuwaambia watu yale yote wanafaa kujua na kulewa. Leo, kama watu hawafahamu mahitaji ya Mungu kwao, kile Mungu alicho, kwa nini wanamwamini Mungu, na jinsi wanafaa kumwamini Mungu na jinsi wanavyojichukulia mbele Zake, basi kuna shida hapa. Sasa hivi tu kila mmoja wenu amezungumza kuhusu kipengele kimoja; mnafahamu kuhusu mambo fulani, yawe ni mambo mahususi au ya jumla—lakini Ningependa kuwaambia mahitaji ya Mungu ya kweli, kamili, na mahususi kwa wanadamu. Ni maneno machache tu, na rahisi sana. Yawezekana tayari mnayajua haya maneno. Mahitaji sahihi ya Mungu kwa wanadamu na wale ambao wanamfuata ni kama ifuatavyo. Mungu anahitaji mambo matano kutoka kwa wale wanaomfuata; imani ya kweli, ufuasi wenye uaminifu, utiifu kamili, ufahamu wa kweli na heshima za kutoka moyoni.
Katika mambo haya matano, Mungu anahitaji kuwa watu wasimshuku tena, wala kumfuata wakitumia fikira zao au mitazamo ikosayo uyakini na iliyo dhahania; Ni lazima wamfuate Mungu bila fikira au dhana zozote. Mungu anahitaji kuwa wote wanaomfuata wafanye hivyo kwa uaminifu, sio kwa shingo upande au bila kujizatiti. Mungu anapokupa mahitaji yoyote, au kukujaribu, kukuhukumu, kukushughulikia na kukupogoa, au kukuadhibu na kukuangamiza, unapaswa kuwa mtiifu kabisa Kwake. Hufai kuuliza kilichosababisha, au kuweka masharti, au hata uongee kuhusu sababu. Utiifu wako lazima uwe usio na shaka. Kumjua Mungu ni kipengele ambacho watu wengi wanakosea. Mara kwa mara wanamlazimishia Mungu misemo, matamshi, na maneno ambayo hayahusiani na Yeye, wakiamini kuwa haya maneno ndiyo ya kweli kuhusu kumfahamu Mungu. Kumbe hawajui kuwa hii misemo, ambayo inatoka kwa fikira za watu, ung'amuzi wao, na busara zao, havina uhusiano wowote na kiini cha Mungu. Na kwa hiyo, Ninataka kukwambia kuwa, katika ufahamu wa watu unaotamaniwa na Mungu, Mungu haulizi tu kwamba umtambue Mungu na maneno Yake, lakini kuwa ufahamu wako juu ya Mungu ni sahihi. Hata kama unaweza kusema sentensi moja tu, au una ufahamu mdogo tu, huu ufahamu mdogo ni sahihi na wa kweli, na unalingana na kiini cha Mungu Mwenyewe. Kwa kuwa Mungu hapendi sifa na wao kumtukuza Yeye kwa hali isiyo halisi na yenye nia mbaya. Zaidi ya hayo, Anachukia watu wanapomchukulia kama hewa. Anachukia ambapo, wakati wa majadiliano juu ya mada kuhusu Mungu, watu wanazungumza kimzaha, wakiongea kwa hiari bila ya kujali, wakiongea wapendavyo; zaidi ya hayo, anawachukia wale wanaojifanya wanamjua Mungu, na wanaringa kuhusu ufahamu wa Mungu, wakijadili mada kuhusu Mungu bila mipaka au kipimo. La mwisho Kati ya yale mahitaji matano lilikuwa ni kumheshimu Mungu kutoka moyoni. Hili ndilo hitaji kuu la Mungu kwa wale wote wanaomfuata. Wakati mtu ana ufahamu wa kweli na sahihi kumhusu Mungu, anaweza kumheshimu Mungu na kuepuka maovu. Heshima hii hutoka ndani ya moyo wake, ni ya hiari, na sio kwa sababu Mungu amemshurutisha. Mungu hataki utoe zawadi ya mwelekeo wowote wa kupendeza, au tabia, au mienendo ya nje Kwake; badala yake, anataka kwamba umheshimu na umwogope kutoka ndani ya moyo wako. Heshima hii inaafikiwa kutokana na mabadiliko katika tabia ya maisha yako, kwa sababu una ufahamu juu ya Mungu, kwa sababu unaelewa matendo ya Mungu, kwa sababu ya uelewa wako wa kiini cha Mungu, na kwa sababu umetambua ukweli kuwa wewe ni mmoja wa viumbe wa Mungu. Na kwa hiyo, nia yangu ya kutumia neno “kutoka moyoni” kwa kurejelea heshima hapa ni kwamba wanadamu waelewe kuwa heshima ya watu kwa Mungu inapaswa kutoka ndani ya mioyo yao.
Sasa yafikirie hayo matakwa matano: kuna yeyote kati yenu anaweza kupata matatu ya kwanza? Ambapo Ninamaanisha uaminifu wa kweli, ufuasi wenye uaminifu, na utiifu kamili. Kuna wowote kati yenu wanaoweza mambo haya? Najua Nikisema yote matano, basi bila kuuliza hapatakuwa na hata mmoja kati yenu anayeweza—lakini nimeyapunguza hadi matatu. Tafakari kama umeyapata au la. Je, “uaminifu wa kweli” ni rahisi kuupata? (La, sio rahisi.) Sio rahisi, kwa kuwa mara nyingi watu humtilia Mungu mashaka. Na, je, “ufuasi wenye uaminifu”? Huu “uaminifu” una maana gani? (Sio kwa shingo upande ila kwa moyo wote.) Sio kwa shingo upande ila kwa moyo wote. Mmegonga ndipo! Kwa hiyo, je, mna uwezo wa kupata hili hitaji? Inabidi mjitahidi zaidi—siyo? Kwa sasa bado hamjapata hili hitaji. Kuhusu “utiifu kamili”—je, mmepata hilo? (Hapana.) Bado hamjapata hilo, pia. Mara nyingi nyinyi si watiifu na ni waasi, mara nyingi hamsikilizi, au kupenda kutii, au kutaka kusikia. Haya ndiyo mahitaji matatu ya msingi wanayopata watu baada ya kuingia katika maisha yao, na bado hamjayapata. Kwa hiyo, kwa wakati huu, mna uwezo mkubwa? Leo, baada ya kunisikia nikisema maneno haya, mna wasiwasi? (Ndiyo.) Ni sawa kuwa mna wasiwasi—. Msiwe na wasiwasi Ninahisi wasiwasi kwa niaba yenu. Sitakwenda katika mahitaji hayo mengine mawili; bila shaka, hakuna anayeweza kuyafikia. Mna shauku. Kwa hivyo mmebaini malengo yenu? Malengo yapi, kuelekeza upande gani, mnapaswa kuyafuata, na kujitolea jitihada zenu? Mna lengo? (Ndiyo.) Lengo lenu ni lipi? (Kuutafuta ukweli, kuutafuta ufahamu wa Mungu katika maneno Yake, na kwa hakika kupata heshima na utiifu kwa Mungu.) Hebu niongee waziwazi: mnapofikia mahitaji haya matano, mtakuwa mmemridhisha Mungu. Kila mojawapo ni ishara, ishara ya watu wakiingia katika maisha wakiwa wamefikia ukomavu, na lengo la mwisho la hii. Hata kama Ningechukua moja kati ya mahitaji na kuongea kwa kina kulihusu na kinachohitajika, haiwezi kuwa rahisi kupata; ni lazima mpitie kiwango fulani cha matatizo na kufanya kiasi fulani cha juhudi. Na ni aina gani ya mawazo mnapaswa kuwa nayo? Yanapaswa kuwa sawa na yale ya mgonjwa wa saratani anayesubiri kwenda kwenye meza ya upasuaji. Na ni kwa nini Ninasema haya? Kama ungependa kumwamini Mungu, na kumpata Mungu na kupata ridhaa Yake, basi kama hutapitia katika kiasi fulani cha shida, au kufanya kiwango fulani cha juhudi, hutaweza kupata vitu hivi. Umesikia mahubiri mengi, lakini kuyasikia hakumaanishi kuwa haya mahubiri ni yako; ni lazima uyachukue na kuyageuza yawe kitu ambacho ni chako, ni lazima uyasimilishe maishani mwako, na kuyaleta katika uwepo wako, ukiyaruhusu maneno na mahubiri haya yakuongoze katika maisha yako, na kuleta dhamana na maana ya uhai katika maisha yako—na hivyo basi itakuwa ni thamani kuwa uliyasikia maneno haya. Kama maneno haya Ninayoyanena hayaleti mabadiliko yoyote katika maisha yenu, au thamani yoyote katika uwepo wako, basi hakuna haja ya kuyasikiliza. Mnaelewa haya, ndiyo? Baada ya kuelewa haya, basi kilichobaki ni juu yenu wenyewe. Ni lazima mfanye kazi! Ni lazima muwe na bidii katika kila jambo! Msiwe huku na kule—wakati unapita upesi! Wengi wenu wameamini kwa zaidi ya miaka kumi. Tazama nyuma kwa hii miaka zaidi ya kumi ya imani katika Mungu: Umenufaika kiasi gani? Na mmesalia na miongo mingapi ya haya maisha? Sio mirefu. Sahau kuhusu iwapo kazi ya Mungu inakusubiri, iwapo Amekuachia nafasi, iwapo Atafanya kazi ile ile tena; usizungumze kuhusu hili. Unaweza kurudisha nyuma miaka yako kumi iliyopita? Kwa kila siku inayopita, na kila hatua unayochukua, siku ambazo unazo hupunguzwa kwa siku moja. Muda haumsubiri mwanadamu yeyote! Utanufaika tu kutokana na imani kwa Mungu kama utaichukulia kama kitu kikubwa zaidi maishani mwako, muhimu zaidi kuliko chakula, mavazi, au kitu kingine chochote! Kama huwa unaamini tu unapokuwa na wakati, na huwezi kutoa umakini wako wote kwa imani yako, kama siku zote umetatizwa na vurugu, basi hutafaidi chochote. Unaelewa hili, ndio? Tutaishia hapa kwa leo. Tuonane wakati ujao! (Shukrani kwa Mungu!)"


kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili


Kujua zaidi: Umeme wa Mashariki Hutoka wapi?

Jumamosi, 6 Aprili 2019

Matamshi ya Mungu | “Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo ya Kazi Yake” Sehemu ya Kwanza


Matamshi ya Mungu | “Namna ya Kujua Tabia ya Mungu na Matokeo ya Kazi Yake” Sehemu ya Kwanza


Kwanza, hebu tuuimbe wimbo wa kumsifu Mungu: Wimbo wa Ufalme (I) Ufalme Umeshuka katika Ulimwengu.
Kiambata: Watu wanamshangilia Mungu, watu wanamsifu Mungu; vinywa vyote vinamwita Mungu mmoja wa kweli. Mfalme unashuka ulimwenguni.
I. Watu wanamshangilia Mungu, watu wanamsifu Mungu; vinywa vyote vinamwita Mungu mmoja wa kweli, watu wote wanainua macho yao kuyatazama matendo ya Mungu. Ufalme unashuka ulimwenguni, nafsi ya Mungu yu tajiri na mwenye ukarimu, tajiri na mwenye ukarimu. Ni nani ambaye hangeshangilia kwa ajili ya haya? (Ni nani ambaye hangeshangilia kwa ajili ya haya?) (Ni nani ambaye hangecheza kwa furaha kwa ajili ya haya?) Oo, Zayuni! (Oo, Zayuni!) Oo, Zayuni! (Oo, Zayuni!) Inua bango lako la shangwe ili kusherehekea Mungu! Imba wimbo wako wa shangwe wa ushindi na kueneza jina takatifu la Mungu!
II. Mambo yote duniani! Sasa jitakaseni kwa haraka katika kutoa sadaka kwa Mungu, katika kutoa sadaka kwa Mungu! Nyota kule mbinguni! Sasa rudini mahali penu na kuonyesha ukuu wa Mungu katika mbingu! Mungu hushughulikia sauti ya watu duniani nchini, wanaomwaga upendo usio na mwisho na heshima kwa Mungu kwenye nyimbo! Kwenye siku hii, viumbe vyote vinarudia ujana, Mungu anakuja kutembea. Wakati huu, maua hunawiri, ndege kuimba, viumbe vyote hujaa shangwe! Ndege wanaimba, viumbe vyote hujaa shangwe! Kusikikapo mlio wa saluti ya ufalme, ufalme wa Shetani ukiangamizwa chini ya kiitikio kinachovuma cha nyimbo za ufalme. Na hautawahi kuinuka tena!
III. Ni nani ulimwenguni anayethubutu kuinuka na kupinga? Mungu hushuka duniani, Mungu huleta moto, huleta hasira, huleta majanga yote, majanga yote. Falme za ulimwengu sasa ni, sasa ni ufalme wa Mungu! Juu mbinguni, mawingu yanagaagaa na kujongea kama wimbi; chini ya mbingu (chini ya mbingu), chini ya mbingu (chini ya mbingu), maji maziwani na mitoni yanabingirika na kutoa tuni ya kusisimua. Wanyama waliokuwa mapumzikoni wanajitokeza kutoka kwenye mapango yao, na watu wote waliokuwa wamelala wanaamshwa na Mungu. Siku iliyosubiriwa na kila mmoja hatimaye imewadia, hatimaye imewadia! Wanatoa nyimbo nzuri kabisa, nyimbo nzuri kabisa, kwa Mungu! Kwa Mungu! Kwa Mungu!
Ni nini mnachofikiria kuhusu kila wakati mnapouimba wimbo huu? (Ukiwa umechangamka; nasisimkwa; nafikiria namna ambavyo utukufu wa ufalme ulivyo mrembo, na mwanadamu na Mungu wataunganishwa daima dawamu.) Je, yupo yeyote aliyefikiria kuhusu umbo ambalo binadamu lazima achukue ili kuweza kuwa na Mungu? Katika kufikiria kwenu, mtu anafaa kuwa vipi ili kuweza kujiunga na Mungu na kufurahia maisha yenye utukufu yanayofuata katika ufalme? (Wanafaa kuwa wamebadilisha tabia.) Wanafaa kuwa wamebadilisha tabia, lakini kubadilisha hadi kiwango gani? Watakuwa vipi baada ya kubadilishwa tabia? (Watakuwa watakatifu.) Ni nini kipimo cha utakatifu? (Fikira na utiliaji maanani wao wote unalingana na Kristo.) Sasa ni vipi ambavyo hali hii ya kuingiliana inavyojionyesha? (Hawamzuii Mungu, wala kumsaliti Mungu, lakini wanajitolea kuwa wenye utiifu kabisa kwa Mungu na kumcha Mungu katika mioyo yao.) Baadhi ya majibu yenu yako katika njia sawa. Fungueni mioyo yenu, nyinyi nyote, na msemezane kile ambacho mioyo yenu inawaambia. (Watu wanaoishi na Mungu katika ufalme wanaweza kutekeleza wajibu wao, kutekeleza kwa uaminifu wajibu wao, kwa kutafuta ukweli na kutozuiliwa na mtu yeyote, hafla yoyote, au kifaa chochote. Na inawezekana kujiondoa kwenye ushawishi wa giza na kulinganisha mioyo yao na Mungu, na kumcha Mungu na kujiepusha na uovu.) (Mtazamo wetu wa kuangalia mambo unaweza kulinganishwa na ule wa Mungu, na tunaweza kujitenga na ushawishi wa giza. Kiwango cha chini zaidi ni kutotumiwa vibaya na Shetani, kutupa nje tabia yoyote ya upotoshaji, na kutimiza utiifu wa Mungu. Tunasadiki kwamba kuwa huru dhidi ya ushawishi wa giza ndiyo hoja kuu. Kama mtu hawezi kujitenga na ushawishi wa giza, hawezi kujipa uhuru kutoka kwenye minyororo ya Shetani, basi hajapata wokovu wa Mungu.) (Kiwango cha kufanywa kuwa mtimilifu na Mungu ni binadamu akiwa na moyo mmoja na akili na Mungu. Binadamu hamzuii Mungu tena; anaweza kujua Mungu mwenyewe, kuweka ukweli katika matendo, kupata uelewa wa Mungu, kumpenda Mungu, na kulingana na Mungu. Hayo ndiyo yote ambayo mtu anahitaji kufanya.)
Uzito wa Matokeo katika Mioyo ya Watu
Yaonekana mnavyo vitu katika mioyo yenu kuhusu njia mnayofaa kutembea na mmeimarisha uelewa na ung’amuzi mzuri kuhusu vitu hivyo. Lakini kama kila kitu mlichokisema kitaishia kuwa maneno matupu au uhalisia halisi inategemea ni nini mnatilia maanani katika mazoea yako ya kila siku. Mmepata mavuno kutoka kwenye dhana zote za ukweli kupitia miaka hii, kwenye falsafa na kwenye maudhui ya ukweli. Hii inathibitisha kwamba watu siku hizi wanatilia mkazo kule kutafuta ukweli. Na kutokana na hayo, kila dhana na kila kipengele cha ukweli kwa hakika kimeweka mizizi kwenye mioyo ya baadhi ya watu. Hata hivyo, ni nini hasa Ninachoogopa sana? Kwamba ingawa wahusika wa ukweli, na nadharia hizi, yameweza kunakili mizizi yao, maudhui halisi bado hayana uzito mkubwa katika mioyo yenu. Wakati mnapokumbana na masuala, mnapopitia majaribio, mnapopitia chaguo—mtaweza kwa kiwango kipi kutumia uhalisia wa ukweli huu vizuri? Je, haya yote yatawasaidia kupitia kwenye ugumu wenu na kuwafanya kuibuka kutoka kwenye majaribio yenu baada ya kutosheleza nia za Mungu? Je, mtasimama imara katika majaribio yenu na kushuhudia kwa sauti na waziwazi kwake Mungu? Je, mmewahi kuwa na kivutio katika masuala haya awali? Mniruhusu kuuliza: Katika mioyo yenu, kwenye fikira na tafakari zenu za kila siku, ni nini hicho ambacho ni muhimu sana kwenu? Mmewahi kuja kwenye hitimisho? Ni nini mnachosadiki kuwa kitu muhimu zaidi? Baadhi ya watu husema “ni kuweka ukweli katika matendo, bila shaka”; baadhi ya watu husema “bila shaka ni kulisoma neno la Mungu kila siku”; baadhi ya watu husema “ni kujiweka mbele ya Mungu na kuomba Mungu kila siku, bila shaka”; na kisha kunao wale wanaosema “bila shaka ni kutekeleza wajibu wangu kwa njia bora kila siku”; kunao baadhi ya watu pia ambao wanasema wanafikiria wakati wote tu kuhusu namna ya kumtosheleza Mungu, namna ya kumtii Yeye katika mambo yote, na namna ya kuchukua hatua kulingana na mapenzi Yake. Je, hivi ndivyo ilivyo? Je, hivi ndivyo kila kitu kinavyohitajika kufanywa? Kwa mfano, kunao baadhi wanaosema: “Mimi ninataka tu kumtii Mungu, lakini kitu kinapofanyika siwezi kumtii Yeye.” Baadhi ya watu husema: “Nataka tu kumtosheleza Mungu. Hata kama ningemtosheleza Yeye mara moja tu, hilo lingetosha, lakini sitoweza kumtosheleza Yeye.” Na baadhi ya watu husema: “Ninataka tu kumtii Mungu. Katika nyakati za majaribio nataka kunyenyekea katika mipango Yake, huku nikitii ukuu na mipangilio Yake, bila ya malalamiko au maombi yoyote. Ilhali karibu kila wakati ninashindwa kuwa mtiifu.” Baadhi ya watu wengine husema: “Ninapokabiliwa na uamuzi, siwezi kamwe kutia ukweli katika matendo. Siku zote nataka kutosheleza mwili, siku zote nataka kutosheleza matamanio yangu ya kibinafsi ninayojitakia.” Ni nini sababu ya haya? Kabla ya jaribio la Mungu kufika, je, mmewahi kujipa changamoto nyinyi wenyewe mara nyingi, na kujijaribu nyinyi wenyewe mara nyingi? Oneni kama kweli mnaweza kumtii Mungu, kuweza kwa kweli kumtosheleza Mungu, na kuwa na hakika kutomsaliti Mungu. Tazameni kama hamwezi kujitosheleza, kutojitosheleza matamanio yenu ya kibinafsi, lakini kumtosheleza Mungu tu, bila ya chaguo lenu la kibinafsi. Je, yupo aliye hivi? Kwa hakika, kunayo hoja moja tu ambayo imewekwa mbele ya macho yenu nyinyi wenyewe. Ni kile ambacho kila mmoja wenu anavutiwa nacho, kile ambacho mnachotaka kujua zaidi, na hilo ni suala la matokeo na hatima ya kila mmoja wenu. Huenda msitambue, lakini hili ni jambo ambalo hakuna anayeweza kulikataa. Ninajua kwamba kunao baadhi ya watu ambao, tunapokuja katika ukweli wa matokeo ya binadamu, ahadi ya Mungu kwa ubinadamu, na aina gani ya hatima ambayo Mungu ananuia kumleta binadamu katika, tayari wamefanyia uchunguzi neno la Mungu katika masuala haya mara kadhaa. Kisha kunao ambao kila mara wanalitafuta na kulifikiria kwenye akili zao, na bado hawapati matokeo, au pengine wanafikia katika hitimisho fulani isiyoeleweka. Hatimaye bado hawana hakika kuhusu ni aina gani ya matokeo yanayowasubiri. Wakati wa kuyakubali mawasiliano ya ukweli, wakati wa kuyakubali maisha ya kanisa, wakati wa kutenda wajibu wao, baadhi ya watu siku zote wanataka kujua jibu wazi kwa maswali yafuatayo: Matokeo yangu yatakuwa yapi? Ninaweza kutembelea njia hii hadi mwisho wake? Mwelekeo wa Mungu kwake binadamu ni upi? Baadhi ya watu huwa hata na wasiwasi: Nimefanya baadhi ya mambo siku zilizopita, nimesema baadhi ya mambo, sikumtii Mungu, nimefanya mambo fulani ambayo yamemsaliti Mungu, kulikuwa na masuala fulani ambapo sikumtosheleza Mungu, niliuumiza moyo wa Mungu, nilimfanya Mungu kunikasirikia, nilimfanya Mungu kunichukia na kuniona kwamba ninachukiza, hivyo basi pengine matokeo yangu hayajulikani. Ni haki kusema kwamba watu wengi zaidi wanahisi wasiwasi kuhusu matokeo yao wenyewe. Hakuna anayethubutu kusema: “Nahisi kwa uhakika wa asilimia mia moja kwamba nitaishi Ninao uhakika wa asilimia mia moja kwamba ninaweza kuzitosheleza nia za Mungu; mimi ni mtu anayefuata moyo wa Mungu; mimi ni mtu anayesifiwa na Mungu.” Baadhi ya watu hufikiria ni vigumu hasa kufuata njia ya Mungu, na kwamba kutia ukweli katika matendo ndilo jambo gumu zaidi la kufanya. Kwa hivyo, watu hawa hufikiria hawawezi kusaidika, na hawathubutu kuwa na matumaini ya kuwa na matokeo mazuri. Au pengine wanasadiki kwamba hawawezi kutosheleza nia za Mungu, na kuweza kuishi; na kwa sababu ya haya watasema kwamba hawana matokeo, na hawawezi kufikia hatima nzuri. Licha ya jinsi watu hufikiria, kila mmoja anastaajabu kuhusu matokeo yao mara nyingi. Kuhusu masuala ya siku zao za usoni, kuhusu maswali ya kile watakachopata wakati Mungu atakapomaliza kazi Yake, watu hawa siku zote wanapiga hesabu, siku zote wanapanga. Baadhi ya watu wanalipia bei mara dufu; baadhi ya watu wanaacha familia zao na kazi zao; baadhi ya watu wanakata tamaa katika ndoa zao; baadhi ya watu wanakubali bila kulalamika kutumia rasilmali kwa ajili ya Mungu; baadhi ya watu huacha nyumba zao ili kutenda wajibu wao; baadhi ya watu huchagua ugumu, na kuanza kufanya kazi ambazo ni chungu zaidi na zinachosha zaidi; baadhi ya watu huchagua kuutoa utajiri wao, kujitolea kila kitu chao; na bado baadhi ya watu huchagua kufuata ukweli na kufuatilia kumjua Mungu. Haijalishi namna mnavyochagua kutenda, namna mnavyotenda ndiyo muhimu zaidi? (Si muhimu.) Ni vipi tunavyoelezea kwamba si muhimu, basi? Kama namna hiyo si muhimu, basi ni nini muhimu? (Tabia nzuri kwa nje si wakilishi wa kutia ukweli katika matendo.) (Kile ambacho kila mmoja anafikiria si muhimu. Cha msingi hapa ni kama tumeweza kutia ukweli katika matendo, na kama tunampenda Mungu.) (Maangamizi ya wapinga Kristo na viongozi bandia hutusaidia kuelewa kwamba tabia ya nje si jambo muhimu zaidi. Kwa nje wanaonekana kuwa wamejinyima mengi, na wanaonekana kuwa radhi kulipa bei, lakini kwa kuchambua tunaweza kuona kwamba hawana moyo kabisa unaomcha Mungu; kwa mitazamo yote wanampinga Yeye. Siku zote wanasimama pamoja na Shetani katika nyakati za hatari, na kuingilia kazi ya Mungu. Hivyo basi, utiliaji maanani mkuu hapa ni upande gani tutasimama wakati ukiwadia, na mitazamo yetu.) Nyote mnaongea vyema, na yaonekana kwamba tayari mnao msingi wa uelewa wa na kiwango cha kuweza kutia ukweli wenu katika matendo, nia za Mungu, na kile Mungu anahitaji kutoka kwa binadamu. Kwamba mnaweza kuongea hivi ni jambo la kugusa kweli. Ingawa kuna maneno machache yasiyofaa hapa na pale, kauli zenu tayari zinakaribia ufafanuzi unaostahili ukweli Hii inathibitisha kwamba mmeimarisha uelewa wenu halisi wa watu matukio, na vifaa vilivyo karibu nanyi, mazingira yenu yote ambayo Mungu amepanga, na kila kitu mnachoweza kuona. Uelewa huu unakaribia ukweli. Hata ingawa kile mnachosema si pana kabisa, na maneno machache hayafai sana, uelewa wenu tayari unakaribia uhalisi wa ukweli. Kuwasikiliza mkiongea kwa njia hii kunanifanya Mimi kuhisi vizuri sana.
Imani za Watu Haziwezi Kubadilishwa na Ukweli
Kunao baadhi ya watu wanaoweza kuvumilia ugumu; wanaweza kulipia bei; tabia yao ya nje ni nzuri sana; wanaheshimika sana; na wanatamaniwa na wengine. Mnafikiria nini: Je, tabia kama hii ya nje inaweza kuchukuliwa kama ya kutia ukweli katika matendo? Mnaweza kusema kwamba mtu huyu anatosheleza nia za Mungu? Kwa nini mara kwa mara watu wanamwona mtu wa aina hii na kufikiria kwamba wao wanamtosheleza Mungu, wanafikiria kwamba wanatembelea njia ile ya kutia ukweli katika matendo, kwamba wanatembea katika njia ya Mungu? Kwa nini baadhi ya watu hufikiria kwa njia hii? Upo ufafanuzi mmoja tu kwa haya. Na ufafanuzi huu ni upi? Sababu ni kwamba kwa kiasi kikubwa cha watu, maswali kama kutia ukweli katika matendo ni nini, kutosheleza Mungu ni nini, ni nini kuwa na uhalisia wa ukweli—maswali haya hayako wazi sana. Hivyo basi kunao baadhi ya watu ambao mara nyingi wanadanganywa na wale ambao kwa nje wanaonekana wa kiroho, wanaonekana wa kilodi, wanaonekana kuwa na taswira za ukuu. Kuhusiana na watu hao wanaoweza kuzungumzia barua na falsafa, na ambao hotuba na vitendo vyao vinaonekana kuwa vyenye kustahili uvutiwaji, wale wanaowatamani hawajawahi kuangalia kiini halisi cha vitendo vyao, kanuni zinazoendesha vitendo vyao, shabaha zao ni nini. Na hawajawahi kuangalia kama watu hawa wanatii Mungu kwa kweli, na kama wao ni watu wanaomcha Mungu kwa kweli na kujiepusha na uovu au la. Hawajawahi kutambua kile kiini halisi cha ubinadamu cha watu hawa. Badala yake, kutoka kwenye hatua ya kwanza ya kujua na kuzoeana nao, hatua kwa hatua wanaanza kuwapenda watu hawa, kuwatukuza watu hawa, na hatimaye watu hawa wanakuwa sanamu zao. Aidha, katika akili za baadhi ya watu, sanamu hizi wanazoziabudu, wanaosadiki wanaweza kuacha familia na kazi zao, na kulipa ile bei kwa juujuu—sanamu hizi ndizo ambazo kwa kweli zinatosheleza Mungu, ndizo zile zinazoweza kupokea kwa kweli matokeo mazuri na hatima nzuri. Katika akili zao, sanamu hizi ndizo wale watu ambao Mungu husifu. Ni nini husababisha watu kuwa na aina hii ya kusadiki? Ni nini kiini halisi cha suala hili? Ni nini matokeo hali hii inaweza kuleta? Hebu na tuzungumzie kwanza suala la kiini chake halisi.
Masuala haya kuhusiana na mitazamo ya watu, vitendo vya watu, ni kanuni gani ambazo watu wanachagua kutenda, na kile ambacho kwa kawaida kila mtu anatilia mkazo, kimsingi haya yote hayahusu mahitaji ya Mungu kwa mwanadamu hata kidogo. Bila kujali kama watu wanazingatia masuala ya juujuu au yale ya kina, wanazingatia barua na falsafa au uhalisia, watu hawatii yale ambayo wanafaa kutii zaidi, na hawajui kile wanachofaa kujua zaidi. Sababu ya hali hii kuwa hivi ni kwamba watu hawaupendi ukweli kamwe. Hivyo basi, watu hawako radhi kutumia muda na jitihada zao katika kutafuta na kuendeleza kanuni katika neno la Mungu. Badala yake, wanapendelea kutumia njia za mkato, na kujumlisha kile wanachoelewa, kile wanachojua, kuwa vitendo vizuri na tabia nzuri. Muhtasari huu nao huwa shabaha yao ya binafsi ya kufuata, unakuwa ukweli wa kutendwa. Athari ya moja kwa moja ya haya yote ni kwamba watu wanatumia tabia nzuri ya kibinadamu kama kisawazisho cha kutia ukweli katika matendo yao, hali ambayo inatosheleza pia matamanio ya watu ili kupata fadhila na Mungu. Hii inawapa watu mtaji wa kushindania ukweli na kutoa sababu ili kumshawishi Mungu na kuingia katika mzozo Naye. Wakati uo huo, watu wanamweka Mungu kando kwa njia za ufidhuli, na kuiweka ile sanamu ya mioyo yao katika nafasi ya Mungu. Kunayo sababu moja tu ya chanzo cha haya ambayo huwafanya watu kuwa na vitendo wasivyovijua, mitazamo wasiyoijua, au mitazamo na vitendo vya upande mmoja, na leo Nitawaelezea kuhusu haya. Sababu ni kwamba ingawa watu wengi wanaweza kumfuata Mungu, kumwomba Yeye kila siku, na kusoma neno la Mungu kila siku, hawaelewi kwa hakika nia za Mungu. Hiki ndicho chanzo cha tatizo. Kama mtu huelewa moyo wa Mungu, huelewa kile anachopenda Mungu, kile humchukiza Mungu, kile anachotaka Mungu, kile anachokataa Mungu, ni mtu wa aina gani ambaye Mungu humpenda, ni mtu wa aina gani ambaye Mungu hampendi, ni kiwango kipi ambacho Mungu hutumia katika kutoa mahitaji Yake kwa binadamu, ni mtazamo gani ambao Anauchukua katika kumfanya binadamu kuwa mtimilifu, je, mtu huyu anaweza bado kuwa na mawazo yake ya kibinafsi? Wanaweza tu kuenda na kumwabudu mtu mwingine? Mtu wa kawaida anaweza kuwa sanamu yao? Kama mtu anaelewa nia za Mungu, mtazamo wake ni wenye kirazini zaidi kuliko hapo. Hawatamwabudu kama Mungu kiongozi aliyepotoka kiholela, wala hawataweza, huku wakitembea njia ya kutia ukweli katika matendo, kusadiki kwamba kutii kiholela katika sheria au kanuni chache rahisi ni sawa na kutia ukweli katika matendo.
Kunayo Maoni Mengi Yanayohusu Kiwango Ambacho Mungu Hutumia Kuasisi Matokeo ya Binadamu

Hebu na turudi katika mada hii na tuendelee kuzungumzia suala la matokeo.
Kwa sababu kila mmoja anajali matokeo yake, je, mnajua namna ambavyo Mungu huamua matokeo hayo? Na ni kwa njia gani ambayo Mungu huanzisha matokeo ya mtu? Na ni kiwango gani ambacho Mungu hutumia kuasisi matokeo ya mtu? Na wakati ambapo matokeo ya mtu yangali bado hayajaasisiwa, ni nini anachofanya Mungu ili kufichua matokeo haya? Je, yupo anayejua haya? Kama Nilivyosema tu, kunao baadhi ambao tayari wamefanyia uchunguzi neno la Mungu kitambo sana. Watu hao wanatafuta dalili fulani kuhusu matokeo ya mwanadamu, kuhusu kategoria ambazo matokeo haya yamegawanywa, na kuhusu matokeo tofauti yanayosubiria aina tofauti ya watu. Wanataka pia kujua namna neno la Mungu linavyoanzisha matokeo ya binadamu, aina za kiwango ambacho Mungu hutumia, na njia ambayo Yeye huasisi matokeo ya binadamu. Ilhali mwishowe watu hawa hawafanikiwi kupata chochote. Kwa hakika, yapo mambo machache yenye thamani yanayozungumzwa kuhusu suala hili miongoni mwa neno la Mungu. Kwa nini hali iko hivi? Ili mradi matokeo ya binadamu yangali hayajafichuliwa, Mungu hataki kumwambia yeyote kuhusu kile kitakachofanyika mwishowe, wala Hataki kumfahamisha yeyote kuhusu hatima yao kabla ya wakati kufika. Sababu ya kufanya hivi ni kwamba Mungu kufanya hivyo hakutaleta manufaa yoyote kwa binadamu. Sasa hivi, Nataka kuwaambia tu kuhusu namna Mungu huasisi matokeo ya binadamu, kuhusu kanuni Anazotumia katika kazi Yake ili kuyaasisi matokeo ya binadamu, na kuonyesha matokeo haya, pamoja na kiwango Anachotumia ili kuanzisha kama mtu ataweza kuishi au la. Hiki sicho kile ambacho mnajali zaidi kuhusu? Hivyo basi, ni vipi ambavyo watu hufahamu njia ambayo Mungu anaanzisha matokeo ya binadamu? Mlizungumzia kidogo kuhusu suala hili muda mfupi uliopita. Baadhi yenu mlisema kwamba ni swali la kutenda wajibu wao kwa uaminifu, kugharamika kwa ajili ya Mungu; baadhi ya watu walisema kumtii Mungu na kutosheleza Mungu; baadhi ya watu walisema kudhibitiwa na Mungu; na baadhi ya watu walisema kuishi maisha ya hadhi ya chini…. Wakati mnapotia ukweli huu katika matendo, wakati mnapotenda kanuni za kufikiria kwenu, je mnajua kile Mungu anachofikiria? Mmewahi kufikiria kama kuendelea hivi ni kutosheleza nia za Mungu au la? Kama kunatilia maanani kiwango cha Mungu? Kama kunatilia maanani mahitaji ya Mungu? Ninasadiki kwamba watu wengi zaidi hawalifikirii suala hili kwa undani. Wanatumia tu bila kutilia maanani sehemu ya neno la Mungu, au sehemu ya mahubiri, au viwango vya watu fulani wa kiroho ambao wanawaabudu, na kujilazimisha kufanya hivi na vile. Wanasadiki kwamba hii ndiyo njia sahihi, na hivyo basi wanaendelea kuitii, kuifanya, liwalo liwe hatimaye. Baadhi ya watu hufikiria: “Nimesadiki kwa miaka mingi siku zote nimetenda mambo kwa njia hii; nahisi kuwa nimemtosheleza kabisa Mungu; ninahisi pia kuwa nimejifunza mengi kutoka kwa haya. Kwani nimekwishaelewa ukweli mwingi katika kipindi hiki, na nimeelewa mambo mengi ambayo sikuyaelewa awali—hasa, wingi wa fikira na mitazamo yangu imebadilika, maadili ya maisha yangu yamebadilika sana, na ninao uelewa mzuri sana wa ulimwengu huu.” Watu kama hao wanasadiki kwamba haya ni mavuno, na ndiyo matokeo ya mwisho ya kazi ya Mungu kwa binadamu. Kwa maoni yenu, kwa viwango hivi na vitendo vyenu nyote vimewekwa pamoja—je, mnatosheleza nia za Mungu? Baadhi ya watu watasema kwa uhakika wote: “Bila shaka! Tunatenda kulingana na neno la Mungu; tunatenda kulingana na kile ambacho ndugu alihubiri na kushiriki nasi; siku zote tunafanya wajibu wetu, siku zote tunamfuata Mungu, hatujawahi kumwacha Mungu. Hivyo basi tunaweza kusema kwa imani kamili kwamba tunamtosheleza Mungu. Haijalishi ni kiasi kipi tunachoelewa kuhusu nia za Mungu, haijalishi ni vipi tunavyoelewa neno la Mungu, siku zote tumekuwa kwa njia ya kutafuta kuweza kutangamana na Mungu. Kama tutachukua hatua kwa usahihi, na kutenda kwa usahihi, basi matokeo yatakuwa sahihi.” Je, mnafikiria nini kuhusu mtazamo huu? Je, ni kweli? Pengine wapo wale wanaosema: “Sijawahi kufikiria kuhusu mambo haya awali. Mimi nafikiria tu kwamba nikiendelea kutimiza wajibu wangu na kuendelea kutenda kulingana na mahitaji ya neno la Mungu, basi nitasalia. Sijawahi kufikiria swali la kama ninaweza kutosheleza moyo wa Mungu, na sijawahi kufikiria kama ninatimiza kiwango kinachohitajika na Yeye. Kwa sababu Mungu hajawahi kuniambia, wala kunipatia maagizo yoyote kwa uwazi, ninasadiki kwamba mradi tu niendelee kupiga hatua mbele, Mungu atatosheka na Yeye hafai kuwa na mahitaji yoyote ya ziada kwangu mimi.” Je, kusadiki huku ni sahihi? Kulingana na Ninavyojua, njia hii ya kutenda, njia hii ya kufikiria, na mitazamo hii—yote yanakuja na madoido fulani na kiasi kidogo cha upofu. Ninaposema hivi, pengine wapo baadhi yenu mnaohisi kuvunjika moyo: “Yaani upofu? Kama ni ‘upofu,’ basi tumaini letu la wokovu, tumaini letu la kuishini dogo mno, na halina uhakika, hapo ni kweli? Je, wewe kulitamka hivyo lilivyo si sawa na kutumwagilia maji baridi?” Haijalishi kile mnachosadiki, mambo Ninayoyasema na kufanya hayanuii kukufanya ninyi kuhisi kama mnamwagiliwa maji baridi. Badala yake, yananuia kuboresha uelewa wenu wa nia za Mungu, na kuboresha ung’amuzi wenu kuhusu kile ambacho Mungu anafikiria, kile ambacho Mungu anataka kukamilisha ni mtu wa aina gani ambaye Mungu anapenda, nini kinachukiza Mungu, nini Mungu anadharau, ni mtu wa aina gani ambaye Mungu anataka kumpata, na ni mtu wa aina gani ambaye Mungu anatupilia mbali. Yananuia kupatia akili zenu uwazi, kuwasaidia kujua wazi ni kiwango kipi vitendo na fikira za kila mmoja wenu yamepotea kutoka kwa kiwango kinachohitajika na Mungu. Je, inahitajika kuzungumzia mada hii? Kwa sababu Ninajua mmesadiki kwa muda mrefu, na mmesikiliza mahubiri mengi, lakini kwa hakika haya ndiyo mambo yanayokosekana zaidi. Mmerekodi kila ukweli katika daftari zenu, mmerekodi pia kile ambacho nyie wenyewe mnasadiki kibinafsi kuwa muhimu katika akili zenu na katika mioyo yenu. Na mnapanga kukitumia kumridhisha Mungu mnapotenda, kukitumia wakati mnahitaji usaidizi, au kukitumia kupitia nyakati ngumu zilizo mbele yenu, au mnaacha ukweli huu uandamane na ninyi mnapoishi maisha yenu tu. Lakini kulingana na Ninavyojua, iwapo mnatenda tu, namna mnavyotenda hasa si muhimu. Nini, basi, ndicho kitu cha muhimu sana? Ni kwamba wakati unatenda, moyo wako hujua kwa uhakika wote kama kila kitu unachofanya, kila kitendo, ndicho kile anachotaka Mungu au la; kama kila kitu unachofanya ni sahihi au la, kila kitu unachofikiria ni sahihi au la, na matokeo na shabaha katika moyo wako yanatosheleza nia za Mungu au la, kama yanatilia maanani mahitaji ya Mungu au la, na kama Mungu anayaidhinisha au la. Haya ni mambo muhimu.
kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili
Kujua zaidi: Matamshi ya Mungu | "Unajua Nini Kuhusu Imani?

Ijumaa, 5 Aprili 2019

Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VI Utakatifu wa Mungu III” Sehemu ya Pili


Matamshi ya Mungu | “Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VI Utakatifu wa Mungu (III)” Sehemu ya Pili
Mwenyezi Mungu anasema, “Zaidi ya mwanadamu kutafuta kwa tamaa umaarufu na faida, daima anaendelea kutekeleza uchunguzi wa sayansi na utafiti wa kina, kisha bila kikomo huridhisha mahitaji yake ya mwili na tamaa; yapi tena ni matokeo ya mwanadamu? Kwanza kabisa hakuna tena usawa wa ikolojia na, pamoja na hili, miili ya wanadamu yote imetiwa doa na kuharibiwa na mazingira ya hali hii, na magonjwa mbalimbali ya kuambukiza na mapigo kusambaa kila mahali. Hii ni hali ambayo mwanadamu sasa hawezi kudhibiti, sivyo? Sasa kwa sababu mnaelewa hili, iwapo wanadamu hawamfuati Mungu, lakini daima wanamfuata Shetani kwa njia hii—kutumia maarifa daima kujitajirisha, kutumia sayansi kuchunguza bila kikomo siku za baadaye za maisha ya binadamu, kutumia mbinu ya aina hii kuendelea kuishi—mnaweza kutambua hitimisho ya asili ya wanadamu itakuwa vipi? Matokeo ya mwisho asilia yatakuwa yapi? Itakuwa uharibifu: kukaribia uharibifu hatua moja kwa wakati. Kukaribia uharibifu kwa hatua moja kwa wakati!”

Kujua zaidi: Swahili Gospel Praise Music "Kila Kitu Kinaishi Chini ya Sheria na Masharti Yaliyowekwa na Mungu". Umeme wa Mashariki Hutoka wapi?



Alhamisi, 4 Aprili 2019

Wimbo wa Injili "Mwana wa Adamu Ameonekana" | Sifu Kurudi kwa Yesu Mwokozi | Watoto Wanacheza Ngoma



Wimbo wa Injili "Mwana wa Adamu Ameonekana" | Sifu Kurudi kwa Yesu Mwokozi | Watoto Wanacheza Ngoma
Kutoka Mashariki ya ulimwengu (Mashariki ... Mashariki ...), mwale wa mwanga unatokea (mwanga ... mwanga ...), ukiangaza njia yote kwenda magharibi. Mwana wa Adamu ameshuka duniani. Mwokozi amerejea, Yeye ni Mwenyezi Mungu. Akionyesha ukweli, Ameanzisha enzi mpya. Mwana wa Adamu ameonekana. (Siyo?) Mungu amekuja. (Eh!) Yeye huwaletea binadamu njia ya uzima wa milele@(njia ya uzima wa milele). Mbingu mpya, dunia mpya, enzi mpya, binadamu wapya, njia mpya, maisha mapya. Yerusalemu mpya umeshuka duniani. Tumerudi kwa familia ya Mungu na tunaishi maisha ya kanisa, kila siku tukila na kunywa neno la Mungu, tukikua katika upendo Wake. Wewe kuja na uimbe! (Sawa!) Nitacheza ngoma! (Ngoma!) Maisha yetu ni ya furaha kweli (furaha kweli). Tuko katika uwepo wa Mungu. (Tunaufurahia kweli.) Tuna baraka za Mungu. (Tuna furaha sana.) Ufalme wa Kristo ni nyumba kunjufu. Mwenyezi Mungu, Kristo wa siku za mwisho, mpendwa wetu apendezaye. Kila mstari Anenao ni ukweli, utunyinyiziao. Anatufundisha jinsi ya kutenda, jinsi ya kuwa waaminifu. Tukiishi kati ya baraka za Mungu, tunampenda Mungu kwa moyo wetu wote. Hukumu ya neno la Mungu inaishinda mioyo ya watu wote. Wakiwa wametakaswa, watu wa Mungu humtolea ushuhuda. Hebu tuwe wenye akili moja (tukitimiza wajibu wetu), tukilipiza upendo wa Mungu (kuwa na ushuhuda kwa Mungu), tukieneza injili ya Ufalme wa Mungu (injili ya Ufalme wa Mungu). Neno la Mungu linaenea duniani kote. Jina takatifu la Mungu linasifiwa na wote. Ufalme wa Kristo unafanyika duniani. Hebu tuwe wenye akili moja (tukitimiza wajibu wetu), tukilipiza upendo wa Mungu (kuwa na ushuhuda kwa Mungu), tukieneza injili ya Ufalme wa Mungu (injili ya Ufalme wa Mungu). Neno la Mungu linaenea duniani kote. Jina takatifu la Mungu linasifiwa na wote. Ufalme wa Kristo unafanyika duniani. Ufalme wa Kristo unafanyika duniani.
kutoka katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

Kujua zaidi: Umeme wa Mashariki Hutoka wapi?